Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Zitto Ameomba msamaha kwa maneno yake makali aliyotoa, nadhani asamehewe 7X70

Mheshimiwa Zito, Maelezo yako kuhusu hali halisi ni mazuri sana na yanatia moyo, LAKINI baada ya hapo umetamka maneno makali sana. Dr. Slaa amewekwa kitimoto sana kama ulivyokiri hata wewe, lakini amejibu hoja kwa busara ya hali ya juu sana.

I am sure if you will go back and read what you wrote, you may not believe it yourself!!

Hata hivyo your apology is highly appreciated,

Kumbuka pia dokta mkubwa na ukubwa dawa.............
 
Halafu Mh. Zitto, mtiririko wa maamuzi ya maana inabidi uwe hivi:::

Tanesco imeona kuna upungufu wa 150MW
Tanesco itabidi inunue generator za MW 150
Generator hizo kwa sheria ya PPRA inabidi ziwe mpya
Tanesco itajaribu kuwasiliana na makampuni yanayotengeneza hizo generator ili tuweze kuzipata haraka na kwa bei nzuri

Na sio, unavyotulazimisha wewe yaani

Dowans wanataka kuuza generator zao kwa mabwege
Tanesco lazima inunue generator za Dowans
Sababu za kununua ni kuna upungufu wa 150MW
Mbona hata za IPTL zinataka kununuliwa??

Yaani hapo mkuu ndio umetuchosha kabisa kwa sababu lazima wewe mjanja kama sisi unayaona haya na ukiamua kutoyaona ndio yale maswala ya blackmail and/or corruption yanapokuja.

May god Bless Tanzania
 
MOELEX!nadhani mh ZITTO amekusoma.amekuelewa zaidi.UMEONGEA KITAALAMU ZAIDI,wakati yeye ameongea KISIASA ZAIDI
 
Zitto,
Nafahamu kuwa wewe si mwanasheria, lakini kuna watu wameandika hapa kuwa kutokana na ubatili wa mkataba tangu mwanzo, serikali inaweza kutaifisha mitambo hiyo. Natumaini hutaupuuza ushauri wa watu hao!
 
Disclaimer:: Just got back its around midnight my time with few drinks kichwani, but all in all: Lets go

Mh. Zitto, I was the one who made serious allegations of blackmail and/or corruption from Mtandao to U guys on this dowans issue. I'm not offended with ur reply though U used some slick words, but since I dished first, its all good.

Now, U are talking about serious problems within Tanesco, which we all agree but the cause of the problems are contracts that were signed in the same way U guys want to do with Dowans. Let us say Tanesco wants 200MW, so the solution is to buy 200MW generators from source companies ie GE or Wartsila right?? Here we all agree no middleman, and with the current financial crisis GE and Wartsila have very good prices, Google what other countries are doing. Unasema Tanesco wanalipa 84% ya mapato kwa kampuni zinazozalisha 42%, sasa tukinunua generators za Dowans, hiyo ratio itapungua?? No, kwa sababu haziingiliani ila ni maneno tu mnatumia kuchanganya wananchi wa vijijini, 84% blah blah, kwa hiyo on top of all those cash flow problems, solution ni kuongeza matumizi mapya ya $80 million to dowans kwenye mitambo chakavu?? Only in TZ.

Why do U insist on Dowans?? We all agree we need generators, but we want the generators from source companies where we will have warranties and other guarantees and a competitive price in this financial climate we are in.

Tanesco signed a bad deal with Songas, and Songas bought their generators from GE, Why don't we go to GE direct??? Mbona hao majambazi tukiwapa contracts wanakimbilia GE au Wartsila??? IPTL went to wartsila and Songas went to GE. This is our issue.

Now, U buy generators from Dowans, a company that does not generate electricity anywhere in this world, sasa baada ya manunuzi ikitokea tatizo na hizo generators tutaenda wapi mkuu?? Mbona Zitto tunakuamini sana lakini hapa unaact kama Viongozi wetu maboga??

