DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

Well mimi katika DECI nimepanda 2Million ambazo zimepelekwa kwa laki 2 kila mpando so mpaka sasa zote zimeshatoa mavuno ya kwanza ambayo ukishatoa makato ya 15% nimepata 2,550,000 ambayo ni kutoka July 08 mpaka Jan 09. Nilipovuna nilipanda tena so kati April na June 09 nitavuna tena 2,550,000. Ukilinganisha hizo hela kama ningeziweka bank nisingeweza kupata hiyo faida. Hivyo si lazima uweke mahela kibao weka kidogo ikusaidie katika mambo madogo kama fees za watoto au hata biashara za kawaida.

Mimi ushauri wangu ni kuwa ni kweli hii system haileweki kwa undani lakini office ziko wazi pale mabibo na kwenye attachment zangu za jana nimeonyesha kuna simu wapigie watakupa majibu.

Hawa jamaa wanautaratibu kwani ukilipa unapewa receipt ambayo utakwenda nayo ukienda kuvuna na pia kuna registration ambayo unapewa kitambulisho. Kwenye receipt yao kuna mpaka TIN NUMBER kwahiyo wanafanya kazi ya halali kabisa.

Tufuatilie kwa undani tusiwakatishe tamaa wengine ambao kwa kweli wana mahitaji ya kweli katika huduma kama hizi. Tusiwe sana negative katika kila kitu. Tufuatilie ili kama kuna utata tuambiana.

Thanx

Kwamba tayari watu wamenufaika hakuna anayekataa.

Kwamba kuna watu wanataka kukatisha tamaa wengine wasipate kipato, sidhani kama ni hivyo.

Kwamba wanaopinga hawajafanya utafiti sawasawa. Sina hakika.

Nilicho na hakika, watu wanahoji msingi wa hili. Na wanaoohoji msingi, naamini ni watu wa fikra, si watu wa juu juu.

Ndugu zangu sehemu mbalimbali duniani watu wameamini michezo hii na wakalizwa. Naweka link hii hapa muone jinsi Columbia watu walivyopoteza mabilioni ya pesa, kwa scheme kama hizo ambazo waliziamini mno, ndo maana wakajiunga kwa wingi.


http://www.latinalista.net/linkinglatinas/2008/11/colombia_pyramid_money_scams_fall_down_a.html

Moja ya picha ya waliolizwa ni hii hapa kwenye attachment. Wakati huo too late!

Well, kama systems kama hizo zingedumu milele, kwa nini watu wangehangaika na pesa za kutokea jasho????

Lakini kama watu wote pia wangepata mahitaji yao katika system kama hizo, uzalishaji wa mahitaji muhimu ungekoma..... Well, at least sioni kama mapato ya hivyo ni sustainable, unless DECI watuoneshe huo mgodi wa dhahabu wanaozalisha za kuvunisha watu.

Mnapojibu mjue tunatafiti.

3767d1236364525-deci-ni-nini-hasa-uripiram.jpg

 

Attachments

  • uripiram.jpg
    uripiram.jpg
    13.9 KB · Views: 72
Last edited:
Swala la DECI mie nadhani uwaachie wahusika kwa sababu najua kwamba mpaka mtu afikie hatua ya kutoa fedha zake na kujiunga atakuw ana akili timamu.
Kwenda DECI hulazimishwi sasa ambacho chakutia wasiwasi ni nini? Ninchokushauri wewe ni kufanya uchunguzi then ndo uje umwage data zako.
"No Research, No Right to speak"

Well, tunahoji MISINGI ya DECI. Hiyo biashara inayozalisha asilimia 100 ndani ya miezi minne, ni ipi?

Je itaendelea hivyo milele?

Hukatazwi kuendelea kupanda na kuvuna, lakini ni vema ukajua kuwa wanakuzalishiaje. Benki tunajuwa wanakopesha kwa riba kubwa kuliko ya akaunti za akiba za watu, pia wanakuwa na vitega uchumi. Lakini chanzo cha uzalishaji wa DECI ni nini? Tunahoji MSINGI wa DECI.

Kuwa na TIN namba si hoja. Just let those who run the system be transparent.

Asante.
 
Mkuu kwa taarifa yako kilio kinakungojea, soma ponzi (Piramids) scheme definition zake halafu angalia zinavyowafanya investors wa hiyo scheme.

