Dhihaka ya karne: Eti wanataka kuhama CHADEMA

Dhihaka ya karne: Eti wanataka kuhama CHADEMA

Hahahaha, ninyi ndiyo mlitumia gharama kubwa. Sisi polisi wanalipwa mishahara, wala hapakuwa na extra duty allowances. Ila intelijensia inaonesha ninyi mlilipa waandamanaji kati ya tshs 10000 na 40000. Na ukichukua ile idadi ya watu mil moja na mamvi utapata kiasi mlichopoteza. Kibaya zaidi mpka octoba mliowagawia watakuwa wameila na kuisha.


Duh! Bandiko laki hilo limenikumbusha mbali sana.....

Yaani kipindi kile twaweza wanasoma tafiti zao mbele ya waandishi wa habari....

Alaf ikafika kipengele cha "wasomi wengi walionekana kuupenda upinzani & vice versa"
 
Kama umeona mleta mada kaleta pumba basi ujijue wewe Ni kuku, maana binadamu tumeona maneno yenye hekima
mshana jr kaspecialize kwenye uganga na ninamkubali ila siasa hazijui kabisa yaani ni mweupe kama dj au mamvi, ndiyo maana huwa namdharau sana, labda angekuwa CCM angekuwa na uwezo wa kuchambua siasa.
 
Hii intelejensia kiboko! Kama iliweza kujua nani walilipwa kwenye maandamano lakini ikashindwa kukamata wauaji wa askari wetu hii intelejensia kiboko


Msamehe tu maana ajui alitendalo....

Huenda akawa ni miongoni mwa wale walio hangaika na Mazoezi mchana jua kali ili kupiga wananchi na mwisho akasikia maandamano yamehairishwa.
 
Siku mkiamua kufanya mambo tofauti na chama tawala kwa kufikiri mile 1000 zaidi yao , mtachukua nchi hii lakini kwa Ku copy na kupaste
Sahauni


Utakuwa bado huamini na siku zote utaishia kutoamini had ukikose ulichoshika mkononi dude lipo toka 1961 cheki range kwa hisani ya lubuva 8-6 kwa mauzzauza haya vipi 2020 na msipofagia leo magu anazid kukiweka chama rehani toka aingie alichafanikiwa had sasa ni fukuza fukuza tu kwa wajuz wa mambo unajua ni kwa nn kikwete alisema siitaji kuombwa ushaur na akakazia ninestaafu kila kitu.
 
Anayetaka taka kuhama chadema amechelewa ili atupinguzie mzigo amfate haraka katibu yule kule mwanza,
 
mshana jr kaspecialize kwenye uganga na ninamkubali ila siasa hazijui kabisa yaani ni mweupe kama dj au mamvi, ndiyo maana huwa namdharau sana, labda angekuwa CCM angekuwa na uwezo wa kuchambua siasa.
[emoji3] [emoji3] [emoji3] mimi sitakudharau hata siku moja
 
Kwa sasa mmepoteza vitu vifuatavyo;

1,integrity
2,ownership
3,credibility
4, Honesty


Integrity( Uadilifu)

Sasa chadema hakuna uadilifu tena , mmebaki kupuyanga tu na kukosa jambo la kuwafanya muwe waadilifu machoni pa watanzania na wanachama wenu , na hii ndio imewagawa mpaka sasa kubalini mkatae kuna kundi la waadilifu bado ni watiifu kwa Dr slaa aliyeweka misingi mizuri ya uadilifu na kuisimamia ndani ya chadema , e.g humu jukwaani wamo kina IDAWA, MTAZAMO n.k ambao hawaipendi ccm lakini wako chadema ila si wanachama hai wana subiri kuhuishwa upya kwa chadema sijui itakuwa lini? Badilikeni


2, Ownership ( umilikaji)
Kwa sasa wapenzi na wanachama wa chadema hawana umiliki wa chadema tena , kimebaki chama cha wachache wenye pesa , ndio maana hata Leo ukianzisha harambee hawachangii maana umilikaji sio wa wanachama tena Bali kundi dogo, hawa wamebaki yatima , mmekopi ya ccm mmepeleka chadema , hvyo lazima mbinu za kiccm zitumike ambazo wao wanaanza kuachana nazo

3, Credibility
Chadema kwa sasa ile credibility na upokelewaji wake umepungua ndani ya jamii na hii heshima inapungua siku baada ya siku msipikuwa makini mtakuwa kama nccr , kinachowabeba ni kutaka kushindana tu ccm ili mtajwe tajwe lakini kiuhalsia mmepoteza sana heshima nzuri mliyokuwa mmejijengea toka 2007, situkeni


4, Honesty ( Uongofu/ uaminifu)

Kwa hili ndilo limezidi kuwapotezea sifa kwa wanachama wenu , moja suala la UKUTA mlilipigia debe japo halikuwa na maana yoyote yaani kama ni silaa ni risasi 1 iliyobaki kwenu either ujiue au umuue adui , mwisho wa siku imewaua ninyi , maana kauli za viongozi, wenu kama msigwa , nanukuu " anayeogopa polisi hafai , lazima totafautishe Men na Boys" hii kauli sijui ataificha wapi ?

