Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Waheshimiwa Dr. Slaa na Zitto Kabwe:::

Finality ya mazungumzo haya inabidi iwe hivi ili kwanza kuliokoa taifa kwenye hasara kubwa ya kununua mitambo chakavu ya Dowans na pili kuwaokoa nyie kwenye huu mtego hatari mlioingia either kwa makosa au kwa blackmail/corruption::

1.Zitto na Dr. Slaa wanasema kuwa wao sio watendaji na walikuwa wakitoa ushauri tu kwa Tanesco kiujumla kama options na sio binded.

2.Wanakubali kuwa Tanesco inakabiliwa na uhaba wa 150MW, lakini sheria ya PPRA lazima ifuatwe to the tee na vile vile ni lazima mitambo inunuliwe mipya kwa sababu ukinunua chakavu in few years tutarudi tena kwenye issue hii hii ya 150MW deficit baada ya mitambo ya Dowans kuharibika kama inavyotarajiwa na vijana wa mjini.

3.Ngeleja na Tanesco ndio wenye maamuzi ya mwisho, na maamuzi yoyote watakayofikia bunge litayapitia kwa uangalifu mkubwa kumake sure kuwa Pesa za walipa kodi hazijatumiwa kifisadi na sheria zote za jamhuri zilizotungwa na Bunge including PPRA zimefuatwa to the tee.

4.Mambo ya kutumia kigezo cha giza kila mwaka for the last 20 yrs ni ishara tosha kuwa kuna matatizo makubwa Tanesco na shirika hili liwaambie wananchi mipango yake ya 1yr, 3 yrs, 5yrs nk ili maamuzi yafanywe kwa long term benefits na sio kukurupuka kila mwaka.


Finally usemi ufuatao utulinde kwenye huu ufisadi wa kina Rostam

Ni Heri kununua mitambo mipya ya umeme na kuteseka na giza kwa miezi michache mwaka 2009, kuliko kununua mitambo chakavu ya Dowans na kuteseka na giza kila mwaka from 2011 mitambo itakapoharibika na kutokuwa na guarantees wala warranty kutoka kwa matapeli Dowans ambao baada ya kuuza mitambo tanesco kampuni nayo inayeyuka.
 
Bob,
...tena kuna mtu hapa hapa JF alisema.......wakati ule tunajadili ile issue ya RDC........kuwa hii mitambo TUTAKUJA KUINUNUA.........na sasa inatokea..........wallahi sijui Tanzania tumeingiliwa na Kichaa gani.......damn!

hehehehe....there you go again na midoti doti yako....
 
Baada ya meneno mengi Mimi ningependa tuwe action oriented, hivi kutatua matatizo ya umeme Tanzania Sasa hivi option tulizo nazo ni Zipi?
1 za Muda Mfupi na faida zake na hasara zake
2. Za muda Mrefu na faida zake na Hasara Zake.
Eg mimi ninakumbuka issue ya umeme wa SADC, je kesho tukitumia Mguvu zetu hizo nyaya haziwezi kutandazwa toka Zambia, zikaingia katika Gridi ya Taifa, au hata toka Mchumbiji?
Je Mradi wa Stglers hauwezi kufufuliwa?
Je Mtera hilo tope haliwezi kusafishwa kama lipo kweli ikawa more efficient.
Je mradi wa rusoma unaweza kuchukua muda gani kuutekeleza etc etc.
Sasa bahati mbaya mimi sina vyanzo vyote tulivyo nazo , sasa naomba wezangu tushauriana hapa Including Zitto ambaye anaonge na Huyo Iddrisa, na Ngeleja
.Tukisha jua Hatima tulizo nazo then kesho tuanze kazi usiku na mchana tuone kama tutashindwa kutatua hilo tatizo, maana nguvu kazi tunayo iwe ni vabarua, au wanajeshi etc etc
 
Baada ya meneno mengi Mimi ningependa tuwe action oriented

Heheheheee....action what?

hivi kutatua matatizo ya umeme Tanzania Sasa hivi option tulizo nazo ni Zipi?

