Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Sitetei Dowans maana hata kuwajua siwajui. Sijui kuanzia mmiliki mpaka hata mlinzi wa Dowans.

Nataka Umeme. Sitaki uchumi utetereke tena kwa kukosa umeme. Tunaumia kwenye Utalii, Pamba na Maua hivi sasa. Makampuni makubwa yameanza kupunguza wafanyakazi na hata kwenye sekta madini. Mwezi Januari, circuit breaker iliharibika pale Kidatu na kusababisha mgawo. Circuit breaker tu - kisa hatuna reserve ya umeme bali tuna nakisi ya 150MW.

Madhara ya kukosa umeme ni makubwa mno na ndio yananitisha na hasa kwenye sekta ya viwanda (manufacturing) ambayo ndio pekee imebakia kutoumizwa na economic meltdown. Tunaposema giza watu wanafikiri ni giza la nyumbani. Hapana industrial production etc.

Ninapoyaona haya na sioni leadership being provided, ni bora umaarufu wangu ufutike wote lakini nchi yangu ibaki imara. Its a risk worth taking and i will triumph.

Mh. Zitto kwa hiyo kama unataka kusolve deficit ya 150MW, kwa nini usiseme tukanunue 200MW from GE with warranty and guarantees for a number of yrs at a cost of less than 100million??

Why do U want to buy defective generators from Dowans @ a cost of $60million + $20million debt they owe to Tanesco with no guarantee and warranty??

If X - Y = 0

Je utakuwa mbali na ukweli tukisema X = Y

Sasa kama Dowans ni richmond na richmond imegundulika kuwa ni matapeli na majambazi, tutakuwa mbali na ukweli tukisema Dowans nao ni majambazi.
 
Kuhusu hili mimi nimenawa mikono, na sitacomment tena ila nitaendelea kuiombea Tanzania na Mungu akipenda tutasonga mbele tu ingawaje power ya maadui imeongezeka sababu wanatumia njia za kila namna kuwarubuni watu wapende wasipende, kwa kutumia hata mbinu chafu.

Personally sasa hivi nitaweka matumaini zaidi kwa wabunge wa CCM kama kina Mwakyembe, Seleli, Mama Kilango sababu wao wako kwenye firing lane kutoka mafisadi which them implies wanatutetea watanzania.

Hawa wapinzani nakuwa forced kuconclude kuwa ni opportunistic na walevi wa madaraka ambayo hata hawajayapata.

Upinzani wakweli utatoka CCM, kwa hiyo hata kama nafanya makosa kwenye hii conclusion potelea mbali, nitajua mbele kwa mbele, maana hawa wapinzani nimegundua kuwa wana misimamo yao wenyewe na hawatusikilizi sisi wananchi.

Kama wajanja wa humu JF tunaburuzwa hivi, wale ndugu zangu kule milimani si watatukanwa mchana kweupe.

Mzee ES naomba mkuu ufikishe ujumbe huko kwa hao wana CCM kina Mwakyembe, Mama Kilango na wengine kuwa sasa tutabase support zaidi kwao na mategemeo yetu yako kwao sababu wakitutupa na wao tutakuwa hatuna pa kwenda.

May God Almighty Bless Tanzania.

We had them all in parliament and EALA since 2000 and 2001 and what did they do before we started to raise corruption issues? Au ufisadi umeanza 2005? Tunadanganyana sana katika siasa za Tanzania.

CCM can never fight corruption as all CCM MPs came to parliament through corruption. All of them used KAGODA funds to be elected. We have all the facts.

We are clean and honest. Tutaimaliza vita tulioanzisha wenyewe. Those CCM MPs who support we welcome them.

Siogopi kusema ninachoamini. Nisulubiwe kwa uamuzi wangu with facts. Wala siogopi kuambiwa nimehongwa kwani sijawahi kuhongwa maishani mwangu na yeyote na wala sijawahi kuhonga.

Nitaendelea kupambana mpaka CCM isambaratike na wale wasafi watatoka CCM na kuiondoa nchi yetu katika ukiritimba wa chama kimoja ambao ndo chanzo cha vurugu zote hizi.

Wewe nyoosha mikono. Sisi tunaendelea na vita. Hili la Dowans ndio linakufanya unyooshe mikono sio? Tena spinns maana hakuna aliyesema tununue Dowans. Tumesema tununue mitambo, Dowans not Dowans tupate mitambo
 
Zitto unasema hurudi tena kugombea Ubunge jimboni kwako na badala yake unaenda kufundisha, kumbe ndo maana umekomalia basi huo ununuzi wa mitambo chakavu ya Dowans since you have nothing to loose.

