Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Jamani fungu la kumi 10% linatumaliza miafrica.
Yaani hata wewe Zitto umo?mmmh hizi 10% ndizo zinazo fanya watu wasimamie mikucha yao kutetea mitambo used.....kwa nini wao magari yao mashangingi wasi nunue used?toka AUTOREC ili kuokoa gharama?
 
Mh. Dr. Slaa,
Mkuu nimekusikia sana tatizo bado unatumia siasa ktk ku solve tatizo hili..Mimi Mbongo na nimeishi miaka yote ya ujana wangu Bongo.. naelewa harufu mbaya ya mnyama hatari kama Simba bila hata kumwona..

Mimi sina haja ya kusoma hadidu za Zitto kwa sababu alivyoanza tu kasema alimwomba ruksa Spika..hapo tu tayari anaingilia kazi isiyokuwa yake kisha swala hili la Dowans ni swala ambalo yeye alitakiwa kukaa mbali kabisa nalo hasa upende huo!...Trust me, sioni tofauti yake na Masha ktk swala la vitambulisho hata kama kuna tofauti za miradi hii.

Sasa tuzungumze kama watu wazima. wewe kama kiongozi na pongine unayeunga mkono kamati ya Zitto nambie sababu ambazo wewe zimekuvutia ktk maamuzi hayo!..Kwa sababu mimi sioni kabisa argument yenye malengo mazuri.. nipe points zako wewe kutokana na hadidu hiyo maanake mimi sikuoina la maana kabisa kufikia maamuzi ya kuunga mkono ununuzi wa mitambo iliyochakaa..
Mkandara,
Thanks once again, kama umenisoma vizuri, my line of argument is completely different. Ninapenda kutenganisha issues, na kujadili kila mmoja kwa nguvu yake ya hoja. Lakini hoja kubwa hapa ni kuwa hatuna majibu kwa vile hatujui yaliyojadiliwa na Kamati ya Zitto na wala yaliyojadiliwa na Kamati ya Shellukindo. Ukitafakari sana, kuna majibu mengi yanahitajika hivyo, namna pekee ya kupata maelezo ya kina ni kukubali kwa Kamati hizi mbili zikae zikajadili kwa kina na Taifa tujulishwe. Vinginevyo hatuna namna ya kujua ukweli kuhusiana na suala hili zima.
 
Nina maswali machache ya kuchangia kwenye hii mada:

1. Hivi mchakato wa kununua mitambo mipya unachukua muda gani? Maana nimeona hoja kwamba kununua mitambo mipya mchakato wake unaweza kuchukua muda mrefu ambao hausemwi.

2. Huyo mtalam aliyekuja kutathimini mitambo ya Dowans tuna uhakika gani kwamba alifanya kazi yake jinsi inavyopaswa? Tuna mifano mingi ya kununua vitu used ambavyo vimekuja kuwa mzigo kwa taifa, mfano ni ndege ya rais ambayo hata JK haitumii tena. Tusidanganyane kwamba mitambo ikikaguliwa tutaweza kuepuka kuingia mkenge.

3. Mkataba wa Tanesco na Dowans ulivunjwa mwaka jana mwezi August, kama Tanesco walijua kwamba kuna upungufu wa umeme kwanini hawakuanza mchakato wa kununua mitambo mipya, na badala yake wakakaa wakatulia wakasubiri dharura ije ndipo waombe kununua mitambo chakavu?

4. Kwanini Bunge linataka kuingia mkenge? Hoja ya kuzikutanisha kamati za Bunge pamoja na Tanesco na serikali, ili kupata muafaka ninapata mashaka kwamba tunaweza kuwa tunatengeneza upenyo wa Bwana Ngeleja kuja kukwepa kusulubiwa iwapo mitambo hiyo itakuja kugundulika kuwa bomu. Bunge litakuwa halina nguvu ya kuihoji serikali kwamba kuna ufisadi umefanyika maana Bunge lilishiriki kutoa baraka na kuruhusu kuvunja sheria kwa kununua mitambo chakavu.

5. Mwaka juzi wakati wa semina ya mswada wa umeme ambao ilikuwa uwasilishwe na Mh. Karamagi wabunge walitaka kupata master plan ya umeme, na nilitarajia ndani ya hiyo master plan kungekuwa na hizi issues ambazo leo wanazileta na kuzifanya kuwa ni dharura. Hivi kwanini kamati haikumkumbusha Dr Rashid hilo? Net Group Solution wametoka miaka karibu 3 iliyopita, hakuna excuse kwamba eti TANESCO hawakuwa na mipango ya muda mrefu kwa kuwa walikuwa wanasubiri kubinafsishwa. Hapa naona wanatafuta excuse kila kona ili mradi hiyo mitambo iweze kununuliwa.
 
Last edited:
Wanasheria naomba msaada wenu hapa;

Quote
"Kwa sasa mitambo hiyo inashikiliwa na Tanesco, ambalo linadai kuwa itatumika kama fidia iwapo shirika hilo litashinda kwenye kesi ambayo Dowans imefungua dhidi ya Tanesco kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara iliyo Paris, Ufaransa."
[end quote]

Kama kuna kesi tayari, hii si inatosha kusimamisha mazungumzo yoyote kuhusu hili deal?