Halafu unathubutu kusema eti mbona serikali inataka kununua mitambo ya IPTL, so vilevile tununue mitambo ya DOwans?? Really Zitto?? Unaona IPTL na Dowans ni sawa sawa?? IPTL tuko kwenye contract kuwalipa capacity charges kubwa mpaka 2018 I believe, so if tukinunua mitambo itasave money, WE ARE ALL UP FOR IT, sababu tutasave in the long run and it will cut down that 84% ratio U were talking about, which will improve Tanesco Cashflow situation. Sasa dowans, hatuna nao contract, kwa nini tununue mitambo yao?? PPRA ina maana gani??? Kwa hiyo msitake kuchanganya wananchi wetu huko vijijini kwa maneno mengi.

Ahsante mkuu, na I hope umeona kwa nini tunaissue na Dowans. U will do ur country a big service kama utatumia letterhead ya kamati kuandika barua GE and Wartsila kuulizia info tu ya NEW 100MW generators availability to Tanzania and at what price, then utaongea kama kijana mjanja na sio eti MD wa Tanesco kasema hivi na vile wakati unajua kabisa Chenge, Rostam, Karamagi, Lowassa wanashirikiana na huyo fisadi hapo Tanesco na Lowassa ndie alimweka hapo.

Dowans generators kwa habari za ndani zinaworth about $15 million, so sababu tunawadai $10milion, TUTAKUBALI KUNUNUA HIZO GENERATORS kwa $5million.

Kama hawataki, Powa tu maana hamna mtu yeyote dunia hii anayetaka kununua hizo generators, na mwisho wa siku Tanesco wakiwa wajanja na kusubiri, Dowans watatupa hizo generators bure maana hamna wanakoweza kupeleka.

Swali la mwisho::: Zitto hao Dowans unajua wanafanya kazi ya umeme sehemu gani dunia hii, ili wana JF walioko kona zote watembelee ofisi zao popote duniani tuone ufanisi wao???

Kamati yangu haijalazimisha Dowans hata kidogo. Mjadala huu ndio umejikita huko. Maelezo yako ni mazuri na tuendelee na mjadala. Kuna maeneo haupo sahihi sana kwani unahitaji maelezo zaidi. Nilisema katika moja ya vikao vya kamati kuwa, ingekuwa wakati wa Mwalimu suala hili lingekuwa rahisi sana kwani tungetaifisha tu. Kwa sasa neno taifisha linaonekana sio zuri masikioni mwa 'investors' lakini ndivyo ingepaswa. Kamati yangu haikujikita hata kidogo kwa Dowans. Hiyo ni option mojawapo ambayo TANESCO wameitoa. Kamati ilijadili options kadhaa

- Kufast track Kinyerezi project (240MW)
- Kufast track Umeme wa Upepo Singida (50MW)
- Kuokoa Umeme wa Mtwara (300MW)

Na haya ndio masuala tulioomba kamati mbili zikutane na kujadili kwa pamoja na kuona ipi itaokoa mambo kwa haraka.

TANESCO wametaka kuongeza uwezo wao wa kuzalisha umeme hizo 100MW kwa haraka kwani tayari mitambo hiyo imeunganishwa katika gridi. Mitambo mipya kutoka GE etc tulijadili kuambiwa kuwa ni sawa lakini itachukua muda mrefu sana mpaka kufungwa na kwamba wanataka kuchukua mtabo wa 60MW kuupeleka Mwanza ili kukabili tatizo lililopo kule sasa hivi. Hivyo suluhisho la muda mrefu ni lazima liwepo na hapo ndio umuhimu wa kikao cha kamati mbili.

Ni muhimu tukumbuke kuwa kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita TANESCO lilikuwa specified company (shirika linalosubiri kubinafsishwa). Hivyo hapakuwa na uwekezaji wowote uliiofanywa. Hivyo sehemu kubwa ya matatizo tunayoyapata sasa yanatokana na maamuzi yetu kama nchi ya kisera.

Kuhusiana na IPTL. Mimi silinganishi bali ninaonesha kuwa kigezo cha sheria ya manunuzi (ambayo haitajwi ni kifungu gani hapa) itakwamisha pia mpango wa kununua IPTL na kuigeuza kuwa gesi. Ninaamini Two wrongs never make it a right. Kununua IPTL kutazuiwa na sheria hii ya manunuzi ijapokuwa uamuzi huo wa kununua mitambo chakavu itasaidia sana TANESCO kutatua tatizo lake la cash flow (tutaokoa $9m altogether kila mwezi kwa uamuzi huo wa kununua IPTL na kugeuza mitambo kuwa ya gesi).