Rmashauri,

Sidhani kama Zitto has "nothing to lose." I think he has, for any number of reasons.

Kwanza, kama ulivyoona, habari zime hit the headlines kwamba Zitto, katika hatua ya kushangaza, ameshabikia, amechochea mpango wa kununua mashine chakavu kinyume hata na matamko ya Waziri aliyesema kwamba wameona busara ya Kamati ya Shelukindo na wameghaili, hawatanunua mitambo ya Dowans. Across the country voters are shocked at the news stand to read that Zitto anataka sheria ibadilishwe kuwa accomodate Dowans! Imefikia kiasi mpaka wabunge wa CCM, Shelukindo na wenzake, wanamu overshadow mbunge wa upinzaji anayetetea such an unpopular effort, kuendelea kulala kitandani na Dowans, mizimwi ya Richmonduli and Lowassa and so forth and so forth.

Unpopular positions are not always unacceptable but suffice is to say the move is having a damaging, a crippling taint on Zitto's profile and legacy. So, hata kama hagombei lazima kichwa kinamuuma sasa hivi.

Zaidi ya ku undo his legacy, Zitto akiondoka na sifa mbaya, hataweza kupata mavuno ya kile alichopanda ndani ya CCM. Zitto alijijengea uzito kwa wazito wa CCM alipoanza kuingizwa kwenye Tume za Rais na kuanza kupendwa pendwa na kukumbatiwa na the powers that be. Na angependa ku maintain hiyo status serikalini, ili, kama hakuna sababu nyingine, aendelee kuwa potential candidate wa kazi kama hizi za serikali. Sasa akiondoka with any cloud on his integrity or tremendous unpopularity hata CCM wenyewe watamuona mzigo siku za mbele. Zitto hawezi kukubali kutupa alichopanda.

But more importantly, hata kama akitoka kupractice siasa akaenda kufundisha siasa, Zitto hataweza kulala usingizi kama wapinzaji wakimrushia yeye zigo la lawama kwa kushindwa kwao kwenye uchaguzi mwaka 2010 kama kina Shelukindo na Makamba watatembea na mabango yanasema "TUMEPIGANA NA WAPINZANI WALIOTAKA KUBADILISHA SHERIA KUWARUDISHA MAFISADI WA RICHMOND KAZINI". Zitto hawezi lala, ataandika kitabu nani atasoma, atafundisha siasa, mtoto wa nani atakuja darasani? AfanjeJe, akauze njugu?

Ndio maana unamwona leo jamvini anahaha mchana kutwa kujibu tundiko la kila mwananchi. Ushawahi kumwona afanya hivyo? Damage control at its perfection. Well, bado tunaangalia kama atafanikiwa kumrudisha huyu panya wa Richmond kwenye gunia alikomtoa.
 
Sitetei Dowans maana hata kuwajua siwajui. Sijui kuanzia mmiliki mpaka hata mlinzi wa Dowans.

Nataka Umeme. Sitaki uchumi utetereke tena kwa kukosa umeme. Tunaumia kwenye Utalii, Pamba na Maua hivi sasa. Makampuni makubwa yameanza kupunguza wafanyakazi na hata kwenye sekta madini. Mwezi Januari, circuit breaker iliharibika pale Kidatu na kusababisha mgawo. Circuit breaker tu - kisa hatuna reserve ya umeme bali tuna nakisi ya 150MW.

Madhara ya kukosa umeme ni makubwa mno na ndio yananitisha na hasa kwenye sekta ya viwanda (manufacturing) ambayo ndio pekee imebakia kutoumizwa na economic meltdown. Tunaposema giza watu wanafikiri ni giza la nyumbani. Hapana industrial production etc.

Ninapoyaona haya na sioni leadership being provided, ni bora umaarufu wangu ufutike wote lakini nchi yangu ibaki imara. Its a risk worth taking and i will triumph.


