Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

kuwepo kwa mgawo wa nguvu...haimaanishi ni kwa sababu ya kutonunua mitambo ya Dowans...........inamaanisha sisi wananchi tunaendelea kufanywa WAJINGA na MABWEGE

No, kuwapo kwa mgao kunamaanisha sisi Miafrika ni Ndivyo Tulivyo, hatuna uwezo wa kutengeneza mitambo yetu wenyewe kwani tungekuwa na uwezo huo tungekuwa tumeshalitatua hili tatizo once and for all. Remember, necessity is the mother of all (or most) inventions.
 
Kuhusu hili mimi nimenawa mikono, na sitacomment tena ila nitaendelea kuiombea Tanzania na Mungu akipenda tutasonga mbele tu ingawaje power ya maadui imeongezeka sababu wanatumia njia za kila namna kuwarubuni watu wapende wasipende, kwa kutumia hata mbinu chafu.

Personally sasa hivi nitaweka matumaini zaidi kwa wabunge wa CCM kama kina Mwakyembe, Seleli, Mama Kilango sababu wao wako kwenye firing lane kutoka mafisadi which then implies wanatutetea watanzania.

Hawa wapinzani nakuwa forced kuconclude kuwa ni opportunistic na walevi wa madaraka ambayo hata hawajayapata.

Upinzani wakweli utatoka CCM, kwa hiyo hata kama nafanya makosa kwenye hii conclusion potelea mbali, nitajua mbele kwa mbele, maana hawa wapinzani nimegundua kuwa wana misimamo yao wenyewe na hawatusikilizi sisi wananchi.

Kama wajanja wa humu JF tunaburuzwa hivi, wale ndugu zangu kule milimani si watatukanwa mchana kweupe.

Mzee ES naomba mkuu ufikishe ujumbe huko kwa hao wana CCM kina Mwakyembe, Mama Kilango na wengine kuwa sasa tutabase support zaidi kwao na mategemeo yetu yako kwao sababu wakitutupa na wao tutakuwa hatuna pa kwenda.

May God Almighty Bless Tanzania.


moelex23......ulitaka Zitto ajiuzulu kutoka kwenye kamati?!!!.......ndio maana watu walitaka sana kujua msimamo wa yeye mwenyewe Zitto ni upi...
 
...................Across the country voters are shocked at the news stand to read that Zitto anataka sheria ibadilishwe kuwa accomodate Dowans! ...............

Kuhani,

Zitto anasema, mtafutieni hiyo sheria mnayodai kuwa inakiukwa!
 
Maslahi gani ya taifa umesimamia?

Sheria ya manunuzi inayosimamia maslahi ya taifa ili kuzuia vitu mitumba visinunuliwe hujaisimamia utasemaje umesimamia maslahi ya taifa?

Ili taifa lipate vitu kwa bei nzuri huhitaji tenda ziitishwe kampuni nyingi zishindanishwe kwa uwazi kila kampuni ilete bids zao ndipo ujue uchague yupi mwenye maslahi kwa taifa wewe Zitto umeshupalia Dowans tu kuna nini na Dowans?

Ungesimamia maslahi ya Taifa ungezungumzia kuitisha tenda ambapo Dowans naye angetaka ange bid lakini kuishupalia Dowans tu inaonyesha una maslahi na Dowans na si Taifa.Kwa nini usishupalie tender bids ziitishwe unashupalia tu Dowans,Namini zingeitishwa Tender Bids Dowans wasinge bid kabisa wao kama Dowans maana wanajua sheria ya manunuzi inavyosema kuwa hairuhusu mitumba.Wasingekubali ku bid na kupoteza ile tender bid fee kienyeji.

Nadhani Dowans kuna wajanja wenye akili wakaona zikiitishwa tenda bids watakwama wakaona watafute watu wasio na uchungu na hela za wananchi wawatumie kama vikaragosi UCHWARA wa ku-twist mambo ili tender bids zisiitishwe ila wao wafanyiwe single sourcing. Ni bahati mbaya kuwa Zitto umenaswa kwenye huo mtego na huyo mkurugenzi wa Tanesco naye akaingia mkenge na usomi wake.Mngekuwa na uchungu kwa maslahi ya taifa wewe na huyo Idrisa mngewaambia Dowans kuwa walete bids zao na mkatangaza Tender bids za ku-supply mitambo haraka mkazisambaza kwa vyombo mbalimbali vya habari na kutoa deadline hata ya muda mfupi muone nini kingetokea kabla ya kumshupalia Dowans kama mshindi pekee.

