Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Kwa karibu masaa sita ka nzi kalikuwa kametulia kwenye ukumbi makao makuu ya Tanesco ambapo Mkurugenzi wa Shirika hilo Dr. Idris Rashid alikuwa aje kuzungumza na waandishi hususan suala kununua majenereta ya kufulia umeme ambayo yanamilikiwa na kampuni yenye utata wa umiliki wake na yenye kuhusishwa na kampuni ya kifisadi ya Richmond, Dowans.

Hata hivyo, muda si mrefu uliopita mtumishi wa Tanesco aliingia ukumbini na kuwaambia waandishi waliokuwa wanasubiri kwa muda mrefu kuwa Bw. Idris hatozungumzia nao na kuwaomba radhi.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vyenye uwezo wa kupenya kuta na madari vinadokeza kuwa suala la Dowans limefikia mahali pagumu ambapo sasa Tanesco wako tayari kuachana na wazo hili ili kutafuta vyanzo vingine vya umeme wa dharura na ya kuwa wametilia maanani "kelele" za wadau mbalimbali. Hili linakuja baada ya sauti za Spika wa Bunge la Muungano Mhe. Samuel Sitta na Mbunge wa Kyela Mhe. Harrison Mwakyembe kupaza sauti zao kupinga mpango huo. Ujumbe ambao umepokelewa toka kwa watunga sheria hao ni kuwa yeyote atakayenunua majenereta ya Dowans ajiandae kuwajibika Dodoma kama walivyowajibishwa wengine!

Tishio hilo ambalo limepokelewa kwa hisia ya kunyong'onyea limetuma ujumbe ulio wazi kuwa endapo serikali itatekeleza au kutoa baraka kwa Tanesco kufanya kitu ambacho wanajua hawapaswi kufanya basi patakuwa hapakaliki. Hadi hivi sasa kundi kubwa la wabunge waliosimama upande wa ripoti ya Kamati Teule kuhusu Richmond, limeshajipanga tayari kuanzisha "kasheshe" jingine ambalo linaweza kabisa kuitikisa serikali.

Hata hivyo, Dr. Idris inaonekana bado amekuwa na 'kichwa ngumu' hasa baada ya serikali na kamati za Bunge zote kuiachia uamuzi wa mwisho kuhusu suala la mitambo. Hata hivyo, kuna imani kuwa alichofanyiwa Dr. Idris ni kupewa kisu ashike, tatizo ni kuwa amepewa upande wa makali huku mpingi ukiwa umeshikwa na wengine ambao wako tayari kuuvuta.

Kutokana na hili, kuna kila dalili Dr. Idris anaweza kutangaza kujiuzulu wadhifa huo kitu ambacho alijaribu kukifanya muda si mrefu uliopita kuhusiana na suala la kampuni ya saruji ya huko Tanga. "Hayuko tayari kujitundika mwenyewe kitanzini kwa kamba yake mwenyewe!" amedokeza mmoja wa watu wanaojua suala hilo.

Sasa hivi kinachosubiriwa ni muda tu kuona Dr. Idris atafanya nini huku akijua kuwa tayari anahusishwa na kashfa ya rada suala ambalo nalo hajalitolea maelezo yoyote. Hadi hivi sasa uchunguzi wetu unaonesha kuwa asilimia 90 ya uamuzi uliofikiwa hadi sasa ni kutoendelea na suala la Dowans.

Hata hivyo upande mwingine bado unadokeza kuwa endapo serikali haitanunua mitambo ya Dowans na hivyo kuwasababishia hasara "wawekezaji" hao ambao walikuwa na uhakika kuwa serikali itanunua mitambo hiyo basi Watanzania "watakiona" kwani upungufu mkubwa wa umeme ambao tulidokeza unakuja mwezi wa nne, utaifanya serikali iipigie magoti Dowans na hata kununua majenereta yale yale katika bei ya juu!!

"Watanzania hawawezi kuvumilia kukaa gizani muda mrefu hasa huku mjini, kwa hiyo usishangae hao hao wanaopinga sasa wakaja baadaye kutaka serikali inunue mitambo hiyo aidha kutoka kwa dowans au kwa mtu atakayekuw ameinunua" alisema mdokezaji huyo.

