Current four star Generals in Tanzania

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,225
113,565
AF4F95E8-C3EB-48B5-AB66-3ED9E21BD470.jpeg


Mimi si mjeda. Sijui mengi kuhusu ujeda. Sijui mengi kuhusu mengi.

Ni mbeba maboksi tu. Wengine husema nimeishia darasa la saba. Wengine hudai nimeishia kidato cha nne.

Hivyo, sina mengi niyajuayo. Ila, ninao uungwana wa kukubali nisiyoyajua.

Na dawa ya kuyajua usiyoyajua ni kujifunza.

Kujifunza kuko kwa namna nyingi. Moja ya hizo namna ni kuuliza.

Leo nauliza hivi: Hivi kwa Tanzania huwa tuna jenerali mmoja tu kwa wakati mmoja aliye jenerali kamili, yaani yule mwenye nyota 4?

Kama sijakosea, mkuu wa majeshi ndo huwa jenerali kamili mwenye nyota 4 tu kwa wakati mmoja. Jenerali huyo akistaafu ndo mwingine [labda luteni jenerali] anapandishwa cheo na kuwa jenerali kamili halafu ndo anakuwa mkuu wa majeshi.

Kwa nini iko hivyo? Tumeiga sehemu labda?

Najua India kwa mfano, kuna four star generals zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

Marekani currently wana four star generals 45, kama sijakosea.

Kwa mnaojua, kwa heshima na taadhima zote, naomba mnifute huu ujinga nilionao.

Shukran jazilan 🙏.
 
Kwenye military organizations, hivi vyeo vya officers ni vyeo vya uongozi wa wanajeshi wenzake. Kama hauna jeshi kubwa sana, 4 star generals hawahitajiki. Jeshi letu bado dogo kwa idadi ya wanajeshi, pengine itafika siku kutakuwa na huo uhitaji.
This kinda makes sense...though I’m not certain if that’s the reason why we don’t have more than one four star general at once...
 
Majenarali wa nyota 4 wako wangapi Tanzania?
Kwenye military organizations, hivi vyeo vya officers ni vyeo vya uongozi wa wanajeshi wenzake. Kama hauna jeshi kubwa sana, 4 star generals hawahitajiki. Jeshi letu bado dogo kwa idadi ya wanajeshi, pengine itafika siku kutakuwa na huo uhitaji.
 
This kinda makes sense...though I’m not certain if that’s the reason why we don’t have more than one four star general at once...
Hata Lieutenant Generals kwa mara ya kwanza tunekuwa nao zaidi ya mmoja baada ya chuo cha ulinzi Kunduchi kuanza. Maana kiheshima vyuo vikuu vya jeshi huongozwa na 3 star generals.

Why we dont have more, issue ni ataongoza team ipi? Jeshi linapangwa kwenye group/units na kila moja ina kiongozi wake. Mfano major anaongoza wanajeshi kati ya 80 mpaka 250, Brigedia kati ya 3000 mpaka 5000. Full General ni 100K kwenda juu. It can vary na wakati mwingine mtu wa cheo fulani anapewa specialised unit bila kujali ina watu wangapi.

Bado wadogo sana, China ina 2mil soldiers. Wana Generals kama utitiri and rightly so
 
sababu ya msingi ni ukubwa wa jeshi la nchi mkuu
ndio maana hata neno "army"huwezi likuta mara kwa mara linapotajwa jeshi la tanzania.

tuna mkuu wa majeshi tz,tukikusudia anga,ardhi,maji nk lakini jwtz inayatambua kama vikosi au komandi.
 
Hata Lieutenant Generals kwa mara ya kwanza tunekuwa nao zaidi ya mmoja baada ya chuo cha ulinzi Kunduchi kuanza. Mara kiheshima vyuo vikuu vya jeshi huongozwa na 3 star generals...
Well, vipi zile branches za military?

Kwa nini zisiongozwe na four star generals?

Jeshi letu halina special forces?

Airforce? Navy? Army?
 
Back
Top Bottom