Hapa ni mojawapo ya hizo scheme ambayo imekuwa kivutio kikubwa duniani Bernard Madoff
On December 10, 2008, Bernard Madoff, the former non-executive chairman of the NASDAQ Stock Market, allegedly told his sons that the asset management arm of his firm was a massive Ponzi scheme - as he put it, "one big lie." The following day he was arrested and charged with a single count of securities fraud - but one that accuses him of milking his investors of $50 billion.[4] This may be the largest Ponzi scheme ever perpetrated, as well as the largest investment fraud ever committed by a single person.[5] One of Madoff's biggest investors, René-Thierry Magon de la Villehuchet of Access International Advisors, committed suicide around December 23, 2008, following the disclosure of $1.5 billion in losses.[6][7]
Ponzi scheme - Wikipedia, the free encyclopedia

Kinachobadirika ni majina, mchezo ni ule ule either uitwe DECI, Piramids, or Ponzi...
Ushauri wa mwisho fikiria kabla ya kuinvest katika kitu usichokijua.
 
Last edited:
kwa taarifa yako, Yesu anataka watu wawe matajiri, alileta uhuru tutoke kwenye umasikini twende kwenye utajiri.

Are you serious?

Is this really what you believe? Materialism?

Well, If Jesus returns today, He may fail to recognise some of those who call themselves His followers!

Mmmmmmh!
 
kama mnajiuliza jinsi inavyofanya kazi, nendeni pale mabibo mkaulize, sio mnakaa kusikiliza mambo ya wachangiaji wa hapa ambao hata hawajui kinachoendelea kule. wengi hapa walikuwa hata hawajui iko ofisi za wapi, kinachoonyesha kuwa hamuijui kabisa hivyo msichangie hadi mwende mkafanye utafiti. mimi nitaishia hapo. isipokuwa, mtu ukipanda kule Deci, unakaa miezi mitatu na nusu ndio unaenda kuvuna, sio mwezi mmoja kama wengine walivyosema hapa. asante.


Mnachofichwa na waendeshaji wa scheme hii ni hiki hapa. Bonyeza hapa uone MSINGI wa "investment" kama za DECI. Hizi zimeleta matatizo pengi tu. Hata sasa kuna kesi ya Madoff huko America ya kutapeli zaidi ya Bilioni 50 kwa scheme ya hivyo.

Kupanga ni kuchagua. Think twice.
 
Pale Mabibo mwisho kuna kampuni inaitwa DECI. Inasema ukiweka pesa unapata faida kubwa tena baada ya muda mfupi. Nimeona pia wamefungua ofisi maeneo mbalimbali ya nchi kama Mwanza, Biharamulo, Bukoba nk. Hati ya kuandikishwa kama kampuni iliyotolewa na Msajili wa Makampuni ni Na. 61334 ya mwaka 2007. Wameandikishwa pia na TRA. Kikubwa zaidi, wanayo barua ya BOT inayoonyesha kuwa wanatambuliwa.

WanaJF wenzangu naomba mwenye data zaidi juu ya kampuni hii aziweke hapa hadharani tujue, isije ikawa ni utapeli. Kilichonistua zaidi ni kuona kuwa wameandikishwa kama kampuni na BOT haielezi kama inawatambua kama financial institution.
 
PanguPakavu heshima mbele. Umesema ukweli. Hi DECI DECI sio kitu kingine ila ni ponzi scheme full stop. Katika ponzi scheme kawaida hufaidka wawekezaji wale wa mwanzo au niwaite wawekezaji wa first stages. watapata faida sawa, lakini ili mchezo uendelee kuzalisha faida inayoahidiwa lazima wanachama wengi waingie kwenye soko la kuwekeza. Wanachama wa mwanzo, kama alivyosema mwanakijiji, hulipwa fedha zao na faida waliohaidiwa kutokana na ada ya wanachama wapya.

Ni lazima wanachama wapya wawe mara dufu (Kawaida ni lazima wawe mara nne au tano) ya wale wa mwanzo ili mchezo uweze kuendelea. Ndugu zangu wa mabibo wanaopiga foleni kujiandikisha wanawalipa watangulizi wao, waombe mungu wapate wafuasui (wawekezaji) wengi nyuma yao ili wapate faida wanayoitamani.