Uwezekano wa kutokea yote mawili ni mkubwa zaidi. Hata hivyo, kama dhamira ya kuwalipa Dowans kwa gharama yoyote itatekelezwa basi kuna dalili Dr. Idris na timu yake watacheza bahati nasibu na kuendelea na mradi huo wakijua kuwa huko Bungeni tayari wana kura za kutosha kuzuia mapigo ya kina "mwakyembe".
 
Kibaya alichokifanya MWAKYEMBE ni kipi? Huo MSIMAMO wenu ndio tusiotaka kusikia kabisa. Sasa ZITO sio swala la msimamo, ni SWALA la KITU KIDOGO TU, hakuna cha msimamo wala nini, kala/kaahidiwa hela ya ukuwadi, basi ndio anayoendelea nayo. Mwisho wake ndio huo. Alipewa ushauri toka mapema, rudisha hela ya mafisadi bado tunakutaka, yeye akaja na matusi hapa. Anyway si haba, nasikia kala fungu la kutosha. >10%

Tatizo ni kuwa kwa kuwa wewe unajiona ni rahisi kununulika basi kila mtu yuko kama wewe. Wenzako wengi wanadiscuss issue lakini wewe kwa kuwa kwako rushwa ni sehemu ya maisha basi kila mtu anafanya maamuzi kwa msukumo wa rushwa.

Hata hivyo sishangai sana maana hali hii ya kutokuaminiana ni zao la MFUMO FISADI ulioanza tangia 1977 kwa kuanzishwa hili zimwi linaloitwa CCM na kubarikiwa rasmi na AZIMIO LA ZANZIBAR....

omarilyas
 
Kwa karibu masaa sita ka nzi kalikuwa kametulia kwenye ukumbi makao makuu ya Tanesco ambapo Mkurugenzi wa Shirika hilo Dr. Idris Rashid alikuwa aje kuzungumza na waandishi hususan suala kununua majenereta ya kufulia umeme ambayo yanamilikiwa na kampuni yenye utata wa umiliki wake na yenye kuhusishwa na kampuni ya kifisadi ya Richmond, Dowans.

Hata hivyo, muda si mrefu uliopita mtumishi wa Tanesco aliingia ukumbini na kuwaambia waandishi waliokuwa wanasubiri kwa muda mrefu kuwa Bw. Idris hatozungumzia nao na kuwaomba radhi.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vyenye uwezo wa kupenya kuta na madari vinadokeza kuwa suala la Dowans limefikia mahali pagumu ambapo sasa Tanesco wako tayari kuachana na wazo hili ili kutafuta vyanzo vingine vya umeme wa dharura na ya kuwa wametilia maanani "kelele" za wadau mbalimbali. Hili linakuja baada ya sauti za Spika wa Bunge la Muungano Mhe. Samuel Sitta na Mbunge wa Kyela Mhe. Harrison Mwakyembe kupaza sauti zao kupinga mpango huo. Ujumbe ambao umepokelewa toka kwa watunga sheria hao ni kuwa yeyote atakayenunua majenereta ya Dowans ajiandae kuwajibika Dodoma kama walivyowajibishwa wengine!

Tishio hilo ambalo limepokelewa kwa hisia ya kunyong'onyea limetuma ujumbe ulio wazi kuwa endapo serikali itatekeleza au kutoa baraka kwa Tanesco kufanya kitu ambacho wanajua hawapaswi kufanya basi patakuwa hapakaliki. Hadi hivi sasa kundi kubwa la wabunge waliosimama upande wa ripoti ya Kamati Teule kuhusu Richmond, limeshajipanga tayari kuanzisha "kasheshe" jingine ambalo linaweza kabisa kuitikisa serikali.

Hata hivyo, Dr. Idris inaonekana bado amekuwa na 'kichwa ngumu' hasa baada ya serikali na kamati za Bunge zote kuiachia uamuzi wa mwisho kuhusu suala la mitambo. Hata hivyo, kuna imani kuwa alichofanyiwa Dr. Idris ni kupewa kisu ashike, tatizo ni kuwa amepewa upande wa makali huku mpingi ukiwa umeshikwa na wengine ambao wako tayari kuuvuta.