Sijui aliwapa nini Dowans mkamhakikishia kuwa akae atulie hakuna cha Tendering process wala nini wewe na Idrisa mkajivika ujemadari wa kumkingia kifua kuhakikisha tendering process isiwepo bali uimbwe wimbo tu wa Dowans.Kwani Dowans ni nani kwenu?

Mumeshupalia Dowans wanauza mitambo wanauza mitambo.Wao si wauzaji pekee wa mitambo wauzaji wako wengi.Zito na mwenzio kwa nini hamkushupalia Tendering process mkashupalia Dowans tu kuwa ndiye mwenyewe huyo mhhhhhh Zitto Kabwe nasikia kaharufu ka ufisadi.

Kwa nini hamkupenda katenda kaitishwe na kipenzi chenu Dowans a-bid ashindane na wengine hata kama si wauza mitambo mipya basi ashindane hata na wauza mitambo mitumba wengine walioko ndani au nje ya nchi? Kwani wanaozalisha umeme kwa kutumia mitambo mitumba na kuiuzia umeme Tanesco si Dowans tu si wapo na wengine pia? Hata kama mitambo mitumba haiko hapa unajuaje kama hawana sehemu nyingine.Naamini ingetangazwa tender ya mitumba tungepata suppliers kibao tena wenye mitumba mizuri na ya kisasa zaidi na bei poa kuliko Dowans. After all nani anahitaji mitumba tungeipata kwa throw away price kama tungeitisha tender na kusema tunahitaji masharti yetu tunahitaji mitambo mitumba.

Wewe kama mbunge unashindwa hata kulinda na kutetea sheria ya manunuzi iliyotungwa na bunge lenyewe hivi kama huwezi tetea hata kilichotungwa na bunge lenyewe hivi wewe ni mbunge au afisa masoko wa Dowans?

Unasema sheria ya Manunuzi si msahafu yaweza badilishwa unajua unachosema? Mimi mpagani ninavyojua sheria ni kubwa kuliko msahafu sababu misahafu Tanzania ni kwa ajili ya kundi la watu wachache mfano Kurani si kwa ajili ya watu wote ni kwa ajili ya waislamu,na Biblia ni kwa wachache wakristo lakini sheria ni kwa ajili ya watu wote.Kimatumizi sheria ni pana zaidi kuliko misahafu ya dini.

.Huwezi tu kuibuka ukiwa umelewa ulevi wa Dowans na kuanza kuiponda sheria tu kirahisi hivyo.Wewe kama mbunge ilipaswa ujue kuwa sheria ni kitu kikubwa haitungwi siku moja na huwezi kuibadilisha kwa siku moja kuna process ndefu sana ya kutunga na kubadilisha sheria.Na taratibu za kubadilsha sheria hazifanywi na kamati yako ya bunge ya mahebu wala ya Mwakyembe ile ya madini wala na Tanesco bali hufanywa na bunge baada ya mchakato mrefu.Sasa unaposema kamati ya akina Mwakyembe wakaonane na Tanesco ili iwe nini.

Ungekuwa kweli unajali maslahi ya Taifa ungeiomba tume ya kurekebisha sheria iangalie uwezekano wa kupeleka mswada bungeni wa kubadili sheria ya manunuzi kama huridhiki nayo au ungewakilisha hoja zako bungeni ukajenga hoja zako kule.Taratibu za kubadili sheria unazijua au huzijui au umepofushwa na Dowans kiasi kuwa hukumbuki na huoni?

Na huyo mkurugenzi wa Tanesco mbumbumbu mwenzio naye anasema sheria ya manunuzi ni kikwazo anatoa kwenye press release. Msomi mzima hajui kama sheria ina utata ukitaka ibadilishwe hajui kuwa mtu anatakiwa apeleke hiyo hoja wapi? Kama anataka sheria ibadilshwe msomi yule hajui kweli pa kuanzia? Hivi press release na usomi wake ndiyo kaona njia ya maana ya kulalamikia sheria ya manunuzi? Matangazo yale pesa kibao zimetumika kuwalipia kufaidisha magazeti yakiwemo yanayomilikiwa na Rostam Azizi mtuhumiwa kwenye Richmond na Dowans.Ufisadi mwingine.Napendekeza pesa ambazo zimetumiwa na Tanesco kwa ajili ya ile press release zikatwe kwenye mshahara wa mkurugenzi mkuu wa Tanesco zirudi kwenye akaunti ya shirika.Aliyewaambia mnaanzia Dowans,Tanesco,au kwenye kamati za bunge za hesabu na madini kubadili sheria ni nani.Nashukuru Mwakyembe na kamati yake kuukataa wito wako feki wa kuwataka wakaongee na Tanesco kuhusu ununuzi wa mitambo mitumba ya Dowans kinyume na sheria ya Bunge.