Hakuna haja ya kununua hizo scraper za dowans tunataka mpya, Kama ni utalii nchi zote zina financial crisis usitegemee mtalii toka kwao kuja kutumbua Tanzania wakati huo hategemei kesho atapata pesa zingine za kuishi, Pia Pamba, ningekuona una matinki kama ungesema pamba tunayozalisha watengeneze nguo na kuexport kuliko sasa hivi pamba inapelekwa nzima nzima nje ya nchi na kununua nguo kwa bei ya juu, kuna viwanda vya nguo hapo Mwanza/ Musoma/Morogoro/Dar wangehamasisha watu kuwekeza kwa kulist shares kwenye stock, tungenunua share nyingi tu na kutengeneza mtaji wa kuwezesha hivyo viwanda kutengeza nguo hapo hapo Tanzania.
 
Viwanda gani hivyo? na kama that is the case kwa nini msiopt kununua mitambo mipya mmeng'ang'ania hayo mamitambo ya Dowans?

Hiyo hasara itakayosababishwa na kukosekana kwa umeme italingana na gharama ya kununua, kugharamia maintanance ya mitambo mikuu kuu? And what if hiyo mitambo ikafa baada ya mwaka mmoja, mtakuwa na garantee ya aina yeyote?

Kuweni cost effective!

Mama nani kakulisha kasa kuwa tunataka mitambo ya Dowans? Nani? Inasikitisha sana kuwa husomi ninachoandika. Nani kakulisha kasa kuwa sisi tunataka Dowans? Tunakata Mitambo.
 
We had them all in parliament and EALA since 2000 and 2001 and what did they do before we started to raise corruption issues? Au ufisadi umeanza 2005? Tunadanganyana sana katika siasa za Tanzania.

CCM can never fight corruption as all CCM MPs came to parliament through corruption. All of them used KAGODA funds to be elected. We have all the facts.

We are clean and honest. Tutaimaliza vita tulioanzisha wenyewe. Those CCM MPs who support we welcome them.

Siogopi kusema ninachoamini. Nisulubiwe kwa uamuzi wangu with facts. Wala siogopi kuambiwa nimehongwa kwani sijawahi kuhongwa maishani mwangu na yeyote na wala sijawahi kuhonga.

Nitaendelea kupambana mpaka CCM isambaratike na wale wasafi watatoka CCM na kuiondoa nchi yetu katika ukiritimba wa chama kimoja ambao ndo chanzo cha vurugu zote hizi.

Wewe nyoosha mikono. Sisi tunaendelea na vita. Hili la Dowans ndio linakufanya unyooshe mikono sio? Tena spinns maana hakuna aliyesema tununue Dowans. Tumesema tununue mitambo, Dowans not Dowans tupate mitambo

Mh. Zitto bado tunasubiri taarifa kutoka jikoni, sisi tutajua tu kinachoendelea usiwe na wasiwasi.

Kama utaendelea kutetea taifa na mungu akubariki, lakini kwenye hil umetuonyesha picha yako ambayo wengine tulikuwa hatujui.

I agree nimekuwa emotional mno kwenye hii issue sababu mimi najua kidogo mambo hayo ya dowans kwa undani na wanachojaribu kufanya, so na wewe kuwa upande wao nadhani imecloud hata judgement yangu so nadhani hapa ni kukubali tu na ninaacha rasmi hii topic (nimeshasema huko nyuma naacha rasmi, lakini hii ni final).
 
Mama nani kakulisha kasa kuwa tunataka mitambo ya Dowans? Nani? Inasikitisha sana kuwa husomi ninachoandika. Nani kakulisha kasa kuwa sisi tunataka Dowans? Tunakata Mitambo.

Heheheee Zitto, umewahi kumpigia mbuzi gitaa? Well...you're doind that now..Lol
 
Rmashauri,

Sidhani kama Zitto has "nothing to lose." I think he has, for any number of reasons.

Kwanza, kama ulivyoona, habari zime hit the headlines kwamba Zitto, katika hatua ya kushangaza ameshabikia, amechochea mpango wa kununua mashine chakavu kinyume hata na matamko ya Waziri aliyesema kwamba wameona busara ya Kamati ya Shelukindo na wamegaili, hawatanunua mitambo ya Dowans. Accros the country voters are shocked at the news stand to read that Zitto anataka sheria ibadilishwe kuwa accomodate Dowans! Imefikia kiasi mpaka wabunge wa CCM, Shelukindo na wenzake, wanamu overshadow mbunge wa upinzaji anayetetea such an unpopular effort, kuendelea kulala kitandani na Dowans, mizimwi ya Richmonduli and Lowassa and so forth and so forth.