Kutokana na hili, kuna kila dalili Dr. Idris anaweza kutangaza kujiuzulu wadhifa huo kitu ambacho alijaribu kukifanya muda si mrefu uliopita kuhusiana na suala la kampuni ya saruji ya huko Tanga. "Hayuko tayari kujitundika mwenyewe kitanzini kwa kamba yake mwenyewe!" amedokeza mmoja wa watu wanaojua suala hilo.

Sasa hivi kinachosubiriwa ni muda tu kuona Dr. Idris atafanya nini huku akijua kuwa tayari anahusishwa na kashfa ya rada suala ambalo nalo hajalitolea maelezo yoyote. Hadi hivi sasa uchunguzi wetu unaonesha kuwa asilimia 90 ya uamuzi uliofikiwa hadi sasa ni kutoendelea na suala la Dowans.

Hata hivyo upande mwingine bado unadokeza kuwa endapo serikali haitanunua mitambo ya Dowans na hivyo kuwasababishia hasara "wawekezaji" hao ambao walikuwa na uhakika kuwa serikali itanunua mitambo hiyo basi Watanzania "watakiona" kwani upungufu mkubwa wa umeme ambao tulidokeza unakuja mwezi wa nne, utaifanya serikali iipigie magoti Dowans na hata kununua majenereta yale yale katika bei ya juu!!

"Watanzania hawawezi kuvumilia kukaa gizani muda mrefu hasa huku mjini, kwa hiyo usishangae hao hao wanaopinga sasa wakaja baadaye kutaka serikali inunue mitambo hiyo aidha kutoka kwa dowans au kwa mtu atakayekuw ameinunua" alisema mdokezaji huyo.

Uwezekano wa kutokea yote mawili ni mkubwa zaidi.


Giza nini wakati Watanzania walikua radhi kula majani ili ndege ya RAIS inunuliwe. Acha tukae Giza hapana matata.
 
duuuh,....Bangusilo Zitto?! katika hili, Namkumbuka Mh. Mzee Warioba na Meremeta.

Au yawezekana Mh. Zitto na kambi yake walikuwa kwenye subotage mission?... not a foggiest.......!!!
 
Tatizo ni kuwa kwa kuwa wewe unajiona ni rahisi kununulika basi kila mtu yuko kama wewe. Wenzako wengi wanadiscuss issue lakini wewe kwa kuwa kwako rushwa ni sehemu ya maisha basi kila mtu anafanya maamuzi kwa msukumo wa rushwa.

Hata hivyo sishangai sana maana hali hii ya kutokuaminiana ni zao la MFUMO FISADI ulioanza tangia 1977 kwa kuanzishwa hili zimwi linaloitwa CCM na kubarikiwa rasmi na AZIMIO LA ZANZIBAR....

omarilyas


UKiniaminisha kwa matendo na maneno, nitakuamini, Hivi kuaminika ni kusema tu niamini basi utaaminika?. Maneno na matendo ndio yanakufanya uaminike vinginevyo atakuamini nani ndugu yangu.?
 
Nadhani hawezi kujiuzulu, kwani akifanya hivyo atakuwa amejiexpose, au tuseme atakuwa hana kinga kuhusu tuhume nyingine za ufisadi zinazomkabili -- hasa katika dili ya radar. SFO wameshasema kuwa wanao ushahidi tosha wa kumpandisha kizimbani Dr Idris na Bwana wa Vijisenti kutokana kupokea kwao mlungula katika dili hiyo.

Akijiuzulu ubosi wa Tanesco, atakamatia wapi? Si unajua kulindana ndani ya utawala wa CCM? Afadhali Vijisenti kwani ingawa yeye alijiuzulu uwaziri, lakini bado ni Mbunge, NEC na nyadghifa nyingine.
 
Unataka chanzo kwa Takwimu zipi?