Mwalimu Julius Nyerere alipokuwa Uingereza aliwahi siku moja kuulizwa ni kitu gani anakiona kigumu kama mwanasiasa akasema kitu kigumu ni kujaribu kutunga uongo na kujaribu kuufikisha kwa wananchi na kuwafanya wananchi waukubali huo uongo.Inavyoonyesha Zitto umefikia mahali pagumu pa namna hiyo.Unapata shida ya kutunga uongo na unapata shida zaidi kuufikisha uongo huo kwa wananchi.

Kumbuka siku zote kuwa kutunga uongo ni kazi kubwa na kuufanya uongo ukubalike ni kazi kubwa zaidi.Pole.

Mwisho nashauri hata kama sheria ya manunuzi itabadilishwa tukasema tunahitaji mitambo mitumba kama ya Dowans Lazima tender process ifanyike na wauza mitumba wengi wa bid.Siyo kuwa ikibadilishwa basi Dowans wapewe hapana.Lazima waingie kwenye tender.Kama wakishinda washindie kwenye tender lakini sio mezani kwenye meza ya Zitto kabwe au Idrisa Rashid mkurugenzi wa Tanesco.

waveche sana baba/mama...............aika mbe.........aika meku.........well done....nina hakika brother zitto ame print hii kitu na anaisoma kwa utulivu then kesho atameza matapishi yake kwa kisingizio cha kupotoshwa..........THIS IS TANZANIA.........teh,teh,teh......
 
Zitto said......(akimjibu Keil)....ya kwamba
Capacity charge haihusiani kabisa na mitambo ya Dowans kwa sasa na hili limelieza katika maelezo yangu hapo awali. Capacity charge inayokwepwa hapa ni iwapo TANESCO itatangaza zabuni ya makampuni kuleta mitambo ya dharura na hivyo kujikuta katika tatizo la capacity charge.

........nafikiri hapo ndio kuna tatizo.......hivi hatuna chombo cha serikali ambacho kinaweza kufanya hayo manunuzi?.........naomba kuelimishwa jamani

Ogah,

Swala siyo chombo bali swali ni kwamba kwani TANESCO hawawezi kutangaza tender ya kununua mitambo mipya? Hivi option ya TANESCO ni kukodi mitambo kila kukicha?

Tendering process ya kukodi mitambo na tendering process ya kununua mitambo mipya inachukua same time. Mitambo hiyo iwe ya kukodi ama kununua bado itabidi isafirishwe kuletwa Tanzania na kuifunga ili kuiunganisha na grid ya taifa. Sasa hapo kuna tofauti gani kati ya option ya kununua mitambo mipya na kutangaza zabuni ya kukodi mitambo?

Tulishaumizwa kwenye kukodi mitambo ya IPTL, SONGAS, AGGREKO na mwishoni RICHMOND/DOWANS, hivi bado hatujajifunza kwamba option hiyo ndiyo inatuumiza kila kukicha na ndiyo maana mpaka leo hii tunaongelea capacity charges.

Mimi nilidhani option nzuri kwa TANESCO ni kutangaza tender ya kununua mitambo mipya badala ya hii idea ya kukodi mitambo. Wakinunua mitambo mipya ni ya kwao na ni ya kudumu na inaweza kukaa hata miaka 30 au zaidi. Lakini hii habari ya kukodi kila siku ndiyo imefanya umeme wa Tanzania uwe ghali na pia TANESCO wajiendeshe kwa hasara.

Je, kununua mitambo ya Dowans ndiyo option pekee? Kwanini tunaji-limit kwenye option ambayo ina-cast doubt mbele ya macho ya wananchi ambao tayari walishaumwa na nyoka na hivyo wakiguswa na unyasi wanaruka wakidhani nyoka karudi tena?
 
Kuhani,

Zitto anasema, mtafutieni hiyo sheria mnayodai kuwa inakiukwa!

