Kiranja,
Asante kwa maswali yako mazuri sana. Nadhani hoja yako inakosa kwa misingi kadhaa:-
i) Hoja yako na maswali yamejikita katika Kifungu cha 2 cha Majukumu ya Kamati ya Mashirika ya Umma kwa mujibu wa Kanuni ya Bunge ambayo umeinukuu. Kwa bahati mbaya hapa nilipo sina Kanuni hivyo ninategemea umeinukuu vizuri hadi ukatuwekea hapa. Lakini-
a) hukugusia kabisa majukumu ya Kanuni kama yalivyo kwenye kipengele cha 3, 4, na 5.Vipengele hivyo vyote vinatoa nafasi kwa Kamati ya Mashirika ya Umma kushughulikia utekelezaji wa Maelekezo ya Kamati ( ingelikuwa busara ungelianzia kwa utafati kama Kamati hiyo iliwahi wakati wowote ilipokuwa inapitia mahesabu imewahi kutoa Mapendekezo yeyote ili kuinusuru hali waliyoikuta wakati wa utekelezaji wa jukumu lao. Ni jukumu lao sasa kufuatilia "utekelezaji wa maagizo yao". Generalization ni hatari sana. Hivyo vyema, kama unazo taarifa kuhusu mapendekezo hayo ungelituwekea hapa ili tufahamu hisia inayoanza kujengeka. Ni vyema Tanzania tusiruhusu "hisia" katika mambo makubwa kama haya.
b)Kifungu cha 2 cha Kanuni uliyoinukuu hapo juu kinazungumzia "tathmini ufanisi". Ni mpaka utakaponiambia kuwa Kamati ya Mashirika ya Umma haijafanya "tathmini" na au haina mamlaka ya kufanya tathmini ya ufanisi wa Tanesco, ndipo nitakapoona kuwa hoja yako ina msingi. Lakini iwapo Kamati katika taratibu zake za kawaida imefanya Tathmini ya shirika la Tanesco, basi ni vizuri "tathmini" hiyo ikafanyiwa mjadala kwa hoja zake bila kuunganishwa na chochote kinachohusiana na maswala ya Richmond/Dowans. Iwapo Kuna mambo ambayo Kamati ya Mashirika ya Umma imeyagundua ambayo ni kwa maslahi ya Taifa, sidhani ni vyema kuyakataa kwa vile tu Kamati nyingine imekwisha kufanya uamuzi. Ndiyo msingi wa hoja ya Kamati mbili kukutana ili mambo mapya yaliyojitokeza yafanyiwe kazi. Mimi nafikiri this is where our system becomes healthy, and with checks and balances. Hatuwezi kuyakataa mambo ambayo Kamati imegundua kwa kuwa tu tumefanya uamuzi, hata katika system ya Mahakama, kuna flexibility katika mazingira fulani fulani. Kama nimesoma sahihi ni kuwa Kamati ya Nishati na Madini ilikuwa haijawahi kuisikiliza TANESCO kama TANESCO . Hatuwezi kuadhibu Taifa kutokana na Technicalities na grounds ambazo hazina tija kwa maoni yangu. Iwapo Kamati mbili zitakaa kwa manufaa ya Taifa, mimi ninaamini kabisa mawazo ya watu wengi yana tija zaidi daima.
c) Kanuni ya 5 uliyonukuu inazungumzia Kufuatilia "utekelezaji wa Sera..." hivyo sioni kabisa mantiki ya hoja yako kwani huwezi kufuatilia utekelezaji wa Sera bila pia kutazama maswala yanayohusu capacity ya Taasisi husika.
2)Kiranja, Wakati nakubaliana nawe kuwa ununuzi wa mitambo hii inaweza kuwa mbinu mmoja ya Wanamtandao kupata fedha za uchaguzi kwa 2010, lakini hoja hii bado ni dhaifu sana, kwani huwezi kuadhibu Taifa zima likakosa umeme kwa sababu za kisiasa. Kuna njia nyingi zaidi za kudhibiti wanamtandao kuliko hii. Hivyo, objective debate na kupata definitive solution kwa maswala ya athari ya ukosefu wa umeme yasichanganywe na maswala ambayo kwangu yanahitaji majibu na hatua za aina tofauti kabisa. Let us sit down and think, and think aloud for the good of our country and avoid simplistic answers to complicated issues as this one.
4) Hoja ya kuwa TANESCO ilizembea kuagiza mtambo unaostahili tangu azimio la Bunge, kwangu pia is non issue. Uzembe wa uongozi wa TANESCO uwe dealt with squarely, bila kuhusisha na maswala ya msingi.
5) What I dont like is having double standards in our country. Tumeruhusu Serikali ijadiliane na IPTL kununua mitambo ya IPTL ambayo imetusumbua kwa zaidi ya miaka 15 sasa, na ni chakavu zaidi kuliko mitambo ya Richmond /Dowans at least one kama ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya Habari. I have no problem kama issue ni kufanya independent assesment ya Wataalamu, hata kama inamaanisha kuingia gharama ya kuwapata wataalamu hao, iwapo tu tutathibitishiwa kuwa mitambo hiyo ni cheaper kuliko ku import mitambo ya aina hiyo hiyo au mipya kabisa. Wakati huo huo tunakataa kununua mitambo ya Richomond/ Dowans.
6) Maswala ya kijinai ya Richmond/Dowans yashughulikiwe kwa utaratibu wa Kawaida, na tunaweza kabisa kutenganisha maswala haya.
7) Swali la kwamba Serikali iliisha kulipa Richmond Dowans advance ya US$ 35 Million appears to me as a new revelation. But this is a separate issue and I think at this stage we need the Government to tell us the full story about its relations na watu hawa.Hata Bunge halikupewa Taarifa hii, and if this is true, this is very serious in my opinion. Hatujaambiwa pia kwanini Dowans hawajalipa hadi leo US $ 10 million ambazo wanatakiwa kutulipa kwa kila siku waliyochelewesha kuingiza umeme kwenye National Grid. Let us discuss the matter soberly na tutafikia ukweli na solution kuliko kujenga hisia.