Unpopular positions are not always unacceptable but suffice is to say the move is having a damaging, a crippling taint on Zitto's profile and legacy. So, hata kama hagombei lazima kichwa kinamuuma sasa hivi.

Zaidi ya ku undo his legacy, Zitto akiondoka na sifa mbaya, hataweza kupata mavuno ya kile alichopanda ndani ya CCM. Zitto alijijengea uzito kwa wazito wa CCM alipoanza kuingizwa kwenye Tume za Rais na kuanza kupendwa pendwa na kukumbatiwa na the powers that be. Na angependa ku maintain hiyo status serikalini, ili, kama hakuna sababu nyingine, aendelee kuwa potential candidate wa kazi kama hizi za serikali. Sasa akiondoka with any cloud on his integrity or tremendous unpopularity hata CCM wenyewe watamuona mzigo siku za mbele. Zitto hawezi kukubali kutupa alichopanda.

But more importantly, hata kama akitoka kupractice siasa leo akaenda kufundisha siasa, Zitto hataweza kulala usingizi kama wapinzaji wakimrushia yeye zigo la lawama kwa kushindwa kwao kwenye uchaguzi mwaka 2010 kama kina Shelukindo na Makamba watatembea na mabango yanasema "TUMEPIGANA NA WAPINZANI WALIOTAKA KUADILISHA SHERIA KUWARUDISHA MAFISADI WA RICHMOND KAZINI" Zitto, hawezi lala, ataandika kitabu nani atasoma, atafundisha siasa, mtoto wa nani atakuja darasani? Afanjeye, auze njugu?

Ndio maana unamwona leo jamvini anahaha mchana kutwa kujibu tundiko la kila mwananchi. Ushawahi kumwona afanya hivyo? Damage control at its perfection. Well, bado tunaangalia kama atafanikiwa kumrudisha huyu panya wa Richmond kwenye gunia alikomtoa.

Kuhani, good analysis

Lakini ninaamini ninachofanya ni sahihi. Sijutii hata kidogo kwani ninaamini nimetoa ushauri sahihi kwa TANESCO na Serikali. Its all recorded and its up to the people kuamini spinns or facts.
 
Mama nani kakulisha kasa kuwa tunataka mitambo ya Dowans? Nani? Inasikitisha sana kuwa husomi ninachoandika. Nani kakulisha kasa kuwa sisi tunataka Dowans? Tunakata Mitambo.


Oooh, okay, toka mwanzo mbona hukuuliza aliyenilisha kasa kuhusu kutaka kwenu mitambo ya Dowans? Tusingefika hapa tulipo hadi kufikia wewe kuwa denounced na wananchi humu jamvini.

Ok, ok. Kwa hiyo unakubaliana na TANESCO wanunuliwe mitambo mipya sio.
Okay, sawa, umeweka sawa kauli yako, na msimamo wako umebadilisha, hutasimama peke yako tena.
 
Oooh, okay, toka mwanzo mbona hukuuliza aliyenilisha kasa kuhusu kutaka kwenu mitambo ya Dowans? Tusingefika hapa tulipo hadi kufikia wewe kuwa denounced na wananchi humu jamvini.

Ok, ok. Kwa hiyo unakubaliana na TANESCO wanunuliwe mitambo mipya sio.
Okay, sawa, umeweka sawa kauli yako, na msimamo wako umebadilisha, hutasimama peke yako tena.

Usinilishe maneno. Sijabadili msimamo katika suala hili hata nchi moja, Nimepata mawazo mengi na mazuri lakini msimamo wangu ni ule ambao nimeandika humu ndani toka nianze kushiriki mjadala huu. Soma upya post zangu uniambie sehemu ambayo nimesema Lazima tununue mitambo ya Dowans.

Naomba usinilishe maneno. Msimamo wangu ni ule ule. Msimamo wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwamba kuna umuhimu wa kununua mitambo ili kuepusha Taifa na mgawo wa umeme na pia kupunguza mzigo wa TANESCO kununua umeme kutoka kwa wawekezaji.

Nipo tayari kusimama peke yangu katika ninachoamini
 
Mama nani kakulisha kasa kuwa tunataka mitambo ya Dowans? Nani? Inasikitisha sana kuwa husomi ninachoandika. Nani kakulisha kasa kuwa sisi tunataka Dowans? Tunakata Mitambo.

Good, Kama tunataka mitambo sheria zipo za manunuzi ya vitu kama mitambo. Na sheria haisemi tununue mitambo kuu kuu. Inachukua muda gani kuagiza mitambo mipya hadi kuifunga na kuanza kuzalisha kabla ya 'mgawo wa mwazi wa nne'?
 
