DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

TRA law stipulates that Any INCOME & Profit made in TZ should be taxed unless exempted

Hawa DECI kuna watu wanapiga kelele humu ndani kuwa wamesajiliwa, wanawithhold Tax portion on profit per TRA law??? Hiyo ndiyo itamake sure kama wako legit au vipi.

Ebu TRA fanyeni kazi yenu mapema ili tuzuie balaa ambalo liko njiani soon na kuna watu nasikia wanaenda kukopa hela ili kuweka huko DECI, yaana I can only imagine siku ya kilio.
 
Biashara za kufanya upate faida ya kulipa watu zipo ila practicability yake ndio ngumu.
Mfano creti moja ya bia ina faida ya 5000. ukimanage kuuza daily kwa mwezi una 150,000/=. Assuming operation cost zinakuwa covered na muuza chipsi na initial cost isiwe considered. Just consider circulation of the cash.
Naa hii inatoka kwenye circulation ya less than 30,000/=.

Lets think big on the manufacturing industry and something else and conside hawa ni walokole walioamua kushare profit 100% inawezekana.
Just imagine kama wanalink na forever living products and just imagine how much those people wanachuma from the product users and assume all this cash is going to be invested in farming aloevera somewhere???

Lets think +vely and hope hawatutapeli.
ila wahusika TRA please lets have data za uhakika maanake google haionekani hii kitu kabisa.
 
Naungana na wenye wasiwasi na huu mradi ambao una kila dalili ya kuwa Dollarjet na upatu vilivyopata kuwaliza watu siku za nyuma LAKINI maybe, just maybe, inawezekana;
Benki ya CRDB wanatoa riba ya 2% kwa SIKU 30 kwa kila shilingi milioni 100 utakazoweka kwenye fixed account. Hii ina maana kuwa kila bada ya siku 30 milioni mia moja yako itakupa shilingi milioni 2.

Suppose hawa jamaa wana mafungu 10 tu ya shilingi milioni 100 kila moja, ina maana kila mwezi wanaingiza shilingi milioni 20 na kwa maana hiyo baada ya miezi minne wana milioni 80!

Surely, hii sum can be enough to pay 'wawekezaji' kadhaa walioweka tulaki mbili twao miezi minne kabla, bila kusahau kuwa hao jamaa bado wata-retain asilimia fulani ya hela hiyo kama alivyosema mchangiaji mmoja hapa?

Going by this hesabu, maybe, just maybe inawezekana...?
 
Biashara za kufanya upate faida ya kulipa watu zipo ila practicability yake ndio ngumu.
Mfano creti moja ya bia ina faida ya 5000. ukimanage kuuza daily kwa mwezi una 150,000/=. Assuming operation cost zinakuwa covered na muuza chipsi na initial cost isiwe considered. Just consider circulation of the cash.
Naa hii inatoka kwenye circulation ya less than 30,000/=.

Lets think big on the manufacturing industry and something else and conside hawa ni walokole walioamua kushare profit 100% inawezekana.
Just imagine kama wanalink na forever living products and just imagine how much those people wanachuma from the product users and assume all this cash is going to be invested in farming aloevera somewhere???

Lets think +vely and hope hawatutapeli.
ila wahusika TRA please lets have data za uhakika maanake google haionekani hii kitu kabisa.


tunaweza kuassume kuwa hawa DECI ni kama wale watumishi waliopewa Talanta na bwana wao. Mmoja talanta 5000, mwingine 1000 na mwingine 100. Yule bwana aliporudi kutoka safari ya mbali aliwaita wote na kuwauliza "mlifanyia nini talanta zile, leteni mahesabu yenu".

yule wa Talanta 5000 akasema "bwana mimi nilianzisha kituo cha mafuta, duka la viyoyozi na pia nimejenga shule ya chekechekea". Akaendelea "kutoka zile talanta 5000, nimepata faida ya talanta 10,000 so hizi hapa hela zako.