I have no doubt, it is just a matter of time before the whole scheme disintergrates. When such a scenerio unfolds the loosers will constitute not less than 70% of the whole participants. It is a sheer imposibilty that a normal investment accrues more than 100% interest rate.
This is a risky endeavour!! think twice before you throw yourself into it!
 
Tatizo, hili jambo halikuwa kwa watu wote ninyi, lilikuwa kwa watz wachache ambao ni walokole, hata halikuwa linawahusu. tumewahusisha mmeanza kutuchefua? tutarudisha liwe kwa walokole tu. sisi kama walokole tunaridhika, na maadam tumesha vuna kwa mara nyingi tukapata faida, hatuna shida. hata ikiisha leo hatuna hasara. pilipili usoila inawawashia nini? wanaotumia wamenyamaza kimya, ninyi ambao hamjatumia mnaongea. mnaweza mkamkomvisi vipi mtu ambaye ameshavuna pesa mara kibao, aliweka laki mbili amesha vuna mle takribani million nne tayari, sasa. tunapata faida, na hatutaiacha, na hata kama watu watasema sana, mnachelewa bure, mtasema matokeo yake mtakuja kuujua ukweli wake muda wakati umeisha na ninyi nafasi ya kufaidika imefungwa. kalaga baho.

Sasa hao walokole wako unlimited numbers Tanzania? Ndio kuna watu watafaidika, hata Madoff amewafaidisha watu wengiu sana, hasa wale wawekezaji wa kwanza, kama umefaidika jihesabu kama una bahati na jitoe now! Hizi pyramid scheme zote mwishoni ni unsastainable lazima wawekezaji wapya waishe labda sio leo au hata kesho lakini lazima waishe.

Halafu kwa watu wa dini hamuoni kuna moral dilemma ya kuwaliza wenzenu watakaofuata? Laima kuna mtu atalizwa na kwa kuvuna nyie mnachangia kuwaliza wenzenu.
All the best.
 
kama ni wezi wamemuibia nani? ninao ndugu zangu wengi tu, nimewakopesha pesa, wakaenda kuziweka huko. wameshavuna mavuno karibia mawili. unaweza ukaweka hela za mtoto wako mmoja mmoja,dada zako hata shangazi nk. na utapata. kuna watu wanavuna karibia kila baada ya miezi mitatu, kutu kama million hadi tano pale, kwasababu waliweka zamani, na ile pesa waliyoingilia walishaipokea na wana kulaga faida. Kwa kifupi DESI SIO KWAMBA WANAKOPESHA AU NINI, NI SAWA NA UMEPANDA MTI WA MATUNDA, HIVYO UNAKUWA UNAVUNA KILA WAKATI HADI MTI HUO UTAKAPOZEEKA. unaweza ukavuna pesa za deci hadi miaka 50. ina faida sana. mimi nilifikiri ni wanigeria mwanzoni, nikaenda kuweka pesa pia, na nimepokea mihela kibao. wapo pale mabibo mwisho, watu wanapaki magari yao pale wanaweka hela na kuondoa. inasaidia sana, na kuna watz wengi wanaishi kwa hiyo.

The question still remains "How do these guys make money?" Wanawezaje kuzalisha pesa yote hiyo katika kipindi hicho kifupi? Hili ndilo swali linanifanya hata mimi kuwa "skeptical" na mpango huu wa kutafuta utajiri wa haraka bila kuutolea jasho. Pia nilishawahi kuona karatasi yao ya kumkaribisha/kumvuta mteja mpya..

Jamaa wamejirizevia haki ya kubadilisha sheria za "Ponzi yao" wakati wowote which for me naona kama ndio inaongeza ile "associated risk" ya kuwa kwenye mpango wa uvunaji wa DECI! Lengo lao ni nini kwanza? Are they after profit au charity? Maswali ya kujiuliza, for a smart person, ni mengi mno jamani!..
 
The question still remains "How do these guys make money?" Wanawezaje kuzalisha pesa yote hiyo katika kipindi hicho kifupi? Hili ndilo swali linanifanya hata mimi kuwa "skeptical" na mpango huu wa kutafuta utajiri wa haraka bila kuutolea jasho...Pia nilishawahi kuona karatasi yao ya kumkaribisha/kumvuta mteja mpya..Jamaa wamejirizevia haki ya kubadilisha sheria za "Ponzi yao" wakati wowote which for me naona kama ndio inaongeza ile "associated risk" ya kuwa kwenye mpango wa uvunaji wa DECI! Lengo lao ni nini kwanza? Are they after profit au charity? Maswali ya kujiuliza, for a smart person, ni mengi mno jamani!..