Wamtafutie wakati yeye amekuwa akii-quote katika maelezo yake? Kui-quote tu ni ushahidi tosha kwamba anayo na alishaisoma sasa waiweke hapa ili iweje? Ichambuliwe ama tuangalie vipengele vya kufanyia marekebisho ili kuruhusu ununuzi wa mitambo chakavu?

Kuna magazeti yaliandika kwamba Mh. Zitto anapendekeza sheria hiyo ifanyiwe marekebisho ili tuweze kununua mitambo ya Dowans, kwa hiyo alishaipitia na anaifahamu vyema sana na anajua hata sehemu ambazo zinaweza kurekebishwa ili kulinusuru taifa lisiingie gizani. Lakini nadhani Mkuu Nentanyahu amemjibu vyema kwamba process ya kurekebisha sheria haiko rahisi kiasi hicho na haiwezi kuchukua muda mfupi na hasa kama kweli tuko kwenye dharura. Maana lazima marekebisho yaende Bungeni yawe discussed na yapitishwe.
 
Wataalam wa sheria naomba mnisaidie maana mimi ni kilaza wa sheria kabisa. Hivi serikali inapotaka kununua vitu huwa inatangaza zabuni ama na yenyewe inaruhusiwa ku-bid?

Nimeuliza hilo kwa sababu maelezo ya Mh. Zitto yanasema kwamba Tanesco wali-bid kununua mitambo ya Dowans baada ya kampuni hiyo kutangaza kwamba wanauza mitambo yao. Je, sheria inaruhusu ku-bid kwenye tender kama hizo? Achilia mbali uchakavu wa mitambo ya Dowans ninaongelea kwa ujumla. Maana sijawahi kusikia serikali ama shirika lake lime-bid kununua kitu kwa zabuni, ila mara nyingi huwa ninaona wao ndiyo wanatangaza zabuni ya kununua vitu.
 
Ogah,

Swala siyo chombo bali swali ni kwamba kwani TANESCO hawawezi kutangaza tender ya kununua mitambo mipya? Hivi option ya TANESCO ni kukodi mitambo kila kukicha?

Tendering process ya kukodi mitambo na tendering process ya kununua mitambo mipya inachukua same time. Mitambo hiyo iwe ya kukodi ama kununua bado itabidi isafirishwe kuletwa Tanzania na kuifunga ili kuiunganisha na grid ya taifa. Sasa hapo kuna tofauti gani kati ya option ya kununua mitambo mipya na kutangaza zabuni ya kukodi mitambo?

Tulishaumizwa kwenye kukodi mitambo ya IPTL, SONGAS, AGGREKO na mwishoni RICHMOND/DOWANS, hivi bado hatujajifunza kwamba option hiyo ndiyo inatuumiza kila kukicha na ndiyo maana mpaka leo hii tunaongelea capacity charges.

Mimi nilidhani option nzuri kwa TANESCO ni kutangaza tender ya kununua mitambo mipya badala ya hii idea ya kukodi mitambo. Wakinunua mitambo mipya ni ya kwao na ni ya kudumu na inaweza kukaa hata miaka 30 au zaidi. Lakini hii habari ya kukodi kila siku ndiyo imefanya umeme wa Tanzania uwe ghali na pia TANESCO wajiendeshe kwa hasara.

Je, kununua mitambo ya Dowans ndiyo option pekee? Kwanini tunaji-limit kwenye option ambayo ina-cast doubt mbele ya macho ya wananchi ambao tayari walishaumwa na nyoka na hivyo wakiguswa na unyasi wanaruka wakidhani nyoka karudi tena?

Keil,

natambua kuwa TANESCO wana authority ku-execute procurement ikiwa kama Gvt parastatal........ninachojiuliza na kutokana na maelzo ya Mh Zitto ni HOW.......procurement procedures ziko wazi.....ndio maana nikauliza walifikiaje hatua ya kwenda ku-BID mitambo ya Dowans...how didi they reach there...?

nakubaliana na maelezo yako kwa sana, na hata ukiangalia mambo mengi uliyoeleza, nimeyasema hapo awali.......ninachojaribu kufanya ni kuchukua one statement after the other ya Mh Zitto...........ili tuichambue

Jibu la ile quotation toka kwa Zitto ni kuwa.......SI LAZIMA KUKODI MITAMBO.....TUNAWEZA KUNUNUA PIA

.....next alichosema Mh Zitto ni kuwa eti.......hiyo sheria ya manunuzi kuwa ni lazima tununue mitambo mipya iko wapi.......and i quote below

PART V
………….Sheria ya manunuzi inasemwa kweli ndugu yangu lakini hakuna hata mtu mmoja hapa ambae kaja na kutoa kipengele gani cha sheria ya manunuzi kinakataza. Sijakiona mie. Hebu tazama na wewe, just google the Act na utueleze. Unajua sheria ya manunuzi inazungumzia kuanzia chaki shuleni mpaka vifaa complicated vya jeshi. Sheria haiwezi kuwa general (nunua kitu kipya...............). Huo mjadala pia hapa sijauona. Tunasema tu, sheria ya manunuzi, hatusemi kipengele gani na kwa mazingira gani.