Akamwita yule wa pili, naye akasema "mimi nilianzisha ujasiriamali wa shamba la vitunguu kwenye mabonde ya Tukuyu, na pia nimelima viazi na kutoka zile zile talanta 1000 nimekuwa nikiagiza matunda toka kwa Mkapa huko Lushoto. Kutokana na kiasi kile nimepata faida ya talanta 5000!, hizi hapa fedha zako".

Yule bwana akamuita yule aliyepewa talanta 100 naye atoe hesabu zake. Yeye akaja na kusema "bwana mimi nilijua wewe ni mtu katili, unakula usivyopika, na unavuna usivyopanda. Kwa kukugwaya wewe niliamua kuzifukia ardhini hadi utakaporudi".

Yule bwana akamuuliza "haya nipe kilicho changu". Jamaa akasema "twende mnisaidie kufukua."

Walipoenda na kufukua wakakuta talanta 100 zimeongezeka na kuwa talanta 100,000!

Yule bwana akamuuliza "umewezaje hili?"

Yule mtumishi akasema "nilianzisha mchezo wa Deci!"

Bwana akashikwa na mshangao akamuambia "hakika na wewe ni fisadi!"
 
Duh, Wanachofanya hawa DECI nii baaabu kubwa...hakuna mfano. Lakini jamani kusema kweli hesabu hazipandi kabisa!..nimejaribu kila njia ya kufikiri nimebakia mtupu yaani uchiii sikuona ndani wala nje..Hakuna chombo chochote duniani (Financial Institution) kama hiki kwa mavuno yake, ni mara ya kwanza kusikia...

Mzunguko wake ni mfupi sana kwa muda mfupi sana kiasi kwamba najaribu kutazama jinsi UPATU unavyochezwa..bado nashindwa kuelewa hizo figures kwani hata Upatu unategemea kuzunguka kutokana na idadi wa wanachama..Sasa hapa DECI inaonyesha idadi ya wanachama sio sababu isipokuwa wana formula yao wenyewe..
Hakika, ningeomba mtu anayefahamu jinsi wanavyocheza Upatu huu ili tuweze kutazama uwezekano wa akina sisi Diaspora tuucheze pia kivyetu vyetu..
 
.....Naungana na wenye wasiwasi na huu mradi ambao una kila dalili ya kuwa Dollarjet na upatu vilivyopata kuwaliza watu siku za nyuma LAKINI maybe, just maybe, inawezekana;
Benki ya CRDB wanatoa riba ya 2% kwa SIKU 30 kwa kila shilingi milioni 100 utakazoweka kwenye fixed account. Hii ina maana kuwa kila bada ya siku 30 milioni mia moja yako itakupa shilingi milioni 2.

Suppose hawa jamaa wana mafungu 10 tu ya shilingi milioni 100 kila moja, ina maana kila mwezi wanaingiza shilingi milioni 20 na kwa maana hiyo baada ya miezi minne wana milioni 80!!
Surely, hii sum can be enough to pay 'wawekezaji' kadhaa walioweka tulaki mbili twao miezi minne kabla, bila kusahau kuwa hao jamaa bado wata-retain asilimia fulani ya hela hiyo kama alivyosema mchangiaji mmoja hapa?
going by this hesabu, maybe, just maybe inawezekana...?!

2% interest kwa siku 30 means the following::

The interest will be 2% if the money is held kwenye hiyo account kwa miezi yote 12, sasa ukiweka kwa siku 30 tu interest ni 2% divide by 12, kwa kufuata mfano wako

100million profit in 30 days === 100mil * 0.02 /12 == 166,666 Tshs
 
Haya ndiyo matatizo yetu tunapoteza muda kwa jambo lililo wazi kabisa kila mwenye akili timamu anajua hiki ni kiini mach😵k mwenye pesa za kuchezea apeleke asiekuwa nazo auchune please no more malumbano about this,BYE.
 
DECI is scheming ponzing just like Bernard Madoff
 
1: Kijiji kina watu 10000

2. Watu wa 10 wa kwanza wasio na fedha wanaanzisha mradi wa DECI.

Wanasema kujiunga nao ni Shs. 200,000

Watu 1000 wanajiunga kwa kutoa Tsh200,000 kila mmoja. (Kijiji kinabakia na watu 8990.

