Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Hongera Mwanakijiji na hongera waziri Ngeleja.

Mwanakijiji kauliza maswali yote kwa makini na yamekidhi haja.

Kwa waziri nimepata yaziada manne:-
1. Ununuzi wa mashine/vifaa vilivyotumika si jambo geni na katoa mifano kadhaa ikiwemo ya hivi karibuni tu ATC.
2. Serikali haiwezi kutangaza tenda kwani muuzaji ndiye anayetaka kuuza. Tanzania ikikataa itawauzia watu wengine. Sasa hapa ni nani mwenye shida?
3. Michakato ya kununua mitambo mingine imo in process. Hapa jamaa wengi wanafikiria kuwa ukinunuliwa mtambo wa Dowans ndio mwisho kumbe mambo siyo hivyo.
4. Issue ya Dowans ilikuwa siyo iliyojadiliwa na Kamati ya Mwakyembe. Wao walijadili Richmond. Kwa hiyo kununua kwa Dowans hakuusiani na maamuzi ya kamati hiyo.

Sasa basi hiyo ya kutojua Dowans ni kampuni ya wapi, waziri kasema imo kwenye records. Hiyo si issue kwa sasa mradi mitambo ipo hapa nchini. Kung'ang'ania hilo ni kutafuta tu vijikosa vidogo vidogo.

Interview hii kwa kweli imetusaidia sana. Endeleza mtindo huu kwa issues nyingine sensitive kama hii.

Hivi hebu niulize. Kama mtu umeshikwa na ugonjwa wa homa katakata akaenda pharmacy kununua dawa na akagundua kuwa pharmacy hiyo ni ya fisadi, wakati huo ni usiku wa manane hakuna pharmacy nyingine, na yeye yuko taaban kwa homa, jee atanunua dawa hapo au atangoja mpaka kesho yake na a risk kifo usiku huo? Jamani nisaidieni..
 
kwa pharmacy inayojulikana inastock madawa feki, ntamshauri angoje kesho yake au atafute nyingine usiku huo isiokuwa na sifa za dawa feki.
 
kwa pharmacy inayojulikana inastock madawa feki, ntamshauri angoje kesho yake au atafute nyingine usiku huo isiokuwa na sifa za dawa feki.

Ndugu hapa hatuzungumzii dawa feki tunazungumzia dawa safi. Jibu swali ndugu... au wewe hujawahi kupata machungu ya kuumwa?
 
Hongera Mwanakijiji na hongera waziri Ngeleja.

Mwanakijiji kauliza maswali yote kwa makini na yamekidhi haja.

Kwa waziri nimepata yaziada manne:-
1. Ununuzi wa mashine/vifaa vilivyotumika si jambo geni na katoa mifano kadhaa ikiwemo ya hivi karibuni tu ATC.
2. Serikali haiwezi kutangaza tenda kwani muuzaji ndiye anayetaka kuuza. Tanzania ikikataa itawauzia watu wengine. Sasa hapa ni nani mwenye shida?
3. Michakato ya kununua mitambo mingine imo in process. Hapa jamaa wengi wanafikiria kuwa ukinunuliwa mtambo wa Dowans ndio mwisho kumbe mambo siyo hivyo.
4. Issue ya Dowans ilikuwa siyo iliyojadiliwa na Kamati ya Mwakyembe. Wao walijadili Richmond. Kwa hiyo kununua kwa Dowans hakuusiani na maamuzi ya kamati hiyo.

Sasa basi hiyo ya kutojua Dowans ni kampuni ya wapi, waziri kasema imo kwenye records. Hiyo si issue kwa sasa mradi mitambo ipo hapa nchini. Kung'ang'ania hilo ni kutafuta tu vijikosa vidogo vidogo.

Interview hii kwa kweli imetusaidia sana. Endeleza mtindo huu kwa issues nyingine sensitive kama hii.

Hivi hebu niulize. Kama mtu umeshikwa na ugonjwa wa homa katakata akaenda pharmacy kununua dawa na akagundua kuwa pharmacy hiyo ni ya fisadi, wakati huo ni usiku wa manane hakuna pharmacy nyingine, na yeye yuko taaban kwa homa, jee atanunua dawa hapo au atangoja mpaka kesho yake na a risk kifo usiku huo? Jamani nisaidieni..