Pia katika ununuzi huu, TANESCO ndio walibid kununua na sio TANESCO waliotangaza tenda. Katika mazingira kama haya sheria ya manunuzi inasemaje?...............
sasa basi inawezekana waandishi wetu wa magazeti walim-quote vibaya Mh. lakini hicho ndicho alichokiandika hapa JF (yeye mwenyewe Zitto)......

tuendelee kujadili
 
Wataalam wa sheria naomba mnisaidie maana mimi ni kilaza wa sheria kabisa. Hivi serikali inapotaka kununua vitu huwa inatangaza zabuni ama na yenyewe inaruhusiwa ku-bid?

Nimeuliza hilo kwa sababu maelezo ya Mh. Zitto yanasema kwamba Tanesco wali-bid kununua mitambo ya Dowans baada ya kampuni hiyo kutangaza kwamba wanauza mitambo yao. Je, sheria inaruhusu ku-bid kwenye tender kama hizo? Achilia mbali uchakavu wa mitambo ya Dowans ninaongelea kwa ujumla. Maana sijawahi kusikia serikali ama shirika lake lime-bid kununua kitu kwa zabuni, ila mara nyingi huwa ninaona wao ndiyo wanatangaza zabuni ya kununua vitu.

Ukiangalia vizuri procurement Act......itakuwa inaelezea ni kwa jinsi gani procurement entity (kama TANESCO) inavyoweza ku-PROCURE i.e renting/leasing, purchasing/buying or acquiring services.....ndicho ninachokumbuka.......kuhusu serikali/TANESCO ku-BID.......mmmhh

hapo nyuma nilisema hivi

Hapa kuna issue Mh Zitto kaigusia

1. Tanesco wame-BID ili kununua mitambo ya Dowans

Well, sihitaji kufahamu Dowans walitangaza lini hiyo tender.........however nahitaji kujua kama kuna option za manunuzi Tanesco walifanya pia, na kama kweli walifanya....je ni akina nani walikuwa approached other than Dowans.....Mh Zitto naomba unielimishe hapo........kama ulishatoa hayo maelezo im sorry.........hapa nauliza swali huku naendelea kusoma posts zaidi......

tuendelee kujadili
 
Mwanakijiji,

Naomba kujua mahojiano hayo yatarushwa saa ngapi ili niweze kuyasikiliza. Maana kwenye post yako umesema yatarushwa leo, ila muda ndo ambao hukusema.
 
mbona una wasiwasi, mimi siandiki maswali wala majibu yake, utasikia mwenyewe haya mambo ya kunukuliwa ndiyo niliyoyakwepa. Kama kuna maswali ya ziada baada ya wewe kusikia niandikie halafu tutamtafuta kumuuliza tena.

Yaweke basi hayo mahojiano na Ngeleja tunayasubiri kwa hamu kuu, unangoja nini tena!?
 
Within the hour.. yataweza kupatikana katika sites zote.. JF.. Mwanakijiji na Podomatic..
 
Inakuwa vipi waziri Ngeleja hajui hiyo Dowans inatoka wapi na inamilikiwa na nani? At the same time anataka kuingia nayo deal kubwa ya kununua mitambo? Wizi mtupu!
 
Yaani Waziri hajui hiyo Dowans ni ya nchi gani,lakini yuko radhi kuwapa tenda! hii ni ajabu!

Unajua kuwa na nia nzuri ni tofauti kabisa na kuitimiza hiyo nia kwa vitendo, pamoja na nia nzuri ya serikali je hii ndo njia bora ya kuondoa ama kupunguza tatizo la umeme nchini?, je option B iko wapi, option C je?
 
