DC mteule ndugu "Mchopanga" alisoma shahada ya kwanza bila kuwa na matokeo ya kidato cha sita licha ya kuisoma kwa miaka mitatu

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Niliposoma gazeti la MWANANCHI la leo ni kuwa yupo DC mmoja mteule ambaye anatokea kwenye tasnia ya wasanii ambaye alienda nchini India kwenye chuo kikuu cha Bangalore akisomea shahada ya kwanza kwenye mambo ya sanaa huku matokeo yake ya kidato cha sita yakiwa hayajatoka.

Kwa mujibu wa gazeti hilo ni kuwa Mchopanga huyo alipata udhamini na moja kwa moja kwenda kwenye masomo hayo kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2009 ambapo aliondoka nchini na kudahiliwa chuoni hapo bila ya kuwa na matokeo hayo.

Upo uwezekano kuwa kwenye elimu ya huyu DC mteule kuna utata na usanii na hata shahada yake ni ya mambo ya usanii.

Anajisemea kuwa anatarajia kwenda chuo kikuu cha Dar es Salaam kusomea shahada ya pili kwenye mahusiano ya umma.

NB: Wapo marafiki zangu kibao waliotokea hapo Bangalore na kujitapa kuwa wana shahada ila walipoambiwa kuleta vyeti wengi wao ni ukweli walitunukiwa shahada zao za kwanza kwa kutumia matokeo ya vyeti vya kidato cha nne kama "Direct entry qualifications" na huenda Mchopanga ni mmoja wao. Je, NACTE wameanza lini kuthibitisha kuwa shahada za aina hii ni credible kwa nchi yetu?
 
Nimesoma hiyo habari hata mimi nikabaki na mshangao.
Mnashangaa kitu gani?

Kwani kusoma chuo kikuu mpaka usome Form Six?

Prof Mwandosya Mark J, hakusoma Form Six, Bali alisoma DIT Halafu akaenda udsm baadae Aston university

Wahindi kule Posta watoto wao wanasoma ulaya vyuo vikuu vya dollar 50,000 kwa mwaka walisoma form Six?

Wahindi wangapi wanafanya kazi Agha khan na Muhimbili tena mabingwa lakini mbona hawakusoma Form Six

Kenya wanaishia Form Four na kwenda chuo kikuu

Mimi niliwahi fanya kazi nikiwa mwaka wa pili chuo Kikuu na Nilimpata ajira rasmi bila hata matokeo ya mwaka wa pili,

Watu wanaangalia uwezo wa Mtu sio cheti

Kuna vyuo unafanyishwa mitihani kabla ya kuingia ukiweza hata ukiwa darasa la saba Unaanza masomo

Elimu hii ya Form Six ni kuwapotezea watoto muda na maisha ya kutafuta Pesa tu

Miaka miwili Form Five na Six, Mtoto anaweza kujifunza utaalamu wa programming na akawa nguli

Miaka miwili inatosha mtoto kusoma Software mbalimbali na kuwa nguli

Form six ni mfumo wa Uganda na Tanzania wa kishamba sana

Ukiwa na pesa na upo vizuri mtoto unamsomesha kuanzia chekechea ulaya unalipa dollar 60,000 kama Milioni 120 Kwa mwaka

Ukiwa na pesa huna haja ya kusoma elimu yetu hii ya kitanzania ya kupotezeana muda,

Mtoto akimaliza Form Four unamtafutia College Marekani au Uingereza anajifunza mambo ya maana hata mwaka baadae unamlipia chuo kikuu huko huko

Angalia wahindi kule Posta na ni matajiri jinsi watoto wao wanavyokuwa smart kichwani baada ya Form Four, Mtoto anapelekwa college ulaya bei dollar za kutosha


Wabongo tatizo pesa, Watanzania wachache wana uwezo wa kumlipia mtoto ada Milioni 200 kwa mwaka au Milioni 100 kwa mwaka

Watanzania Tuendelee na Bodi yetu ya mikopo huku tukilia lia Retention fee

Ahaaaa
 
DC Hana kazi. Akchuali kile Ni cheo Kama zawadi kwa makada na wanaosifu na kuabudu. Mkurugenzi ndio anatakiwa awe angalau na certificate ya CBE.

Elimu ya ukweli inatakiwa bungeni na sio kwenye u DC. Hapa kwetu Kuna wabunge wasiojua kazi za bunge lkn wako bungeni (sio maneno yangu Ni mbunge mwenyewe) Kuna wabunge hawajui hata kutamka trilion wakiona tarakimu zake, of course Kuna drs la Saba ambao nashangaa chama Chao kuwapendekeza wagombee.
 
Vyuo vya kitapeli hata uko nje vipo.
Huna pesa ya kusoma nje ya nchi wewe

Hakuna mtanzania asiyependa mwanae akasome Oxford, University of london

Ada ni kubwa wenzetu wahindi wamewekeza kumlipia mtoto wa chekechea dollar 30,000 Marekani ni kawaida sana

Kuna wahindi Bongo watoto wao wanasoma chekechea uingereza wanalipa dollar 40,000 kwa mwaka

Wewe huna uwezo huo ndio maana unabaki Udsm, Mzumbe. Ukijitahidi mpaka msaada wa serikali bado matumizi binafsi utalia lia

kubali kushindwa mkuu

Mtu smart unaweza soma engineering Coet kule kweli

Ukifika Coet udsm ni shida, Engineering gani kule Coet, Hakuna vifaa ni kukariri tu

Pale BICO udsm kuna machine za enzi za old stone age
 
Mwenda kwa jinsi alivyokuwa Kama mama alidharau ukurugenzi akawaweka wajinga wa mwisho kuwa wakwanza. Mama ni mweupe kichwani uweupe wenyewe
 
Elimu ina dynamics zake mkuu. The most important ni kwamba Chuo kilimchukua kwa vigezo kilichoweka.

Vyuo vya nje vingi vina utaratibu wa kuchukua watu based on their profession or experience. Kama una miaka mitano hadi saba kwenye kazi fulani basi wata ku enroll tu.

Ni bongo tu ndiyo hata kama umefanya kazi miaka mingapi watataka uka resit darasa la saba, then form four n.k
 
Kama ingekuwa form 6 lazima, waliosoma kenya wote.. ama wakenya wasingekuwa na degree holder hata mmoja?

Unajua kuna wakenya kibao wamesoma udsm wakina miguna miguna na jaji mkuu wao ila kenya hawakusoma form 6 sababu haipo kwao.

Pia unajua kujua michezo kama soka, basketball, riadha inaweza kukupa nafasi ya kusoma havard ama yale bila kujali hujafika form 6 wala nini?
 
Back
Top Bottom