Option tuliyonayo ni kutengeneza mitambo na vifaa vya kuzalisha umeme sisi wenyewe. Swali, je tunao huo ubavu? Do we have what it takes? You be the judge...
 
Heheheheee....action what?



Option tuliyonayo ni kutengeneza mitambo na vifaa vya kuzalisha umeme sisi wenyewe. Swali, je tunao huo ubavu? Do we have what it takes? You be the judge...

Una maana Luhanga na Engineering yake Hawezi Kutengeneze? Basi tuwaulize wa Finnish lakini cha msingi sasa tuanze kufanya kitu
 
Una maana Luhanga na Engineering yake Hawezi Kutengeneze? Basi tuwaulize wa Finnish lakini cha msingi sasa tuanze kufanya kitu

Ahahahahahahaa...Lu Who? Puh-lease...ana ubavu wa kufanya hivyo
 
Nyani Ngabu,
Hapana mkuu kuchagua tunaongoza labda kosa ni kuchagua vinono!..toka kwenye nyama choma bila mafuta (nundu) mtu hanunui.. mke bila trailer nyuma sii mke.. basi ili mradi starehe ni ya mtu binafsi, sio maslahi ya Umma.
T. Dot umeme hukatika pia sio mara kwa mara, mwaka huu kuna siku umeme ulikatika baadhi ya sehemu tena mjini kwa masaa 12.. Ilikuwa kasheshe!

Kifupi matatizo mengi yetu sisi ni ya kujitakia, nakumbuka wakati ule wa Dorwans ktk msafara wa Lowassa nilikutana na mshikaji wangu ambaye nilimwambia kuhusiana na kununua mitambo mipya toka Kohler na nilimwambia hata mtu wa kumwona pale ili kazi ifanyike haraka..kazi yote nilikwisha ifanya kivyangu vyangu.. sikutaka nikatiwe kitu chochote lakini Unajua tena hapa hatuna personality tunaonekana wahuni tu...hivyo waliniacha kama nilivyo... ati wameikwisha pata mashine baab kubwa!..

Ebu fikiria mkuu wangu hata kufunga Generators tunatafuta middleman (tender) wakati mashirika kama GE, Siemen, Kohler, Cummin, Caterpillar na mengine mengi yanakuletea hadi mlangoni kweli unahitaji kutafuta mtu wa kati?...hawa wote wanakuja wenyewe kufunga na utapatiwa warrant na guarantee juu..tena kwa miaka..leo tunakuja na ujinga wa Dorwans kama vile hawa jamaa ni watengenezaji wa generators..Nakuhakikishia hakuna gari la kiongozi yeyote linaweza kununuliwa mtumba na toka kwa mtu binafsi... sijui kama sheria ya kutonunua mitumba ipo kwenye magari tu..
 
ngoja nikalale kicwa kinauma, zito ebu nenda pale siemens nyerere road mtafute thomas ngwandu au allan bosch(mjerumani), acha kupotoshwa na akina mafisadi wa tanesco na ngeleja

THOMAS NGWANDU, SALES CONSULTANT(ELECTRICAL ENGINEER-SIEMENS

+255754560973
 
mkandara,
Lakini ilishawahi tokea kwa ndugu zetu wa visiwani, wakati wa Salmini walinunua gari ya mtumba tena ilikuwa benzi kwa ajili ya Rais aka mwenyekiti baraza la mapinduzi . Kwa bara nafikiri sheria iko wazi ingawaje kwa sasa mambo ni rahisi kupindishwa na mafisadi
 
Kama Dowans ingekuwa contract yake haina ufisadi, tungeweza kuangalia kama tunaweza hata kuongelea uwezekano wa kudiscuss manunuzi.

Katika somo la historia shirikishi nilifundishwa kuwa IPTL ndio mama wa CONTACT ZA KIFISADI katika Tanzania ya baada ya Mwalimu....
 