Last edited:
WanaJF,

Sikuwa katika mazingira ya kupita humu jamvini na kushiriki katika mjadala. Nimerudi safari na nilipopita nimekuta masuala mengi ya kujibu kwa upendo wangu kuhusiana na mjadala huu wa Mitambo ya kuzalisha Umeme. Ni mjadala mkali na wenye kubeba uchungu wa Taifa letu. Nimeona mumemuweka kiti moto kweli Dr. Slaa. Nadhani ni mwafaka mimi mwenyewe kujibu baadhi ya hoja na kama kuna maswali, basi niweze kujibu kadiri nitakavyoweza.

Kwanza Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (Public Investments Committee) haina mamlaka ya kikanuni au ya kikatiba kuiamrisha Serikali au Shirika la Umma kufanya au kutofanya manunuzi. Kamati kazi yake ni oversight (kusimamia). Kwa kweli hii ndio kazi ya Bunge na Kamati zake. Hata Kamati ya Nishati na Madini haina mamlaka ya kuingilia suala la utendaji wa kila siku wa Serikali. Ukishaifanya kamati ifanye kazi hiyo maana yake ni kuwa siku mhimili wa utendaji ukiboronga, Bunge halitaweza kusimamia kwani litakuwa ni sehemu ya uborongaji huo.

Pili, Kamati yangu imepewa mandate ya kufuatilia ufanisi wa mashirika ya Umma. Baada ya kuangalia income statement, na balance sheet, ambazo ndizo nguzo kuu zetu kufuatia taarifa ya CAG huwa tunaangalia je, Shirika linaendana na Corporate Plan yake? Melengo yanafikiwa? Huduma kwa wananchi ni bora, etc.

Kamati ilikutana na TANESCO mwezi Januari mwaka 2009 ili kutizama hesabu zao zinazoishia Disemba 2007. Tuligundua masuala yafuatayo:
- TANESCO katika mwaka unaoishia Disemba 2006 walipata 'Disclaimer Audit Opinion' kutoka kwa mkaguzi. Hesabu zao zilikuwa chafu sana kiasi cha Mkaguzi kuzikataa na kushindwa kutoa Opinion.
- TANESCO katika mwaka unaoishia Disemba 2007 walipata 'Unqualified Audit Opinion' kutoka kwa mkaguzi. Walifanikiwa kuruka hatua kadhaa (hati chafu, hati yenye mashaka) na kufikia hati safi. Hili lilikuwa jambo la kupongeza sana. Hasa ukizingatia kuwa wakati Kampuni ikiwa chini ya menejiment ya wageni (Net Group solutions) tulipata hati 'disclaimer' na ndani ya mwaka mmoja wa menejimenti ya Watanzania, tukapata hati safi na kusafisha madudu yote.

Hata hivyo, tulikuta matatizo kadhaa ndani ya TANESCO. Moja ya tatizo kubwa sana tulilolikuta ni kwamba gharama za kununua umeme kutoka kwa wauzaji (kama IPTL na Songas) zilikuwa zinachota fedha nyingi sana wakati umeme wanaozalisha ni kidogo sana ukilinganisha na umeme unaozalishwa na TANESCO wenyewe. Hebu fikiria: TANESCO inanunua kutoka kwa wawekezaji 42% ya umeme wote wanaouza. Hivyo TANESCO yenyewe inazalisha asilimia 58 ya umeme wote. Hata hivyo asilimia 84 ya mauzo yote ya umeme yanalipia umeme unaonunuliwa kutoka kwa wawekezaji (cost of sales) - yaani katika kila sh 100 ambayo TANESCO inakusanya kutoka kwa wateja wake, sh 84 zinatumika kununua 42% ya umeme ambao TANESCO inauza kwa wateja. Hivyo TANESCO inabakia na sh 16 kwa ajili ya kujiendesha ikiwemo kusambaza umeme zaidi kwa wananchi (kumbuka 12% ya watanzania ndio wenye umeme, na kwa Dar 50% ya wakazi hawana umeme - Household Budget survey 2007 iliyotoka November 2008). Kamati yangu ikasema, he, hili mbona halikubaliki?

Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, Kamati ikaagiza TANESCO waje kujieleza mbele ya Kamati juu ya hatua wanazochukua ili kupunguza gharama (cost of sales) na kuongeza mapato. (Kamati yangu imejiwekea lengo la kuhakikisha kuwa mpaka itakapokuwa inamaliza muda wake mwaka 2010 Agosti, mashirika yote muhimu ya Nchi yawe ama yana-break-even au yanapata faida. Ndio maana huwa hatupitishi hesabu mpaka tupate commitment za ma-CEO).