Maana ni kauli tata tata tu mfano ile ya kipindi kile nanukuu " atakayemuunga mkono lowasa akapimwe akili"


Kauli tata kabla ya kuhairishwa ukuta za mnyika, mbowe ,tundu lisu n.k zimewaondolea uaminifu kwa wanachama wenu

Pia imewaondolea uaminifu kwa vyama vingine vya upinzani , maana kuanzisha UKUTA ilikuwa ni kuua UKAWA bila makubaliano , hvyo ukawa imekufa kibudu , UKUTA imekufa kibudu sasa ni mmeanzisha internal strife katika vyama vya upunzani maana hakuna wa kuwaamini tena

Ushauri , mkubali mmekosea sana na kosa lenu ni Kumkaribisha Lowasa na kingine zaidi hamuaminiki katika kile mnachosimamia


" Kiongozi Mzuri ni yule anayelinda kauli zake na kuzisimamia hata kama kawekewa mtutu wa bunduki like kina Che Guevara na the like ". Sio nyie wajasiliamali wa siasa

Nimeshauri nasubiri Matusi
Ushauri wako ni sawa, lakini inaoñyesha pia jinsi ulivyo mdumavu wa mawazo. Kwani wewe kipimo cha uadilifu wa wanachadema ni Dr. Slaa. Lakini unàamini pia kwamba ccm kuna uadilifu, mlinganisho wako ndiyo uwezo wa matumizi ya akili yako. Kila wakati una Sifa zake na wàtu wake. Kama wanachadema mnawaita nyumbu utaachaje kuwaona nyumbu?

Kuhusu umiliki wa chama, kwanza ni kujilisha upepo kwa kukaa unapambana nao. Umiliki wa chama ni jukumu la wanachama. Mpiga zumari mtandaoni anajitafutia ulcers na pressure. Yako nje ya uwezo wako, hata usiposema hayo jamii unayokufamu haiwezi kubadili mtazamo juu yako. Umbra ni Tania ya kujifikirisha juu ya mtu/watu wengine na kisha kukitamka kwake au kwa mwingine
 
Ushauri wako ni sawa, lakini inaoñyesha pia jinsi ulivyo mdumavu wa mawazo. Kwani wewe kipimo cha uadilifu wa wanachadema ni Dr. Slaa. Lakini unàamini pia kwamba ccm kuna uadilifu, mlinganisho wako ndiyo uwezo wa matumizi ya akili yako. Kila wakati una Sifa zake na wàtu wake. Kama wanachadema mnawaita nyumbu utaachaje kuwaona nyumbu?

Kuhusu umiliki wa chama, kwanza ni kujilisha upepo kwa kukaa unapambana nao. Umiliki wa chama ni jukumu la wanachama. Mpiga zumari mtandaoni anajitafutia ulcers na pressure. Yako nje ya uwezo wako, hata usiposema hayo jamii unayokufamu haiwezi kubadili mtazamo juu yako. Umbra ni Tania ya kujifikirisha juu ya mtu/watu wengine na kisha kukitamka kwake au kwa mwingine
Nikitegemea michango Kama hii kwa nyie bendera fuata upepo

Endelea kutukana
 
Baada ya jana kuahirishwa maandamano ya UKUTA kwa mwezi mmoja zimefumuka post za kukejeli hiki kitendo

Kila mtu kasema lake, lakini wengi wakijikita kwenye kusema kuwa eti

-CHADEMA ni vigeugeu
-CHADEMA ni mabingwa wa kubadili gia angani
-CHADEMA inapoteza mwelekeo chini ya Lowassa (utafikiri ndio mwenyekiti)

Kejeli ni nyingi kweli na hili halina tatizo kwakuwa wale waliokuwa wamejiandaa kuumiza wananchi wasio na hatia hawataweza tena kufanya hivyo! Maandalizi yalikuwa mengi na kabambe mno ya kukipaka damu chadema kama maandamano haya yangefanyika
Kichekesho na dhikaha ya kukera sana ni wale wanaojifanya kutaka kuihama CHADEMA eti tu kwakuwa wameahirisha maandamano! Hilo tu likufanye uhame chama? Maandamano yangefanyika wewe ungeenda? Uhame Chadema uende chama gani? CCM? kama kuhama chama kungekuwa rahisi hivyo Lipumba asingeng'ang'ania cuf....unazi wetu uko nyuma ya keyboard tuu lakini waandamanaji wa kweli wasioogopa chochote iwe virungu iwe maji ya kuwasha ile jela, hawapo hapa na hawa wamekubaliana na maamuzi! Hakuna haja ya kutishia kuhama FANYA SASA

Dhima ya CHADEMA haikuwa kuandamana!maandamano huwa silaha ya mwisho kabisa kwenye nchi ya kidemokrasia kama njia zote zikishindikana

CHADEMA kwenye hili wamefanikiwa sana tena sana, harakati za ukuta zimeleta matunda mengi