Kwa kiyo Mtaji wa kwanza ni: Tsh. 200,000,000 (za wale watu 10)

Hawa wanaambiwa wasubiri miezi minne ili “wavune” faida.


3. Wanatangaza na watu wengine 1500 wanajiunga kijiji kinabakiwa na watu 7490

Watu wale 1500 wanaleta mtaji mpya wa milioni 300,000,000

Miezi minne inapopita wale 1000 wa kwanza wanalipwa fedha yao milioni 200, na kila mmoja anapata “faida” ya laki moja moja hivyo kila aliyeingia na laki mbili miezi minne anatoka na laki tatu!

4. Wanaingia watu wengi zaidi sasa nao wanafikia 2000 nao wanataka haya mavuno! Kijiji kinabakiwa na watu 5490 ambao sio wanachama.

5. Wale watu 2000 wanaingia na mtaji wa 400,000,000.

Sasa hapa ndipo kuna kitu cha kuangalia vizuri

a. kuna watu 1500 ambao wanatakiwa kulipwa laki mbili zao (kwa jumla ya milioni 300 za mbegu). Lakini pia wanatajia kupata kila mmoja laki moja zaidi kama faida.

b. Hivyo pamoja na kiasi hicho unatakiwa mradi wa milioni 150 zaidi kama faida ya kundi lile la pili.

c. Kiasi hicho kinatolewa kwa wale waliokuwa na milioni 400 na hivyo kufanya wale wanaoingia na milioni mia nne kimsingi kuwa wamekingia na milioni 250! (hilo si tatizo kwa sasa).

d. So wale wa kundi la pili wanaondoka na wao na laki tatu tatu kwa furaha ya “mvunaji”

6. Hivyo kampuni yetu inaanzisha recruitment drive nyingine na watu wengine 3000 wanajiunga na kampuni yetu hii ya mavuno. Kijiji kinabakiwa na 2490 ambao wengi wao wanaonekana kuwa ni wanachama wa JF!! Hao nao wanaingia na mtaji wa 600,000,000!

7. Hivyo muda umefika wa kuwalipa walioingia na milioni 400! So wale milioni mia nne kwanza wanalipwa “seed money yao) ambayo ni kiasi hicho hicho. Lakini wanataka faida yao ya laki moja moja kila mmoja.

- Hivyo zinahitajika milioni 200 nyingine na hivyo kuchukua kabisa mtaji wa wale wa milioni 600, kuwalipa wao na hivyo wale wa milioni 600.

So wale wa milioni mia nne wanaondoka kwa furaha kwani wamepata fedha yao.

8 Wale wa milioni mia sita (ambao ni wengi zaidi – 3000) na wenyewe wanaambiwa wasubiri fedha zao hadi mwisho wa miezi minna.

9. Sasa recruitment inaenda na kuwashawishi wale 2490 waliosalia kijijini kujiunga ili “wavune. Nao wanaingia na mtaji wa 498000! (mara moja tunaona kuwa wanaingia na kiasi pungufu.

Kampuni yetu ifanye nini basi;

10. Kampuni inawashawishi wale waliokwisha pewa mavuno yao kuzizungusha fedha hizo hizo tena kwenye mfumo huo. Kwa hiyo wale wa 1000, na wale 1500 na wanatakiwa kuzungusha fedha zao humo kwa humo.

NOW THIS HOW THE SYSTEM COLLAPSES:

SCENARIO ONE:

a. Baada ya wale 2490 kuingia na kulipa milioni 498 wale wa milioni 600 watajikuta wanapungukiwa Sh 102! Bila ya fedha kuzungushwa tena kundi la milioni 600 wataanza kulalamika.
b. Wakati hao wanaanza kulalamika kundi lile la 2490 linasubiri kiasi walichoingia nacho (kwa maana angalau waliokwishalipwa awali idadi kama yao wawe wamzungusha tena fedha). Na pia wanasubiri milioni 249 kama faida! (kwa maana ya kwamba wanahitajika watu wengine kama 50 hivi kujiunga kuweza kuzalisha hiyo faida.