HOW DO THEY MAKE MONEY?
Wanazungusha hela kama upatu, sema mfano mpo mia,kila mwezi anachukua hela mtu mwingine. Ila kwenye hii, pool ya watu ni wengi sana,hela mingi sana watatoa tuu. mwisho wao wanachukua chao nyie mnabaki mnalia....
 
HOW DO THEY MAKE MONEY?
Wanazungusha hela kama upatu, sema mfano mpo mia,kila mwezi anachukua hela mtu mwingine. Ila kwenye hii, pool ya watu ni wengi sana,hela mingi sana watatoa tuu. mwisho wao wanachukua chao nyie mnabaki mnalia....



Hawa jamaa sijui wanapataje pesa zote hizi,kimahesabu hamna jinsi ambavyo unaweza pata faida kubwa namna hiyo kwa muda mfupi, nafikiri they are after something, hapa tuwaombe wanausalama washughulike nao tupate uhakika wao vinginevyo mwisho wa siku usipolia wewe atalia mkeo, au dada yako, kama sio Mama.
 
Wana JF, naomba kama mwenye muda wake ajaribu kusoma hii email niliyoipata kutoka kwa mchangiaji mmoja wa hizi schemes zinazojadiliwa hapa. Labda itatoa uwamja mzuri wa kujadili.


Dear brethren

Although you have seen good user interface of this game, you have has well
been binded to the backend of the same

Just answer this quetion if you have alternative answer
Where on Earth you can have a business where you invest tsh 200,000/= for the
three months only you gain tsh 2,000,000/=? 10,000% gain in 1 or 2 yrs????

The answer is clear , that is in ufisadis, embezzlement, robbery , theft ,
conning, blackmail and the likes

this is totally against the business/commercial rules as well as a God's Law

how can just someone post a large amount of money int my account without
offering any service, any consultancy, any goods to sell and even he does
not know me!! . Can I account it as an income!!

you see the business rules require exchange of goods or services with
money. gain money out of that (unless otherwise it is reward)it is
shamefully and it is contrary to God's which state that "In the sweat of
thy face shalt thou eat bread"

dear brothers and sisters, the reality of this game is to mastermind you
and enter into state of either been a robber or someone will be robbed. in
order for game to be successfully there must be few robbers and many
loosers. At the end those who entered first will be robberers and many
later comers will be loosers. Just check illustrations below

It is like bussinessman/promoter who invited people to come with their
money into closed playground. That promoter just take entrance fees from
them and then tell them to play themselves with the money remain. and the
game is this, just handle you money to the First In. the problem with this
is that at the saturation point when ground is full and no any other who
is comming in, the First In who are few will remain with money, promoter
will remain with fees and Last In who are many will remain with forms. and
because there is no referees after 90 minutes gainers and promoter will go
they are ways lefting loosers puzzled in the ground because they have no
even the fare to aboard a bus to Manseze. Will a bus conductor accept a
form? the answer is BIG NO.

While the game like 'Bahati Nasibu' (which I hate too) people enter with
knowledge that they can either win or loose, The pryramid games assure
someone that he will gain, that there is no loosers which is cheatings and
because of that I DOUBLE hate it. you can just take example of dollar Jet.

Brethren stay away from this game, stick to rules and regulations that
govern your income, be smart and God will bless you for renouncing the
shamefully income. In order for people to gain unlawfully, they have to
break rules and regulations thereof. Look into Dowawn saga, they want to
break the procurement act so that they can rob our money. I concur with
Dr. Mwakyembe who said "It is better to stay in darkness than breaking the
law" Such words are comming from someone who know the VALUE OF KEEPING THE
LAW, THE PRICE OF BREAKING IT AND OUTCOME THEREOF. and this is the
Outcome: At the end you will inherit the SHAME.

So compete according to rules and shun away from sinfull way. it is better
to be looser than gainer just because you will bring shamefull(cursed)
income into your familly and that is terrible.

Let those who have ears hear the words of this article. At the end they
will inherit the PEACE.
 