Quote
""Hii inatokana na ukweli kwamba, ni vigumu kubuni mradi unaoweza kukamilika kabla ya mwaka 2009 kuisha," alisisitiza." [end quote]

Waziri anaonyesha wazi jinsi alivyoshindwa hii kazi. JK yuko nje ya nchi most of the time kutangazia wawekezaji, na kama nakumbuka vizuri, mwaka jana alisema tatizo la umeme litatatuliwa muda si mrefu. Kwa maana hiyo (ya wawekezaji na matumizi ya kila siku kuongezeka) Waziri anaweza kutupa plan ya miaka 3? 5? 10? ijayo? What's in the pipe production wise? Suala la ukame linajulikana kwa muda mrefu sasa, Waziri atakuwa anatangaza tender kila mwaka?

Actually nilifikiri suala la ukame sio issue tena baada ya EL kupata wataalamu wa mvua mashariki ya mbali.

Waziri, please layout your plan here and inform us what are you going to do to solve the whole issue in a long run.
 
Cry my beloved country............. !!!!!!!!! tatizo naloliona hapa ni kupoliticize kila issue lakini haya ndiyo matunda ya taratibu za CCM na serikali yake. Ni kwa nini sisi watz kila issue inakuwa na politiki ndani yake. I fail to understand kuhusu ni kwa nini ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme siasa itawale badala ya utaalamu.

Je ni kweli kwamba matatizo ya wizi na uporaji wa mali ya umma yatakuwa solved na siasa? Ndiyo nafahamu kwamba siasa safi ni mojawapo ya nyenzo muhimu katika kuleta maendeleo. Lakini sijapata kusikia hata siku moja siasa kutumika kufanya maamuzi ya kitaalamu.
 
...hoja kubwa hapa ni kuwa hatuna majibu kwa vile hatujui yaliyojadiliwa na Kamati ya Zitto na wala yaliyojadiliwa na Kamati ya Shellukindo. Ukitafakari sana, kuna majibu mengi yanahitajika hivyo, namna pekee ya kupata maelezo ya kina ni kukubali kwa Kamati hizi mbili zikae zikajadili kwa kina na Taifa tujulishwe. Vinginevyo hatuna namna ya kujua ukweli kuhusiana na suala hili zima.

Mkuu, Dr. W. Slaa, heshima mbele.

Kwanza niseme, kama siku zote, ahsante kwa kuja kujadili mambo nasi hapa, ukiwa mmoja wa viongozi wachache nchini, pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ambao wanajitolea kuhojiana moja kwa moja na wananchi. Binafsi nadhani kuna kujitoa muhanga fulani kwenye hadhi yako unapokuja kwenye jamvi la kila mtu hapa. Rais Kikwete jana Ikulu amegomba kwamba maoni juu ya serikali yake yatolewe kama anavyofanya Mzee Kawawa, ndani vyumba vya viyoyozi, maji ya chupa na usiri mkuu, na sio kwenye "vijiwe." Tafadhali usinunue maneno ya Rais, ukakitupa kijiwe chetu. Ahsante kwa hilo.

Sasa, Mkuu, mimi siamini wewe Dr. Slaa hujui yaliyoendelea ndani ya Kamati ya Kudumu ya Zitto Kabwe.

Kwanza, Kamati ya Kabwe imemaliza kazi ya kutathmini swala la TANESCO na mitambo ya Dowans, imetoa ushauri wake. Wajumbe nadhani hawafungwi na kanuni inayokataza kujadili mambo ya Kamati kabla haijamaliza kazi, kipengele 50 ( 4 ), na ndio mana hata Shelukindo, wa Kamati ya Kudumu ya madini anaongea wazi wazi. Mh. Kabwe nadhani anaweza kujadili haya mambo na wewe, kama ungetaka, na najua unataka, kujua.

Kabwe pia, kama wewe, ni kiongozi mwandamizi wa chama chako, CHADEMA, nyote mna kila sababu ya kushirikiana kisiasa, na la chini kuliko yote mnaloweza kufanya ni kuwasiliana. Lenu moja. Sasa ukisema Katibu Mkuu wa CHADEMA na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA hawaongei kuhusu siri walizonazo kuhusu shughuli au udhoofu wa serikali ya CCM, hususan yahusuyo Bunge ambalo nyote ni wajumbe, mimi sielewi, nataka kukataa.

Hilo la pili, lakini la tatu, zaidi ya ukaribu wa kichama ulionao na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ni kwamba ni watu wachache Tanzania, kama wapo, ambao wanapata nyeti na siri za serikali, mpaka "siri za kijeshi," achilia mbali za mabenki na ma akaunti ya mafisadi na nyeti nyingine za nchi zaidi yako wewe Dr. Slaa. Sasa leo utanambia eti hujui yanayoendelea kwenye Kamati ya Zitto? Umejua ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya "siri za kijeshi" utashindwa ya Kamati ya CHADEMA mwenzio? Wamarekani wanasema give me break Mr. Politician. Acha kumsafisha mwenzio kwa kukunjakunja mada eti hatujui yaliyotokea ndani ya Kamati ya Kabwe, tusubiri. Baada ya kupigana na "siri za kijeshi na madini" sasa na wewe umeanza kulea "siri za kamati na umeme"?

Isitoshe mna ukaribu wa binafsi. Wa kusafishana. Kama jana ulivyokuja kumsafisha hapa kabla hajaja kututukana mchana mchana kwamba wananchi hatujui chochote wala lolote, tusubiri atuambie. Amempiku Samuel Malecela wa CCM katika vitabu ya historia ya maneno fidhuli kwa wananchi. Kwamba tuna "stupidity," tuko Marekani na Ulaya tuna neema ya kutokatiwa umeme! Zitto wako huyo huyo ambae mwaka jana alitamka akiwa Detroit Marekani kwamba Watanzania waishio nchi moja tu ya ng'ambo wameiingizia nchi hela (dola milioni 450) mara sita zaidi ya faida iliyopatikana kwenye sekta ya madini kuanzia 2007 kwenda nyuma miaka 10 ( dola millioni 73 )! Leo aja kututukana? Uko tayari kumsafisha mwanasiasa mfurahisha halaiki kama huyo ndio utashindwa kuongea nae kuhusu ya serikali, na CCM , na Bunge na CHADEMA kweli?

