Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Wengi wanaamini kiingereza ni kipimo cha ustaarabu na kuwa na akili.
hakika, kama hii nliisikia " yani mimi tangu nijielewe na kuwaelewa watu sina rafiki my friend " 😇
Kiswahili tunakichukulia kama lugha ya kuombea chenji
tuithamini lugha yetu na iendelee kukua kimataifa 💪
 
Ni ngumu kuondoa lafudhi, chamsingi unazingatia sarufi ya lugha husika. Sisi sarufi inatutesa.
AHaha hao wahindi inawatesa kama wengi wetu huku mkuu .bahati nzuri kozi nyingi nilizosoma nimefundishwa na Madoctor wa kihindi na moja ya kozi nilifundishwa na Professor kabisa.
Huwezi kuconclude totally kwamba ufasaha wa kuongea kiingereza ndio kipimo cha elimu ya mtu. Waturuki wanamaengineer kibao ila unakuta english yao ya kudokoa dokoa, hao wachina usipime.
 
AHaha hao wahindi inawatesa kama wengi wetu huku mkuu .bahati nzuri kozi nyingi nilizosoma nimefundishwa na Madoctor wa kihindi na moja ya kozi nilifundishwa na Professor kabisa.
Huwezi kuconclude totally kwamba ufasaha wa kuongea kiingereza ndio kipimo cha elimu ya mtu. Waturuki wanamaengineer kibao ila unakuta english yao ya kudokoa dokoa, hao wachina usipime.
Una hoja. Mtu anaweza kuwa vizuri kwenye maandishi na kusoma, ila matamshi hawezi.

Lakini naamini kwa nchi masikini kama hii yetu kiingereza ni lazima aisee.

Ufahamu wa kidunia(global awareness) wa masuala kama AI, stablecoins nk. tunaupataje bila kiingereza? Na hatupaswi kuachwa nyuma kabisa.
 
Nje ya mada,

Hivi kwanini ni rahisi zaidi mtu kukosolewa anapokosea neno la kingereza kuliko kukosolewa pale anapoongea neno/sentensi kwa lugha ya Kiswahili na kukosea?

Mfano unakuta humu JF mtu akisahihishwa kuandika Kiswahili kwa ufasaha anakua mkali!

leo dada
Mbona wanasahihishwa sana tu. Tena alikuwepo kiranja mkuu FaizaFoxy akikunasa anakuuliza "huko shuleni mlisomea ujinga eeh".
 
Una hoja. Mtu anaweza kuwa vizuri kwenye maandishi na kusoma, ila matamshi hawezi.

Lakini naamini kwa nchi masikini kama hii yetu kiingereza ni lazima aisee.

Ufahamu wa kidunia(global awareness) wa masuala kama AI, stablecoins nk. tunaupataje bila kiingereza? Na hatupaswi kuachwa nyuma kabisa.
Yeah ufahamu wa english ni muhimu sana hilo silipingi. Mwaka fulani nilikuwa najaribu kufatilia jinsi mtu anaweza kuwa wakala wa P2P kwenye binance,, kiufupi kule kama english yako ni ya darasa la 2 huwezi kutoboa. Kwa lughs nyepesi kwenye Crypto kama hujui english kaa napo mbali labda kwavile watu wanatransilate siku hizi.
 
AHaha hao wahindi inawatesa kama wengi wetu huku mkuu .bahati nzuri kozi nyingi nilizosoma nimefundishwa na Madoctor wa kihindi na moja ya kozi nilifundishwa na Professor kabisa.
Huwezi kuconclude totally kwamba ufasaha wa kuongea kiingereza ndio kipimo cha elimu ya mtu. Waturuki wanamaengineer kibao ila unakuta english yao ya kudokoa dokoa, hao wachina usipime.
Kuna kitu huelewei,
Ukiwakuta Wahindi, Wachina, Wairan, Wafaransa, Wajerumani, Waturuki n.k ambao wana English ya kudokoa basi ujue hawakusoma English, tatizo ni kwamba sisi mtu anakuwa amefundishwa kwa English miaka takribani kumi ukiondoa miaka ya primary ambapo English ni somo la lazima pia na bado hawezi kujieleza au kufanya mazungumzo ya maana kwa Kingereza hata kwa dakika kumi tu. Kubalini tu tuna matatizo katika bongo zetu au mfumo wetu wa elimu ni mbovu.
 
Hiyo lugha sio yetu , kinachoshangaza upo busy kumkosoa mtu kwa lugha ambayo sio asilia yake.
Usomi sio kujua kiingereza.
Tazama china, tazama India, Pakistan, Japan ENGLISH wanayoiongea ni mbovu sana ila.....

Huko China, india, Pakstan unako kutaja huyo ambaye hajui Kingereza either hajasoma hau hakufundishwa kwa Kingereza. Hakuna Mhindi ambaye amesoma hajui Kingereza.
 
Back
Top Bottom