Je, amerejea CHADEMA? Tusubiri tuone
Aliyewahi kuwa Katibu wa CHADEMA Taifa na baadaye Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Dkt. Wilbrod Slaa kwa mara ya kwanza jana Jumapili amehudhuria mkutano wa Chadema Wilaya ya Karatu na kuahidi atashirikiana na chama hicho kudai Katiba mpya.
Dkt. Slaa aliondoka CHADEMA akiwa Katibu Mkuu wakati wa mchakato wa uchaguzi Mkuu mwaka 2015 baada ya chama hicho, kumteua Edward Lowassa kugombea urais kupitia chama hicho.
Dkt. Willibrod Peter Slaa anasema:
“Mimi sina chama, nawaambia CCM ili kuwasaidia, kuna sababu gani ya kuchagua kama hawajirekebishi, lakini kwa sasa twende na chama ambacho angalau kinaonesha kina wafikiria na kuwajali Watanzania hiyo ni katika uchaguzi unaoakuja, maandalizi yaanza ndani ya chama
“Hatua ya pili twende katika mikutano ya Katiba, CCM wanasema Katiba itakuletea Uji, Wali au chakula kingine chochote nyumbani kwako? Niwaambie Katiba ni kila kitu.
“Ugali unaoupata maamuzi ya huo bei ya ugali na chakula kingine unachopata inatokana na Katiba.
“Katiba ya sasa imetoa mamlaka yote kwa Rais, simlaumu Rais peke yake bali nalaumu mfumo uliotengeneza Katiba.”
SLAA NI PROFESA
Mimi ni Profesa wa Siasa, kazi yangu ni kutoa ushauri na nitawaelekeza, Profesa amepita mengi na magumu ana uzoefu
Ndio maana naongea kwa uhuru kabisa katika Nchi yangu najua Sheria najua haki zangu na hakuna wa kuniuliza kwanini nazungumza na CHADEMA, nitasema bila kumung’unya maneno
Bei ya Mchele inapanda licha ya kuwa tunalima hapahapa Nchini, bei ya nyama ya ng’ombe nayo inazidi kupanda
Aliyewahi kuwa Katibu wa CHADEMA Taifa na baadaye Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Dkt. Wilbrod Slaa kwa mara ya kwanza jana Jumapili amehudhuria mkutano wa Chadema Wilaya ya Karatu na kuahidi atashirikiana na chama hicho kudai Katiba mpya.
Dkt. Slaa aliondoka CHADEMA akiwa Katibu Mkuu wakati wa mchakato wa uchaguzi Mkuu mwaka 2015 baada ya chama hicho, kumteua Edward Lowassa kugombea urais kupitia chama hicho.
Dkt. Willibrod Peter Slaa anasema:
“Mimi sina chama, nawaambia CCM ili kuwasaidia, kuna sababu gani ya kuchagua kama hawajirekebishi, lakini kwa sasa twende na chama ambacho angalau kinaonesha kina wafikiria na kuwajali Watanzania hiyo ni katika uchaguzi unaoakuja, maandalizi yaanza ndani ya chama
“Hatua ya pili twende katika mikutano ya Katiba, CCM wanasema Katiba itakuletea Uji, Wali au chakula kingine chochote nyumbani kwako? Niwaambie Katiba ni kila kitu.
“Ugali unaoupata maamuzi ya huo bei ya ugali na chakula kingine unachopata inatokana na Katiba.
“Katiba ya sasa imetoa mamlaka yote kwa Rais, simlaumu Rais peke yake bali nalaumu mfumo uliotengeneza Katiba.”
SLAA NI PROFESA
Mimi ni Profesa wa Siasa, kazi yangu ni kutoa ushauri na nitawaelekeza, Profesa amepita mengi na magumu ana uzoefu
Ndio maana naongea kwa uhuru kabisa katika Nchi yangu najua Sheria najua haki zangu na hakuna wa kuniuliza kwanini nazungumza na CHADEMA, nitasema bila kumung’unya maneno
Bei ya Mchele inapanda licha ya kuwa tunalima hapahapa Nchini, bei ya nyama ya ng’ombe nayo inazidi kupanda