Dr. Slaa, mmepata pata mafanikio upande wa upinzani miaka ya karibuni sasa msianze kuharibu kwa kutufanya - mpaka kutuita - stupid. Mnahitaji kuungwa mkono na wananchi ambao ndio kwaaaanza wanaanza kuelewa dhana nzima ya upinzani. Msianze kuwapoteza kwa siasa za usanii na kulindana na kusafishana; hiyo karata siku hizi hata CCM wameona inawalostisha, ndio maana hata Kikwete anawatema maswahiba na kuwatosa jela siku hizi. Sasa Dr. Slaa, si itakuwa matusi nikikwambia wapinzani muende kuangalia, kujifunza CCM?
 
4. Kwanini Bunge linataka kuingia mkenge? Hoja ya kuzikutanisha kamati za Bunge pamoja na Tanesco na serikali, ili kupata muafaka ninapata mashaka kwamba tunaweza kuwa tunatengeneza upenyo wa Bwana Ngeleja kuja kukwepa kusulubiwa iwapo mitambo hiyo itakuja kugundulika kuwa bomu. Bunge litakuwa halina nguvu ya kuihoji serikali kwamba kuna ufisadi umefanyika maana Bunge lilishiriki kutoa baraka na kuruhusu kuvunja sheria kwa kununua mitambo chakavu.

Hoja ya kamati mbili kukutana ni hoja ya kamati ya Mashirika ya Umma, sio hoja ya Serikali. Hoja hii imekuja baada ya kukataa kuingana na Kamati ya Nishati na Madini ambayo ilikwishasema kuwa serikali isinunue mitambo. Kamati ya Hesabu inasema hapana, tuwasikilize TANESCO ili kuona hoja yao na tusijikite kwa mitambo ya Dowans tu. Hakuna mbadala?
Nakubaliana nawe kuwa iwapo kamati za Bunge zitajiingiza katika mjadala wa tununue au tusinunue, likiharibika kwa uamuzi wowote, Bunge ndio litalaumiwa na serikali kutua mzigo. Kazi yetu ni Oversight


5. Mwaka juzi wakati wa semina ya mswada wa umeme ambao ilikuwa uwasilishwe na Mh. Karamagi wabunge walitaka kupata master plan ya umeme, na nilitarajia ndani ya hiyo master plan kungekuwa na hizi issues ambazo leo wanazileta na kuzifanya kuwa ni dharura. Hivi kwanini kamati haikumkumbusha Dr Rashid hilo?

Kamati ilizungumza kuhusu MasterPlan. Kimsingi hoja ya Masterplan ndio imeleta hoja zote hizi kwani miradi yote iliyopo kwenye masterplan iliyopangwa kumalizika mwaka huu haiwezi kumalizika.

- Kiwira walitakiwa waingize MW50 mwezi March, hawataingiza na 150MW mwezi Oktoba hawataingiza.
- Kinyerezi 240 MW haitaingia
- Upepo Singida mazungumzo bado yanaendelea na hayaishi na hivyo 50MW hazitaingia.
- Mtwara 300 MW Barrick wamejitoa due to global financial crisis


Net Group Solution wametoka miaka karibu 3 iliyopita, hakuna excuse kwamba eti TANESCO hawakuwa na mipango ya muda mrefu kwa kuwa walikuwa wanasubiri kubinafsishwa. Hapa naona wanatafuta excuse kila kona ili mradi hiyo mitambo iweze kununuliwa.


Hapana. Mimi binafsi suala hili sio la lazima. Kwamba do or die. Hapana. Options zingine ziangaliwe pia au hata kutonunua kabisa Dowans bali tununue mtambo wa kuziba hii nakisi. TANESCO imekuwa despecified mwaka 2007 na hivyo kuweza kuwekeza na hata kukopa. These are facts and tuziweke facts mezani bila kuzipinda. Mjadala huu tusichukue sides. Tuelimishane na kwa sisi wawakilishi wenu Bungeni tukiona hoja hapa tunaibeba wazee. Tumefanya hivyo mara kadhaa. Tuweke hoja na tukate issues an hatimae kufikia hitimisho. Mtu mmoja adraft maazimio hapa na mwishowe tuseme, haya ni ya JF, Zitto peleka huko. Hapo JF itakuwa imesaidia Taifa. Hii kulalama lalama hapana!
 
Drama Queen Kuhani kaanza kunya na yeye...basi subirini muone patakavyoanza kunuka hapa.

Halafu nani ana definition ya neno "matusi" au "tusi" hapa?
 
Mkandara,
Lakini hoja kubwa hapa ni kuwa hatuna majibu kwa vile hatujui yaliyojadiliwa na Kamati ya Zitto na wala yaliyojadiliwa na Kamati ya Shellukindo. Ukitafakari sana, kuna majibu mengi yanahitajika hivyo, namna pekee ya kupata maelezo ya kina ni kukubali kwa Kamati hizi mbili zikae zikajadili kwa kina na Taifa tujulishwe. Vinginevyo hatuna namna ya kujua ukweli kuhusiana na suala hili zima.

