CPJ: Wanahabari na wafanyakazi wa vyombo vya habari 95 wameuawa katika vita vya Israel na HAMAS

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,800
Waandishi Israeli Gaza.jpg

Kufikia Machi 20, 2024, uchunguzi wa Shirika la Kimataifa la Kutetea Waandishi wa habari (CPJ) unaonesha kuwa takribani waandishi habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari 95 ambao ni miongoni mwa zaidi ya watu 32,000 waliouawa tangu vita vilipoanza Oktoba 7—ambapo zaidi ya Wapalestina 31,000 wamekufa katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na vifo vya watu 1,200 vimeripotiwa nchini Israel.

Vikosi vya Ulinzi vya Israel (IDF) viliiambia shirika la habari la Reuters na Agence France Press mwezi wa Oktoba kwamba havikuweza kuhakikisha usalama wa waandishi wao wanaofanya kazi katika Ukanda wa Gaza, baada ya kufuatilia uhakikisho kwamba waandishi wao hawangelengwa na mashambulizi ya Israel, kulingana na ripoti ya Reuters.

Waandishi wa habari katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hatari kubwa hasa wanapojaribu kuripoti mgogoro wakati wa uvamizi wa ardhini wa Israel, ikiwa ni pamoja na mashambulizi makali ya angani ya Israel, kukatika kwa mawasiliano, uhaba wa mahitaji muhimu, na kutokuwepo kwa umeme kwa muda mrefu.

Kufikia Machi 20:
  • Waandishi habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari 95 wamethibitishwa kufa: Wapalestina 90, Waisraeli 2, na Walebanoni 3.
  • Waandishi wa habari 16 wameripotiwa kujeruhiwa.
  • Waandishi habari 4 wameripotiwa kutoweka.
  • Waandishi habari 25 waliripotiwa kukamatwa.
CPJ pia inachunguza ripoti nyingi ambazo hazijathibitishwa za waandishi wengine kuuawa, kutoweka, kushikiliwa, kujeruhiwa, au kutishwa, na uharibifu wa ofisi za vyombo vya habari na nyumba za waandishi wa habari.

“CPJ inasisitiza kwamba waandishi wa habari ni raia wanaofanya kazi muhimu wakati wa nyakati za mgogoro na hawapaswi kulengwa na pande zinazopigana,” alisema Sherif Mansour, mratibu wa CPJ wa programu ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. “Waandishi habari katika eneo hili wote wanafanya kazi kubwa kufunika mgogoro huu wa kuhuzunisha. Wale wa Gaza wamegharimika, na bado wanagharamika kwa kiwango kisichokuwa cha kawaida na wanakabiliwa na vitisho vingi. Wengi wamepoteza wenzao, familia, na vituo vya habari, na wamekimbia kutafuta usalama wakati hakuna mahali pa salama au njia ya kutoroka.”

Chanzo: CPJ
 
Wajichunguze na wenyewe kwa kutuletea habari za Uongo kila siku kuwa wanaouliwa Gaza ni Wanawake na Watoto tu na raia.. na IDF pekee no Hamas Member aliyekufa...

Wajue malipo ni hapa hapa... Waandishi mchana usiku magaidi
 
IDF walimchunguza wakakuta mtot wake ni Gaidi na yeye anaingia front line anapeleka news kwa Hamas alipewa onyo akabisha baada ya kipigo kama cha Farao akatulia ila mbishi kwa sasa bado anauguza mkono wake
Yeah nakumbuka mtoto wake wa Kiume ambaye pia alikuwa reporter wa Aljazeera IDF walimu eliminate.
 
