Baada ya jana kuahirishwa maandamano ya UKUTA kwa mwezi mmoja zimefumuka post za kukejeli hiki kitendo
Kila mtu kasema lake, lakini wengi wakijikita kwenye kusema kuwa eti
-CHADEMA ni vigeugeu
-CHADEMA ni mabingwa wa kubadili gia angani
-CHADEMA inapoteza mwelekeo chini ya Lowassa (utafikiri ndio mwenyekiti)
Kejeli ni nyingi kweli na hili halina tatizo kwakuwa wale waliokuwa wamejiandaa kuumiza wananchi wasio na hatia hawataweza tena kufanya hivyo! Maandalizi yalikuwa mengi na kabambe mno ya kukipaka damu chadema kama maandamano haya yangefanyika
Kichekesho na dhikaha ya kukera sana ni wale wanaojifanya kutaka kuihama CHADEMA eti tu kwakuwa wameahirisha maandamano! Hilo tu likufanye uhame chama? Maandamano yangefanyika wewe ungeenda? Uhame Chadema uende chama gani? CCM? kama kuhama chama kungekuwa rahisi hivyo Lipumba asingeng'ang'ania cuf....unazi wetu uko nyuma ya keyboard tuu lakini waandamanaji wa kweli wasioogopa chochote iwe virungu iwe maji ya kuwasha ile jela, hawapo hapa na hawa wamekubaliana na maamuzi! Hakuna haja ya kutishia kuhama FANYA SASA
Dhima ya CHADEMA haikuwa kuandamana!maandamano huwa silaha ya mwisho kabisa kwenye nchi ya kidemokrasia kama njia zote zikishindikana
CHADEMA kwenye hili wamefanikiwa sana tena sana, harakati za ukuta zimeleta matunda mengi
Maamuzi mengi ya kibabe yamepungua ama kubatilishwa
Kupayuka payuka kumepungua
Utawala wa sheria unaanza kurejewa
Utawala ulioanza kujisahau umekuwa makini zaidi sasa
Viongozi wengi wameamua kuingia kwenye mazungumzo
CHADEMA SASA IMEANZA KUSIKILIZWA NA ITASILIKOLIZWA..hii ndio ilikuwa dhima ya yao KUSIKILIZWA
CHADEMA itasikilizwa bila kusababisha madhara kwa wananchi bila uharibifu wa mali na kwa gharama bei chee kabisa
CHADEMA imepiga hatua kumi zaidi mbele waliokamatwa kwa mashtaka ya kutunga na kunjuka ni viongozi tuu raia hawafiki watano! Huu ni ushindi mkubwa sana
Kama unahama CHADEMA Salam zao huko uendako
Kwa sasa mmepoteza vitu vifuatavyo;
1,integrity
2,ownership
3,credibility
4, Honesty
Integrity( Uadilifu)
Sasa chadema hakuna uadilifu tena , mmebaki kupuyanga tu na kukosa jambo la kuwafanya muwe waadilifu machoni pa watanzania na wanachama wenu , na hii ndio imewagawa mpaka sasa kubalini mkatae kuna kundi la waadilifu bado ni watiifu kwa Dr slaa aliyeweka misingi mizuri ya uadilifu na kuisimamia ndani ya chadema , e.g humu jukwaani wamo kina IDAWA, MTAZAMO n.k ambao hawaipendi ccm lakini wako chadema ila si wanachama hai wana subiri kuhuishwa upya kwa chadema sijui itakuwa lini? Badilikeni
2, Ownership ( umilikaji)
Kwa sasa wapenzi na wanachama wa chadema hawana umiliki wa chadema tena , kimebaki chama cha wachache wenye pesa , ndio maana hata Leo ukianzisha harambee hawachangii maana umilikaji sio wa wanachama tena Bali kundi dogo, hawa wamebaki yatima , mmekopi ya ccm mmepeleka chadema , hvyo lazima mbinu za kiccm zitumike ambazo wao wanaanza kuachana nazo
3, Credibility
Chadema kwa sasa ile credibility na upokelewaji wake umepungua ndani ya jamii na hii heshima inapungua siku baada ya siku msipikuwa makini mtakuwa kama nccr , kinachowabeba ni kutaka kushindana tu ccm ili mtajwe tajwe lakini kiuhalsia mmepoteza sana heshima nzuri mliyokuwa mmejijengea toka 2007, situkeni
4, Honesty ( Uongofu/ uaminifu)
Kwa hili ndilo limezidi kuwapotezea sifa kwa wanachama wenu , moja suala la UKUTA mlilipigia debe japo halikuwa na maana yoyote yaani kama ni silaa ni risasi 1 iliyobaki kwenu either ujiue au umuue adui , mwisho wa siku imewaua ninyi , maana kauli za viongozi, wenu kama msigwa , nanukuu " anayeogopa polisi hafai , lazima totafautishe Men na Boys" hii kauli sijui ataificha wapi ?
Maana ni kauli tata tata tu mfano ile ya kipindi kile nanukuu " atakayemuunga mkono lowasa akapimwe akili"
Kauli tata kabla ya kuhairishwa ukuta za mnyika, mbowe ,tundu lisu n.k zimewaondolea uaminifu kwa wanachama wenu
Pia imewaondolea uaminifu kwa vyama vingine vya upinzani , maana kuanzisha UKUTA ilikuwa ni kuua UKAWA bila makubaliano , hvyo ukawa imekufa kibudu , UKUTA imekufa kibudu sasa ni mmeanzisha internal strife katika vyama vya upunzani maana hakuna wa kuwaamini tena
Ushauri , mkubali mmekosea sana na kosa lenu ni Kumkaribisha Lowasa na kingine zaidi hamuaminiki katika kile mnachosimamia
" Kiongozi Mzuri ni yule anayelinda kauli zake na kuzisimamia hata kama kawekewa mtutu wa bunduki like kina Che Guevara na the like ". Sio nyie wajasiliamali wa siasa
Nimeshauri