Give me break Dr, sipendi na sipendi unikatishe tamaa. i am proud of you ila hapa sikuelewi kabisa. Ina kwenye fungua mabandiko ya Zitto utaona aliyosema au kuna mengine?

Sitaki kusikia sitaki kuwa tunampa hata penny Rostam Aziz. Sitaki Dr sitaki wewe ukasupport. Tunateseka na magigambo sitaki, umeshakutana na crew ya Rostam? sitaki Dr, sitaki kusikia. Naomba Dr kama ni giza wewe unauwezo wa kununua gen set. Sitaki waachie CCM wakubaliane wenyewe. Sitaki Slaa na Zitto muingizwe mkenge. Taifa hili sio lenu pekee. NASEMA SITAKI
 
Wadanganyika kwanza lazima tumjue huyu Idris Rashid ni nani katika vita yetu na hawa mafisadi.; huyu bwana ni mdau wa kampuni zote mbili anzia Richmond na sasa Dowans. Ubia wa Rashid katika kampuni hizi unapitia kwa watu wawili ambao ni partners wake kibiashara nao ni Rostam na Noni wa BOT ambao waliwekeza pamoja toka Vodacom na hata wakati fulani yeye Rashid akawa kinara wa Vodacom kwa muda mfupi!! Sasa katika biashara zao, hii mitambo yao ya Dowans wasipoiuzia Tanzania watakula hasara kibiashara kwahiyo lazima watafute kila hila waiuze hapa si kwa manufaa ya wadanganyika bali kwa kupunguza hasara zao. Sasa wanatumia hila through position ya Rashid Tanesco to create panic [fear factor] kwamba bila kuinunua hii mitambo, basi nchi itaathirika kiuchumi; kudhihilisha hilo Rashid anacreate artificial shortage ya umeme na kuanzisha load shedding as a way ya blackmail watu waamini kuwa bila kununua hii mitambo chakavu nchi haina alternative nyingine isipokuwa giza !! Hii nddio deal yao mpaka sasa wameishaiuza kwa wakina Zitto nao wameuvaa Mkenge!! Hawa mafisadi wabaya sana; Rashid kishatuibia kwenye Radar na Chenge wake leo huo uzalendo wa kutuonea huruma ameutoa wapi? Jamani tuamke huyu hatutetei sisi anatetea commission yake hapo!!
 
Dr.Slaa,
Mheshimiwa kwanza heshima mbele... nakusikia mkuuu na ningependa sana kujadili swala hili kwa fikra huru zaidi hasa pale napoona kiongozi wangu (Zitto) anajiingiza ktk mkenge ambao mimi nafahamu kuwa umepikwa..Nahofu kufikiria nje ya sanduku.. trust me.
Sina haja ya kusema mengi sana isipokuwa tu inanishangaza pale mtu kama Zitto anapokuja kwa jazba kwa sababu tu kuna mtu/watu wametumia vigezo au mifano ambayo hakuipenda kisha naye anarudia makosa yaleyale..

Kifupi Ununuzi wa mitambo ta Dowans ni kosa kubwa sana kisiasa na hata kufikiria tu kwamba hatuna njia isipokuwa wao.. kwa sababu ukisoma mwanzo wa mkataba mitambo hii iliagizwa kwa mkataba wa muda mfupi yaani miezi 24 kama sikosei..Na viongozi waliokuwepo madarakani walituambia kuwa hili ni tatizo la muda tu.. wananchi hatukutaka kabisa habari ya Richmond from day one na kama unakumbuka hapa JF tulianza kupiga kelele zetu..vijana wa Houston waliweka hadi picha za ofisi za Richmond na kadhalika, hao Richmond walikuwa hawana site wakaunda ya harakaharaka na kujihusisha na Boieng ili kutuzuga zaidi bahati vijana wetu waliendelea kufuatilia hadi ukweli ukawa wazi kabisa kuwa hili lilikuwa kanyaboya..
Sasa pamoja na yote hayo, matumizi ya mitambo hii ilikuwa ni ya muda mfupi tu, ajabu serikali (Tanesco) haikuweza kufanya lolote pamoja na jipu zima kupasuka kuiandaa nje ya mkataba feki..badala yake wakaingia ktk mkataba mwingine na Dorwans jambo ambalo nina hakika Tanesco walisukumwa na wanasiasa tena kama mwanzo.. Kuna taarifa kamili zinazoonyesha Lowassa akishauri mkataba uhamishiwe Dorwans.. badala ya kushauri tender mpya ifanyike.. Wapi hao Dorwans wametokea hatufahamu.. leo hii tujiingize katika kununua mitambo yao huku tumefukia vichwa vyetu mchangani kama mbuni kuficha ukweli kwamba mitambo hiyo ni ya Richmond sio Dorwans..Aliyenunua mitambo ni Richmond na ku sub contract kwa Dorwans hivyo mchezo bado upo palepale kwani mmiliki ni yule yule...
Hakuna kati yetu anayefahamu mkataba kati ya Richmond na Dowans, hakuna anayefahamu tofauti ya mmiliki wa Richmond na Dorwans.. ni jambo la kawaida kabisa hapa Ulaya kuuwa kampuni moja ukaunda nyingine..
Nakubaliana na maneno ya Zitto anaposema kwamba Tanesco wanahitaji hizo 100Kwt za umeme, well kama tunawadai basi tuendelee na contract yetu hadi fedha zetu zitakapo kwisha wakati huo huo tukiagiza mitambo yetu...ni jambo ambalo lilitakiwa kufanyika toka zamani na nadhani lilikuwepo ktk mpango wa serikali auTanesco wenyewe walipoweka makataba na Richmond kwa kuhitaji mitambo hiyo kwa miezi 24, kama haikufanyika basi ifanyike leo..Na kama Zitto anataka vijana hapa waende mbio kutafuta generators zenye uwezo zaidi ya hiyo ya Dorwans atupe kazi hiyo aone kama kweli mitambo hiyo itafika nchini baada ya mwaka 2009 kama wanavyodai wao.. Siemen wapo Tanzania, nakuombeni nendani ofisini kwao kamwone kijana mmoja anaitwa Alaf muulizeni kuhusiana upatikana wa mitambo hii kama kweli inaweza chukua miezi sita toka leo hii tunavyozungumza..
Kinachonipa shida mimi ni pale tunapotaka kununua mitambo hii kwa sababu tuna shida.. Ni sawa na kuposa mke kwa sababu una kiu (nyege) na hicho kiu ndicho kinatazamwa kama kigezo cha manunuzi badala ya kufikiria ni mke gani unayemhitaji na kwa sababu gani..
Nina hakika kabisa hakuna uchunguzi wa kina umefanyika kuziangalia hizo generators za dorwans (mke) badala yake tumefikira zaidi nyege za Tanesco hata kama kweli wanahitaji mke mwenye kizazi..
Kama nilivyosema hapo awali siwezi kununua mali yoyote ya mwizi hata kama naihitaji kiasi gani...nitakwenda kununua dukani..
 