Maana kuna takwimu za Idrisa, za Mawaziri na Takwimu halisia , kwani zilizopo sasa zinzonyesha kuwa wanaotumia umeme ni asilimia 12 tuu ya watanzania .

Hiii 12% ni kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mkukuta.


Napenda kujua mahitaji ya umeme nchini (tunahitaji megawatts ngapi kwa siku- matumizi yote kwa ujumla, majumbani, viwandani na maofisini).

Na kiasi gani cha umeme (megawatts) kinachozalishwa ni ngapi kwa ujumla? Na kiasi hicho kinakidhi asilimia ngapi ya mahitaji ya nchi?

Kama unazo zote sio mbaya (yaani takwimu ya Idris, Mawaziri na hata halisia).

Natanguliza shukrani.
 
Kama uwezekana kwa yote mawili ni mkubwa basi ngoma droo ,ila kununua itakuwa ni ufisadi tu wa 10% kwa aliewazidi kete wenziwe.
Sultani CCM na wafuasi wake wanatafuta njia ya kutokea maana nchi imeshawashinda feza waliyoiba si kidogo ,na kuirudisha ni mbinde ,sijui hali ya mitambo ya kusukumia maji ikoje ?

Kikwete jiuzulu baba usishindane na nguvu za mageuzi hutaziweza kabisa mageuzi yanaikabili Tanzania kwa bei yeyote ile bora ujikate na mapema kabla hujaaibika ,unafahamu fika matatizo ambayo yanamfika aliedhulumu ukaaji wa Sultani CCM kwenye madaraka umetokana na wizi hivyo hautazidisha lolote kwa Mtanzania isipokuwa hasara tu ,kama ilivyokuwa pesa ya wizi haidumu muda mrefu na inakuwa haina faida ndivyo hivyo hivyo kuwa kiongozi ndani ya utawala wa Sultani CCM unakuwa hauna faida ni kujitafutia matatizo hapo baadae ,tunamuona Mkapa hana raha anajikurupusha kila sehemu angalau aonekane hana wasiwasi lakini kusema kweli yupo kwenye mashaka makubwa maana madai ya wananchi wanamhitaji kujibu tuhuma za kuigeuza Ikulu soko huria..
 
Mwiba , neno Sultan inaonyesha limekukaa sana yakhe, ila njoo kaweke vizuri kuhusu gazeti lako la alasiri kufutika.
 
Sasa hivi Zitto kazama kisiasa na kimaadili vile vile. Zitto hawezi kuandikwa vizuri kwenye RAI ya sasa na bado ukaamini kuwa ni Zitto yule yule. Hivi rai ilinunuliwa na nani vile? Sasa nilipoona tu positive news za Zitto ndani ya RAI nikajua kumekucha. Inawezekana CHADEMA bado wanaangalia upepo. Lakini naibu katibu mkuu wa CHADEMA akiandikwa vizuri kwenye RAI hatuhitaji kuuliza maswali mengi. RAI si Tanzania Daima na kwa siku za nyuma tulikuwa tukiona. Tusubiri kuona makala za Mbowe tena kwenye rai? Let's wait and see...... Pengine ni mawazo tu!
 
Napenda kujua mahitaji ya umeme nchini (tunahitaji megawatts ngapi kwa siku- matumizi yote kwa ujumla, majumbani, viwandani na maofisini).

Na kiasi gani cha umeme (megawatts) kinachozalishwa ni ngapi kwa ujumla? Na kiasi hicho kinakidhi asilimia ngapi ya mahitaji ya nchi?

Kama unazo zote sio mbaya (yaani takwimu ya Idris, Mawaziri na hata halisia).

Natanguliza shukrani.

Itanichukua muda kidogo kupekua sehesehemu hapa , ntajitahidi kuweka
 
Mwiba , neno Sultan inaonyesha limekukaa sana yakhe, ila njoo kaweke vizuri kuhusu gazeti lako la alasiri kufutika.

Unajua nimepata nibu kama tatu hivi,sasa hakuna sababu yeyote ile ambayo CCM haiwezi kuwa Sultani wa Tanzania, kila sifa ambazo unazijua wewe ambazo Sultani au Masultani wanakuwa nazo basi CCM anayo.