Usinilishe maneno. Sijabadili msimamo katika suala hili hata nchi moja, Nimepata mawazo mengi na mazuri lakini msimamo wangu ni ule ambao nimeandika humu ndani toka nianze kushiriki mjadala huu. Soma upya post zangu uniambie sehemu ambayo nimesema Lazima tununue mitambo ya Dowans.

Naomba usinilishe maneno. Msimamo wangu ni ule ule. Msimamo wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwamba kuna umuhimu wa kununua mitambo ili kuepusha Taifa na mgawo wa umeme na pia kupunguza mzigo wa TANESCO kununua umeme kutoka kwa wawekezaji.

Nipo tayari kusimama peke yangu katika ninachoamini

Mh. Zitto kama huo ndio msimamo wako unataka kukutana na kamati ya Shelukindo ya nini??? Si ulisema unataka kukutana nayo ili kamati mbili ziwe na msimamo mmoja na zisiwe kwenye conflict right?? Kamati ya Shelukindo msimamo wake ulikuwa ni NO DOWANS, kwa hiyo common sense tu inasema kamati ya Zitto ilikuwa na mawazo opposite ya Kamati ya shelukindo, si ndio Mh. Zitto??? Sasa OPPOSITE YA NO DOWANS si ni YES DOWANS Mh????Kwa ufupi tu kuanzia Spika, Magogoni, mpaka wabunge wengi wanashangaa yaliyokusibu ni yapi mpaka kutaka kuforce mambo, lakini in few days tutazinyaka tu info zitakazopelekwa magogoni kutoka huko kwa kina Othman na itatusaidia wengine kujua hasa movie hii iko vipi.
 
Usinilishe maneno. Sijabadili msimamo katika suala hili hata nchi moja, Nimepata mawazo mengi na mazuri lakini msimamo wangu ni ule ambao nimeandika humu ndani toka nianze kushiriki mjadala huu. Soma upya post zangu uniambie sehemu ambayo nimesema Lazima tununue mitambo ya Dowans.

Naomba usinilishe maneno. Msimamo wangu ni ule ule. Msimamo wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwamba kuna umuhimu wa kununua mitambo ili kuepusha Taifa na mgawo wa umeme na pia kupunguza mzigo wa TANESCO kununua umeme kutoka kwa wawekezaji.

Nipo tayari kusimama peke yangu katika ninachoamini

......Majuzi nilimsikia Dr. Mwakyembe akizungumza katika TBC kuwa Tanesco wasinunue mitambo ya Dowans. Hoja yake kuu ni kuwa wakinunua mitambo ya Dowans watakuwa wamekiuka taratibu za ununuzi. Hakutoa sababu nyingine yeyote ya kiuchumi.

Leo nimeskiliza Mh. Zitto Kabwe katika TBC hiyo hiyo. Yeye ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo kwa sababu kuu tano za kiuchumi na kiutendaji:-

1. Mitambo hiyo ipo nchini na inazalisha umeme bila matatizo. Pia moja ya mtambo huo ni mpya kabisa.
2. Tanesco inaendeshwa kwa hasara kutokana na high capacity charges. Zaidi ya 80% ya mapato yake hutumika kununulia umeme toka kwa wazalishaji binafsi unaofikia 42% tu ya umeme wote unao gawiwa.
3. Hivi sasa Tanesco inaendeshwa kwa hasara. Ununuzi wa mitambo hiyo pamoja na mingine ya IPTL etc utaisadia Tanesco kuendeshwa kwa faida. Serikali/Tanesco imo katika mazungumzo na wazalishaji wote hao binafsi. Kwa hiyo, inaonyesha kuwa, zoezi hilo si la Dowans peke yake bali ndio sera ya serikali/Taneso hivi sasa.
4. Mitambo hiyo ikinunuliwa sasa itaepusha sokomoko la mgao wa umume baadae mwaka huu.
5. Katika sheria za manunuzi kuna kipengele cha waiver ikiwa kuna umuhimu wa kununua mitambo ambayo si mipya.

Pitia tena hii thread kama utapenda na una muda, soma news outlets nyingine na pia recall kauli zako kuhusu suala la hili ndipo useme kwamba nimekulisha maneno kwamba mnataka nunua mitambo ya Dowans. Mfano huu.