SCENARIO TWO:

a. Hii inategemea idadi ya watu ambao wako tayari kuzungusha fedha zao ndani kwa ndani. Kinachofanyika hapa ni saikolojia ya fedha. Wakikupa laki moja faida na wakakuambia uziingize tena kwenye system itabadi urudishe laki mbili kwao tena, na wewe unabakiwa na laki moja! Katika mfano halisi wa DECI ni kwamba wanakulipa laki tatu, na unaweza kuzirudisha kwa mafungu laki mbili mbili, hivyo utarudisha kwao zile za kwako (laki mbili) za kwao (laki mbili) na wewe unabakia na laki moja! Ulichofurahia kimsingi ni wewe kuwa na “laki tatu” kwa muda fulani, siyo kuzitumia.
b. Hili hata hivyo linatabia ya kuchosha huwezi kuwa na fedha usiyoitumia! Hivyo collapse ya pili itatokea pale watu ambao wamekuwa wakizungusha fedha zao huko kwenye kampuni watakapoamua kuziondoa kwenye mzunguko! Kwa maneno mengine wale 1000, na wale 2000 na wale wa 3000 watakapoamua kuondoka na fedha zao wale wa mwisho 2490 watajikuta wameliwa karibu milioni 500!


So:

a. Kwa kadiri ya kwamba watu wapya wanazidi kujiunga ndivyo watu walio chini wanazidi kupata fedha!

b. Kwa kadiri waliochini hawatumii fedha zao kujihudumia (wanaishia kuzizungusha katika mzunguko usiokoma) vivyo hivyo waliojuu yao kidogo na wanapata fedha.

c. Siku wale wa chini watakapokoma kuzungusha fedha zao na kuziondoa basi wataondoa msingi mkubwa wa scheme hii so, IT WILL COLLAPSE!

d. Siku hakuna watu wapya hawajiungi tena na wale wa chini wamezungusha fedha yao basi utakuta kuna kundi kubwa halilipwi isipokuwa lile kundi la kati; so the scheme will still COLLAPSE!

e. Siku deni la wale waliiojuu (waliojiunga) linazidi fedha iliyopo kuwalipa waliokati ili nao wazungushe fedha, the scheme will still collapse.

HOWEVER you CAN BEAT THEIR SYSTEM IF YOU ARE NOT GREEDY!

- Kama kuna kiasi kikubwa cha fedha kinazungushwa kwa mfumo wa tahadhari isianguke mapema, basi scheme hii inaweza kuchukua angalau miaka si chini ya matano kuanguka, so kama unataka hela ya haraka haraka, ingia na mafungu na milioni moja katika mafungu matano:

a. 200,000 itakuzalishia 255,000 za ziada * 5 + 1,275,000 (faida)
b. Usizungushe fedha unayochuua mwanzo hadi uchukue yote 1.275 plus your initial seed money.

b. Ile milioni moja ya kwanza USIIRUDISHE!

c. Ile milioni 1.275 USIIRUDISHE IPELEKE KWENYE biashara nyingine tradition (weka akiba, weka paa jipya, n.k n.k)

d. Repeat this scheme so that when the scheme collapses na wakati huo ukiwe umewekeza laki mbili, wala huna sababu ya kulalamika!
 
Mwanakijiji,
Mkuu wangu jaribu kila njia huwezi kupata suluhu kirahisi hivyo..
Tuache hizo hesabu za kijiji kuwa na watu wangapi hata iwe millioni moja swala bado linahusiana na watu wanaotoa fedha zao kujiunga..

Mfano wa kwanza umezungumzia watu 1000 kujiunga na mtaji wa Tsh. 200,000 hawa wanaleta millioni 3,... Sawa kabisa lakini kumbuka tu kwamba hawa jamaa miezi 4 ijayo wanachukua 300,000 against 200,000 walizoweka..meaning DECI watawezxa kuzalisha millioni 1 within 4 month (faida ya watu 1000) na hata kama imetokana na watu wengine 1500 waliojiunga upya iwe mtaji wa kutoa hizo millioni 1. Kumbuka tu DECI haitakuwa tena na zile Tsh. 2 millioni za watu 1000 waliojiunga mwanzo..wametumia million 3 za wateja wapya na bado kubakia na deni la hawa watu 1500 na faida yao..