TANESCO wakaja katika kamati tarehe 21 Februari an kuwasilisha hatua mbalimbali wanazochukua. Katika hatua hizo ni pamoja na kutaka kununua mitambo ya DOWANS. Wakatueleza sababu zao zote. Tukawauliza maswali yetu. Ilikuwa ni mjadala sober sana katika Kamati. Kamati ikaona kuwa hoja za TANESCO zina mantiki.

Tukawauliza TANESCO, haya mnayotuambia mliiambia kamati ya Nishati na Madini? Kama ndio, mbona wao wamewakatalia? TANESCO, wakatujibu na kusema kamati haijawahi kutoa nafasi kwao kuelezea hoja zao. Tukasema, kama ndio hivyo basi, tunataka haya mnayotueleza sisi mwende mkayaseme tukiwa ni kamati mbili kwa pamoja kwani sisi hatupendi tupingane na wenzetu. Kamati ikaazimia hivyo.

Tukawauliza, Kamati ya Richmond walituambia DOWANS hawazalishi umeme. Iweje leo mitambo yao iwe inafaa ilhali wao walishindwa kuzalisha? TANESCO wakasema sio kweli, kwa mwaka mzima na tulikuwa tunanunua umeme wao MW 100 na hata wakati Dr. Mwakyembe anasoma taarifa ile, tulikuwa tunatumia mitambo ya Dowans. Wakaongeza kuwa ndio maana kipindi kama hiki (ambacho uzalishaji viwandani hukua na kutumia umeme mwingi) mwaka jana hatukuwa na mgawo kwani tulikuwa na 100MW kutoka Dowans mpaka tulipovunja mkataba mwezi Agosti. Pia kulikuwa na AGGREKO ambayo ilikuwa na 40MW. Hivi sasa kuna deficit ya 150MW ya umeme katika gridi.

Tukawauliza, hawa jamaa tunawadai. Wakasema ni kweli. Wamelipa deni lote ambalo tulikuwa tunawadai Richmond (35% of the value of the contract advanced to Richmond) na mpaka tunavunja mkataba tulikuwa tunawadai dola 8m tu maana walikuwa wanakatwa katika malipo yao. Hivyo tukiwanunua pia tunakata na pesa yetu.

Tukawauliza, sheria ya manunuzi inakataza. Wakasema ni kweli inakataza. Ilikuwa inakataza hata mitambo ya IPTL ambayo ni mikuukuu zaidi lakini sheria zina waiver kulingana na mahitaji ya nchi. Hata Ugiriki wakati wa Olimpiki walinunua mitambo iliyotumika nk. Ndio maana huwa tunanunua ndege zilizotumika. Mitambo ya miundombinu mara nyingi huwa ina special cases kisheria na ni nchi zote duniani.

Kamati ikasema sawa. Tutakutana Kamati mbili, Serikali na PPRA ili tuangalie suala hili. Nikafunga kikao

Haya jamani niambieni kosa langu lipo wapi?

Tatizo Watanzania mmezoea viongozi wanaowaambia mnayoyapenda tu. Hamjazoea na kwa mtindo huu hamtazoea viongozi ambao wanathubutu kuingia hata kwenye maeneo msiyoyapenda kusikia. Ndio maana maamuzi hayafanywi serikalini kwa sababu ya midomo.

Hapa JF kila mwanachama kawa leo mtaalamu wa Umeme, wengine wataalamu wa kanuni za Bunge, wengine wataalamu wa manunuzi lakini hata hawawezi kusema kifungu gani cha sheria ya manunuzi kinazungumzia suala la kununua mpya au hapana na kwa mazingira gani. Siasa tuuuuuu. Wengine mnahoji credibility yangu. Bila hata soni mnadhani mimi ni mpumbavu sana wa kuweza kujiwekea bei, at my age!

I am proud to what i have done for my country. I can die today smiling for my achievements. Wengine mdomo tuuuuuuuuuuu.

Wengine mnasema twende gizani. Mpo Ulaya na Marekani. Mnajua giza nyinyi? Mnajua madhara kwenye uchumi kwa umeme kukatika saa moja? Mwaka 2006 this sector grew at -2.5 kwa sababu ya giza and costed 2 points growth to our economy (read my speech bungeni katika mjadala wa richmond and economic survey 2006). Today the sector grow at 8% na mnataka twende nose diving again. Someni EIU survey feb 2009, kale kamgao ka Januari kalisababishwa na nini mnajua? Socket breaker tu iliungua na nchi ikaingia gizani kwani hakukuwa na reserve energy. Grid yetu ipo over done.