Mengi yamesemwa, nayaunga mkono.

Kila lenye heri nisije nambiwa chuki binafsi bure kwani sikio la kufa hilo...
 
Mambo yamenavyokwenda katika issue ya DOWNS hatumuamini mtu sasa hivi. wanaliosababishia wasiwasi wa kutomwamini mtu bila shaka unawajua. wanatoa kauli tata kila wakati.

Mimi binafsi swali lenye uuhimu mkubwa ni deni wanalodaiwa Richmond/Dowans na TANESCO/Serkali la shilingi 23 bilioni. Je watalilipa lini? Je, kuna riba ambayo serikali/TANESCO watapata kutokana na deni hilo kubwa? Kama Dowans watashindwa kulilipa je, kuna uwezekano wa Serikali/TANESCO kuichukua mitambo yao kama fidia ya deni hilo kubwa. Thanks Mkjj kwa kazi nzuri unazozifanya.
 
Mwanakijiji,

Hayo mahojiano yatawekwa hapa au kwenye website ya Cheche?

Asante,
 
Mkjj nakushukuru sana kwa michango yako mingi ambayo kwa kweli unasaidia sana. Lakini naomba na naomba sana uwe mwangalifu maana hata mimi naisubiri hayo mahojiano lakini ukiangalia kwa undani kuna haja kweli ya kujali ngeleja kasema nini??

Si kila mtu anajua huyu anavutia upande wa magodfather zake?? toka mwanzo wizara hii, ya fedha, mambo ya ndani ilikuwa lazima wawepo vijana wa magodfather, so utaona alipotolewa masha baada ya Richmond alipelekwa mambo ya ndani kumake sure 200billion zielekee kwa magodfather. So Ngeleja akavutwa minerals ili afundishwe na partner wao kule bandarini ambaye alipewa uwaziri.

Mramba alitolewa Miundombinu akawekwa senior partner vijisenti mpaka alipoharibu ndio mkuu wa kaya sasa kaweka mtu wa kwake na magodfather walikasirika mno kama ambavyo foreign ilivyowakasirisha.

All in all, Tanesco, Wizara na ofisi ya mwanasheria mkuu zote ziko under control ya Rostam/Lowassa angle waliyoikosa ni hizi kamati za bunge tu, lakini Mh. Zitto amewapa cover either kwa kutojua au kwa makusudi kabisa, so tusubiri tu soon tutajua kinachoendelea.
 
Tumezingatia sheria za nchi na Mahitaji ya nishati ya Umeme kwa Taifa

Maslahi gani ya taifa umesimamia?

Sheria ya manunuzi inayosimamia maslahi ya taifa ili kuzuia vitu mitumba visinunuliwe hujaisimamia utasemaje umesimamia maslahi ya taifa?

Ili taifa lipate vitu kwa bei nzuri huhitaji tenda ziitishwe kampuni nyingi zishindanishwe kwa uwazi kila kampuni ilete bids zao ndipo ujue uchague yupi mwenye maslahi kwa taifa wewe Zitto umeshupalia Dowans tu kuna nini na Dowans?

Ungesimamia maslahi ya Taifa ungezungumzia kuitisha tenda ambapo Dowans naye angetaka ange bid lakini kuishupalia Dowans tu inaonyesha una maslahi na Dowans na si Taifa.Kwa nini usishupalie tender bids ziitishwe unashupalia tu Dowans,Namini zingeitishwa Tender Bids Dowans wasinge bid kabisa wao kama Dowans maana wanajua sheria ya manunuzi inavyosema kuwa hairuhusu mitumba.Wasingekubali ku bid na kupoteza ile tender bid fee kienyeji.

Nadhani Dowans kuna wajanja wenye akili wakaona zikiitishwa tenda bids watakwama wakaona watafute watu wasio na uchungu na hela za wananchi wawatumie kama vikaragosi UCHWARA wa ku-twist mambo ili tender bids zisiitishwe ila wao wafanyiwe single sourcing. Ni bahati mbaya kuwa Zitto umenaswa kwenye huo mtego na huyo mkurugenzi wa Tanesco naye akaingia mkenge na usomi wake.Mngekuwa na uchungu kwa maslahi ya taifa wewe na huyo Idrisa mngewaambia Dowans kuwa walete bids zao na mkatangaza Tender bids za ku-supply mitambo haraka mkazisambaza kwa vyombo mbalimbali vya habari na kutoa deadline hata ya muda mfupi muone nini kingetokea kabla ya kumshupalia Dowans kama mshindi pekee.

