Current four star Generals in Tanzania

Current four star Generals in Tanzania

weee.

us wako kibao halafu kuna mwenyekiti wao kama incharge,yani cdf.
Chairman of the Joints Chiefs of Staff.

5342D55E-F318-4BEE-8C3F-E2A8AFD282BC.jpeg
 
Nyani Ngabu,

Nadhani uko sahihi.

Lakini kupata uhakika zaidi tuwaite Kichuguu, Echolima, Pascal Mayalla.

Ninavyoelewa mimi kwa, JWTZ, askari mwenye cheo cha juu kabisa, au mkuu wa majeshi, huwa na rank ya Jenerali / 4-star-general.

Utaratibu wa Cdf kuwa 4-star-general ulianza miaka ya mwisho ya Mwalimu Nyerere, na mwanzoni mwa utawala wa Ali Hassan Mwinyi.

wakati jeshi la wananchi limeundwa, mkuu wa majeshi wa kwanza alikuwa na cheo cha Brigadier au 1-star-General.

Baadae nadhani kutokana na jeshi kuwa kubwa zaidi mkuu wa majeshi akawa na cheo cha Major General au 2-star general.

Utaratibu huo uliendelea mpaka wakati wa vita vya kagera, ambapo mkuu wa majeshi akawa na rank ya Lieutenant General au 3-star general.

Wakati Mwalimu Nyerere anaondoka madarakani, alitoa nishani kwa maafisa mbalimbali wa vyombo vya ulinzi na usalama, na akawavalisha rank za 4-star-General, Abdalah Twalipo, na David Musuguri, in that order. Lakini Abdalah Twalipo alikuwa hayuko tena jeshini, Musuguri ndio alikuwa mkuu wa majeshi.

Baada ya General Musuguri kustaafu, wakuu wote wa majeshi waliomfuatia wamekuwa na rank ya 4-star-General.

NB:
Tumainieli Kiwelu ndiye 4-star-General pekee hapa Tanzania ambaye hajashika nafasi ya mkuu wa majeshi / cdf. Vilevile Tumainieli Kiwelu ndiye Mtanzania pekee ambaye amewahi kuwa mnadhimu mkuu / CoS chini ya Maraisi, na wakuu wa majeshi, wawili tofauti. Mara ya kwanza ilikuwa chini ya Rais Nyerere na CDF Abdalah Twalipo; mara ya pili ilikuwa chini ya Rais Mwinyi na CDF Ernest Mwita Kiaro.

Pia Raisi Mkapa alimpandisha cheo Mkuu wa kwanza wa Jwtz, Major General Mirisho Hagai Sarakikya kuwa 4-star-general miaka kadhaa baada ya Sarakikya kuwa ameshaondoka jeshini.
 
sababu ya msingi ni ukubwa wa jeshi la nchi mkuu
ndio maana hata neno "army"huwezi likuta mara kwa mara linapotajwa jeshi la tanzania.

tuna mkuu wa majeshi tz,tukikusudia anga,ardhi,maji nk lakini jwtz inayatambua kama vikosi au komandi.
Sio Tanzania 'Army' naomba kufahamu inafahamika vipi?
 
This kinda makes sense...though I’m not certain if that’s the reason why we don’t have more than one four star general at once...
Nini, nafasi ya mkuu wa Majeshi inapatikana kwa namna mbili '' sifa(merits) na siasa (appointment).

Mkuu wa nchi ndiye anayemteua mkuu wa Majeshi na ili kumpa nafasi ni vema asiwe na ''limit''.

Ukiwa na 4 Star generals wanne (4) ina maana uteuzi wa next CDF lazima uwe miongoni mwa hao.
 
NN, nafasi ya mkuu wa Majeshi inapatikana kwa namna mbili '' sifa(merits) na siasa (appointment).
Mkuu wa nchi ndiye anayemteua mkuu wa Majeshi na ili kumpa nafasi ni vema asiwe na ''limit''
Ukiwa na 4 Star generals wanne (4) ina maana uteuzi wa next CDF lazima uwe miongoni mwa hao
Kwa nini lazima uwe miongoni mwao? Katiba inasema hivyo?