Ni kweli hatuwezi kusema hawa ni wezi au matapeli kwani mpaka sasa hatujasikia taarifa nyingine tofauti, bali kuchukua tahadhari ni jambo muhimu sana. Ningeshauri hawa jamaa wajipange vizuri kwenye mambo ya management kuwa na watu ambao ni professionla ili watatnzania wenzetu wasije kubaki midomo wazi siku moja.

Bali watanzania wakati umefika kufikiria zaidi kuzalisha mali kulikoni njia hizi za kiusanii katika kujiletea maendeleo. Watu wafikirie zaidi katika miradi midogo midogo endelevu katika sekta ya kilimo na ufugaji.
 
Ni kweli hatuwezi kusema hawa ni wezi au matapeli kwani mpaka sasa hatujasikia taarifa nyingine tofauti, bali kuchukua tahadhari ni jambo muhimu sana. Ningeshauri hawa jamaa wajipange vizuri kwenye mambo ya management kuwa na watu ambao ni professionla ili watatnzania wenzetu wasije kubaki midomo wazi siku moja. Bali watanzania wakati umefika kufikiria zaidi kuzalisha mali kulikoni njia hizi za kiusanii katika kujiletea maendeleo. Watu wafikirie zaidi katika miradi midogo midogo endelevu katika sekta ya kilimo na ufugaji.


Mkuu Heshima mbele

kama ulivyosema wakati umefika sasa watu kufikiria zaidi kuzalisha mali kulikoni njia hizi za kiusanii katika kujiletea maendeleo ni kweli kabisa. Tatizo kubwa ni kuwa umaskini ukizidi na ikatokea vitu kama DECI ndo watu wanakurupuka wakidhani kuwa ndo njia mbadala ya kutokea.

Fanya reseach kidogo then utaona watu wanaojiunga DECI ni wa aina gani,
mtu mwenye uwezo sidhani hata kama ana muda wa kujua DECI ni nini.

In Short DECI is a typical Ponzi scheme, time will tell itazuka tafrani ya hali ya juu wakati wamiliki wamesha varnish.

By the way Stan check your PM.
 
kama ni wezi wamemuibia nani? ninao ndugu zangu wengi tu, nimewakopesha pesa, wakaenda kuziweka huko. wameshavuna mavuno karibia mawili. unaweza ukaweka hela za mtoto wako mmoja mmoja,dada zako hata shangazi nk. na utapata. kuna watu wanavuna karibia kila baada ya miezi mitatu, kutu kama million hadi tano pale, kwasababu waliweka zamani, na ile pesa waliyoingilia walishaipokea na wana kulaga faida. Kwa kifupi DESI SIO KWAMBA WANAKOPESHA AU NINI, NI SAWA NA UMEPANDA MTI WA MATUNDA, HIVYO UNAKUWA UNAVUNA KILA WAKATI HADI MTI HUO UTAKAPOZEEKA. unaweza ukavuna pesa za deci hadi miaka 50. ina faida sana. mimi nilifikiri ni wanigeria mwanzoni, nikaenda kuweka pesa pia, na nimepokea mihela kibao. wapo pale mabibo mwisho, watu wanapaki magari yao pale wanaweka hela na kuondoa. inasaidia sana, na kuna watz wengi wanaishi kwa hiyo.


Mwana wa Mungu,
It seems you're out of point. No one denied you of getting 'mahela kibao', yes you got it. The point is that, as long as people would continue pour money, into DECI, DECI will survive and pay people larger amount of money. But if it will happens that people stopped investing in DECI is where you will cry like an hyena. Remember, UPATA. DECI works in the same princples like UPATA. When UPATU began, many people harvested a lot of money, this move, attracted others to join UPATU.

When the number of people increased, UPATU failed to pay its members according to scheduled program. Therefore, if you had assessed UPATU adequately, the same it will happens to DECI. Let us wait and see.
 
Unajaribu kutuaminisha kuwa walokole ni malaika? Kama umekiri kuwa sasa walokole wako kwenye madhehebu mengi, na kama unakumbuka kuwa kuna baadhi ya wachungaji walokole ambao wako jela au kesi zao bado zinaendelea kwa makosa ya wizi, una ushahidi gani wa kutueleza kuwa hawa ni tofauti? Ningefurahi sana kama ungejibu hoja za watu wenye wasi wasi na DECI badala ya kutuletea hadithi za walokole katika mambo ambayo yanaonekana ni wizi mtupu!!

