Unamaanisha nini ukisema hiyo lugha siyo yetu?
English na Kiswahili ni lugha rasmi za Tanzania ambazo kila mtu anatakiwa kuzijua kwa ufasaha.
Msemo wa ..' hiyo lugha siyo yetu' , hautakiwi kuwa kichaka cha kuficha mapungufu yaliyosababisha watu wengi kutojua kwa ufasaha hiyo lugha.
Mapungufu yaliyosababisha hilo tatizo linajulikana....kwamba tuna walimu wachache sana wenye sifa ya kufundisha English....achilia mbali maeneo mengi hakuna hata hao walimu wa kubabisha.
Na ukweli mchungu ni kwamba tuna uhaba mkubwa wa walimu bora katika masomo yote...ila kushindww kwa wanafunzi kumudu kuongea na kuandika kwa kingereza ni kielelezo cha wazi cha mapungufu au uhaba wa walimu.
Ni kweli tunatakiwa kujivunia kuongea na kuandika kiswahili ,lakini vilevile hatuwezi kuacha kujua kingereza kwa ufasaha.
Kusema kwamba kwanza hiyo lugha siyo yetu ....kwa hiyo siyo ya lazima ni sawa na kutumia msemo wa sungura...."sizitaki mbichi hizi'....,baada ya kurukia ndizi zilizoiva kwa muda mrefu na kushindwa.
Haiwezekani tatzo likawa ni mwanafunzi....kwamba apewe somo la kingereza kwa miaka 5 au 7 lakini ahitimu shule ya msingi asimudu hiyo lugha.