Sasa nikisema Miafrika Ndivyo Tulivyo mnanikasirikia. Mnaona sasa? Najua Tanzania tuna wahandisi wa umeme. Mnataka kunambia hawa wahandisi wameshindwa kutengeza jenereta au mitambo mingine ya kuzalisha umeme? Si mnadai Sivyo Tulivyo? Sasa kama Sivyo Tulivyo mtu ungedhani huu ndio wakati mzuri wa kuthibitisha kuwa na sisi tunaweza na hakuna linalotushinda. Lakini nooooo...mko hapa mnabishania majenereta yaliyotengenezwa na wazungu ambayo sijui serikali inataka kuyanunua au kuyakodisha.

Bottom line is this: Miafrika Ndivyo Tulivyo! Leo tuko karne ya 21 lakini bado hata kuunda mamitambo ya kuzalisha nguvu za umeme hatujui licha ya kuwasoma wazungu ma pioneer wa fani hiyo (hizo) na kujidai tumewaelewa. Puh--lease!

Heheheheheee....nawahakikishia Tanzania haitakuja kutatua tatizo la umeme. Mtazaa watoto wenu, watoto wenu watazaa wajukuu wenu, wajukuu wenu watazaa watoto wao na kuendelea lakini haitakuja tokea hata siku moja Tanzania na nchi zingine za Kiafrika kuondoa tatizo la umeme.

Mwenye ujasiri na anithibitishe mimi muongo (mwongo).
 
Kamati yangu haijalazimisha Dowans hata kidogo. Mjadala huu ndio umejikita huko. Maelezo yako ni mazuri na tuendelee na mjadala. Kuna maeneo haupo sahihi sana kwani unahitaji maelezo zaidi. Nilisema katika moja ya vikao vya kamati kuwa, ingekuwa wakati wa Mwalimu suala hili lingekuwa rahisi sana kwani tungetaifisha tu. Kwa sasa neno taifisha linaonekana sio zuri masikioni mwa 'investors' lakini ndivyo ingepaswa. Kamati yangu haikujikita hata kidogo kwa Dowans. Hiyo ni option mojawapo ambayo TANESCO wameitoa. Kamati ilijadili options kadhaa

- Kufast track Kinyerezi project (240MW)
- Kufast track Umeme wa Upepo Singida (50MW)
- Kuokoa Umeme wa Mtwara (300MW)

Na haya ndio masuala tulioomba kamati mbili zikutane na kujadili kwa pamoja na kuona ipi itaokoa mambo kwa haraka.

TANESCO wametaka kuongeza uwezo wao wa kuzalisha umeme hizo 100MW kwa haraka kwani tayari mitambo hiyo imeunganishwa katika gridi. Mitambo mipya kutoka GE etc tulijadili kuambiwa kuwa ni sawa lakini itachukua muda mrefu sana mpaka kufungwa na kwamba wanataka kuchukua mtabo wa 60MW kuupeleka Mwanza ili kukabili tatizo lililopo kule sasa hivi. Hivyo suluhisho la muda mrefu ni lazima liwepo na hapo ndio umuhimu wa kikao cha kamati mbili.

Ni muhimu tukumbuke kuwa kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita TANESCO lilikuwa specified company (shirika linalosubiri kubinafsishwa). Hivyo hapakuwa na uwekezaji wowote uliiofanywa. Hivyo sehemu kubwa ya matatizo tunayoyapata sasa yanatokana na maamuzi yetu kama nchi ya kisera.

Kuhusiana na IPTL. Mimi silinganishi bali ninaonesha kuwa kigezo cha sheria ya manunuzi (ambayo haitajwi ni kifungu gani hapa) itakwamisha pia mpango wa kununua IPTL na kuigeuza kuwa gesi. Ninaamini Two wrongs never make it a right. Kununua IPTL kutazuiwa na sheria hii ya manunuzi ijapokuwa uamuzi huo wa kununua mitambo chakavu itasaidia sana TANESCO kutatua tatizo lake la cash flow (tutaokoa $9m altogether kila mwezi kwa uamuzi huo wa kununua IPTL na kugeuza mitambo kuwa ya gesi).

