Current four star Generals in Tanzania

Yaani Clinton na Gore, ambao ni Democrats, walimbagua General Colin Powell?

Haiwezekani bana. Democrats siyo wabaguzi. Wanawapenda watu weusi.
Nyani Ngabu, inawezekana sana tuu, Gen. Powell alikuwa Republican. Kwa Marekani misimamo ya Vyama vyao vina nguvu sana hata kwenye Supreme Court appointments .
 
Thanks for this.
P
 
Elezea kwa upana, mara zote kwa tulivyo zoea nchini, yakifanyika mabadiliko ya CDF na CoS hubadilika. Na hii ni kwa kuwa Ma CoS ndio huwa CDF, kwa hiyo nafasi ya CoS huwa wazi.

...mwanzo nilikuwa sijakuelewa, ila hapa umeeleza vizuri.
 
Ahaa! Well nimekuelewa vizuri Mkorinto. Kama hutojali, naomba unipangie uzito from JWTZ to Mgambo.

Like;- JWTZ, JKT, Polisi, FFU and co.
JKT iko ndani ya JWTZ.

FFU iko ndani ya Police (ni Unit ya Police kama ilivyo Traffic police).

1. JWTZ,
2. Police, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto (level moja)
3. Mgambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Field Marshal ana nyota 5?!!?? Kwa nini rank hito Tanzania hatuna?!
Field Marshal kiuhalisia siku hizi hicho cheo ni almost hakuna, mara ya mwisho walikuwepo world war 2 huko, maana unakuta jeshi lina watu milion 4. Sasa hivi hakuna hayo mambo, na sidhani kama yatatokea
 
Naunga mkono hoja, maslahi yanafanana with tofauti ndogo
P
Nimekuelewa na kukubali, lakini naamini ilikuwa rahisi sana kwa kuwa Aliopo ndio mmoja wa Maafisa wenye elimu ya juu na mafunzo makubwa Jeshini. Lakini hiyo hiyo Elimu na Mafunzo ya juu yali mchelewesha kupendekezwa kwa nafasi za juu.
 
Nasikia JWTZ huwa hamna surprise yani wameshajipanga wenyewe na wanajua nani akistaafu CDF anakuwa nani.
 
Ni kweli, nilidhani anaongelea kwenye ranks za generals peke yake. Mayalla kaelezea vizuri hapo juu
 
Kwenye military organizations, hivi vyeo vya officers ni vyeo vya uongozi wa wanajeshi wenzake. Kama hauna jeshi kubwa sana, 4 star generals hawahitajiki. Jeshi letu bado dogo kwa idadi ya wanajeshi, pengine itafika siku kutakuwa na huo uhitaji.
Sio kwamba jeshi letu bado dogo,huo ni mfumo wetu wa namna ya kulifanya jeshi liwe na utii,
 
Mkuu unaweza kutusaidia elimu ya Mabeyo ?,
 
JKT iko ndani ya JWTZ.

FFU iko ndani ya Police (ni Unit ya Police kama ilivyo Traffic police).

1. JWTZ,
2. Police, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto (level moja)
3. Mgambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mgambo ni kamandi iko chini ya MMJ na kuna Brigedia ndo anaisimamia mkuu au mie nimepitwa???(RFC)

Na inashuka mpaka mikoani kote wa RC(Defence attaçhe mkoani,Mshauri wa mgambo mkoa na Wanakuwaga maMajor) na wilayani kuna Mshauri wa mgambo pale kwa DC ambaye ni mjumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama

Mgambo sema tu hawana kazi maalum wakaanza kupewa kazi za kupiga mateke sufuria za ubwabwa wa mama ntilie ndomaana tunawaona sio

Ila kipindi Fulani hapo nyuma(Nadhani hata mwanzoni kwa utawala wa Mkapa) ilikua Mgambo ni bora kuliko Polisi😂😂. Enzi zile polis wanavaa sare zina viraka na raba
 
Mtu kijana ni range ya umri gani?

Mtu akiwa luteni usu na miaka24, ukiongezea na hiyo 24 mingine uliyoitaja, by 48 au 49 anaweza akawa full general?

Mtu mwenye miaka 48 ni mzee?
Sijui utamwitaje , tunayo fahamu sisi kijana mwisho miaka 35-40.
 
Sio kwamba jeshi letu bado dogo,huo ni mfumo wetu wa namna ya kulifanya jeshi liwe na utii,
Sababu pia Jeshi ni dogo mkuu. Kamandi zenyewe ziko 6 ambazo zina askari labda 30,000 kila moja

Sio kama India, US au China ambako watu wanalinganisha sana
 

Halafu Sarakikya alipata mtelemko ambao ni nadra sana kutokea. Alipandishwa cheo kutoka lieutenant mpaka brigadier na kufanywa kuwa mkuu wa majeshi. Hivyo, hakuwahi kuwa captain, major, lieutenant colonel wala colonel. Miaka hii hilo haliwezi kutokea!
 
Mkuu unaweza kutusaidia elimu ya Mabeyo ?,
Duu!, swali hili limenifanya nijitafakari sana, mimi ni Msukuma wa aina gani, kwasababu japo Mabeyo, tunatoka naye kijiji kimoja, Masanza, nyumbani kwake na kwetu ni just accros the main road, lakini huwezi amini, sijawahigi hata kujua alipandaje ghafla na kuwa generali, wala siijui CV yake, nasikia ni highly learned, and he is good!.
P
 
Yeah kwa wakati mmoja general ni mmoja ambaye anakuwa ni CDF au mkuu wa majeshi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…