Comparing: Lowassa vs Pinda

Comparing: Lowassa vs Pinda

Ndugu umemsahau sokoine na Nyerere wote hawa wameshawahi kuwa mawaziri wakuu...Sijajua pia kumuweka Malecela na Lowassa kwenye kundi moja?... for what .(kupenda vyombo vya habari)..nieleze chombo cha habari cha wakati huo ambacho kilikuwa kinambeba Malecela. Lowassa -mkurupukaji, Malecela siyo mkurupukaji thet dont fit in one bucket list..unless nieleweshe zaidi.

waberoya


Kuna kipindi Warioba aliulizwa ni kwa nini kwenye kipindi chako cha uwaziri mkuu ulikuwa hutumii majukwaa ya kisiasa... kutoa promises etc...

Majibu yake yalikuwa haya: "Kwa nchi kama Tanzania mkuu wa nchi ni rais wa Jamhuri... hivyo waziri mkuu kazi yake ni kusimamia serikali na kuhakikisha ahadi za Rais zinatekelezwa... kwa kawaida waziri mkuu sio wa kutoa ahadi tena..."

Hivyo properly waziri mkuu anatakiwa kukaa na timu yake... mawaziri, wakuu wa mikoa... wakuu wa wilaya... kuwa instruction kufanya mambo na kuripoti kwake... hii sio lazima kila siku kuwepo kwenye majukwaa ya siasa na mihadhara...

Warioba na Msuya walikuwa hivi... Malecela, Sokoine, Lowassa hawakuwa hivi...

Kwa kusema hayo... sijasema nani amekosea... bali nimesema style mbili za uongozi za mawaziri wakuu....

Nachelea kumzungumzia Nyerere kama waziri mkuu kwa kuwa nilikuwa sijazaliwa...
 
BAADHI yetu tuna matatizo katika kujua vipi majukumu ya serikali yanapaswa kutekelezwa.

Isitoshe serikali nayo imekuwa na kichwa kigumu katika kubuni mikakati ya strategic planning na performance management strategies.

Pinda anaweza akawa mpole na mtaratibu lakini huu si ndio utendaji mzima wa serikali. Chukulia jambo lolote lile hapa nchini utakuta linachukua muda mrefu kweli kutekelezwa kutokana sio hasa na bureaucracy au red-tape bali 'culture' ya Kitanzania ambaye imebobea katika kuacha tatizo kuendelea kuwa tatizo.

Katika miaka hii kiongozi wa nchi anastahili kuzungukwa na jopo la watu wa fikira [na kiasi kikubwa blogi hii imesaidia sana ombwe lililopo hata kama wanatuona tuna huu sana].

Kidzogolae una hoja ya msingi lakini tusikurupuke tu na kumsulubu Pinda. Kila kazi ya serikali ina mtu wake. Mimi simhusudu mtu anayetumia vyombo vya habari kuonesha kwamba wenzake hawajui kazi ila ni yeye tu ndiye anayejua kazi. Kiafrika hili sio jambo zuri hata kidogo.

Katika fasihi moja niliyosoma 'Money Changers' staa au stalingi wa kitabu mfanyakazi hodari sana wa benki aliyekuwa anafanya hata yasiyomhusu ndiye huyo huyo aliyekuwa jizi lililoiba karibu kuifilisi benki aliyokuwa akifanyia kazi. Ilichukua kwa hakika muda watu kukubali kijana huyo mtanashati, thrii pisi suti na ubwabwa huu na ule ndiye aliyekuwa jizi la kutisha kiasi hicho.

Nirudie kwenye pointi yangu. Rais si kachagua baraza lake la Mawaziri. Je, kawapa Wizara kwa majina tu au anawaruhusu wahahe huku na kule kuona majukumu yao kama yanatekelezwa ipasavyo au Rais mwenyewe hataki mawaziri wake waonekane kama ni wachapa kazi kuliko yeye. Ninadhani, bwamkubwa ana tatizo la delegation na span of control management. Ieleweke kwamba Meneja mzuri (badili neno hilo kuwa Rais au Waziri mkuu ruksa... hafanyi kazi. Wanaofanya kazi ni mawaziri wake na sio yeye. Ukimuona Rais au Waziri Mkuu ndiye anayeonekana kuhenya basi jamaa hao sio leaders bali ni mameneja uchwara tu.]

Hivi hilo la shule sio la Wazri wa Elimu. TOR zake za kazi zinasemaje? Ana ruhusa au hana ruhusa.

Tujie usafi ambao hata yeye Lowassa hakuumudu [makampuni mengi yenye tenda za usafi jijini zilikuwa bomu] je, hapa utamlaumu Waziri Mkuu.