Maamuzi mengi ya kibabe yamepungua ama kubatilishwa

Kupayuka payuka kumepungua

Utawala wa sheria unaanza kurejewa

Utawala ulioanza kujisahau umekuwa makini zaidi sasa

Viongozi wengi wameamua kuingia kwenye mazungumzo

CHADEMA SASA IMEANZA KUSIKILIZWA NA ITASILIKOLIZWA..hii ndio ilikuwa dhima ya yao KUSIKILIZWA

CHADEMA itasikilizwa bila kusababisha madhara kwa wananchi bila uharibifu wa mali na kwa gharama bei chee kabisa

CHADEMA imepiga hatua kumi zaidi mbele waliokamatwa kwa mashtaka ya kutunga na kunjuka ni viongozi tuu raia hawafiki watano! Huu ni ushindi mkubwa sana
Kama unahama CHADEMA Salam zao huko uendako

Hivi nyie watu mnawafikiliaje watu wenzenu. Mnawafikiria kuwa ni mambumbu kiasi cha kuwaongopea namna hiyo?

Kwani ni nani alisema atafanya maandamano na mikutano tena isiyo na kikomo kuanzia tarehe mosi september?

Kama ilijuwa kuwa maandamano si kitu kizuri kitamwaga damu kwanini hawKughairisha tangia zamamni au kwanini waliamua kutumia njia hoyo wakati njia za amani zipo kutatua mogogoro?

Makamanda wenu wangapi wako Rumande hadi sasa?

Utawala upi wa sheria ulioanza kutumika ambao zamani haukutumia?

Chedema gani imeanza kusikilizwa, tena imeanza kusikilizwa na nani? Wakati mtaalamu wako wa kubadili gia angani jana kasema kanpbisaaa wazi kuwa Raisi alishakataaga kuongea na chadema...

We unayemuona kuwa ni mbumbu kama wewe ni nani hasa?

Acha kupenda sana kijana. Usipokubali kumshauri kiongozi wako na ukawa ni mjumbe ndiyooooo hautakuwa na tofautii sana na ccm.

Mlishasema tatzo la wanzania ni kusherehekea kila kitu kinachosemwa na kufanywa na Magufuri, na ndio maana anafanya mambo pasipo kushauriwa...

Sasa na wewe na wenzio msipomshauri kiongozi wenu ( mataalamu wa gia) naye ataendelea kufanya mambo ya kijinga na kukurupuka kama mkuu wa kaya na hatimaye chama kitakosa watu na wafiasi kila uchwao...
Amka wewe...
 
Nawashauri wapinzani wetu waachane na negative approach na waanze kutumia positive approach itawasaidia,kwamfano huwa mimi nikiingia kwenye kale kaboksi kakupiga tiki siku ya uchaguzi huaga gafla nakumbuka nimesoma vidudu CCM Mwinjuma yaani hata kama nilikua nataka kupigia kura upinzani kwakuwaonea huruma basi ghafla nabadilisha uamuzi na kupiga tiki kwenye rangi ya kijani kwani ndio rangi ambayo nimeizoea kuiangali tangu nikiwa mtoto.

Ni bora tu waanzishe shule zao za vidudu na watoto wasome bure lakini madarasa wayapake rangi ya chadema na kuchora nembo yao madarasani.Kwakufanya hivi itawasaidia sana mwaka 2800
 
serikali ilisitisha kazi zake nyingi ikiwemo kuhamia Dodoma ikajikita kupambana na UKUTA,kama Mshana JR unakumbuka Thread yako moja ilio kuwa inahusu wanamkakati waliopo CHADEMA nimesahau kichwa chake cha habari,lakini ulielezea kinagaubaga ni namna gani Chadema ilivyo retain popularity na kuendelea kuonyesha ni chama makini,rudi kwenye comment za wengi wa wanaccm na vijana wao walivyo kuwa hawana chembe ya haya wala huruma walikuwa wanahamu ya kushuhudia watu wakipewa vilema,majeraha au kuuwawa.

Bila kujali ni watanzania wenzao tena wengine ni ndugu zao wa damu wakasahau kuwa vita au machafuko hayana macho ni sawa nakokoro, huenda majeshi yange salim amri na wananchi wangejitangazia mapinduzi..!!CCm na washirika wake ikiwemoa jeshi la polisi wajue kuwa kuwanyanyasa UKAWA ni kudhulumu haki ya wananchi na mimi nawataka waendelee hivyo ilikuzijaza chuki nafsi na roho za watanzania wapenda haki na amani ili siku kikitokea chakutoke wakose mahala pakuweka msiba wao...!!

Watoa matamko wa ccm wangekuwa na busara wangekaa chini nakutafakari matukio kadhaa yalio wahusu polisi na idadi kubwa ya wananchi kuonyesha kuwakebehi au kuwalaumu polisi,kuliko kusimama tena mtu mzima bila kuwa nachembe ya aibu usoni pake nakurudia kauli za vitisho ambazo kamwe hazijawahi kushinda katika aridhi au ukanda uliokubali kuwa na mfumo wa kidemokrasia..!!! It's not over until it

over,mapambano yanaendelea octoba 1 tarehe ya mkataba mwingine wa mwendelezo wa UKUTA..Tukatane Bungeni
 
Back
Top Bottom