Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,580
- 23,914
Kibaya alichokifanya MWAKYEMBE ni kipi? Huo MSIMAMO wenu ndio tusiotaka kusikia kabisa. Sasa ZITO sio swala la msimamo, ni SWALA la KITU KIDOGO TU, hakuna cha msimamo wala nini, kala/kaahidiwa hela ya ukuwadi, basi ndio anayoendelea nayo. Mwisho wake ndio huo. Alipewa ushauri toka mapema, rudisha hela ya mafisadi bado tunakutaka, yeye akaja na matusi hapa. Anyway si hapa nasikia kala fungu la kutosha. >10%
Punguza jazba ndugu yangu - the world is full of surprises and Tanzania tops the list !! Do not rule out anything. Kuna watu wamebobea katika usanii - yes, ndiyo jadi yao. Inawezekana Zitto amechukua msimamo ambao wengi hawakuutegemea, lakini hebu jiulize jambo moja. Kweli katika wakati huu ambao watu wamekuwa na mwamko mkubwa kama huu, Zitto, of all the people, atakuwa mjinga kiasi gani kujimaliza kirahisi hivyo ? Mnachosema ni kuwa Zitto amenunuliwa - na nani ? Kweli jibu linaweza kuwa rahisi namna hiyo ?
Wengi tunamlaumu lakini nachelea kusema tusitoe hukumu ya haraka haraka. Kuna wanaoshabikia hili kwa kuwa Zitto, kwa matendo na matamshi yake, amekuwa kero kubwa kwao - wengi wa hawa sasa hivi wanajichana na kujipongeza na kutupa maneno ya kejeli. Kwa nini tusiwaangalie hawa ambao kuanguka kwa Zitto kutawapa ahueni ni akina nani hasa ? Je ni wenzetu wale wale tulio nao vitani kupinga ufisadi au mafisadi wenyewe kwa kupata angalu mwanya wa kupumua kwa kuwa mawe sasa yanaelekezwa kwa Zitto.
Simtetei Zitto mpaka sasa lakini siko tayari kumhukumu. Niliwahi kusema katika hii vita dhidi ya hawa wezi na wahujumu uchumi, kila aina ya silaha itatumika. Wenzetu wamejitayarisha miaka mingi kulinda matumbo yao na tukilegeza kibano tu wataweza kujipanga tena upya. Hii ni lifetime opportunity ya kuiumbua mzimu wa Richmond na shemeji yake Dowans. Mwakyembe aliyewasilisha ripoti nusu nusu kuinusuru serikali, bila shaka atapata nafasi ya kufunua aliloficha kwa sababu safari hii hana tena namna ya kukwepa - daggers are drawn, twende kazini.