Sasa mathlan nao wamerudisha tena 200,000 zao kwa matumaini ya kuzalisha tena 100,000 within next 4 month, DECI itatakiwa kulipa wale 1500 millioni 4 including faida, baada ya miezi 4 na mwezi unaofuata tena kulipa hawa 1000 millioni 3 nyingine..Hivyo pamoja na kwamba DECI wamekusanya millioni 7 (2+3+2) watakuwa wamelipa millioni 10 (3+4+3) within 12 month of a year...kuna millioni 3 hapa hatufahamu wameweza vipi kuzalishwa unless DECI wanatumia tena fedha za wengine hao 2000 wakatao jiunga upya na kuwa wadeni vile vile..

Itaendelea hivyo hivyo unless tufahamu hawa jamaa hizo faida wanazilipa toka wapi na kama wanatumia mifuko ya watu au wanachama kujiunga.. Itatokea kitu gani siku (jumla ya miezi minne) wanachama wapya wakijiunga less than 1000 au hesabu ya watu wanaotegemea kulipwa mwezi unaofuata!.. Kwa sababu inaonyesha ni kitu kama Upatu ambao unategemea watu lakini dhamana ya waliowekesha hela zao inategemea na hesabu ya watu wangapi watajiunga.

Hivyo kwa mfano wako wa mwanzo chukulia kinyume yaani imefika siku waliojiunga ni 100,000 (kijiji kizima) na wanasubiri miezi 4 wachukue fedha zao na faida.. DECI watazipata wapi hizo faida hata kama mtaji wa watu 100,000 wanao.

Mkuu wangu hata ukizungusha vipi ni lazima miezi minne mtaji wa 200,000 uzalishe zaidi ya 100,000 ili upate kugawa faida, haiwezekani kabisa kutumia fedha ya watu ktk upatu unaochukua muda mfupi hivyo wa miezi 4 na kikubwa zaidi ni kwamba wanachukua faida sio juu.
 
.....debate sasa basi maana huu ni wizi wa mchana kila mtu anajua, mlio Dar naomba msaidie kuwaripoti hawa watu kwenye vyombo vya sheria kabla ya mwanawamungu na wasioelewa hizi game hawajapoteza mitaji yao,mtakuwa mmefanya good public service na itapunguza umaskini kwa wale wanaoelekea kupoteza pesa zao soon or later,mnaweza kureport police,TRA au wizarani!
 
.....debate sasa basi maana huu ni wizi wa mchana kila mtu anajua, mlio Dar naomba msaidie kuwaripoti hawa watu kwenye vyombo vya sheria kabla ya mwanawamungu na wasioelewa hizi game hawajapoteza mitaji yao,mtakuwa mmefanya good public service na itapunguza umaskini kwa wale wanaoelekea kupoteza pesa zao soon or later,mnaweza kureport police,TRA au wizarani!

aaaah... uuuhhh.. well.. police ndiyo wanatoa ulinzi kwenye hivyo vituo.. na hao wengine ndio wametoa leseni so...
 
.....Naungana na wenye wasiwasi na huu mradi ambao una kila dalili ya kuwa Dollarjet na upatu vilivyopata kuwaliza watu siku za nyuma LAKINI maybe, just maybe, inawezekana;
Benki ya CRDB wanatoa riba ya 2% kwa SIKU 30 kwa kila shilingi milioni 100 utakazoweka kwenye fixed account. Hii ina maana kuwa kila bada ya siku 30 milioni mia moja yako itakupa shilingi milioni 2.
Suppose hawa jamaa wana mafungu 10 tu ya shilingi milioni 100 kila moja, ina maana kila mwezi wanaingiza shilingi milioni 20 na kwa maana hiyo baada ya miezi minne wana milioni 80!!
Surely, hii sum can be enough to pay 'wawekezaji' kadhaa walioweka tulaki mbili twao miezi minne kabla, bila kusahau kuwa hao jamaa bado wata-retain asilimia fulani ya hela hiyo kama alivyosema mchangiaji mmoja hapa?
going by this hesabu, maybe, just maybe inawezekana...?!