DarkCity,
Huyu anayejiita mlokole asitake kuleta unafiki. Kama ulivyosema ajibu hoja kisayansi na si kusingizia ulokole. Kwa taarifa yake, kwa sasa hakuna watu wasioaminika kama walokole. Wengi wako mahabusu kwa makosa ya aibu, Mchungaji kukutwa na viungo vya albino, kulawiti, wizi wa fedha za kanisa, kufanya mapenzi na walokole wake za watu na mengineyo.

Kama DECI, inaongozwa na walokole, namuhakikishia huyo anayejiita Mwana wa Mungu kwamba milango ya gereza Keko na Segerea iko wazi na mipana tayari kwa kuwapokea. Ninachokiona kutakuwa na kelele, vilio na maombolezo ya walala hoi, masikini waliouza kila kitu walichonacho ili wakawekeze huko DECI. Sasa kama walokole dhambi hiyo itakuwa juu yao.
 
Hey fellows! Mbona hii DECI nayo imekuwa issue? Kwanini kwa wale ambao wanafikiri kuwa DECI ni wezi au baadaye watanzania watakuja kuumia wasiende pale ni mabibo mwisho tu, office ziko wazi you go there you asked them questions then utumwagie hapa ulichopata. Hata kukiweka nukuu kibao kama kuna mtu ambaye yeye kwa kuwekeza kidogo kidogo pale DECI ameweza kujenga nyumba utmamweleza nini?

Hivyo kama tunataka hii kitu iende kisayansi then utafiti ni lazima. Wewe ambaye huamini then fuatilia ujue ukweli wake utakuwa umewasaidia wengi na wakati huo huo umeokoa wengine watao jiingiza na kupoteza hela zao. Maana you can find they have their own way to increase the amount. May be there is an investment? Because your an outsider its difficult to know whats going on inside unless you go inside.

FUATILIENI ACHENI MANENO TU....
 
Hey fellows! Mbona hii DECI nayo imekuwa issue? Kwanini kwa wale ambao wanafikiri kuwa DECI ni wezi au baadaye watanzania watakuja kuumia wasiende pale ni mabibo mwisho tu, office ziko wazi you go there you asked them questions then utumwagie hapa ulichopata. Hata kukiweka nukuu kibao kama kuna mtu ambaye yeye kwa kuwekeza kidogo kidogo pale DECI ameweza kujenga nyumba utmamweleza nini?

Hivyo kama tunataka hii kitu iende kisayansi then utafiti ni lazima. Wewe ambaye huamini then fuatilia ujue ukweli wake utakuwa umewasaidia wengi na wakati huo huo umeokoa wengine watao jiingiza na kupoteza hela zao. Maana you can find they have their own way to increase the amount. May be there is an investment? Because your an outsider its difficult to know whats going on inside unless you go inside.

FUATILIENI ACHENI MANENO TU....

Kamanda IT IS A PONZI SCHEME pure and simple! There is no investment which can consistently deliver gains of more than 100%!!! In 20 Weeks!! With no RISK of losses!!
And it is not a matter of IF it will collapse but WHEN, its simply impossible to run it forever because sooner or later you will go through all available investors.
You will be lucky to get 8% consistent return in a legitimate investment.
 
I think majority of Tanzanians need a sort of PUBLIC EDUCATION ON HOW TO INVEST - vyombo vinavyohusika na investment vinawajibika kuelimisha jamii ya Kitanzania - wengi wamejiunga DECI na hela zao kidogo wanazopata - wakijua ndio investment - lakini hawajaui kama its sustainable or not - profit and loss yake etc. HIVI KIONGOZI WA DECI NI MTANZANIA? kwa vile nchi yetu haiko makini - PYRAMID SCHEMES ziko nyingi sana hapa Dar na wengine ni foreigners wanaendesha - home afffairs iko kimya wala haijui - VIONGOZI WAKO BUSY NA KUJINUFAISHA - na kwa vile watu wana shida sana ya hela - na hawako educated - hawaelewi kuwa PYRAMID SCHEMES MWISHO SIO MWEMA - GOD HELP US TANZANIANS.
 