Jamani msisahau kuwa waziri Ngeleja alikuwa mwanasheria wa Vodacom kabla ya kwenda kugombea ubunge. Na Rostam Aziz ni share holder wa Vodam na ndiye aliyempeleka Ngeleja kugombea Ubunge na inasemekana ndo aliyemfadhili kushinda nafasi hiyo. Na mara tu baada ya kushida nafasi hiyo, bila shaka Rostam ambaye ni swahiba wa mkuu wa nchi alimpendkeza akapewa unaibu waziri kabla ya kuwa waziri kamili. Na sote twajua ya kuwa Dowans ni ya Rostam Aziz na Ngeleja anataka tu kulipa fadhila kwa huyu fisadi. Ndugu tk tatizo la umeme linalozungumziwa hapa si la leo wala mwezi ujao bali ni miaka miwili ijayo. Na habari za uhakika zinasema kuwa mitambo mipya kama hiyo huko Marekani inauzwa kwa bei nafuu kuliko bei ya hii mitumba ya Dowans. Kwahiyo kama ni kuweka tahadhari ya miaka miwili ijayo basi ikanunuliwe mitambo mipya tena kwa bei nafuu. Hapa kuna jambo (ufisadi na uhujumu uchumi wa nchi) si bure.
 
Keil,

natambua kuwa TANESCO wana authority ku-execute procurement ikiwa kama Gvt parastatal........ninachojiuliza na kutokana na maelzo ya Mh Zitto ni HOW.......procurement procedures ziko wazi.....ndio maana nikauliza walifikiaje hatua ya kwenda ku-BID mitambo ya Dowans...how didi they reach there...?

nakubaliana na maelezo yako kwa sana, na hata ukiangalia mambo mengi uliyoeleza, nimeyasema hapo awali.......ninachojaribu kufanya ni kuchukua one statement after the other ya Mh Zitto...........ili tuichambue

Jibu la ile quotation toka kwa Zitto ni kuwa.......SI LAZIMA KUKODI MITAMBO.....TUNAWEZA KUNUNUA PIA

.....next alichosema Mh Zitto ni kuwa eti.......hiyo sheria ya manunuzi kuwa ni lazima tununue mitambo mipya iko wapi.......and i quote below

PART V
sasa basi inawezekana waandishi wetu wa magazeti walim-quote vibaya Mh. lakini hicho ndicho alichokiandika hapa JF (yeye mwenyewe Zitto)......

tuendelee kujadili

Ninaomba kipengele cha sheria kinachosemwa hapa. Maana tunasoma tu kuwa sheria ya manunuzi inakataza lakini hatuambiwi kipengele gani cha sheria ya manunuzi? Mimi nimetafuta sijaona na ndio maana nimeomba nisaidiwe.
Pia nisaidiwe pale ambapo TANESCO ndio wamebid na sio wao kutangaza zabuni.

Nashukuru sasa mjadala umeondoa emotions na tumekuja kwenye issues. Ninaamini tutafikia Azimio based on facts and according to the law.
 
Hivi hebu niulize. Kama mtu umeshikwa na ugonjwa wa homa katakata akaenda pharmacy kununua dawa na akagundua kuwa pharmacy hiyo ni ya fisadi, wakati huo ni usiku wa manane hakuna pharmacy nyingine, na yeye yuko taaban kwa homa, jee atanunua dawa hapo au atangoja mpaka kesho yake na a risk kifo usiku huo? Jamani nisaidieni..

Ndugu yangu ulimsikiliza vizuri Bwana Ngeleja? Kama ulimsikiliza vyema hili swali lako liko irrelevant.

Ngeleja kasema hakuna ulazima wa kununua hiyo mitambo kwa kuwa hali ya umeme iko shwari na kina cha maji kiko poa kwenye mabwawa. Wananunua mitambo ya dowans kwa sababu ya opportunity imejitokeza. Nakisi ya umeme anayoiongelea imekuwepo siku siku zote. Ni sawa na mtu aliyepitia duka la dawa akaona liko wazi na akaamua kununua dawa kwa kuwa kahisi ana dalili za malaria, lakini bado anaweza kusubiri kesho yake akaenda hospitali ili apimwe kabisa ajue anaumwa nini na apewe dawa iliyo sahihi badala ya kukurupuka kunywa dawa la malaria na kumbe ana homa tu.
 
Asante sana Mzee Mwanakijiji kwa mahojiano, nimemsikiliza Mh. Ngeleja alipokuwa akijikanyaga kanyaga kujibu maswali yako pamoja na kutoa maelezo.

Kitendo cha yeye kukuomba ufunike funike kimenipa mashaka kiasi. Hivi kama serikali na Tanesco wana nia njema kuna haja ya kuomba msaada wako ili utuelimishe zaidi. Ametumia neno baya, kwamba wewe ni kama "kiongozi wa dini na una wafuasi wengi". Kwa hiyo yeye anaamini kwamba ukisema chochote kiwe kibaya ama kizuri wafuasi wako wataitikia AMEEEENI ama AMIIIIIN (kwamba watakubali kuwa kiko sawa tu)!

Mh. Zitto na wewe una watu wengi sana wanaokuamini, nina mashaka unaweza kuwa ulipewa info nzuri na ukaruka hewani ili wao (serikali) wapate nguvu ya kuendelea na kununua hiyo mitambo ya Dowans. Itafakari sana kauli ya Ngeleja aliyoisema kwenye haya mahojiano na Mwanakijiji. Ombi langu kwako ni moja, jiridhishe kwamba hujalishwa kasa, maana mitambo hiyo ikinunuliwa na ikaja kubuma after 3 yrs, utakuwa umeua upinzani kwa bua, sidhani kama CHADEMA watakuja kuaminika tena. Msimamo wa Kamati yako naona umekaa kimtego mtego.

Uzuri wa maelezo ya Mh. Ngeleja ni kwamba amekiri kwamba hakuna ulazima/uharaka wa kununua mitambo ya Dowans ila kwa kuwa opportunity imejitokeza ndiyo maana wanataka kununua. Kwa hiyo kauli kwamba ama tununue mitambo ya Dowans au tuingie gizani, ilikuwa ni spinning.

Ukisoma press release ya Dr. Rashid inapingana na maelezo ya Ngeleja. Dr. Rashid anaonyesha kwamba ni lazima mitambo hiyo inunuliwe, wakati Ngeleja anasema hali ya maji kwenye mabwawa yetu ni shwari na nakisi ya umeme iliyopo imekuwepo siku zote ingawa hapo mbeleni kidogo kutakuwa na ongezeko la mahitaji ya umeme. Sasa hizi contradictions zinatoka wapi au labda Ngeleja ana info nusu?

Idea ya kununua mitambo ya Dowans ilianza tangu mwaka jana Oktoba, leo ni March 2009 ambao ni mwezi wa 6 tangu wapate hiyo idea, kwanini hawakuamua kuanza mchakato wa kununua hiyo mitambo mipya tangu kipindi hicho? Nina uhakika mpaka kufikia mwezi June mwaka huu tayari mitambo ingekuwa Dar na ingekuwa imefungwa.

Swala la capacity charges kumbe kampuni karibu zote mikataba ilishakwisha kasoro IPTL tu ambao bado wanaendelea nao. Maelezo waliyopewa kamati yanasema wazalishaji binafsi wanakomba hela za capacity charges na kumbe kabaki mmoja tu. Kwa hiyo hata tukinunuwa mitambo ya Dowans bado mzigo wa kuibeba IPTL uko pale pale mpaka watakapokubali kuuza mitambo yao.

Ngeleja anasema bei ya mitambo ya Dowans ni kama shilingi bilioni 60 hivi (ambayo inazalisha MW 100), kuna mtu hapa jamvini kasema kwa bilioni 70 tunaweza kupata mitambo ya kuzalisha MW 200. Ngeleja anasema bei ya mitambo mipya kutoka GE ni kama bilioni 90. Kwa wenye data na utalaam wa bei tunaomba watumwagie hapa, lakini bei hizo ziwe za mitambo kama ya Dowans ambayo wanasema inatumia gas kwa kuwa gas ni bei poa.

