Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Done your proper research?! Kingereza cha ugoko cha Bashite

Hiyo lugha sio yetu , kinachoshangaza upo busy kumkosoa mtu kwa lugha ambayo sio asilia yake.
Usomi sio kujua kiingereza.
Tazama china, tazama India, Pakistan, Japan ENGLISH wanayoiongea ni mbovu sana ila.....
Halafu nimekuja kugundua watu wengi wakishaona kiingereza kinawapiga chenga wanaanza kusingizia kwamba kiingereza sio lugha yetu.... Sasa tunakiongea cha nini wakati sio lugha yetu... Kiingereza kikikupiga chenga kubali tu usilete visingizio.
 
Shida tuliyonayo wengi hatuna mazoea ya kuongea huyo lugha mara kwa mara sasa inapotokea upo kwenye kundi la watu unataka kuonekana na wewe umo unaishia kutoa boko, unaweza kuwa kitu unakijua kabisa ila ndio ile shetani anapenda kuabisha mbele ya watu
 
Ujue hili tatizo ni la watanzania wote sio Makonda tu.

Tunaweza tukawa sahihi kwa kuwakosoa hawa viongozi hapa na pale, lakini tatizo linaishaje?

Nina uhakika mleta mada naye akipewa nafasi ya kujieleza kwa kiingereza ataboronga.
Hili tatizo kuisha ni mfumo mzima wa elimu kubadilishwa, Kingereza kiwe lugha ya kufundishia kuanzia darasa la kwanza(shule zote ziwe ni English medium), tofauti na hapo viongozi waongee Kiswahili tu kama vile China, India, Urusi, Iran na Ethiopia ambavyo viongozi wanatumia lugha zao na wanakuwa na wakalimani kutafsiri.
 
Usomi sio kujua kiingereza.
Hii hoja haina nguvu kabisa.

Mtanzania wa kawaida aliyehitimu chuo kikuu anakuwa amesoma kiingereza kwa miaka 9(4 O level, 2 A level, 3 degree).

Ubovu wa taasisi za elimu ndo mzizi wa hili tatizo.

Kiingereza ni lugha kuu ya kibiashara ya dunia, nchi masikini kama yetu itawezaje kuzalisha wafanyakazi bora na kuchangia kwenye mijadala migumu ya kiuchumi bila kiingereza? Kumbuka sisi ni masikini, hatuwezi kuipangia dunia.

Lee Yuan Kew aliwekea mkazo elimu ya kiingereza ili wananchi wa Singapore wapate ufahamu mpana wa kidunia, angalia Singapore ilipo sasa.
 
UDSM , UDOM , SAUT pemajaa wahadhiri Wahindi kwenye department za sayansi unajua kwanini?
Kwasababu ya tafiti. Mhadhiri bora ni yule aliyechapisha tafiti nyingi na mpya kwenye taaluma husika.

Wanaajiriwa hao wahindi kwasababu wana vigezo. Watanzania weusi hatuna utamaduni wa kujali kuhusu taaluma.
 
Nje ya mada,

Hivi kwanini ni rahisi zaidi mtu kukosolewa anapokosea neno la kingereza kuliko kukosolewa pale anapoongea neno/sentensi kwa lugha ya Kiswahili na kukosea?

Mfano unakuta humu JF mtu akisahihishwa kuandika Kiswahili kwa ufasaha anakua mkali!

leo dada
Waafrika tulio wengi bado tuna ukoloni mamboleo vichwani mwetu.

Wengi wanaamini kiingereza ni kipimo cha ustaarabu na kuwa na akili.

Kiswahili tunakichukulia kama lugha ya kuombea chenji sokoni au kupiga majungu vijiweni.

Ni ugonjwa wa kisaikolojia wa kutaka kuonekana msomi kwa lugha ya mkoloni huku ukiwa kilaza wa lugha yako mama.
 
Kwanini mtu akiongea kiswahili kibovu na ni mswahili kabisa huwa hatumcheki?
Huko mtaani hata humu JF, asilimia kubwa ya watu hawajui sarufi ya kiswahili fasaha.

Sasa utamcheka vipi mtu anayeandika " kuhairisha " badala ya "kuahirisha " wakati na wewe mwenyewe ukiandika unachanganya R na L?

Kifupi , tumezoea ujinga wa pamoja kiasi kwamba usahihi umeanza kuonekana ni ushamba.
 
Nje ya mada,

Hivi kwanini ni rahisi zaidi mtu kukosolewa anapokosea neno la kingereza kuliko kukosolewa pale anapoongea neno/sentensi kwa lugha ya Kiswahili na kukosea?
Tunathamini visivyo vyetu
Mfano unakuta humu JF mtu akisahihishwa kuandika Kiswahili kwa ufasaha anakua mkali!

leo dada
Wana Ugonjwa wa akili tu hao!!!!! Lugha yako unatakiwa utambe nayo kiufasaha.
 
Back
Top Bottom