Mnajifanya mnajua, si lolote si chochote. Sisi ndio wawakilishi wenu. Tuulizeni. Tutawajibu. Tuulizeni tena. Tutawajibu. Tena na tena. Dont call us names.

This stupidity kills the courage of some of us to question myths of our society.

Lakini ninaelewa. Nchi imekuwa na wanasiasa wezi na waongo kwa muda mrefu sana. Hivyo trust to political class hakuna tena. Mpo paranoid. Kila mwanasiasa mnamwogopa masikini. Mnapata viongozi aina yenu Watanzania, kwani wengi ambao wanahoji humu pia hata ukimpa kijiji atakula mpaka bata wa kijiji (78% of Tanzanians dont trust each other - PHDR 2007).
ZITO na SLAA mmenikatisha tamaa kupita kiasi katika hili,nikiwa mfuasi wa CHADEMA nasikitika kusema kuwa kwa mtaji huu ni heri ZIMWI TULIJUALO CCM,naona huu unaweza kuwa kama mwendo wa Zambia kumtoa KENNETH KAUNDA kumuweka madarakani fisadi FREDRICK CHILUBA,kweli " Mi-Wana-SiHasa-ya-Kiafrika-Ndivyo-Ilivyo".
 
Hivi hawa viongozi wetu wamekumbwa na pepo gani?... Yani Ngeleja anataka kutuambia nchi imekubali kabisa kuwa held hostage na predatory businessmen?...Nchi yenye dola kamili na balozi zimezagaa mataifa yote makubwa.

Ana maana gani kusema kuwa, serikali haiwezi kuwashindanisha Dowans eti sababu ni kuwa aliyetangaza tenda ya kuuza mitambo ni Dowans, kwa maana nyingine serikali yetu kwenye hili imegeuka kuwa ni bidder. Complete reverse of roles, yaani tutanunua kwa bei atakayotaka huyo vendor ambaye ni Dowans.

Halafu anaongelea best practices. Best practices za wapi za kusource such heavy infrastructure equipment kwa kumfuata vendor mmoja?... Ambapo utanunua kwa bei aliokupangia na utanunua mashine hizohizo huna alternatives za kufananisha, badala ya kushindanisha masupplier wengi ili uweze kupata the best possible deal....Siku zote kwenye such sectors za suppliers wachache(olygopolies), best deal utaipata kwa kuwashindanisha manufacturers wenyewe sio kina Dowans.

Anataka kutuambia kwa vile mtu unajua ATC wanamatatizo, unaenda ulaya unanunua dege lako, unakuja kuliweka JNIA pale, then ghafla unatangaza kuliuza kwa bei yako. Halafu unakua na certificate ya mtaalam flani kuwa ndege inaruka. Then serikali itakuja kusema the same porojo au vipi?...Kuwa tununue tu kwa vile mwenye dege kaamua kuliuza na uzuri limeshafika JNIA, na ATC ina matatizo. Kwahiyo ni kulinunua tu na kuanza safari. Manunuzi gani ya umma yanafanywa kwa style hii.

Atuambie if that is the case, serikali ingefanya nini au iliandaa nini kama Dowans wasinge tangaza kuuza mitambo yao?...Maana to me Dowans kuamua kuuza mitambo ni kitu adhoc kwa serikali. Wao walipanga nini in the first place kukabiliana na hilo giza linalopigiwa mayowe?....Yaani anataka tuamini kuwa ni mere coincidence kwamba crisis ya umeme imebite na Dowans wametangaza kuuza mitambo yao, as if hao Dowans wanategemea wateja wengine weengi apart from Tanesco...

Hii cheap talk ya kutuambia tusidhani kila mtu ni fisadi wala asituletee. Sijawahi kumsikia fisadi yeyote including waliokutwa na vijisenti na wakashindwa kuvitolea maelezo aliyewahi kukubali, ametuchezea mchezo mchafu. It will be pretty naive kwa mtu kuiamini tu kauli ya "mimi sina maslahi binafsi" wakati vitendo vyake mashaka matupu.
 
Unajua Mitanzania kwa 10% yaani wapo lazi wanunue hata kitu cha kutumia wiki 2 ila wao wanajali 10% kwa matumbo yao na hawajali kuwa baada ya wiki 2 hizo na wao watasuffer.Huku Kwetu Kigali tunatupilia mbali mutu kama hizi.
 
Back
Top Bottom