Suala la nishati ya Umeme, kwa mwono wangu, ni suala linalohitaji mjadala uliotulia na wenye kuona picha kubwa (broader picture). Ndio maana Kamati yangu iliamua ilivyoamua.

Mh Zitto nimeonelea nigusie jambo moja specifically kwenye highlights...Sitopenda kuendelea na malalamiko kuhusiana na kauli zako za kuwaponda watanzania walioko nje ya nchi kama europe na marekani kwamba hawana uchungu na nchi yao na kwamba hawajui shida na wakati wengi wetu kilichotutoa bongo ni utafutaji...Kusema ukweli hapo ni upotoshaji...Hivi Zitto mimi na wewe kama mbunge na mwanamikamati kibao nani anaishi vizuri? Ama Mwanakijiji na Rostama nani anapeta? Kwanini ujiingize kwenye siasa chafu kiasi hicho kama mafisadi..?Sasa ccm si ndio wanatembeza bakuli na kujidai kuwa wana shida kubwa sana kama wananchi na huku wao ni mabilionea na wana pesa lukuki na majumba nje ya nchi? Watu wanaotafuta life unawaita stupid kwasababu wametofautiana na wewe unaesema una uchungu kwasababu uko Tanzania?

Ni nchi gani iliyoendelea kama hawakusafiri na kuona wengine wanafanya nini na wao kupeleka chamgamoto nchini kwao? Unakumbuka Industrial Revolution?

Waingereza wangekaa tu nchini kwao wote ingekuwaje?
Back to the point hapa...Unaposema utaifishaji hautawafurahisha wawekezaji, je unafuatilia siasa za waasisi wa ubepari. Hata mabenki hapa USA na baadhi ya mashirika yako mikononi mwa serikali kwa muda flani hadi hapo solution itakapopatikana....Ni kwamba Nationalism iko inaendelea hapa marekani ila wanadai ni kwa muda...Sasa unaposema utawachukiza wawekezaji una maana kuwa maslahi ya Taifa ndio wananchi waliwe tu simply kwasababu ya wawekezaji?

Ni bora mafisadi washughulikiwe na katika process wananchi wakiathirika wajuwe ni kwasababu ya maamuzi yao wakati wa kupiga kura....Mambo ya kubebana yamepitwa na wakati,na inasikitisha kuwa ikifikia kubebana eti kuna madai kuwa walioko nchini ndio wenye uchungu...Yani wewe na kina Chenge na Rostam mna uchungu sana na Taifa na ndio maana hamko majuu....Hii kali....Hivi na wewe bado huna nyumba huku?
 
Huyo mtalam aliyekuja kutathimini mitambo ya Dowans tuna uhakika gani kwamba alifanya kazi yake jinsi inavyopaswa? Tuna mifano mingi ya kununua vitu used ambavyo vimekuja kuwa mzigo kwa taifa, mfano ni ndege ya rais ambayo hata JK haitumii tena. Tusidanganyane kwamba mitambo ikikaguliwa tutaweza kuepuka kuingia mkenge.

Swali lingine je huyo anayeitwa mtathmini mitumba alipatikanaje? Sheria za manunuzi zilizingatiwa? Je kupatikana kwake kulitangazwa katika vyombo vyovyote vya kimataifa ili watu wa bid tender hiyo kwa ushindani ulio wazi? Au kupatikana kwake pia ni ufisadi mwingine? Idrisa Rashid Mkurugenzi wa Tanesco inabidi atueleze vizuri huyo mtaalamu wa kutathimini mitambo mitumba alivyopatikana na walimlipa kiasi gani? Na nani aliyehitaji hiyo tathmini ya hiyo mitambo mitumba ifanyike na kwa lengo gani alitaka hiyo tathmini ifanyike akiwa katumwa na nani?
 
Wakuu naomba nieleweshwe kidogo hapa hii inayoitwa mitambo ni majenereta tu au ni pamoja na switch gears, transformers, capacitor banks etc.??????
 
Wakuu naomba nieleweshwe kidogo hapa hii inayoitwa mitambo ni majenereta tu au ni pamoja na switch gears, transformers, capacitor banks etc.??????

Mazee...kila kitu kinachohitajika ktk kuzalisha umeme. Hatutengenezi vyote hivyo so it is safe to say ni hayo mazagazaga yote na mengineyo yanayohitajika ktk uzalishaji wa nishati hiyo
 
Nyani ngabu,
Mkuu swala la miafrika ndivyo tulivyo ni ukweli unaokubalika, sisi ni WAJINGA (hatuna elimu) lakini sio wajinga hivyo mkuu wangu..Kweli tumeshindwa kutengeneza vitu hivyo basi iwe hata kuchagua kipi kizuri?..
Mbona ndio sifa kubwa ya Miafrika ktk kuchagua!..
 
Dr.Slaa,
Mheshimiwa kwanza heshima mbele... nakusikia mkuuu na ningependa sana kujadili swala hili kwa fikra huru zaidi hasa pale napoona kiongozi wangu (Zitto) anajiingiza ktk mkenge ambao mimi nafahamu kuwa umepikwa..Nahofu kufikiria nje ya sanduku.. trust me.
Sina haja ya kusema mengi sana isipokuwa tu inanishangaza pale mtu kama Zitto anapokuja kwa jazba kwa sababu tu kuna mtu/watu wametumia vigezo au mifano ambayo hakuipenda kisha naye anarudia makosa yaleyale..

