DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

kama ni wezi wamemuibia nani? ninao ndugu zangu wengi tu, nimewakopesha pesa, wakaenda kuziweka huko. wameshavuna mavuno karibia mawili. unaweza ukaweka hela za mtoto wako mmoja mmoja,dada zako hata shangazi nk. na utapata. kuna watu wanavuna karibia kila baada ya miezi mitatu, kutu kama million hadi tano pale, kwasababu waliweka zamani, na ile pesa waliyoingilia walishaipokea na wana kulaga faida. Kwa kifupi DESI SIO KWAMBA WANAKOPESHA AU NINI, NI SAWA NA UMEPANDA MTI WA MATUNDA, HIVYO UNAKUWA UNAVUNA KILA WAKATI HADI MTI HUO UTAKAPOZEEKA. unaweza ukavuna pesa za deci hadi miaka 50. ina faida sana. mimi nilifikiri ni wanigeria mwanzoni, nikaenda kuweka pesa pia, na nimepokea mihela kibao. wapo pale mabibo mwisho, watu wanapaki magari yao pale wanaweka hela na kuondoa. inasaidia sana, na kuna watz wengi wanaishi kwa hiyo.

...acha kutetea upumbavu,hawa matapeli wanatakiwa kusimamishwa kabla ya kupelekea watu vilio!
 
Nyani inakuwaje tena? Au ule mfano wa babu aliyenunua manyanui kwa dola kumi ndio 'umekufufua?'
 
Jamani hawa watu wanaoperate kwa mtindo wa money triangle watu wa mwanzo watafaidika lakini watakaofutia lazima watalia kwani triangle ikifika juu lazima hawa wa juu wawalipie waliko chini yao na wao wakose, kwa hiyo swala la kuwa wanaoperate vizuri hapa hakuna.

UPATU haikuwa na tofauti na wao nao walikuwa hivyo hivyo kwahiyo sioni kwanini serikali inawangalia tu kwani one day wataliza wanachi.
 
Mwanakijiji amebreak up hii issue kwa upeo mkubwa sana!!

DECI wanatoa Rate of Return almost 300% per yr, kwa biashara gani Tanzania????

DECI wangetoa rate of return 30% kwa mwaka, at least tungeweza kusema kuna viability ya hiyo scheme.

THERE IS NO WAY IN HELL, They will survive in the next 12 months wakiendelea na hiyo trajectory na pse Mwanakijiji ungesaidia sana jamii kama Gazeti la cheche likiweza kudeal na hii issue au hata kama unaweza kupush Tanzania Daima na magazeti mengine nyumbani yakazuia ili balaa, sababu we all know where it will end.
 
Kabla hatujazua zali hili ningependa hasa kujua wao Deci wanafanya biashara gani? Nitawaandikia na majibu ya "Muujiza wa Mungu" hayakubaliki.
 
Nionavyo mimi kutokana na kauli za wengi hapa, ni kwamba hii DECI inasaidia wengi. Inawezekana sana kutengeneza pesa nyingi kwa kuzizungusha katika biashara has ndani ya miezi minne (4 months). Inachotakiwa ni kuwa na plan nzuri ya kuzizungusha. Mtaji unaotokana na wanaoamini kutajirika na hiyo DECI ni mkubwa sana. Kwa mfano, ukipata watu 100 wanaoweka pesa zao (TZS 200,000/- kila mmoja), unakuwa na jumla ya TZS 20m. Ukiongeza watu zaidi pesa zaidi inaongezeka. Wanaweza wakawa na jinsi ya kuizungusha na kupata walau 50% profit ya pesa yote waliyonayo kila mwezi.

Vile vile, wanatakiwa ku-operate in low profile and very carefully ili wasipoteze pesa za watu. Kwa maana hiyo, hawahitaji kuwa na domain yao wenyewe (kwa maana wanaweza kupata mawasiliano bure kupitia yahoo/hotmail/gmail n.k) wala hawana haja ya kufanya manunuzi ya assets za gharama kubwa. Ili mradi tu wanafikia malengo yao ya kupata pesa (mtaji) kutoka kwa watu ili wafanya biashara zao zenye faida nzuri.

Wasiwasi wangu ambao pia wengi mmeuonyesha ni kwamba, operation ya DECI haina guarantee ya maisha marefu. Sababu za kusema hivyo ni kama zifuatazo;
1. Ni kampuni simple sana, na hivyo endapo mmiliki wake akipata janga kama kifo (Mungu aepushe), au sheria za nchi, basi biashara yote inafika mwisho na walioweka pesa zao wanaweza kuzipoteza
2. Sina uhakika kuwa imesajiliwa katika taasisi za kusajili kampuni za kukopesha pesa. Kama haijasajiliwa vizuri, inaweza kuingia katika tatizo la kisheria hapo juu, na ikawa mwisho wake
3. Endapo mmiliki akiamua kuachana na biashara hiyo na akatoroka, basi wawekezaji wa pesa zao nao watakuwa wameliwa
4. Endapo biashara zake zikiingia matatani (kwa maana biashara nyingi TZ ni za msimu) na hivyo kuathiri kipato, inaweza kusababisha uwezo wake wa kulipa watu kupungua na hivyo kushindwa kulipa kama alivyotakiwa na watu wengi kupoteza pesa zao
5. Endapo idadi ya watu wanaoweka pesa zao DECI ikiwa kubwa sana kuliko mapato anayopata kokote anakoyapata, pia inaweza kula mtaji wake na hivyo kushindwa kulipa watu. Ili kuepuka hili, inabidi DECI wawe makini sana kusoma alama za nyakati na alama za mtiririko wa biashara zao zote ili kujua ni wapi pa kuishia

Madhara ni dhahiri kuwa ipo siku yanaweza kutokea. Na yakitokea, kuna watakaolia na kuna watakao ona si mbaya sana (mrija tu ukatika).