Na kwa muda huu tuliokuwa nao hana jina jingine linalowafaa ,na masultani wanaondoshwa kwa mtutu na inavyoelekea tuendako hakuna ishara njema ,wafuasi wa Sultani huyu kila wanavyoambiwa hawasikii wao ndio wao ,viongozi ndio wao,majambazi ndio wao mapolisi ndio wao mahakimu ndio wao ,majeshi ndio ,wengine tumebaki kushangilia kama tunaoshangilia mwendawazimu.
 
Napenda kujua mahitaji ya umeme nchini (tunahitaji megawatts ngapi kwa siku- matumizi yote kwa ujumla, majumbani, viwandani na maofisini).

Na kiasi gani cha umeme (megawatts) kinachozalishwa ni ngapi kwa ujumla? Na kiasi hicho kinakidhi asilimia ngapi ya mahitaji ya nchi?

Kama unazo zote sio mbaya (yaani takwimu ya Idris, Mawaziri na hata halisia).

Natanguliza shukrani.

si ufanye utafiti, taarifa zote hizo ziko kwenye mtandao. Mahali pa kuanzia ni Tanesco.com sidhani kama hili ni gumu hadi umuombe mtu mwingine.
 
hivi kwanini watendaji wasiaminiwe? mpaka Bunge ndio liamue? to me bunge is just a bunch of political ****** who wants to be re-elected. Can you guys imagine when other countries have long done away with power rations, and these countries are a way poor than us?Maswala ya utendaji tunaleta siasa, sasa spika amekuwa na uwezo kuliko rais? JK you are too soft.
 
si ufanye utafiti, taarifa zote hizo ziko kwenye mtandao. Mahali pa kuanzia ni Tanesco.com sidhani kama hili ni gumu hadi umuombe mtu mwingine.


Wewe kama huwezi tulia tu kama unanyolewa. Hebu acha kunidanganya kwamba maswali niliyouliza yanajibika na data za mtandaoni.

Mpaka Kieleweke kanielewa na ataenda kupekuapekua na kunipatia takwimu zote kuanzia za Idris, za Mawaziri na zile halisia.
 
Mama,
Nimeitoa hii kule Tanesco nadhani inaweza kusaidia pamoja na kwamba mahitaji yetu yanaweza kabisa kuwa mara mbili ya kiwango kilichoelezewa..

TANESCO's generation system consists of hydro, thermal and gas. Hydro contributes the lion's share of TANESCO's power generation. The total generation from TANESCO own sources in 2003 was 2,662,027,682 kWh out of which 2,551,416,842 is from hydro power stations.

TANESCO operates an interconnected grid system comprising of hydropower generating stations. The installed capacity are: Kidatu 204 MW; Kihansi 180 MW; Mtera 80 MW; Pangani 68 MW; Hale 21 MW; and Nyumba ya Mungu 8 MW totaling to 561 MW of hydro generation.

There are several diesel generating stations connected to the national grid in Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Dodoma, Musoma and Mbeya. These have installed capacity of 80 MW but they effectively contribute about 35 MW due to running problems. Some regions, districts and townships are dependent on isolated diesel – run generators (Kigoma, Mtwara, Lindi, Njombe, Mafia, Mpanda, Tunduru, Songea, Liwale, Ikwiriri, Masasi and Kilwa Masoko). These have installed capacity of 31 MW but they effectively contribute about 15 MW due to aged machinery and lack of spare parts.

Two private independent power projects (IPP's) which are connected to TANESCO grid are IPTL (Independent Power Tanzania Ltd) with 100 MW installed capacity and SONGAS (Songo Songo gas – to electricity project) which by the end of 2004 had 120 MW capacity although more gas turbines will be installed to increase the capacity to 200 MW before the end of year 2005. TANESCO also imports 10 MW of electric power for Kagera Region from Masaka substation in Uganda while Sumbawanga, Tunduma and Mbozi districts receive about 3 MW from neighbouring Zambia. Bulk supply of electricity is made to Zanzibar from Ras Kilomoni substation at the Indian Ocean coast in Dar es Salaam.
 
Back
Top Bottom