Suala la nishati ya Umeme, kwa mwono wangu, ni suala linalohitaji mjadala uliotulia na wenye kuona picha kubwa (broader picture). Ndio maana Kamati yangu iliamua ilivyoamua.
 
"Suala kubwa ni ununuzi wa mitambo ya wezi au kama mitambo hiyo inafaa au haifai?" - Zitto.

Today I have heard the unexpected from this "fighter"!God bless Tanzania.

Nimeuliza ili kuweka mjadala mahala pake maana niliona unachukua sura ambayo haitatusaidia hapa. Nadhani mjadala wa hapa JF ni wa hatimae kuona maeneo tunayokubaliana na hivyo rhetorics hazitusaidii.
 
Hadi mtatoana ngeu! Nunueni mitambo ya Dowans, mwachilieni Gire.. yaishe! tuangalie mengine.

Kama hili linaendana? Gire kashtakiwa na Jamhuri kwa makosa yanayotokana na kampuni ya Richmond. Suala mbele yetu ni mitambo ya kuzalisha 100MW. Nadhani tusikate tamaa mapema ndugu yangu. Tujadiliane. Mwalimu alikuwa anasema, waafrika tulikuwa na utamaduni wa kukaa chini ya mti na kujadiliana wee mpaka mwafaka ukafikiwa. Ninaamini hapa sio ubishani wa kutafuta mshindi bali ni mjadala wa kutufikisha kwneye mapendekezo mwafaka. Tusiwe reactioneries, tuwe proactive.
 
Mkuu Zitto, waiver ya IPTL itakuwa sio issue kwa sababu itaokoa pesa ambazo tayari tuko liable kuzilipa kutokana na contract, hapo hamna issue.

Kama Dowans ingekuwa contract yake haina ufisadi, tungeweza kuangalia kama tunaweza hata kuongelea uwezekano wa kudiscuss manunuzi.

Lakini mkuu tunajua real owners wa Dowans ni real owners wa richmond, so tutakuwa vichaa hata kuongea nao. Kumbuka hao dowans mkataba wao ulivunjwa na Tanesco. kwa nini ulivunjwa?? Sasa leo tena mnasema kuna uwezekano wa kudeal nao hao watu. NO WAY, DOWANS NI NON STARTER, na kama ni giza tuingie gizani hamna haja ya kutisha watu sababu IPTL< SONGAS<RICHMOND contract zote zilisainiwa kwa kisingizio hicho hicho cha giza.

Halafu Zitto naomba uwe careful sana, sababu sio kazi ya Bunge kujikita kwenye uendeshaji wa makampuni, nyie ni wasimamizi lakini wenzako wanakutega kwenye hii issue unaonekana wewe ndio unangangania hii issue ya Dowans, ingawaje mimi mwenyewe moyoni najua mambo ya kifisadi huna, lakini angle hii sababu wewe ni mwanasiasa inabidi uangalie angle zote mkuu.

Kwa hio Mh. Zitto, mambo ya DOWANS hata usiyatamke mdomoni mwako, waachie Tanesco wewe zungumzia hayo mambo sijui windmill, solar, Coal blah blah lakini DOWANS Mkuu, kama member wa JF na mwenzetu achana nalo, kama hujui vizuri wenzako wengi humu ndani wanajua kinachoendelea kwa hiyo mkuu achana na Dowans. Utaona kuanzia week ijayo vyombo vyote vya habari vitasema Zitto aikubali Dowans, Dowans ni safi per Zitto blah blah. Hiyo Cliff Mh. Zitto ni kubwa mno na wengi humu ndani tunakutegemea mno kwa mambo mengi ya kulinusuru taifa, so hatutaki kuona unabebeshwa huu mzigo bila sababu kwa ujanja wa hawa watu wachache wanaoliibia taifa.
 
Zitto, mimi nakuelewa sana lakini hili la Dowans linashughulikiwa kwa namna ya kushangaza sana. Langu ni moja tu. Nasema tununue mitambo itakayofaa kutupatia umeme tunaohitaji. Katika kufanya hivyo tusivunje sheria.