Na kama mtu kafikia kuwa a four star general, basi atakuwa kafika hapo kwa merit.

Hivyo kuchagua kati ya hao waliopo sioni kama ni tatizo.
 
This kinda makes sense...though I’m not certain if that’s the reason why we don’t have more than one four star general at once...
Jeshi halitakiwi kuwa na Brigadiers wengi kuliko Brigades.

Utaishia kuwa na Brigadiers hawana Bridages.

Halafu vyeo vingine vinatuzwa kwa mafanikio yanayotikana na upiganaji vitani.

Nchi yetu haijapigana vita kamili tangu vita vya Kagera kipindi cha Nyerere, wanajeshi sanasana wanaenda kwenye UN na AU engagements tu.

Ukiacha hao Ma General wa Ukuu wa Majeshi utampa mtu cheo cha u General kwa vita ipi aliyopigana?
 
tanzani peoples defence forces(tpdf).
Hapa ndio mimi huanza kuchanganyikiwa! Samahani nipatie elimu...

Tanzania People's Defence Forces ndio JWTZ ambayo ndani yake ndio kuna Police Tanzania, Magereza, Fire, JKT na majeshi ya Anga, Maji na Special Forces?

Kama unaweza naomba unipatie orodha kamili ya majeshi yote na vitengo.
 
Ukistaafu ina maana cheo nacho ndio basI? Wakina Mwamunyange, Waitara, Mboma hawawezi kuitwo in case of emergency?
Ukistaafu unaitwa General mstaafu. Kwani marais tunao wangapi?

Kuitwa labda kwa ushauri, lakini kama kunahitajika more general mbona rais anaweza kumpa mtu vyeo hata vitano kwa siku moja.

Na vyeo vya jeshi wengine wanapewa hata baada ya kustaafu kama alivyopewa Sarakikya na Mkapa, alistaafu akiwa 2 star, akaopewa 4 starts baadae akiwa mstaafu. Tofauti ni benefits tu
 
Pia Luteni Generali yupo juu kwa Meja Generali

..kweli.

Ngazi ya General huanzia cheo cha Brigadier-General, zamani walikuwa wakiitwa Brigadier.

Sasa ngazi za Majenerali / Generals zinakwenda namna hii.

General / 4-Star-General.

Lieutenant General / 3-Star-General.

Major General / 2-Star-General.

Brigadier General / 1-Star-General.

NB:
Kwa Tanzania, huwa tuna Active 4 star general mmoja na huyo kuwa ndio mkuu wa majeshi.

Pia mnadhimu mkuu wa majeshi, au Chief of Staff, huwa ni 3-star-general.
 
Jeshi halitakiwi kuwa na Brigadiers wengi kuliko Brigades.

Utaishia kuwa na Brigadiers hawana Bridages...
Kwa hiyo, kama si ukuu wa majeshi, kama askari hajapigana vita hawezi kupanda ngazi hadi kufikia cheo cha ujenerali?

Hii ni kwa mujibu wa nini, kama ni kweli? Kitabu? Gazeti? Katiba? Stori za mitaani?
 
Kwa nini lazima uwe miongoni mwao? Katiba inasema hivyo?

Na kama mtu kafikia kuwa a four star general, basi atakuwa kafika hapo kwa merit...
Ni kweli unachokisema. Ninaona unaliangalia suala hili kwa mtazamo wa US au India ambako military ni independent institution. Hapa tunazungumzia developing countries

Si lazima awe miongoni mwa hao 4 star generals lakini kumbuka kuwa uteuzi nje ya hao ni uteuzi wa chini kuwa mkubwa. Kutakuwa na chuki.

Fikiria hivi, kuna 4 star generals wanne ambao ni ''CDF in waiting''
Uteuzi wa CDF ukamchukua Luteni jenerali, hivi hawa 4 star watajisikiaje?
Kutakuwa na stability kweli ukijua hizi ni developing countries?

Ukinisoma vizuri nimesema kuna suala la 'merits na appointment'' . Appointment ni kisiasa zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom