Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Hiyo lugha sio yetu , kinachoshangaza upo busy kumkosoa mtu kwa lugha ambayo sio asilia yake.
Usomi sio kujua kiingereza.
Tazama china, tazama India, Pakistan, Japan ENGLISH wanayoiongea ni mbovu sana ila.....
Utetezi sampuli hii kama yako huwa inanishangaza sana.Aisee!
 
Waafrika tulio wengi bado tuna ukoloni mamboleo vichwani mwetu.

Wengi wanaamini kiingereza ni kipimo cha ustaarabu na kuwa na akili.

Kiswahili tunakichukulia kama lugha ya kuombea chenji sokoni au kupiga majungu vijiweni.

Ni ugonjwa wa kisaikolojia wa kutaka kuonekana msomi kwa lugha ya mkoloni huku ukiwa kilaza wa lugha yako mama.
swali ni je kwa nini aongee lugha ambazo haiwezi?
 
Kwani kalazimishwa kuongea kingereza, kama hajui si atafute mkalimani kuliko kuongea madudu.
Hata ingekuwa ni sehemu ya lazima yeye kuongea kiingereza bado watu wangecheka tu, ndio utamaduni tuliyojijengea. Kiswahili kibovu akiongea mzungu au muhindi huwa hatuna muda wa kucheka tunasikiliza ili kumuelewa na sio kutaka aongee kiswahili kizuri ila linapokuja suala la sisi kuongea kiingereza hapo ndipo ufasaha wa lugha unapozingatiwa.
 
Ujue hili tatizo ni la watanzania wote sio Makonda tu.

Tunaweza tukawa sahihi kwa kuwakosoa hawa viongozi hapa na pale, lakini tatizo linaishaje?

Nina uhakika mleta mada naye akipewa nafasi ya kujieleza kwa kiingereza ataboronga.
Hilo mbona liko wazi kabisa, wengi wanafikiri wabongo tungepaswa kuwa na uwezo mzuri wa kuongea kiingereza et kisa tu shuleni tunafundishwa kwa kiingereza.
 
Hii hoja haina nguvu kabisa.

Mtanzania wa kawaida aliyehitimu chuo kikuu anakuwa amesoma kiingereza kwa miaka 9(4 O level, 2 A level, 3 degree).

Ubovu wa taasisi za elimu ndo mzizi wa hili tatizo.

Kiingereza ni lugha kuu ya kibiashara ya dunia, nchi masikini kama yetu itawezaje kuzalisha wafanyakazi bora na kuchangia kwenye mijadala migumu ya kiuchumi bila kiingereza? Kumbuka sisi ni masikini, hatuwezi kuipangia dunia.

Lee Yuan Kew aliwekea mkazo elimu ya kiingereza ili wananchi wa Singapore wapate ufahamu mpana wa kidunia, angalia Singapore ilipo sasa.
Unaamini kusoma somo la kiingereza basi moja kwa moja kunafanya kuwa na uwezo mzuri wa kuweza kuongea kiingereza fasaha?
 
Hata ingekuwa ni sehemu ya lazima yeye kuongea kiingereza bado watu wangecheka tu, ndio utamaduni tuliyojijengea. Kiswahili kibovu akiongea mzungu au muhindi huwa hatuna muda wa kucheka tunasikiliza ili kumuelewa na sio kutaka aongee kiswahili kizuri ila linapokuja suala la sisi kuongea kiingereza hapo ndipo ufasaha wa lugha unapozingatiwa.
Are you that dumb??
Mzungu anayejifunza Kiswahili mtaani na Google miezi miwili mitatu unataka kumfananisha na Bashite aliyesoma Kingereza tangu primary mpaka chuo kikuu??
 
Huko mtaani hata humu JF, asilimia kubwa ya watu hawajui sarufi ya kiswahili fasaha.

Sasa utamcheka vipi mtu anayeandika " kuhairisha " badala ya "kuahirisha " wakati na wewe mwenyewe ukiandika unachanganya R na L?

Kifupi , tumezoea ujinga wa pamoja kiasi kwamba usahihi umeanza kuonekana ni ushamba.
Ndio maana nikasema hiki kiswahili tunachoongea kuna kiasi kikubwa si kuswahili fasaha na wenyewe tushazowea hatujui kama si fasaha na kudhani hivyo ndivyo sahihi.
 
Unaamini kusoma somo la kiingereza basi moja kwa moja kunafanya kuwa na uwezo mzuri wa kuweza kuongea kiingereza fasaha?
Kama tumeshakubali kwamba sisi hata tukisoma Kingereza hatuwezi basi tuachane nacho kabisa, tusome Kiswahili secondary na chuo kikuu.

Kwa nini Kenya na Uganda wakisoma Kingereza wanakuwa na uwezo mzuri wa kuzungumza??
 
Kuna kitu huelewei,
Ukiwakuta Wahindi, Wachina, Wairan, Wafaransa, Wajerumani, Waturuki n.k ambao wana English ya kudokoa basi ujue hawakusoma English, tatizo ni kwamba sisi mtu anakuwa amefundishwa kwa English miaka takribani kumi ukiondoa miaka ya primary ambapo English ni somo la lazima pia na bado hawezi kujieleza au kufanya mazungumzo ya maana kwa Kingereza hata kwa dakika kumi tu. Kubalini tu tuna matatizo katika bongo zetu au mfumo wetu wa elimu ni mbovu.
Ina maana hizo nchi hawana somo la english katika masomo yao?
 
Back
Top Bottom