Ngeleja anasema kwamba kununua mitambo mipya ni process ambayo inaweza kuchukua si chini ya miezi 20 mpaka 24. Hivi hiyo mitambo inatoka hapa hapa kwenye hii dunia ama inatoka sayari ya Mars? Tendering inaweza kuchukua muda mrefu lakini kuna exception na nina uhakika within 6 months tunaweza kumpata supplier na akashusha mzigo Dar. Hiyo miaka miwili inatoka wapi? Lini procurement ya mitambo ya kufua umeme ilichukua muda wa miezi 20 mpaka 24?
 
Ndugu hapa hatuzungumzii dawa feki tunazungumzia dawa safi. Jibu swali ndugu... au wewe hujawahi kupata machungu ya kuumwa?

Toka lini fisadi akauza kitu safi? kumbuka yale madege yaliyotoka Lebanon, angalia leo ATCL, Mabehewa ya TRL toka India etc kenge ni kenge tu haachi mila zake asilani
 
Pia nisaidiwe pale ambapo TANESCO ndio wamebid na sio wao kutangaza zabuni.

Mh. Zitto naomba msikilize Mh. Ngeleja kwenye mahojiano yake na Mwanakijiji. Amesema kwamba baada ya Dowans kutangaza zabuni ya kuuza mitambo yake, serikali iliomba mahakama isimamishe zoezi hilo ili kwanza TANESCO walipwe dollar milioni 8. Halafu wakati wakiwa wameweka pingamizi mahakamani, TANESCO hao hao waka-bid kununua mitambo hiyo. Ambacho hakusema ni matokeo ya bid ya TANESCO. Lakini ni wazi kwamba TANESCO walishinda hiyo zabuni na ndiyo maana wakaja na idea ya kuomba kununua hiyo mitambo. Au labda nilimsikiliza vibaya Mh. Ngeleja.
 
Jamani msisahau kuwa waziri Ngeleja alikuwa mwanasheria wa Vodacom kabla ya kwenda kugombea ubunge. Na Rostam Aziz ni share holder wa Vodam na ndiye aliyempeleka Ngeleja kugombea Ubunge na inasemekana ndo aliyemfadhili kushinda nafasi hiyo. Na mara tu baada ya kushida nafasi hiyo, bila shaka Rostam ambaye ni swahiba wa mkuu wa nchi alimpendkeza akapewa unaibu waziri kabla ya kuwa waziri kamili. Na sote twajua ya kuwa Dowans ni ya Rostam Aziz na Ngeleja anataka tu kulipa fadhila kwa huyu fisadi.

......na Dr Idris Rashid nae alikuwa MD wa Vodacom ya RA! Kwa hiyo RA effectively ameshikilia Energy Sector pia? Maana 'kote' ameweka watu wake! Duh, nchi hii.
 
Dowans ilibidi itaifishwe mbona hawajafanya hivyo. Walilipwa 127 bilion right to the wrong person no one knows the owner now they want to buy from a ghost and pay 60million dollars. This is really an incredible country. Not even Nigeria this is possible.
 
This is simply a BLACKMAIL by DOWANS...wasipotuuzia sisi hii mitambo itawadodea hawana pa kuipeleka.
 
Noamba wote wa JF muende kwenye mtandao kutafuta bei ya Generator alafu mlinganishe na bei ya Dowans.
 
Kama kweli tunataka kuisaidia nchi yetu tuanze kwenye procurement ili tusizulumiwe. Saidieni Tanesco kupata mitambo wengi tuko ughaibuni angaikeni jamani kabla hawajanunua mitumba.
 
Mh. Zitto naomba msikilize Mh. Ngeleja kwenye mahojiano yake na Mwanakijiji. Amesema kwamba baada ya Dowans kutangaza zabuni ya kuuza mitambo yake, serikali iliomba mahakama isimamishe zoezi hilo ili kwanza TANESCO walipwe dollar milioni 8. Halafu wakati wakiwa wameweka pingamizi mahakamani, TANESCO hao hao waka-bid kununua mitambo hiyo. Ambacho hakusema ni matokeo ya bid ya TANESCO. Lakini ni wazi kwamba TANESCO walishinda hiyo zabuni na ndiyo maana wakaja na idea ya kuomba kununua hiyo mitambo. Au labda nilimsikiliza vibaya Mh. Ngeleja.