Tahadhari: Watu wanaoiamini sana hii DECI wafanye hivyo kwa kuzingatia hatari zote zilizopo kama ambavyo zimewekwa na watu mbalimbali hapa. Ni ushauri tu.
 
Huu ni mfumo walioupata kutoka kwa prof. Yunus kutoka kule Bangladesh ambaye kama mnafahamu alipata nobel price kwa kuwainuia watu wa kipato cha chini na kama ilivyoelezwa hapo nyuma kanisa la deliverance church pale mabibo walituma wawakilishi wao wakapate mafunzo namna ya kuendesha hii scheme.

Scheme inaendeshwa vizuri ndio hadi hivi sasa ni miaka mitatu watu wanavuna vizuri bila ya matatizo. Pia imeanzishwa scheme nyingine inaitwa Elimika scheme hiyo ni kwaajili ya watu wa kima cha kati.

My take ni kuwa watu hawapendi watanzania wanufaike kila siku imekuwa ni jadi kuwa watanzania wanaibiwa, hadi lini Tushikamane Revolving fund ndio mkombozi pekee kuondokana na umaskini.

Mbona kila siku tunasikia mabenki yanadai mwisho wa mwaka yametengeneza faida bilion 50 hata majuzi CRDB na NMB yametengeneza faida hizo lakini ukiangalia wanachotoa kama interest kwa wateja wao ni peanut.

TUSHIKAMANE
 
Recta, wanazungusha hizo fedha kwenye biashara gani inayoweza kulipa faida ya zaidi ya asilimia 300 kwa mwekezaji mmoja? ukinionesha na mimi nitawatumia dola 200 niingie maana KLHN inahitajia kamtaji kanguvu! shoot..
 
Recta, wanazungusha hizo fedha kwenye biashara gani inayoweza kulipa faida ya zaidi ya asilimia 300 kwa mwekezaji mmoja? ukinionesha na mimi nitawatumia dola 200 niingie maana KLHN inahitajia kamtaji kanguvu! shoot..

Hahahaha, Mkuu MKJJ, zipo biashara kadhaa zinazoingiza pesa nyingi tu. Miezi minne kupata faida ya mtaji wako mwenyewe ya 250% si nyingi, hasa kama unaijua vyema biashara hiyo. Mabenki hufanya biashara kubwa na pesa zetu kidogo kidogo tunazoziweka (kwa siku). Inawezekana. Swala ni je, itadumu?
 
Hahahaha, Mkuu MKJJ, zipo biashara kadhaa zinazoingiza pesa nyingi tu. Miezi minne kupata faida ya mtaji wako mwenyewe ya 250% si nyingi, hasa kama unaijua vyema biashara hiyo. Mabenki hufanya biashara kubwa na pesa zetu kidogo kidogo tunazoziweka (kwa siku). Inawezekana. Swala ni je, itadumu?

Nafahamu zipo biashara za namna hiyo hata bahati nasibu, n.k sasa hawa Deci wao wanazungusha kwenye biashara gani? Wanawekeza kwenye vitu gani?
 
Jamani kweli watu wanavuna si mchezo na wala hakuna wizi wowote unaofanyika ila tatizo la watanzania tangu upatu utukumbe na dhoruba na kama mnakumbuka, jamaa waliojiita faidikanao wakja wakalala mbele na millions za watu, ushaidi huu unawafanya watanzania kutaka kujua chanzo halisi cha upatikanaji wa hayo mavuno,naomba wahusika wasiilewe vibaya JF lengo lao ni kuwlinda na kuwasaidia watanzania .incase of immergency wanakumbuka waliambiwa hiki na kile wakakataa kusikia.

Sasa kama ndugu zetu DECI mko humu ama kuna watu wanawajua vyema waje kutusaidia hili swali kirahisi na nina uhakika nitajitahidi kuwatafutia wateja hata
huku"IRAQ "nilipo wenye pesa nzuri tu...

Usiku mwema jamani
 
mama yangu mzaazi aliniomba million moja nikampa laki tano akachanganya laki tano zake akapeleka kweli amevuna na akataka kunirudishia namwambia apande tena aiongezee so tunasubiri mwezi wa tatu tena kama neeme itaendelea hivi ...nitawakumbuka na nduguzangu wa JF....
 
mama yangu mzaazi aliniomba million moja nikampa laki tano akachanganya laki tano zake akapeleka kweli amevuna na akataka kunirudishia namwambia apande tena aiongezee so tunasubiri mwezi wa tatu tena kama neeme itaendelea hivi ...nitawakumbuka na nduguzangu wa JF....

Mr. Impossible hakuna anayebisha "mavuno" kuwa hayafanyiki. Hakuna anayekataa kuwa watu wanapata mavuno!! Tatizo hizo mbegu zinapandwa wapi!?

Labda itabidi nitumie vielelezo kufafanua hili; tunachosema ni kuwa hii scheme will have to collapse. Itakapocollapse watakaolia watakuwa wengi zaidi kuliko wale waliovunja na kuchomoka zao! It is not sustainable.
 
Back
Top Bottom