Wadanganyika kwanza lazima tumjue huyu Idris Rashid ni nani katika vita yetu na hawa mafisadi.; huyu bwana ni mdau wa kampuni zote mbili anzia Richmond na sasa Dowans. Ubia wa Rashid katika kampuni hizi unapitia kwa watu wawili ambao ni partners wake kibiashara nao ni Rostam na Noni wa BOT ambao waliwekeza pamoja toka Vodacom na hata wakati fulani yeye Rashid akawa kinara wa Vodacom kwa muda mfupi!! Sasa katika biashara zao, hii mitambo yao ya Dowans wasipoiuzia Tanzania watakula hasara kibiashara kwahiyo lazima watafute kila hila waiuze hapa si kwa manufaa ya wadanganyika bali kwa kupunguza hasara zao. Sasa wanatumia hila through position ya Rashid Tanesco to create panic [fear factor] kwamba bila kuinunua hii mitambo, basi nchi itaathirika kiuchumi; kudhihilisha hilo Rashid anacreate artificial shortage ya umeme na kuanzisha load shedding as a way ya blackmail watu waamini kuwa bila kununua hii mitambo chakavu nchi haina alternative nyingine isipokuwa giza !! Hii nddio deal yao mpaka sasa wameishaiuza kwa wakina Zitto nao wameuvaa Mkenge!! Hawa mafisadi wabaya sana; Rashid kishatuibia kwenye Radar na Chenge wake leo huo uzalendo wa kutuonea huruma ameutoa wapi? Jamani tuamke huyu hatutetei sisi anatetea commission yake hapo!!

Interesting....
 
Jamani bei ya hii mitambo ya Dowans inajulikana? Tunaweza tukafanya some cost comparison labda. Post zimekua nyingi siwezi kuipata bei.
 
Wakuu mimi hapa naona bado ni changa la macho.

Mitaambo hii wakati wa mchakato wa Richmond tuliambiwa ni kutoka "Pratt and Whitney" ambayo ni kampuni ya marekani halafu leo hii tunaambiwa kwamba eti kuna the so called "mtaalamu kutoka ujerumani" ameikagua na kuona ni safi hatuambiwi huyo mtaalamu ni kutoka kampuni gani, na je kampuni hiyo inatambulika na pratt & Whitney kama insperctors???????? Na after all huyo manayeitwa mtaalamu ana uzoefu gani na shughuli za ukaguzi wa mitambo kama hiyo.? Je is the guy insured kutokana na ukaguzi wake?

Well kuna hili la guarantee!!!! Guarantor wa hiyo mika kumi ni nani? na kama ni Dowans mbona kampuni yenyewe imekaa kisanii sanii, kwani ni wapi ina shughuli zingine kama hizi?

Halafu eti tunatishwa kwamba tusiponunua nchi itaingia gizani! wht a joke?????????? si kisingizio hiki hiki EL alitumia kuhalalisha Richmond?????? Hawa jamaa wamekuwa wapi miaka yote hii toka 2006?

Pia kuna hili la kuchekesha zaidi eti kwamba Tanesco inaidai Dowans kama USD 11m, na kwamba eti tukinunua hiyo mitombo tutakatana humo humo. Huu ni utani tena utani wa masuala ya nguoni!!!!!!!! Yaani ina maana Tanesco inaogopa kumdai Dowans ambaye ana mitambo kwenye yadi ta Tanesco???????? Deni ni Deni hata Tanesco isiponunua hiyo mitambo bado Dowans anadaiwa.

Halafu juzi nimemsikia yule Mkurugenzi Idris aking'aka kwamba mitambo lazima inunuliwe na eti watu wengine wanafikiri wengine hawakwenda shule. Hv huyu jamaa anafahamu kwamba ana questionable credibility?

Hivi hawa wakulu wanatuonaje watanzania?????? Wanatuona sisi mafala sana eeh??? Wanatuona sisi ni kuku????

Pia nashindwa kumshangaa mtu nayemuheshimu Zitto kushabikia ununuzi huu. Yeye ni mwanasiasa anafahamu nini kuhusu mitambo ya umeme? These people should know kwamba huwa tunawasapoti pale wanapokuwa na facts na si kwamba we have just aligned to them. When they are wrong wanapaswa kukosolewa!!!!! Na katika hili nnaamini opinion ya Zito si sahihi!!!!!!
 