Kifupi Ununuzi wa mitambo ta Dowans ni kosa kubwa sana kisiasa na hata kufikiria tu kwamba hatuna njia isipokuwa wao.. kwa sababu ukisoma mwanzo wa mkataba mitambo hii iliagizwa kwa mkataba wa muda mfupi yaani miezi 24 kama sikosei..Na viongozi waliokuwepo madarakani walituambia kuwa hili ni tatizo la muda tu.. wananchi hatukutaka kabisa habari ya Richmond from day one na kama unakumbuka hapa JF tulianza kupiga kelele zetu..vijana wa Houston waliweka hadi picha za ofisi za Richmond na kadhalika, hao Richmond walikuwa hawana site wakaunda ya harakaharaka na kujihusisha na Boieng ili kutuzuga zaidi bahati vijana wetu waliendelea kufuatilia hadi ukweli ukawa wazi kabisa kuwa hili lilikuwa kanyaboya..
Sasa pamoja na yote hayo, matumizi ya mitambo hii ilikuwa ni ya muda mfupi tu, ajabu serikali (Tanesco) haikuweza kufanya lolote pamoja na jipu zima kupasuka kuiandaa nje ya mkataba feki..badala yake wakaingia ktk mkataba mwingine na Dorwans jambo ambalo nina hakika Tanesco walisukumwa na wanasiasa tena kama mwanzo.. Kuna taarifa kamili zinazoonyesha Lowassa akishauri mkataba uhamishiwe Dorwans.. badala ya kushauri tender mpya ifanyike.. Wapi hao Dorwans wametokea hatufahamu.. leo hii tujiingize katika kununua mitambo yao huku tumefukia vichwa vyetu mchangani kama mbuni kuficha ukweli kwamba mitambo hiyo ni ya Richmond sio Dorwans..Aliyenunua mitambo ni Richmond na ku sub contract kwa Dorwans hivyo mchezo bado upo palepale kwani mmiliki ni yule yule...
Hakuna kati yetu anayefahamu mkataba kati ya Richmond na Dowans, hakuna anayefahamu tofauti ya mmiliki wa Richmond na Dorwans.. ni jambo la kawaida kabisa hapa Ulaya kuuwa kampuni moja ukaunda nyingine..
Nakubaliana na maneno ya Zitto anaposema kwamba Tanesco wanahitaji hizo 100Kwt za umeme, well kama tunawadai basi tuendelee na contract yetu hadi fedha zetu zitakapo kwisha wakati huo huo tukiagiza mitambo yetu...ni jambo ambalo lilitakiwa kufanyika toka zamani na nadhani lilikuwepo ktk mpango wa serikali auTanesco wenyewe walipoweka makataba na Richmond kwa kuhitaji mitambo hiyo kwa miezi 24, kama haikufanyika basi ifanyike leo..Na kama Zitto anataka vijana hapa waende mbio kutafuta generators zenye uwezo zaidi ya hiyo ya Dorwans atupe kazi hiyo aone kama kweli mitambo hiyo itafika nchini baada ya mwaka 2009 kama wanavyodai wao.. Siemen wapo Tanzania, nakuombeni nendani ofisini kwao kamwone kijana mmoja anaitwa Alaf muulizeni kuhusiana upatikana wa mitambo hii kama kweli inaweza chukua miezi sita toka leo hii tunavyozungumza..
Kinachonipa shida mimi ni pale tunapotaka kununua mitambo hii kwa sababu tuna shida.. Ni sawa na kuposa mke kwa sababu una kiu (nyege) na hicho kiu ndicho kinatazamwa kama kigezo cha manunuzi badala ya kufikiria ni mke gani unayemhitaji na kwa sababu gani..
Nina hakika kabisa hakuna uchunguzi wa kina umefanyika kuziangalia hizo generators za dorwans (mke) badala yake tumefikira zaidi nyege za Tanesco hata kama kweli wanahitaji mke mwenye kizazi..
Kama nilivyosema hapo awali siwezi kununua mali yoyote ya mwizi hata kama naihitaji kiasi gani...nitakwenda kununua dukani..

Bob,
...tena kuna mtu hapa hapa JF alisema.......wakati ule tunajadili ile issue ya RDC........kuwa hii mitambo TUTAKUJA KUINUNUA.........na sasa inatokea..........wallahi sijui Tanzania tumeingiliwa na Kichaa gani.......damn!
 
Mkuu, Dr. W. Slaa, heshima mbele.

Kwanza niseme, kama siku zote, ahsante kwa kuja kujadili mambo nasi hapa, ukiwa mmoja wa viongozi wachache nchini, pamoja na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ambao wanajitolea kuhojiana moja kwa moja na wananchi. Binafsi nadhani kuna kujitoa muhanga fulani kwenye hadhi yako unapokuja kwenye jamvi la kila mtu hapa. Rais Kikwete jana Ikulu amegomba kwamba maoni juu ya serikali yake yatolewe kama anavyofanya Mzee Kawawa, ndani vyumba vya viyoyozi, maji ya chupa na usiri mkuu, na sio kwenye "vijiwe." Tafadhali usinunue maneno ya Rais, ukakitupa kijiwe chetu. Ahsante kwa hilo.

Sasa, Mkuu, mimi siamini wewe Dr. Slaa hujui yaliyoendelea ndani ya Kamati ya Kudumu ya Zitto Kabwe.