BabaDesi, haitawezekana kwa kuweka kwenye account za 2%. Inawezekana tu kwa kuzifanyia biashara inayoingiza pesa nyingi na yenye wateja wengi.

Nionavyo mimi, DECI wametumia akili zao vizuri sana ili kujipatia mtaji. Ukweli ni kwamba, biashara yao hii, inawaruhusu kuanza na ZERO capital. Wachangiaji ndio watakaowapa wao fedha. wanachotakiwa ni ku-monitor carefully flow ya members wao.
 
Tatizo, hili jambo halikuwa kwa watu wote ninyi, lilikuwa kwa watz wachache ambao ni walokole, hata halikuwa linawahusu. tumewahusisha mmeanza kutuchefua? tutarudisha liwe kwa walokole tu. sisi kama walokole tunaridhika, na maadam tumesha vuna kwa mara nyingi tukapata faida, hatuna shida. hata ikiisha leo hatuna hasara. pilipili usoila inawawashia nini? wanaotumia wamenyamaza kimya, ninyi ambao hamjatumia mnaongea.

Mnaweza mkamkomvisi vipi mtu ambaye ameshavuna pesa mara kibao, aliweka laki mbili amesha vuna mle takribani million nne tayari, sasa. tunapata faida, na hatutaiacha, na hata kama watu watasema sana, mnachelewa bure, mtasema matokeo yake mtakuja kuujua ukweli wake muda wakati umeisha na ninyi nafasi ya kufaidika imefungwa. kalaga baho.
 
Wewe kama mwana wa Mungu usiseme hivyo unakosea, wewe kama ni nuru endelea kuangaza hatimaye mwanga wako utaonekana, kama mwanga wenyewe upo. Usikate tamaa kuwaongoza wasio ona mwanga.

Ila bado hujajibu swali, deci wakikusanya hiyo hela wanafanyia nini huko nyuma ya pazia?
 
Tatizo, hili jambo halikuwa kwa watu wote ninyi, lilikuwa kwa watz wachache ambao ni walokole, hata halikuwa linawahusu. tumewahusisha mmeanza kutuchefua? tutarudisha liwe kwa walokole tu. sisi kama walokole tunaridhika, na maadam tumesha vuna kwa mara nyingi tukapata faida, hatuna shida. hata ikiisha leo hatuna hasara. pilipili usoila inawawashia nini? wanaotumia wamenyamaza kimya, ninyi ambao hamjatumia mnaongea. mnaweza mkamkomvisi vipi mtu ambaye ameshavuna pesa mara kibao, aliweka laki mbili amesha vuna mle takribani million nne tayari, sasa. tunapata faida, na hatutaiacha, na hata kama watu watasema sana, mnachelewa bure, mtasema matokeo yake mtakuja kuujua ukweli wake muda wakati umeisha na ninyi nafasi ya kufaidika imefungwa. kalaga baho.

Naomba unielewe utakavyopenda ila niwe wazi tu kwamba wewe si mwana wa Mungu bali wa shetani!

Nimesema huko nyuma na nitaendelea kusema tu kwamba walokole si malaika. Wapo wachungaji na waumini kibao tu huko jela kwa makosa ya jinai. Nadhani itakuwa busara kama mkiendelea na mambo yenu kwa siri, kuliko kutuletea kichefu chefu cha wizi wa wazi na kujaribu kutetea upuuzi. Tunaamua kunyamaza tu, ila inaeleweka wazi kwamba yapo mambo mengi sana yanayoendelea ndani ya fellowships za walokole. Hata ngono tunajua zinaendelea kwa kulana wenyewe kwa wenyewe.