Hivi hwa Tanesco wanafahamu kwamba Catapiller wanauza mitambo(Containerized power stations) mipya ya kuweza kuzalisha 5MW each kwa bei ya USD 2.5 MILLION.

See specs below:

5 MW Caterpillar 3516 Gas Power Plant
Consists of four 1250 KW, 3516 Gas engines coupled to two 2.5 MW SR4
Alternators, Fuel: natural gas,diesel or HFO - 1500 rpm, 400 volts, 50HZ, includes control suit, silencers, Gas system and etc


Uliza quotation hapo Bongo mantrac unapata bei fasta!!

Ina maana kwa 100MW ni container 20 = USD 50m.............mitambo mipya. Kumbuka hizi ngoma ni offshelf na zinakuja kila kitu kikiwa kimeunganishwa!
 
Hii mitambo ya Dowans isije kuwa kama hii!!!!!!! - Sell The Used Generator 5MW 12units - 60MW


Features Specifications: Sell The Used Generator 5MW 12units - 60MW


We are very pleased to send you our offer for the used 5MW Generator 12 units That have operated in Seoul&Incheon Korea like as below: ---- Offer ---- Used Generator 5,000 KW x 12 units [Capacity:60MW] 1. Used Generator 5MW 6 units [made in Japan] AA. Engine Manufacturer: Fuji [Japan] Capacity:5MW Type: Diesel Engine Driven [16PC-2V 400 4cycle] Revolution:514 rpm Cylinder:16 V-type Bore/Stroke:400mm x 460mm Compression:90 kg/cm2 Exhaust GasTemperature:400~480 deg C Cooling: Cooling Tower&Water Jacket Starting: Compression Air Starting Turbo-Charger:4/unit Governer Type: Wood Ward UG-40 Fuel: B. C and Diesel Oil Fuel Consumption:0.28 L/kwh Dimension: Weight:68.5 Ton/unit Operated Hour: Less than 30,000 hrs Designed Life Hour:500,000 hrs [60 years] Built Year:1968 BB. Generator Manufacturer: Brush Electric Engine Co [UK] Type: F505/33-14 Capacity:6,250KVA x 6 units Revolution:514 rpm Wounding: Y,80% Voltage&Ampare6,600V/547 A Pole/Cycle:14P/60Hz Cooling: Air Exitor Capacity:68 kw Exitor Type: AGV-280 Exitor Voltage/Ampare:220V/223A Exitor Pole:4 P Insulation: B class Dimension:3.4m x 3.4m x 2.1m Weight:34 ton Serial No:222461A,222462A,222463A,222464A,222465A,222466A Built Year:1968 2. Used Generator 5MW 6 units [made in UK] AA. Engine Manufacturer: Mirrlees Blackstone [UK] Type: Diesel Engine Driven [16KV MAJOR 4 cycle] Capacity:5MW Revolution:514 rpm Cylinder:16 V-type Bore/Stroke:381mm x 457.2mm Compression:98.43 kg/cm2 Exhaust GasTemperature:443~471 deg C Cooling: Cooling Tower&Water Jacket Starting: Compression Air Starting Turbo-Charger:2/unit Governer Type: Wood Ward UG-40 Fuel: B. C and Diesel Oil Fuel Consumption:0.24 L/kwh Design Efficiency:39.1 % Dimension:8.4m x 2.15m x 3m Weight:73.3 Ton/unit Operated Hour: Less than 25,000 hrs Designed Life Hour:500,000 hrs [60 years] Built Year:1968 BB. Generator Manufacturer: Brush Electric Engine Co [UK] Type: S140 ~ 108 Capacity:6,250KVA x 6 units Revolution:514 rpm Wounding: Y,80% Voltage&Ampare6,600V/546 A Pole/Cycle:14P/60Hz Cooling: Air Exitor Capacity:35.3 kw Exitor Type: DKK-6134 Exitor Voltage/Ampare:127V/238A Exitor Pole:4 P Insulation: B class Dimension:3.4m x 3.4m x 2.1m Weight:34 ton Serial No:506071,506073,506075,506077,506079,5060711 Built Year:1968 3. Terms&Conditions Price: Fuji Generators [Japan]: USD 200,000 x 6 unts = 1,200,000 Spare Parts: USD 300,000 Blackstone Generator{UK]: USD 200,000 x 6 units = 1,200,000 Spare Parts: USD 300,000 ---------------------------------------------------