Maana yake:

a. Tenda itangazwe upya Dowans kama makampuni mengine ishindane fair and square.

b. Endapo baada ya tenda bado Dowans wakabakia miongoni mwa makampuni na wakawa kweli wanatupa kitu value for our money well and good.

c. Nje ya hapo tutatatua tatizo moja (la kukosa umeme) kwa kutengeneza tatizo jingine (la uvunjaji sheria, upendeleo, and unfair advantage!).

d. Kama itatokea kampuni nyingine ambayo inaweza kutimiza masharti yale ya tenda basi hiyo kampuni ipewe jukumu hilo.


Lakini jingine (well ninayo mawili) ni kuwa Dowans ambayo tunataka kununua mitambo yake ni kampuni ya nchi gani, na iliingiaje Tanzania?

Na la tatu (pardon me), ni kuwa why Dowans? NI mitambo ya aina gani waliyonayo dowans ambayo tukitaka kununua aidha toka kwa watengenezaji itatugharimu mara mbili ya madalali? (tukimuamini Ngeleja?). Naomba utupe specification ya hayo majenereta ya Dowans ambayo hatuwezi kuyapata sehemu nyingine yoyote duniani kwa bei inayolingana na Dowans au chini ya hiyo?
 
Halafu Mh. Zitto, mtiririko wa maamuzi ya maana inabidi uwe hivi:::

Tanesco imeona kuna upungufu wa 150MW
Tanesco itabidi inunue generator za MW 150
Generator hizo kwa sheria ya PPRA inabidi ziwe mpya
Tanesco itajaribu kuwasiliana na makampuni yanayotengeneza hizo generator ili tuweze kuzipata haraka na kwa bei nzuri

Na sio, unavyotulazimisha wewe yaani

Dowans wanataka kuuza generator zao kwa mabwege
Tanesco lazima inunue generator za Dowans
Sababu za kununua ni kuna upungufu wa 150MW
Mbona hata za IPTL zinataka kununuliwa??

Yaani hapo mkuu ndio umetuchosha kabisa kwa sababu lazima wewe mjanja kama sisi unayaona haya na ukiamua kutoyaona ndio yale maswala ya blackmail and/or corruption yanapokuja.

May god Bless Tanzania

Nimelazimisha wapi? Hakuna sehemu yeyote ambayo mimi nimelazimisha chochote na wala siwezi kufanya hivyo maana sio mamlaka yangu. Mimi nimeomba kikao cha pamoja cha kamati mbili (yenu - Nishati na Madini na yetu - Public Investments) ili kujadiliana na kupata mwafaka juu ya ushauri wa kutoa. Naomba isipotoshwe kabisa kuwa ninalazimisha chochote hapa.
 
Zitto, mimi nakuelewa sana lakini hili la Dowans linashughulikiwa kwa namna ya kushangaza sana. Langu ni moja tu. Nasema tununue mitambo itakayofaa kutupatia umeme tunaohitaji. Katika kufanya hivyo tusivunje sheria.

Maana yake:

a. Tenda itangazwe upya Dowans kama makampuni mengine ishindane fair and square.

b. Endapo baada ya tenda bado Dowans wakabakia miongoni mwa makampuni na wakawa kweli wanatupa kitu value for our money well and good.

c. Nje ya hapo tutatatua tatizo moja (la kukosa umeme) kwa kutengeneza tatizo jingine (la uvunjaji sheria, upendeleo, and unfair advantage!).

d. Kama itatokea kampuni nyingine ambayo inaweza kutimiza masharti yale ya tenda basi hiyo kampuni ipewe jukumu hilo.

Ndivyo nilivyoshauri kwa mujibu wa kanuni za Bunge. Kamati ya Nishati na Madini ilipokutana na Serikali haikutoa mbadala. Walikasirika na kusema hatutaki na kuondoka zao. Sisi tunasema hapana. Ninyi TANESCO njooni mueleze kamati hizi mbili, ile ya kisera na ile ya oversight. Kisha tunatoa alternative. Hivi ulivyoandika ndio fikra za kamati yangu. Busara ilitutuma kutotoa ushauri bila wenzetu kuwa on the loop. Hili lipo katika maandishi na ninaamini ipo siku litakuwa ni public domain.
 
Nimelazimisha wapi? Hakuna sehemu yeyote ambayo mimi nimelazimisha chochote na wala siwezi kufanya hivyo maana sio mamlaka yangu. Mimi nimeomba kikao cha pamoja cha kamati mbili (yenu - Nishati na Madini na yetu - Public Investments) ili kujadiliana na kupata mwafaka juu ya ushauri wa kutoa. Naomba isipotoshwe kabisa kuwa ninalazimisha chochote hapa.


