Comparing: Lowassa vs Pinda

Comparing: Lowassa vs Pinda

Hivi Watanzania tukiacha Ushabiki wa Siasa na Kuangalia Utendaji wa kazi na Uwajibikaji.. Pinda ana nini cha kujivunia katika miaka yake yoote alio kua waziri mkuu??

Ukiniuliza kumhusu Lowassa pamoja na ubaya wake lakini alituletea shule za kata, watoto wa wakulima tunasoma, aliwatimua ma DC na Wakandarasi wazembe, Mfano mkandarasi wa barabara ya Shekilango.. Sasa haya machache yana jirudia kwenye kichwa changu... Lakin kila nikijaribu kusaka Jitihada za Pinda sizipati..
Emu wadau Nisaidieni lipi jema Pinda kafanya kumzidi Lowassa kwenye Kazi??
N.B
Ukiondoa issue ya tuhuma ya wizi!!
 
Labda KILIMO KWANZA...nadhani ame-initiate ila sijui kama kinapumua.
 
Hakuna anachofanya huyo Pinda. Afadhali fisadi anayeiba lakini kazi inafanyika kuliko msamaria mwema asiyeiba lakini kazi nazo zinalala
 
Pinda hana alicho fanya... Kilimo kwanza kampeni ya Kitaifa ilianzishwa kwa suport Kikwete!
 
Hivi Watanzania tukiacha Ushabiki wa Siasa na Kuangalia Utendaji wa kazi na Uwajibikaji.. Pinda ana nini cha kujivunia katika miaka yake yoote alio kua waziri mkuu??

Ukiniuliza kumhusu Lowassa pamoja na ubaya wake lakini alituletea shule za kata, watoto wa wakulima tunasoma, aliwatimua ma DC na Wakandarasi wazembe, Mfano mkandarasi wa barabara ya Shekilango.. Sasa haya machache yana jirudia kwenye kichwa changu... Lakin kila nikijaribu kusaka Jitihada za Pinda sizipati..
Emu wadau Nisaidieni lipi jema Pinda kafanya kumzidi Lowassa kwenye Kazi??
N.B
Ukiondoa issue ya tuhuma ya wizi!!

Mkuu shule za kata ilikuwa ni idea ya Sumaye na ikawekwa kwenye Ilani ya CCM kwa hiyo Lowasa aliirithi tu na kwa kuwa ilipata utashi wa kisiasa kutoka kwa Rais then ikawa rahisi kuimplement. Lakini pia inatakiwa ujue kwamba by the time pinda yuko Tamisemi Lowasa was the PM na shule za kata zilikuwa zinaangukia moja kwa moja kwenye wizara ya Pinda sasa ni nani alifanikisha ujenzi?

Anyway mine is not to vie for any one ila before we just bluff lets have facts clear.... Give dues where applicable na ponda kwa nguvu zote pale penye makosa!
 
Pinda hana alicho fanya... Kilimo kwanza kampeni ya Kitaifa ilianzishwa kwa suport Kikwete!

Wakubwa hata hiyo the so called "Kilimo Kwanza" hakuna jipya!!!! Kilimo kwanza ni DADPs tu walichofanya ni kubadili jina!!! Hakuna cha ziada wala jambo jipya!!! DADPs zilikuwepo toka mwaka 2006!!!! Hiyo ni geresha tu iliwaonekane ni wabunifu wakati hakuna kitu chochote!!! Kwa kifupi Pinda is good for nothing!!!.... ohhoo sorry.... I forgot.. he is good for nothing but weeping!!!...
 
Nakuunga mkono Marytina.

Hata hizi shule za kata wanazojivunia CCM, na ambazo mamia ya maelfu ya wanetu wanasoma huko pamoja na mapungufu yake, ni 101% kazi ya Lowassa.

Katika kuchagua mashetani wawili kwa kweli nitamchagua Lowassa...

Kweli HERI ADUI MWEREVU KULIKO RAFIKI MPUMBAVU.:A S 112:
 
Tunaweza kumjadili kama atafanya yaliyofanywa na Tajiri Zakayo:-

1. Agawe nusu ya mali zake zote kwa maskini (Lowassa anasadikiwa kuwa na more than 50b.)
2. Kama Aliiba mali yoyote ya Umma alipe mara mbili zaidi.

Kisha aje kwetu atubu then tunaweza kumfikiria kuanzia hapo.
 
Naunga mkono hoja jamaa mchapa kazi kama vipi ni - PM niwape namba yake mumpigie Mmwambie haya mnayoyasema atashukuru. Pamoja na kuitwa fisadi yeye ndiye Mkuu pekee asiyeogopa kupokea simu ukimpigia muda wowote.
 
umeishiwa sera huna la maana hapa uliloongelea nenda ukafikirie tena mada nyingine ya kupost hapa jamii forums
 
Mh,si mulisema ni slaa jamani tena haifiki mei atakua magogöni sasa munawajadili wa nini hawa kama sio UNAFIKI.Mijitu mingine bana full double standard.
 
Ukiondoa Ufisadi, Lowasa kamzidi sana Pinda. Karibu mambo yote anayojaribu kushughulikia ameshindwa. Hebu angalia mashangingi ya serikali. Hana meno. Amshukusu mama Kilango.
 
Wote hao wana mambo yao makubwa tuuuuuuu!!!! Lakini angalau Lowasa anakemea kwa sauti ya ukali na anasikiwa. Anatumia muda wake kutembea nchini na ripoti zote anazisoma sio kusomewa. Ripoti ikiwa ni ile ile anaifahamu na anaibrush hapo hapo. Anatafakari kabla ya kunena na hajawahi kunena hovyo mpaka akatuhumiwa kama mtoto wa mkulima (issue ya walemavu wa ngozi). Anaweza akasimamia maamuzi yake. Pinda amesema mashangingi basi lakini ndiyo kwanza yameongeza kwanza yale ya milioni 280 na ambayo ni mabovu ambayo nchi zingine zinarudisha.
Kuna mengi sana ambayo ni tofauti kati ya hawa jamaa wawili na pia mengi yanayolandana yapo!!!
 
pinda ni coward, hana jipya zaidi ya unafikinafiki tu

he..!!we kama si mnafiki sijui nikuiteje brucilii.mwaka jana kabla sijawa member ulisema humu unataka kuwaassasinate mafisadi wote ,sasa unapojadili sasa yupi anafaa kati ya hawa wawili NAKUSHANGAA...badala ya kupiga soga hilo ungekua busy unatafuta hiyo assasination rifle na scope,night vision gear for the job.
Unapopiga aboutturn kujadili nani anafaa kati ya pinda na lowasa UNAONESHA huna imani kuwa mwanasiasa ulokua ukimpigia debe kama ana even a chance of succeeding,ama you just like to talk even to da thing u dont mean.
Hence ma suggestion bro u oughter put a zipper on yer mouth.
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?
Wote takataka tu. Chombo kichafu hakitoi chakula safi. Lowassa kwa aliyoyafanya hasafishiki kupitia JAMII FORUM.
 
Back
Top Bottom