kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,992
- 17,892
Mlokua mnamzushia kifo mna hali gani?Mlokua mnatangaza na kujiapiza kwamba akionekana mtafuta page zenu mshafuta?Mlokua mnapiga ngoma ya nchimbi na kuanza kumpost mpo wapi?Huwezi kushindana na Mungu hata kidogo!! Kwa mara nyingine wahuni na genge lenu mmefail again!!
Kama mnadhani mtafanikiwa kama mlivyofanikiwa kipindi kile basi safari hii mmechemka Mungu wetu hawezi kuruhusu hilo liwe labda atake yeye
Hii tabia ya kuzushia watu vifo siyo nzuri hata kidogo!! Na ingekua ni busara hawa wahuni washughulikiwe humo humo ndani ya chama na mtandao wao!!Lakini inakua ni vigumu maana wana mizizi kila mahali.
=======
Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na Mapadre mara baada ya kushiriki Ibada ya Jumapili ktk Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege Dodoma leo tarehe 10 Desemba 2023.
Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Philip Mpango ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege mkoani Dodoma katika Ibada ya Jumapili leo Desemba 10, 2023. Ibada hiyo imeongozwa na Padre Dionis Paskal Safari.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa ibada hiyo, Dk Mpango amewaasa Watanzania kutumia vema mitandao ya kijamii.
Amesema matumizi yasiofaa ya mitandao ya kijamii yamekuwa yakiumiza watu wengi hivyo yampasa kila mmoja kutumia vema pamoja na kuwa na hofu ya Mwenyezi Mungu.
Makamu wa Rais amewashukuru waumini hao kwa kuendelea kumuombea ili aweze kutekeleza vema majukumu yake.
Kama mnadhani mtafanikiwa kama mlivyofanikiwa kipindi kile basi safari hii mmechemka Mungu wetu hawezi kuruhusu hilo liwe labda atake yeye
Hii tabia ya kuzushia watu vifo siyo nzuri hata kidogo!! Na ingekua ni busara hawa wahuni washughulikiwe humo humo ndani ya chama na mtandao wao!!Lakini inakua ni vigumu maana wana mizizi kila mahali.
=======
Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na Mapadre mara baada ya kushiriki Ibada ya Jumapili ktk Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege Dodoma leo tarehe 10 Desemba 2023.
Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Philip Mpango ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege mkoani Dodoma katika Ibada ya Jumapili leo Desemba 10, 2023. Ibada hiyo imeongozwa na Padre Dionis Paskal Safari.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa ibada hiyo, Dk Mpango amewaasa Watanzania kutumia vema mitandao ya kijamii.
Amesema matumizi yasiofaa ya mitandao ya kijamii yamekuwa yakiumiza watu wengi hivyo yampasa kila mmoja kutumia vema pamoja na kuwa na hofu ya Mwenyezi Mungu.
Makamu wa Rais amewashukuru waumini hao kwa kuendelea kumuombea ili aweze kutekeleza vema majukumu yake.