Mh. Zitto, sasa naamini kabisa kuwa U are not seeing the whole picture and U are being naive. U are talking as if, this is so serious and Tanesco is trying to save wananchi from giza, Come on Mh. Zitto!!

Let me give U final warning:: U are just a pawn on a big chess move being played by Rostam/Lowassa using everyone U think is trying to help Tanesco. They can care less, everyone Idris, Ngeleja, Serukamba, Malima and all of them are just pieces to be used to help Rostam/Lowassa from massive losses if Tanesco does not buy those generators. U are being pawned my friend in this big disaster and as we speak it will be very hard for U to recover in the eyes of Tanzanians, kumbuka siasa hamna haja ya ukweli ni vijimambo tu na utaona from next week ukiendelea na huo msimamo wako wa kamati kukutana ( sijui umetoa wapi hiyo gear ya kamati kukutana, nyie kama kina nani??? ili iweje mkikubaliana, msipokubaliana inahusu nini nyie ni wabunge). Sasa ebu fikiria serikali ikiboronga baada ya kununua hiyo mitambo, bunge litawekwa mahali gani?? Si unataka kuuza bunge na vyama vyote vya siasa kwenye hili?? For what???

Zitto wake up and stop, u are just about to fall into the cliff.

goodluck and all the best. I'm out
 
Halafu Zitto naomba uwe careful sana, sababu sio kazi ya Bunge kujikita kwenye uendeshaji wa makampuni, nyie ni wasimamizi lakini wenzako wanakutega kwenye hii issue unaonekana wewe ndio unangangania hii issue ya Dowans, ingawaje mimi mwenyewe moyoni najua mambo ya kifisadi huna, lakini angle hii sababu wewe ni mwanasiasa inabidi uangalie angle zote mkuu.

Ushauri wako mzuri sana na nimeuchukua. Kuwa careful ni muhimu sana. Kuwa real na kuconfront existing problems ni muhimu zaidi. Tatizo tulilonalo ni kwamba hivi sasa nchi imekuwa polarised (kama ni sahihi neno hilo). Huwezi kuwa na hoja na watu wasikupe kundi. Hili ndio ninalolipnga kwa nguvu zote. Ni lazima watu wawe huru kufikiri na kusema bila kupewa makundi (and U did it).

As i said before, on IPTL it was a matter of exemplifying cases of waiver etc maana watu wanaona sheria ya manunuzi kama msahafu tena bila kutaja kipengele.
 
Ndivyo nilivyoshauri kwa mujibu wa kanuni za Bunge. Kamati ya Nishati na Madini ilipokutana na Serikali haikutoa mbadala. Walikasirika na kusema hatutaki na kuondoka zao. Sisi tunasema hapana. Ninyi TANESCO njooni mueleze kamati hizi mbili, ile ya kisera na ile ya oversight. Kisha tunatoa alternative. Hivi ulivyoandika ndio fikra za kamati yangu. Busara ilitutuma kutotoa ushauri bila wenzetu kuwa on the loop. Hili lipo katika maandishi na ninaamini ipo siku litakuwa ni public domain.

Lakini hili hata halikuhitaji kamati yenu kulishauri! NI jambo ambalo Ngeleja au mtu yeyote Tanesco angeweza kuliona. Tatizo linakuja pale tunapoambiwa kuwa "aidha tununue ya Dowans au tuingie gizani!" Hii inaitwa the "fallacy of false dilemma". Kwamba kuna uchaguzi wa vitu viwili tu aidha Mitambo ya Dowans au Giza.

Kinachosikitisha ni kuwa serikali imeamini fallacy hii to the point kwamba hawazungumzii other alternatives. Ibara ya 58:1 na 2 ya PPRA iko wazi kuhusu manunuzi ya umma kwa njia ya tenda. Tukiamua kufanya nje ya tenda ndiyo mgongano ulipo lakini tukifuata sheria basi kifungu cha pili lazima kizingatiwe.

Lakini pia ibara ya 72 nayo lazima izingatiwe.