Sijui aliwapa nini Dowans mkamhakikishia kuwa akae atulie hakuna cha Tendering process wala nini wewe na Idrisa mkajivika ujemadari wa kumkingia kifua kuhakikisha tendering process isiwepo bali uimbwe wimbo tu wa Dowans.Kwani Dowans ni nani kwenu?

Mumeshupalia Dowans wanauza mitambo wanauza mitambo.Wao si wauzaji pekee wa mitambo wauzaji wako wengi.Zito na mwenzio kwa nini hamkushupalia Tendering process mkashupalia Dowans tu kuwa ndiye mwenyewe huyo mhhhhhh Zitto Kabwe nasikia kaharufu ka ufisadi.

Kwa nini hamkupenda katenda kaitishwe na kipenzi chenu Dowans a-bid ashindane na wengine hata kama si wauza mitambo mipya basi ashindane hata na wauza mitambo mitumba wengine walioko ndani au nje ya nchi? Kwani wanaozalisha umeme kwa kutumia mitambo mitumba na kuiuzia umeme Tanesco si Dowans tu si wapo na wengine pia? Hata kama mitambo mitumba haiko hapa unajuaje kama hawana sehemu nyingine.Naamini ingetangazwa tender ya mitumba tungepata suppliers kibao tena wenye mitumba mizuri na ya kisasa zaidi na bei poa kuliko Dowans. After all nani anahitaji mitumba tungeipata kwa throw away price kama tungeitisha tender na kusema tunahitaji masharti yetu tunahitaji mitambo mitumba.

Wewe kama mbunge unashindwa hata kulinda na kutetea sheria ya manunuzi iliyotungwa na bunge lenyewe hivi kama huwezi tetea hata kilichotungwa na bunge lenyewe hivi wewe ni mbunge au afisa masoko wa Dowans?

Unasema sheria ya Manunuzi si msahafu yaweza badilishwa unajua unachosema? Mimi mpagani ninavyojua sheria ni kubwa kuliko msahafu sababu misahafu Tanzania ni kwa ajili ya kundi la watu wachache mfano Kurani si kwa ajili ya watu wote ni kwa ajili ya waislamu,na Biblia ni kwa wachache wakristo lakini sheria ni kwa ajili ya watu wote.Kimatumizi sheria ni pana zaidi kuliko misahafu ya dini.

.Huwezi tu kuibuka ukiwa umelewa ulevi wa Dowans na kuanza kuiponda sheria tu kirahisi hivyo.Wewe kama mbunge ilipaswa ujue kuwa sheria ni kitu kikubwa haitungwi siku moja na huwezi kuibadilisha kwa siku moja kuna process ndefu sana ya kutunga na kubadilisha sheria.Na taratibu za kubadilsha sheria hazifanywi na kamati yako ya bunge ya mahebu wala ya Mwakyembe ile ya madini wala na Tanesco bali hufanywa na bunge baada ya mchakato mrefu.Sasa unaposema kamati ya akina Mwakyembe wakaonane na Tanesco ili iwe nini.

Ungekuwa kweli unajali maslahi ya Taifa ungeiomba tume ya kurekebisha sheria iangalie uwezekano wa kupeleka mswada bungeni wa kubadili sheria ya manunuzi kama huridhiki nayo au ungewakilisha hoja zako bungeni ukajenga hoja zako kule.Taratibu za kubadili sheria unazijua au huzijui au umepofushwa na Dowans kiasi kuwa hukumbuki na huoni?

Na huyo mkurugenzi wa Tanesco mbumbumbu mwenzio naye anasema sheria ya manunuzi ni kikwazo anatoa kwenye press release. Msomi mzima hajui kama sheria ina utata ukitaka ibadilishwe hajui kuwa mtu anatakiwa apeleke hiyo hoja wapi? Kama anataka sheria ibadilshwe msomi yule hajui kweli pa kuanzia? Hivi press release na usomi wake ndiyo kaona njia ya maana ya kulalamikia sheria ya manunuzi? Matangazo yale pesa kibao zimetumika kuwalipia kufaidisha magazeti yakiwemo yanayomilikiwa na Rostam Azizi mtuhumiwa kwenye Richmond na Dowans.Ufisadi mwingine.Napendekeza pesa ambazo zimetumiwa na Tanesco kwa ajili ya ile press release zikatwe kwenye mshahara wa mkurugenzi mkuu wa Tanesco zirudi kwenye akaunti ya shirika.Aliyewaambia mnaanzia Dowans,Tanesco,au kwenye kamati za bunge za hesabu na madini kubadili sheria ni nani.Nashukuru Mwakyembe na kamati yake kuukataa wito wako feki wa kuwataka wakaongee na Tanesco kuhusu ununuzi wa mitambo mitumba ya Dowans kinyume na sheria ya Bunge.