Kwanza, Kamati ya Kabwe imemaliza kazi ya kutathmini swala la TANESCO na mitambo ya Dowans, imetoa ushauri wake. Wajumbe nadhani hawafungwi na kanuni inayokataza kujadili mambo ya Kamati kabla haijamaliza kazi, kipengele 50 ( 4 ), na ndio mana hata Shelukindo, wa Kamati ya Kudumu ya madini anaongea wazi wazi. Mh. Kabwe nadhani anaweza kujadili haya mambo na wewe, kama ungetaka, na najua unataka, kujua.

Kabwe pia, kama wewe, ni kiongozi mwandamizi wa chama chako, CHADEMA, nyote mna kila sababu ya kushirikiana kisiasa, na la chini kuliko yote mnaloweza kufanya ni kuwasiliana. Lenu moja. Sasa ukisema Katibu Mkuu wa CHADEMA na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA hawaongei kuhusu siri walizonazo kuhusu shughuli au udhoofu wa serikali ya CCM, hususan yahusuyo Bunge ambalo nyote ni wajumbe, mimi sielewi, nataka kukataa.

Hilo la pili, lakini la tatu, zaidi ya ukaribu wa kichama ulionao na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ni kwamba ni watu wachache Tanzania, kama wapo, ambao wanapata nyeti na siri za serikali, mpaka "siri za kijeshi," achilia mbali za mabenki na ma akaunti ya mafisadi na nyeti nyingine za nchi zaidi yako wewe Dr. Slaa. Sasa leo utanambia eti hujui yanayoendelea kwenye Kamati ya Zitto? Umejua ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya "siri za kijeshi" utashindwa ya Kamati ya CHADEMA mwenzio? Wamarekani wanasema give me break Mr. Politician. Acha kumsafisha mwenzio kwa kukunjakunja mada eti hatujui yaliyotokea ndani ya Kamati ya Kabwe, tusubiri. Baada ya kupigana na "siri za kijeshi na madini" sasa na wewe umeanza kulea "siri za kamati na umeme"?

Isitoshe mna ukaribu wa binafsi. Wa kusafishana. Kama jana ulivyokuja kumsafisha hapa kabla hajaja kututukana mchana mchana kwamba wananchi hatujui chochote wala lolote, tusubiri atuambie. Amempiku Samuel Malecela wa CCM katika vitabu ya historia ya maneno fidhuli kwa wananchi. Kwamba tuna "stupidity," tuko Marekani na Ulaya tuna neema ya kutokatiwa umeme! Zitto wako huyo huyo ambae mwaka jana alitamka akiwa Detroit Marekani kwamba Watanzania waishio nchi moja tu ya ng'ambo wameiingizia nchi hela (dola milioni 450) mara sita zaidi ya faida iliyopatikana kwenye sekta ya madini kuanzia 2007 kwenda nyuma miaka 10 ( dola millioni 73 )! Leo aja kututukana? Uko tayari kumsafisha mwanasiasa mfurahisha halaiki kama huyo ndio utashindwa kuongea nae kuhusu ya serikali, na CCM , na Bunge na CHADEMA kweli?

Dr. Slaa, mmepata pata mafanikio upande wa upinzani miaka ya karibuni sasa msianze kuharibu kwa kutufanya - mpaka kutuita - stupid. Mnahitaji kuungwa mkono na wananchi ambao ndio kwaaaanza wanaanza kuelewa dhana nzima ya upinzani. Msianze kuwapoteza kwa siasa za usanii na kulindana na kusafishana; hiyo karata siku hizi hata CCM wameona inawalostisha, ndio maana hata Kikwete anawatema maswahiba na kuwatosa jela siku hizi. Sasa Dr. Slaa, si itakuwa matusi nikikwambia wapinzani muende kuangalia, kujifunza CCM?

.....hapo tupo ukurasa mmoja Mkuu...maneno mazito
 
Nyani ngabu,
Mkuu swala la miafrika ndivyo tulivyo ni ukweli unaokubalika, sisi ni WAJINGA (hatuna elimu) lakini sio wajinga hivyo mkuu wangu..Kweli tumeshindwa kutengeneza vitu hivyo basi iwe hata kuchagua kitu kizuri?..
Mbona ndio sifa kubwa ya Miafrika ktk kuchagua!..

Hahahahaa...Bob hata kuchagua hatuwezi. Tungekuwa tunaweza hata hilo tusingekuwa na viongozi tulionao sasa ambao tunajua kabisa wanaiba lakini tunaendelea kuwachagua kucha kutwa.

Wewe umeona wapi tatizo linalotatulika kiurahisi hivi linachukua milele kulitatua. Bob, hivi hapo T-Dot ni mara ngapi kwa mwezi kunakuwa na power outages? Au power rationing?

Mimi tokea niko shule ya vidudu hili tatizo lipo. Na kulingana na stori za wazee lilikuwepo hata kabla sijawa wazo kichwani mwa wazazi wangu...na mind you, mimi siyo dogo tena. Punde si punde nitaanza kuitwa babu..Lol

Sasa jamani kila mwaka tuna go through mambo yale yale. Kila mtu anakuja na utatuzi wake. Kama mtu hutujui na unatusikiliza tu tunavyochonga domo mwenyewe utadhani haya majamaa kiboko aisee. Lakini in actual reality tuko watupu kabisa. Tuna maneno mengi sana. International Olympic Committee wakianza ku include kupiga soga ktk michezo yao nadhani tutakuwa tunashinda medali nyingi sana na kuacha kuwa watalii na wasindikizaji kila baada ya miaka minne.
 
Back
Top Bottom