Kama kweli upo ulazima wa kuinunua mitambo ya Dowans na siyo mtu mwingine au toka mahali pengine popote hata kama ni bei ya chini basi sheria ya manunuzi ifuatwe. Kama hili hawaliwezi basi wanunue tu yaishe. That is my point. Kwa sababu hili la Dowans haliwezi kutufanya tuendelee kupiga kambi kwenye hizi kashfa mwaka wa tatu sasa.
 
Zitto,
Kutokana na mabandiko yako ina maana unapigia chepuo haya magenereta. i have got some questions to you.

Baada ya bunge kutoa mapendekezo serikali iliunda kamati tena kuangalia utelekezaji wa yale maazimio. Kwa mtazamo wako je? utekelezaji wake umeekwenda kwa asilimia ngapi. just guess tu sitaki upatie. Huoni kama yangekuwa yametekelezwa ingekuwa ni rahisi kwa wananchi na hata wewe kuridhia kuwa tuyanunue hata kwa mkopo?

Unajua watz wengi including myself ni/tuna mchukia sana sana sana Rostam Aziz? amekuwa chanzo cha matatizo yote hapa tz mimi niko zangu huku kijijini kasulu wala sitaki kumsikia kwa gharama zozote. Unaleta na hili tena? unamjua mmliki wa Dowarns?

Hivi unajua wakati wa kushusha bei za mafuta washikaji wote walikuwa tayari kutembea kutoka tegeta kwenda kwenye vibarua vyao posta kwa miguu kuunga mkono EWURA? Lije hili la Dowarns? tena mpaka mwezi wa nne? Tutajipanga tu kuliko? Nito tayari kuunga mkono hata kundamana kama yangekuwa hayo.

Hivi unajua akina mkwawa walikataa kukamatwa wakaamua kujiua? Huu ndo utaifa tunaouhitaji sio wa kuogopa mvua......... Pia kuna ile mikataba ya kiwira mbona hujaingumzia katika mipango yako ya tanesco? huoni kama pia ni tatizo hililopelekea tanescon kwenye 84%?

Mwisho, Zitto hulka yako haitofautiani sana na yangu lakini kwa kuwa umeshaamua kuwa mwanasiasa, plz kutugombeza na kutujudge sio mtaji hata kidogo. Nimeona hili muda mrefu pale watu wanapotofautiana na wewe. Pls sisi ndo mtaji wako. Tunakupenda sana ila chota hekima hii. Kuwa mstahimilivu na jua kuwa nchi hii inamatatizo mengi na we don need to hear Rostam anymore.

Tatizo na ufisadi wa nchi hii ni Rostam na sitaki kusikia amepewa hata penny
 
zitto,
kutokana na mabandiko yako ina maana unapigia chepuo haya magenereta. I have got some questions to you.

Baada ya bunge kutoa mapendekezo serikali iliunda kamati tena kuangalia utelekezaji wa yale maazimio. Kwa mtazamo wako je? Utekelezaji wake umeekwenda kwa asilimia ngapi. Just guess tu sitaki upatie. Huoni kama yangekuwa yametekelezwa ingekuwa ni rahisi kwa wananchi na hata wewe kuridhia kuwa tuyanunue hata kwa mkopo?

Unajua watz wengi including myself ni/tuna mchukia sana sana sana rostam aziz? Amekuwa chanzo cha matatizo yote hapa tz mimi niko zangu huku kijijini kasulu wala sitaki kumsikia kwa gharama zozote. Unaleta na hili tena? Unamjua mmliki wa dowarns?

Hivi unajua wakati wa kushusha bei za mafuta washikaji wote walikuwa tayari kutembea kutoka tegeta kwenda kwenye vibarua vyao posta kwa miguu kuunga mkono ewura? Lije hili la dowarns? Tena mpaka mwezi wa nne? Tutajipanga tu kuliko? Nito tayari kuunga mkono hata kundamana kama yangekuwa hayo.

Hivi unajua akina mkwawa walikataa kukamatwa wakaamua kujiua? Huu ndo utaifa tunaouhitaji sio wa kuogopa mvua......... Pia kuna ile mikataba ya kiwira mbona hujaingumzia katika mipango yako ya tanesco? Huoni kama pia ni tatizo hililopelekea tanescon kwenye 84%?