Shida waandishi wa habari walichukulia poa na kuingia front ili Israel iogope kushusha mabomu, kumbe hawajui amri za jesho, mbona hao waandishi hawaendi kuripoti vita vya Rusia na Ukraine? Au Alquaida, Bokoharamu, Alshababu? Haiti? Habari zao nyingi zilikuwa hazijabalance, wanatangaza jeshi la Israel limeua watoto na wanawake au Israel imepoteza wanajeshi wake huko Ghaza. Hawajawahi kutangaza wapiganaji wa Hamas wamekamatwa au wameuliwa.
Swali la kujiuliza, hao wanaopigana na IDF huko Gaza na kuiba vyakula vya misada ni akina nani?
Nia wanawake na watoto au Hamas?
 
Shida waandishi wa habari walichukulia poa na kuingia front ili Israel iogope kushusha mabomu, kumbe hawajui amri za jesho, mbona hao waandishi hawaendi kuripoti vita vya Rusia na Ukraine? Au Alquaida, Bokoharamu, Alshababu? Haiti? Habari zao nyingi zilikuwa hazijabalance, wanatangaza jeshi la Israel limeua watoto na wanawake au Israel imepoteza wanajeshi wake huko Ghaza. Hawajawahi kutangaza wapiganaji wa Hamas wamekamatwa au wameuliwa.
Swali la kujiuliza, hao wanaopigana na IDF huko Gaza na kuiba vyakula vya misada ni akina nani?
Nia wanawake na watoto au Hamas?
Elimu za shule za kata hizi

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 

Kufikia Machi 20, 2024, uchunguzi wa Shirika la Kimataifa la Kutetea Waandishi wa habari (CPJ) unaonesha kuwa takribani waandishi habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari 95 ambao ni miongoni mwa zaidi ya watu 32,000 waliouawa tangu vita vilipoanza Oktoba 7—ambapo zaidi ya Wapalestina 31,000 wamekufa katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na vifo vya watu 1,200 vimeripotiwa nchini Israel.

Vikosi vya Ulinzi vya Israel (IDF) viliiambia shirika la habari la Reuters na Agence France Press mwezi wa Oktoba kwamba havikuweza kuhakikisha usalama wa waandishi wao wanaofanya kazi katika Ukanda wa Gaza, baada ya kufuatilia uhakikisho kwamba waandishi wao hawangelengwa na mashambulizi ya Israel, kulingana na ripoti ya Reuters.

Waandishi wa habari katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hatari kubwa hasa wanapojaribu kuripoti mgogoro wakati wa uvamizi wa ardhini wa Israel, ikiwa ni pamoja na mashambulizi makali ya angani ya Israel, kukatika kwa mawasiliano, uhaba wa mahitaji muhimu, na kutokuwepo kwa umeme kwa muda mrefu.

Kufikia Machi 20:
  • Waandishi habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari 95 wamethibitishwa kufa: Wapalestina 90, Waisraeli 2, na Walebanoni 3.
  • Waandishi wa habari 16 wameripotiwa kujeruhiwa.
  • Waandishi habari 4 wameripotiwa kutoweka.
  • Waandishi habari 25 waliripotiwa kukamatwa.
CPJ pia inachunguza ripoti nyingi ambazo hazijathibitishwa za waandishi wengine kuuawa, kutoweka, kushikiliwa, kujeruhiwa, au kutishwa, na uharibifu wa ofisi za vyombo vya habari na nyumba za waandishi wa habari.

“CPJ inasisitiza kwamba waandishi wa habari ni raia wanaofanya kazi muhimu wakati wa nyakati za mgogoro na hawapaswi kulengwa na pande zinazopigana,” alisema Sherif Mansour, mratibu wa CPJ wa programu ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. “Waandishi habari katika eneo hili wote wanafanya kazi kubwa kufunika mgogoro huu wa kuhuzunisha. Wale wa Gaza wamegharimika, na bado wanagharamika kwa kiwango kisichokuwa cha kawaida na wanakabiliwa na vitisho vingi. Wengi wamepoteza wenzao, familia, na vituo vya habari, na wamekimbia kutafuta usalama wakati hakuna mahali pa salama au njia ya kutoroka.”

Chanzo: CPJ
ingekuwa ni kule Ukrine ungeona mijadala kule BBC
 
Back
Top Bottom