Mwalimu Julius Nyerere alipokuwa Uingereza aliwahi siku moja kuulizwa ni kitu gani anakiona kigumu kama mwanasiasa akasema kitu kigumu ni kujaribu kutunga uongo na kujaribu kuufikisha kwa wananchi na kuwafanya wananchi waukubali huo uongo.Inavyoonyesha Zitto umefikia mahali pagumu pa namna hiyo.Unapata shida ya kutunga uongo na unapata shida zaidi kuufikisha uongo huo kwa wananchi.

Kumbuka siku zote kuwa kutunga uongo ni kazi kubwa na kuufanya uongo ukubalike ni kazi kubwa zaidi.Pole.

Mwisho nashauri hata kama sheria ya manunuzi itabadilishwa tukasema tunahitaji mitambo mitumba kama ya Dowans Lazima tender process ifanyike na wauza mitumba wengi wa bid.Siyo kuwa ikibadilishwa basi Dowans wapewe hapana.Lazima waingie kwenye tender.Kama wakishinda washindie kwenye tender lakini sio mezani kwenye meza ya Zitto kabwe au Idrisa Rashid mkurugenzi wa Tanesco.
 
Mkuu alikua anatest temperature huyu...maana huu msimamo wake "mpya" angeuweka bayana tangu mwanzo, im sure hii thread ingekua imekufa zamani...Kang'ang'ania kulibeba zigo la miba Dowans,...Anaona haeleweki, sasa hivi anatuchanganya kuwa hawabebi Dowans...Hivi angekua hawabebi hii fuss yote ya magazeti na hapa JF ingekuwepo?

Haiwezekani mbunge wa upinzani kushupalia manunuzi tata ya serikali, wakati ambapo wabunge wa chama chenye serikali wanaona kuna tatizo, tena la msingi....

Kunani???????.....
 
Last edited:
Hpa kuna issue Mh Zitto kaigusia

1. Tanesco wame-BID ili kununua mitambo ya Dowans

Well, sihitaji kufahamu Dowans walitangaza lini hiyo tender.........however nahitaji kujua kama kuna option za manunuzi Tanesco walifanya pia, na kama kweli walifanya....je ni akina nani walikuwa approached other than Dowans.....Mh Zitto naomba unielimishe hapo........kama ulishatoa hayo maelezo im sorry.........hapa nauliza swali huku naendelea kusoma posts zaidi......
 
Mh. Zitto.

Nimefurahishwa sana na msimamo wako na hoja zako za kisomi. Katika mjadala huu mawazo ya wengi ni Taneso wasinunue mitambo ya Dowans lakini ukiangalia hoja zinazotolewa hakuna hata moja yenye nguvu. Wachache akina sisi tunaunga mkono hoja hii kwa sababu za msingi kabisa.

Sasa hawa jamaa wasikuingize katika mambo ya kitoto kama vile issue za Hammer, kugombea ubunge na ufisadi. Hoja hizi zinaonyesha wazi kuwa wamefilisika na hoja za msingi na wanakimbilia kuleta issues za kukutibua. Lakini nafurahi kuwa umewatambua kutokana na umakini wako katika kuwajibu. Sababu ya yote hayo ni roho ya korosho.

Nakuhakikishia kuwa endapo ununuzi huu hautokamilishwa na ikabidi uwepo mgao wa nguvu huko baadae, ni hao hao wanaotoa hoja za kupinga ndio watakaokuwa msitari wa mbele kupiga kelele na kulalamika. Mark my words. Wewe waandike tu majina yao pembeni na utaamini ninayo yasema.

Nakushauri achana nao. Sisi tumekuelewa na natumai serikali itakuelewa zaidi.

kuwepo kwa mgawo wa nguvu...haimaanishi ni kwa sababu ya kutonunua mitambo ya Dowans...........inamaanisha sisi wananchi tunaendelea kufanywa WAJINGA na MABWEGE
 
Back
Top Bottom