Mwisho, zitto hulka yako haitofautiani sana na yangu lakini kwa kuwa umeshaamua kuwa mwanasiasa, plz kutugombeza na kutujudge sio mtaji hata kidogo. Nimeona hili muda mrefu pale watu wanapotofautiana na wewe. Pls sisi ndo mtaji wako. Tunakupenda sana ila chota hekima hii. Kuwa mstahimilivu na jua kuwa nchi hii inamatatizo mengi na we don need to hear rostam anymore.

Tatizo na ufisadi wa nchi hii ni rostam na sitaki kusikia amepewa hata penny


MImi naona kama huyu kijana sasa amejaa kiburi cha ajabu kabisa.

Kwa kweli si bure analake jambo. Anaulizwa swali, hivi hao downs unawajua? Wanatoka nchi gani? Anajizungusha tu ooh kamati mbili zikutane, ili iweje? Anataka amushinikize shelukindo abadili msimamo. Harafu unajua binafsi ya mh ZITO mabandiko yake kwenye hii mada yanachefua sana.

Hivi zito hujui kama umaarufu wako umetokana na kutetea misimamo flani.?

Sasa utakataa kwamba umaarufu wako utaisha kwa kutetea msimamo huu usiofaa na wa ajabu

Au mwenzetu umeshajiunga nao unataka uwaziri sasa.

Hivi wewe unamkumbuka dr kaburou. Kiko wapi sasa hata ujiji anaogopa kurudi. Chunga sana kijana, sisi ndio tunakupigia debe mtaani lakini kwa hili tunajifanya kama hatujasikia, ingawa ikifika siku tutasema kwa sauti kabisa kwmba sasa huyu kijana si mwenzetu tena, kisha kuwa mwana mtandao. Downs itakumaliza sasa hivi.

Swali. Kama nakumbuka mitambo ya downs imeshikiliwa na Tanescco ili iwe fidia pindi Downs wakishindwa kesi waliyoifungua dhidi ya Tanesco, sasa hili swala la kuinunua tena hii mitambo linatoka wapi? Kesi imeisha?
 
Ushauri wako mzuri sana na nimeuchukua. Kuwa careful ni muhimu sana. Kuwa real na kuconfront existing problems ni muhimu zaidi. Tatizo tulilonalo ni kwamba hivi sasa nchi imekuwa polarised (kama ni sahihi neno hilo). Huwezi kuwa na hoja na watu wasikupe kundi. Hili ndio ninalolipnga kwa nguvu zote. Ni lazima watu wawe huru kufikiri na kusema bila kupewa makundi (and U did it).
As i said before, on IPTL it was a matter of exemplifying cases of waiver etc maana watu wanaona sheria ya manunuzi kama msahafu tena bila kutaja kipengele.
Hiyo paragraph ya mwisho mkuu,nimeshindwa kukupata!!Sheria ya manunuzi si msahafu,kweli.Lakini je,ndo tumeanza utaratibu wa kuvunja/kupindisha sheria zetu ili tu zikidhi matakwa fulani??Kwakuwa tu leo hii tunataka kununua mitambo used ya Dowans ndipo tusahau kuwa kuna sheria zinazotuongoza katika manunuzi??Hii ikiendelea tutajikuta tukisema kuwa sheria zote kwa ujumla wake sio misahafu,so where could there be the Rule of Law???
Jambo zuri nadhani ni kufanya analysis kwenye hii sheria ya manunuzi,pale penye mapungufu basi tuparekebishe kwa manufaa ya leo na kesho.Tukiendekeza hili la sheria si msahafu hapatakuwa hata na mmoja tunayeweza kumshtaki kwa kuvunja sheria.
 
Nik kweli kwenye taarifa za saa 2 usiku huko nyumbani Waziri Ngeleja amesema serikali wameiamuru Tanesco kutoshiriki kwenye zabuni ya ununuzi wa mitambo hiyo kufuatia ushauri wa kamati ya bunge.

Nadhani uamuzi wa awali ulichochewa na ushawishi wa watu fulani ambao wanaaminika kuimiliki Dowans; bila shaka ni mzimu wa Richmond bado unaiandama serikali.
Hebu angalia 'waliofinance' kampeni za ccm kwa vipindi tofauti vya uchaguzi mkuu:
1995- Robert Mugabe (Kafilisika)
2000- EPA and Rostam Aziz
2005- EPA (mtoji emeumbuka "akafa") RA, EL and NK(Bado wanadunda)
2010- nani wa kupigiwa magoti, na atabembelezwaje?
 
Back
Top Bottom