Total USD3,000,000

Price Condition: FOB Incheon Korea Payment: Irrevocable L/C at sight in favor of ECI Inspection: Buyer inspection final Packing: International Packing Standard Option: [1] Freight&Insurance [2] Installation&Construction for 60MW Power Station. [3] Supervision for Installation and Start-up. If you are interested in it, don't hesitate to contact us. And refer to our internet web-site for your reference ; We would like to have a deal with you for mutual favour&prosperity. I'm looking forward to hear of your response soon. Thanks&Regards.
 
Hapana. Mimi binafsi suala hili sio la lazima. Kwamba do or die. Hapana. Options zingine ziangaliwe pia au hata kutonunua kabisa Dowans bali tununue mtambo wa kuziba hii nakisi. TANESCO imekuwa despecified mwaka 2007 na hivyo kuweza kuwekeza na hata kukopa. These are facts and tuziweke facts mezani bila kuzipinda. Mjadala huu tusichukue sides. Tuelimishane na kwa sisi wawakilishi wenu Bungeni tukiona hoja hapa tunaibeba wazee. Tumefanya hivyo mara kadhaa. Tuweke hoja na tukate issues an hatimae kufikia hitimisho. Mtu mmoja adraft maazimio hapa na mwishowe tuseme, haya ni ya JF, Zitto peleka huko. Hapo JF itakuwa imesaidia Taifa. Hii kulalama lalama hapana!

Mh Zitto na Dr Slaa,

Kwanza naomba sana muachane na suala hili. Nitafurahi sana kusikia kutoka midomoni mwenu kwamba "LIWALO NA LIWE LAKINI HAKUNA KUNUNUA MITAMBO YA DOWANS". Yaani neno Dowans liondoeni midomoni mwenu na hapo ndio mtaweza kurejesha heshima zenu. Mnakoenda siko waheshimiwa.
Pili nyie mmetumwa bungeni kutusaidia sisi wananchi na siyo serikali. Kama wameshindwa kuweka mikakati madhubuti hadi wanatutangazia leo kuwa bado mwezi mmoja tuingie gizani, achana nao, mrudi huku kwetu tuanze kuwashikisha adabu. Hiyo hurumu waliyojaribu kuitafuta toka kwenu (na sasa wameshaipata) itawagharimu kiasi ambacho sasa hivi hamuwezi kuelewa.
Tatu, katika Tz kila kitu kinaanza na hisia (rejea EPA, Richmond etc). Kwa hiyo naomba sana msitudharau sisi tunaofanya mambo yetu kwa hisia. Kwa sababu huko nyumba hisia zetu zimeonekana kuwa za kweli na kwa hiyo hatuna sababu ya kutoziamini.
Nne, wananchi wengi (tena wenye mapenzi na nchi yao) hawana imani na watu wanaoshabikia hili suala. Ukianzia na Dr Idrisa, serikali kwa ujumla wake (kwa kuwa ndio wapishi wakuu wa skandali za kifisadi) na makampuni yanayozungumziwa hapa ya Dowans (ambayo kwa imani ya watu wengi ni Richmond). Kwa hiyo kujaribu kujiingiza kwenye huo ushirika ni kujichimbia kaburi siyo tu la kisiasa bali hata la heshima zenu kwenye jamii.

Mwisho naomba kama kuna uwezekano mtuwekee kumbukumbu zetu sawa kwa kututajia wamiliki wa Richmond (ambao hadi leo sijawahi kuwajua) na wale wa Dowans. Kujua wamiliki wa hizi kampuni na washirika wao itasaidia kuelewa mahusiano ya hawa watu na serikali na mwisho kutuonesha uhalali wa hili dili au jinsi tunavyoingizwa mkenge.