Kwa hiyo nakuomba ulete mambo ya maana hapa badala ya kutetea hoja kwa ngonjera!
 
deci aka tushikamane revolving fund wamesajiliwa na wana tin number
105 797 095.
Maelezo ya waliotangulia yana mapungufu ambayo nitarekebisha hapa.
Kiwango cha chini '' kupanda'' ni sh. Elfu kumi na kiwango cha juu ni sh. Laki mbili. Hata hivyo mtu anaweze kupanda zaidi ya sh. Laki mbili kwa mafungu, mfano ukipanda laki nne unahesabiwa umepanda laki mbili mara mbili. '' kuvuna'' ni mara moja kwa wiki hivyo basi hata kama ukipanda laki nne kwa siku moja lakini wakati wa ''kuvuna'' utazivuna kwa wiki mbili tofauti.
Mahesabu ya kuvuna kwa aleyepanda sh. Laki mbili yako hivi: Baada ya miezi minne laki mbili inakuwa laki tano. Ni lazima utrudishe sh. Laki mbili shambani na wewe unabaki na laki tatu. Katia hiyo laki tatu unakatwa tax ya asilimia 15 ambayo ni sh. Elfu 45. Kwa hiyo unabakiwa na sh. 255,000. Kila baada ya miezi minne cycle hiyo inajirudia. Hivyo basi kwa kupanda sh laki mbili unavuna sh. 765,000 kwa mwaka (miezi 12).
Well cha msingi ni kwamba mpaka sasa waliojiunga hawana malalamiko,ingawa ukweli ni kwamba kuna siku deci itatetereka kwa sababu kadhaa nilizozibaini. Sitazitaja zote hapa kwa usalama wa walioweka pesa zao ila sababu moja kubwa ni ukosekanaji wa professionalism katika money handling.naomba nisilielezee hili kwa undani pia kwa sababu za kiusalama.
Idara ya fedha kama deci ambayo sasa ina pesa nyingi ilitarajiwa kuendeshwa kitaalamu zaidi ya ilivyo sasa.mfano rahisi wa kuchallenge jinsi inavyoendeshwa ni email address yao ambayo ni decitanzania@yahoo.com
deci kama multibillion project inatarajiwa kuwa na domein yake na si kutumia yahoo etc...!!!
Ushauri ninaoutoa ni kwa walio na access na deci wajiunge mapema ili waweze kunufaika kabla muda wake wa kutetereka haujafika. Hakuna anayeweza kusama hadharani muda huo ni lini lakini tukumbuke kuwa no risk, no profit.

huu ni upatu through and through,ndugu zangu wekezeni hapo at your own peril!!
 
Last edited:
Mwanawa Mungu,
Mkuu unapofungua Financial Institution yoyote ile hata kama ni kwa baadhi members Only, serikali na wananchi wake wanatakiwa kufahamu kinachoendelea...Hakuna mtu anayesema DECI iwashirikishe watu wote isipokuwa tunaulizia jinsi mnavyofanya kazi ili kesho kama kuna uvunjaji wa sheria (Utapeli) ifahamike wazi kina nani wahusika.

Binafsi sioni kama swala hili haliwezekani kabisa maadam DECI wanafahamu wapi wana invest fedha hizo na kwa muda mfupi sana wakaingiza faida kubwa ambayo bila kuchukua interest wao wakazigawa kwa wahusika..
Najua vizuri kwamba Tanzania kuna biashara ambazo huingiza faida mara 5, biashara kama za kwenda China kuchukua mali feki ambazo huuzwa kwa bei ya juu. Kuna madini, na mengineyo ambayo kuna vijana wengi sana wametajirika toka msingi mbuzi kabisa...

DECI kwa kutumia jina la dini (misaada) kupata tax exemptions ambazo zinaongeza pato au faida..kwa hiyo inawezekana maadam hakuna mazishi. Isipokuwa tu kinachonipa/tupa wasiwasi ni kama hakuna biashara yoyote ila ni Upatu ambao unazaa kwa miujiza ya Mungu..Na ndio sababu kubwa tunajaribu kuwatahadhalisha wananchi..
Mlokole ni binadamu, hata mimi kesho naweza kuwa mlokole haina maana walokole huzaliwa kama taifa la Walokole..
 
Back
Top Bottom