Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA John Mnyika, akizungumza na Vyombo vya habari kuelekea kusikilizwa Kesi ya Mwenyekiti wa Chama hicho, Tundu Lissu kesho Juni 11, 2026 Mahakama ya Rufaa, ametoa wito kwa Jeshi la Polisi kuacha taarifa za uongo zinazoendelea ndani ya Jeshi hilo kuwa za Kiitelinjesia kwamba CHADEMA inataka kumuokoa Tundu Lissu mikononi mwa Polisi na Magereza
Mnyika amerejea tukio la Jeshi la Polisi kupiga watu mahakama ya Kisutu wakati kesi ya Lissu inakwenda kwenye hatua ya komito mwezi Aprili mwaka 2025
"Mambo mawili kwa Jeshi la Polisi. La kwanza: wapuuzie taarifa za uongo za ndani ya Jeshi la Polisi lenyewe zinazodaiwa kuwa za kiintelijensia kwamba watu wa CHADEMA, maanake kuna habari hizo wamelishana uongo huko ndani, kwamba CHADEMA inataka kufanya vurugu ya kumnyakua walichokiita kumwokoa Tundu Lissu kutoka kwenye mikono ya magereza na mikono ya polisi. Uongo mtupu.
Uongo ambao umetengenezwa ili kutekeleza nia ovu ya kupiga raia na kupiga wananchi na kufanya vurugu. Watu wa polisi wenye kuheshimu utawala wa sheria, haki, na maadili waepukwe kuingizwa kwa uongo kwenye mzozo na mgogoro ambao utalichafua zaidi Jeshi la Polisi, ambalo tayari limeshajichafua kwa matendo mbalimbali ya siku ya nyuma."
Mnyika amerejea tukio la Jeshi la Polisi kupiga watu mahakama ya Kisutu wakati kesi ya Lissu inakwenda kwenye hatua ya komito mwezi Aprili mwaka 2025
Uongo ambao umetengenezwa ili kutekeleza nia ovu ya kupiga raia na kupiga wananchi na kufanya vurugu. Watu wa polisi wenye kuheshimu utawala wa sheria, haki, na maadili waepukwe kuingizwa kwa uongo kwenye mzozo na mgogoro ambao utalichafua zaidi Jeshi la Polisi, ambalo tayari limeshajichafua kwa matendo mbalimbali ya siku ya nyuma."