Hata hivyo narudia kusema kuwa potelea mbali, tukapambane na giza lakini siyo kununua mali za wezi ambazo labda ni za wizi pia.
 
Wakuu mimi hapa naona bado ni changa la macho.

Mitaambo hii wakati wa mchakato wa Richmond tuliambiwa ni kutoka "Pratt and Whitney" ambayo ni kampuni ya marekani halafu leo hii tunaambiwa kwamba eti kuna the so called "mtaalamu kutoka ujerumani" ameikagua na kuona ni safi hatuambiwi huyo mtaalamu ni kutoka kampuni gani, na je kampuni hiyo inatambulika na pratt & Whitney kama insperctors???????? Na after all huyo manayeitwa mtaalamu ana uzoefu gani na shughuli za ukaguzi wa mitambo kama hiyo.? Je is the guy insured kutokana na ukaguzi wake?

Well kuna hili la guarantee!!!! Guarantor wa hiyo mika kumi ni nani? na kama ni Dowans mbona kampuni yenyewe imekaa kisanii sanii, kwani ni wapi ina shughuli zingine kama hizi?

Halafu eti tunatishwa kwamba tusiponunua nchi itaingia gizani! wht a joke?????????? si kisingizio hiki hiki EL alitumia kuhalalisha Richmond?????? Hawa jamaa wamekuwa wapi miaka yote hii toka 2006?

Pia kuna hili la kuchekesha zaidi eti kwamba Tanesco inaidai Dowans kama USD 11m, na kwamba eti tukinunua hiyo mitombo tutakatana humo humo. Huu ni utani tena utani wa masuala ya nguoni!!!!!!!! Yaani ina maana Tanesco inaogopa kumdai Dowans ambaye ana mitambo kwenye yadi ta Tanesco???????? Deni ni Deni hata Tanesco isiponunua hiyo mitambo bado Dowans anadaiwa.

Halafu juzi nimemsikia yule Mkurugenzi Idris aking'aka kwamba mitambo lazima inunuliwe na eti watu wengine wanafikiri wengine hawakwenda shule. Hv huyu jamaa anafahamu kwamba ana questionable credibility?

Hivi hawa wakulu wanatuonaje watanzania?????? Wanatuona sisi mafala sana eeh??? Wanatuona sisi ni kuku????

Pia nashindwa kumshangaa mtu nayemuheshimu Zitto kushabikia ununuzi huu. Yeye ni mwanasiasa anafahamu nini kuhusu mitambo ya umeme? These people should know kwamba huwa tunawasapoti pale wanapokuwa na facts na si kwamba we have just aligned to them. When they are wrong wanapaswa kukosolewa!!!!! Na katika hili nnaamini opinion ya Zito si sahihi!!!!!!


Hapa tupo ukurasa mmoja mkuu!
Kwani haingii akilini kwamba tununue mitambo ya mtu aliye tushitaki, tena tuliye zuilia mitambo yake kwa misingi kwamba ni halali yetu kuitafisha!

Sijui mh. Zito anasemaje kuhusu hilo kwamba tununueje kitu ambacho ni halali yetu kukitaifisha? Afu kesi iko mahakamani ya tugombeacho wewe unataka tununue kidhibiti/ushahidi? sasa hapo kesi itakuwa juu ya nini tena?

Heri giza kuliko kumuhonga mwizi wetu mamilioni mengine!
 
Ochu, heshima mbele mkuu

Asante kwa analysis yako but with due respect I have to differ with your opinion.

Kama sheria ya Tanzania ndio imeanishwa kutumika katika huo mkataba basi uchambuzi wa sheria hapo juu waweza kuchukua mkondo wake.

Lakini, as i can feel it, this was a kind of International Business Transaction na inanifanya nichelee kukubaliana na wewe kuhusu hizo principles ulizoweka hapo juu unless umeona mkataba unasimamiwa na sheria ya nchi gani au kanuni zipi; yote yanawezekana, unaweza kuta Tanzania courts do not have jurisdiction on the matter na kwamba ikitokea kukiwa na msuguano wa mkataba, labda Iternational Arbitration will take over mfano mzuri ni Kesi ya IPTL na TANESCO ambayo ilifanyika hapa marekani.