1. TANESCO walivunja mkataba na DOWANS baada ya ushauri wa kisheria kutoka REX Attorneys kuonyesha kuwa hawatapa madhara ya kisheria.

2. DOWANS waliishitaki TANESCO kuhusiana na mkataba wao huko Paris.

3. Wakati huo huo DOWANS wakatangaza zabuni ya kuuza mitambo yao iliyopo Ubungo, Dar es Salaam. Tangazo lilionekana katika magazeti ya Tanzania na East Africa.

4. TANESCO wakabid kununua turbines hizo

5. Kamati ya Nishati na Madini ikatoa Tamko la kuikataza serikali kununua mitambo hiyo iliyotumika kwani sheria ya manunuzi inakataza (sijapata kipengele hicho cha sheria ya manunuzi mpaka sasa). Serikali ikaikataza TANESCO kununua.

6. TANESCO wakafungua kesi kuzuia mitambo hiyo kuondoka nchini mpaka kesi iishe ili itumike kama fidia na pia kuhusiana na deni.(TANESCO wanasema ni $8m, lakini kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya POAC ni shs 11bn yaani $10.8m)

Huo ndio mtiririko ambao kamati yetu imeuona. Highlighted and blued sentence sio sahihi.
 
Tusubiri magogoni, kuna taarifa tutapata karibuni.

Na wale wengine wanaojua mambo kuna vitu vitaibuka karibuni kwa hiyo haya ya Zitto aachiwe Zitto mwenyewe, Hana nguvu wala say yoyote. Kamati yake kumbe haina hata say kwenye hili, yeye alijiingiza tu bila kujua, kazi yao ni kuangalia hali ya hayo mashirika na kusimamia mahesabu yao after the fact, na sio before the fact. Ofisi ya Spika wala haina mpango wa kudeal naye kwenye hili kwa hiyo umaarufu wake ni humu humu JF, his idea is rotten to the core na reasons za yeye kungangania inasemekana zitajulikna huko mbeleni. Kangangania PPRA as if tunahitaji kufundishwa sheria na huyu mtu wakati wanasheria waliobobea wameshatoa legal opinion zao.

Kwa hiyo jamani Zitto tumuache, tuangalie huko kwenye nguvu na vitu vitajulikana karibuni.
 
Ndugu yangu ulimsikiliza vizuri Bwana Ngeleja? Kama ulimsikiliza vyema hili swali lako liko irrelevant.

Ngeleja kasema hakuna ulazima wa kununua hiyo mitambo kwa kuwa hali ya umeme iko shwari na kina cha maji kiko poa kwenye mabwawa. Wananunua mitambo ya dowans kwa sababu ya opportunity imejitokeza. Nakisi ya umeme anayoiongelea imekuwepo siku siku zote.

Mimi nimemsikiliza tena. Yeye kasema kuwa licha ya hali ya uzalishaji umeme kuwa nzuri etc, bado kuna upungufu wa kama 150 na huu ni lazima ujazwe. Hayo uliyoyasema kuwa hakuna ulazima kwa kweli sijayasikia. In fact anasisitiza kuwa mitambo hii ya Dowans inaweza kutuvusha hapo hivi sasa ili tusiingie gizani. Urgument kuwa nakisi hiyo imekuwepo siku zote haimaanishi kuwa iendelee kuwepo na isishughulikiwe kwa haraka.
 
Kinachonifanya nimshuku Zitto ni kubadilika kwa kauli zake: Mara anasema, issue ni kununua mitambo yoyote si lazima Dowans; mara aseme mitambo ya Dowans ni bei poa na mtambo mmoja ni mpya!? Hii ni lugha kikuadi kabisa, ameacha msimamo wake wa kutetea taifa anatetea Dowans. Sitaki awe adui wa watu wanaonuka ufisadi lakini ukaribu wake na wahariri wa Habari Corporation, Ngereja na Masha unatia shaka. Najua kumfahamu na kumshabikia Zitto.
 
Back
Top Bottom