Hey fellows! Mbona hii DECI nayo imekuwa issue? Kwanini kwa wale ambao wanafikiri kuwa DECI ni wezi au baadaye watanzania watakuja kuumia wasiende pale ni mabibo mwisho tu, office ziko wazi you go there you asked them questions then utumwagie hapa ulichopata. Hata kukiweka nukuu kibao kama kuna mtu ambaye yeye kwa kuwekeza kidogo kidogo pale DECI ameweza kujenga nyumba utmamweleza nini?

Hivyo kama tunataka hii kitu iende kisayansi then utafiti ni lazima. Wewe ambaye huamini then fuatilia ujue ukweli wake utakuwa umewasaidia wengi na wakati huo huo umeokoa wengine watao jiingiza na kupoteza hela zao. Maana you can find they have their own way to increase the amount. May be there is an investment? Because your an outsider its difficult to know whats going on inside unless you go inside.

FUATILIENI ACHENI MANENO TU....


Nilishabahatika kufanya mahojiano mafupi na mfanyakazi wa hapo mabibo mwisho, na naomba niweke hapa baadhi ya mambo machache tu yaliyonitia wasiwasi. (Usiniulize jina lake)

1. Kuweka au kutoa fedha ni kwa keshi (cash). Na hizo fedha hukaa ndani ya makabati yaliyowekewa vidude vya kuita security kama kuna mtu anataka kuiba.
2. Fedha zinazowekwa na kutolewa zinahifadhiwa zote katika ofisi ya kufanyia malipo na kupokelea. Ila kwa data ambazo sijazidhibitisha, wamefungua akaunti katika benki moja ya hapa dar hivi majuzi tu.
3. Fedha zilezile "zinazopandwa" na kiasi fulani kidogo cha ada ya kujiunga ndizo zinazotumika katika kulipia security, wafanyakazi, pamoja na kulipa wale wanaokuja kuvuna.
4. Kuna ulinzi mkali ndani na kamera za kulindia hizo fedha.

Hayo tu hapo juu yananifanya niwe na sababu za kuitilia shaka DECI.
1. Kama hawana mfumo wa kuhifadhi fedha au kuziwekeza kule wanakozi"MULTIPLY" au kuzizalisha kama vile mti uzaavyo matunda kutakuwa wapi?
2. Kwa mtu anayejua fedha na accounting hesabu za kuweza kupokelea fedha sehemu moja tu bila hata kukopesha, au kuzitumia kuzalisha ni vigumu sana kuweza kuzi"MULTIPLY" kama wanavyodai.
3. Kama zilezile ndio zinatumika basi hapo itakuwa ndio PONZI SCHEME yenyewe.
4. Fedha zilizofungiwa mahali na kulindwa zitakuwa zinapungua kwa sababu ya INFLATION na kwa hesabu za haraka tu haiwezekani kupata faida ya kulipia hayo mavuno.

Jambo la pili ambalo sijalifanyia uchunguzi kama ni kweli au la, ni kuwa kuna taarifa zilishafika polisi ili waweze kuwakagua taarifa za mahesabu za hawa DECI. Kuna taasisi inaitwa

capital market and security authority(Capital Markets & Securities Authority - Tanzania)
6th Floor, PPF Tower, Ohio Street/Garden Avenue.
DAR ES SALAAM. TANZANIA.
Tel:+255-22-2114959/61 Fax:+255-22-2113846 e-mail: omaceo@cmsa-tz.org

Hii taasisi ndio inahusika na haya mambo kama kuna anayetaka kujiridhisha zaidi anaweza kuulizia.


Mwisho nitoe tahadhari tu kwa walio na "HIZI HISA" wafikirie zaidi ya hapo. na kufuatilia taarifa kutoka kwenye taasisi za fedha wajaribu tu angalau kujiridhisha.

Ila nina uhakika katika mfumo wa PONZI ni kuiba au kuibiwa, Ukifanikiwa kuiba bila mkono wa sheria kukupitia dhambi ya kuiba ukiwa na ufahamu haitaondoka kwa kufanikiwa kwako. Hata kama mtu akipata faida kubwa na kujenga majumba yatakuwa ya wizi. Hivyo kwa hili ni bora kujiridhisha kwanza kabla ya kuchukua hatua zaidi.
 
Back
Top Bottom