Deal kubwa kama hiyo, I am sure jamaa watakuwa wameweka kifungu kinachoonyesha sheria ya nchi gani itatumika au vitu kama Incoterms au UCP.

Kwa hiyo tukiupata huo mkataba itakuwa vema na rahisi kuuchambua otherwise we are just dealing with some kind of speculation.

**************

Inavyoonekana Mawakala wa mafisdadi hawakosekani. Wako kila mahali, watajaribu kuweka uhalali katika kila haramu, wataliita giza kuwa mwanga, watachimbua kila sheria, watachunguza kila kipengele, kanuni, taratibu -- watatembea kila urefu wa kilometre hapa duniani na hata ahera ili tu watafute kisingizio cha kuwaibia Watanzania masikini.
INAONEKANA KAMA VILE HAKUNA SERIKALI HAPA KUZUIA HII. SERIKALI INAYO KILA HAKI KUSTOP -- KWANI LAZIMA??? WANANCHI TUSIKUBALI MAFISADI WATUZIDI KETE, TUSIKUBALI KABISAAAAAAAAAAA!

hakuna nchi au mahakama yeyote duniani inayoweza kupokea kesi ya kampuni ambayo haijulikani kisheria... pia fraud and misrepresentation for the sake of justice nowhere it can stand.
 
Majuzi nilimsikia Dr. Mwakyembe akizungumza katika TBC kuwa Tanesco wasinunue mitambo ya Dowans. Hoja yake kuu ni kuwa wakinunua mitambo ya Dowans watakuwa wamekiuka taratibu za ununuzi. Hakutoa sababu nyingine yeyote ya kiuchumi.

Leo nimeskiliza Mh. Zitto Kabwe katika TBC hiyo hiyo. Yeye ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo kwa sababu kuu tano za kiuchumi na kiutendaji:-

1. Mitambo hiyo ipo nchini na inazalisha umeme bila matatizo. Pia moja ya mtambo huo ni mpya kabisa.
2. Tanesco inaendeshwa kwa hasara kutokana na high capacity charges. Zaidi ya 80% ya mapato yake hutumika kununulia umeme toka kwa wazalishaji binafsi unaofikia 42% tu ya umeme wote unao gawiwa.
3. Hivi sasa Tanesco inaendeshwa kwa hasara. Ununuzi wa mitambo hiyo pamoja na mingine ya IPTL etc utaisadia Tanesco kuendeshwa kwa faida. Serikali/Tanesco imo katika mazungumzo na wazalishaji wote hao binafsi. Kwa hiyo, inaonyesha kuwa, zoezi hilo si la Dowans peke yake bali ndio sera ya serikali/Taneso hivi sasa.
4. Mitambo hiyo ikinunuliwa sasa itaepusha sokomoko la mgao wa umume baadae mwaka huu.
5. Katika sheria za manunuzi kuna kipengele cha waiver ikiwa kuna umuhimu wa kununua mitambo ambayo si mipya.

Sasa mimi najiuliza:-
1. Hivi kung'ang'nia kikataza Tanesco kununua mitambo hiyo kwa sababu tu ya kukiuka taratibu ambapo Mr. Zitto kisha eleza hapo kuwa kuna uwezekano wa waiver, ni kwa maslahi ya nchi au ni kwa maslahi ya kulinda heshima za kisiasa? Yaani kuonekana tu kama kichwa cha thread hii kuwa Dowans wataonekana wameshinda?
2. Surely katika jambo nyeti kama hili ni lazima mtu atoe hoja nzito za kiuchumi, kama alivyotoa Mr. Zitto. Sasa kweli hoja moja tu ya kukiuka taratibu ndio inatosha kuzuia project ya muhimu kwa taifa kama hii?

Jamani lazima tuwe serious. Tuachane na ubinafsi, chuki na kujijenga kisiasa na tuzingatie zaidi maslahi ya taifa na huduma kwa umma. I for one, hakuna kitu kinacho nikera na kunikasirisha kama kukatika kwa umeme.
 
Back
Top Bottom