Kuna tatizo la barabara na foleni zisizokwisha, je, hapa ni waziri wa Miundo Mbinu au na mawaziri wengine pia wanahusika kama Waziri wa Mambo ya ndani kwani polisi wa usalama barabarani wanachangia sio haba kwa taratibu mbovu za kazi na tamaa yao ya kitu kidogo.

Umekwishasikia nini kinafanywa kuhusu umwagiliaji maji? Utamlaumu Waziri Mkuu, lakini najua fika waziri husika halali katika jitihada za kuhakikisha miradi ya uanzishaji umwagiliaji maji inaanza.

Utasema kwa kuwa Membe anasikika sana basi ndiye waziri mchapa kazi au Wizara yake kwa kuvamiwa na vyombo vya habari anatangazwa zaidi?

Waziri wa Utalii anafanya nini? Kuna mambo mengi anaweza akafunzwa kama angelikuwa na website kama hii ikawa kazi kwake. Kwa mfano, angeliweza kuwa na mkakati wa kuondosha umasikini kwa kuwawezesha wananchi pwani kujenga hoteli za makuti kama alivyofanya Mzungu kule Pangani/Sadani. Au kuzigeuza hoteli zetu za Kiswahili kwa kushirikiana na TBS zikawa na usafi na hadhi ambayo Wazungu na wageni wengine hawasiti kula na kustarehe humo. Ni kitu kidogo tu kuongeza ubora wa vijihoteli hivyo maana vingi nina hakika vina chakula kitamu kuliko cha mahoteli makubwa jijini.

Yapo mengi ya kuzungumza mwenzangu kidzogolae lakini muhimu sana hapa tukitaka kuwa na nchi inayofanya kazi tusimtarajie mtu mmoja. Lazima tufanze kama timu. Na sisi tumesomea menejimenti na human resource management lakini mchango wetu pengine hauhitajiki kwa hiyo wenzetu wanaiendesha nchi kibahatibahati tu.

Waziri wa Michezo anajua kuingia na kutoka ofisini tu na kwenda kwenye vijiwe vyake. Lakini bwana au bibi huyu angelikuwa na busara na hekima hivi asingeona umuhimu kwa kuinitiate mambo badala ya kumsubiri rais amfundishe kazi. Hakuona kama Jamaica imefanya maajabu Beijing na angeliomba tripu ya kwenda kujifunza toka kwa Waziri wa Michezo wa Jamaica siri ya mafanikio yao, je, serikali ingemnyima nauli. Ukweli ni kuwa haoni umuhimu wa kwenda kwenye nchi kama Jamaica lakini kungelikuwa na tripu ya kwenda Marekani au Londo angeliililia tu....

Lazima kila wizara iwe na Visheni na Misheni yake. Je, wizara zetu zina vitu hivyo. Wizara ya Elimu ingelikuwa na wavuti yake data zote kwamba jana wamejenga shule ngapi au wameboresha vipi masiha ya walimu ungelipata. Lakini wavuti na tovuti kwa serikali imekuwa ni ishuuu ...labda wanangoja tajamala na fadhilatu toka kwa Mapatna wa maendeleo huku fedha imetoka mlango wa nyuma benki kuu.

Ni watu wa maneno tu kuhusu TEKNOHAMA lakini kivitendo tunashindwa na kijinchi kama Rwanda aibu iliyoje? Ndio maana hali kama hii sasa inaanza kuwafanya watu wa mikoa fulani fulani ambayo ni mikubwa kuliko Rwanda na Burundi kuanza kudai ni vyema mikoa yao ingelijitawala yenyewe kuliko kutawaliwa kama sehemu ya nchi kubwa ambayo hakuna mwenye nia, ucha-Mungu na uwezo wa kuiongoza ili kuleta hali bora zaidi kwa watu wao.
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?

Hapa sio mahali pa kumsafisha Lowassa. Better find another forum.
Describe Lowassa in one word:
1.MWIZI
2.
3.
 
Hapa sio mahali pa kumsafisha Lowassa. Better find another forum.
Describe Lowassa in one word:
1.MWIZI
2.
3.

si kweli,wengi wanaojua mambo na kuyaangalia katika upeo na ukweli wake watakubaliana nami kuwa Lowasa ni kiongozi na mtawala mchapa kazi wa kweli kuliko kiongozi yeyote nani ya CCM,wengi ni wanafki ila Lowasa sio mnafki na alitolewa mbuzi wa sadaka ndio hapo matatizo yalipoanza,CCM wakimsimamisha Lowasa kugombea Uraisi 2015 japo hawatashinda lakini wataisumbua CHADEMA kuliko kumsimamisha JUHA mwingine yeyote
 
Nakuunga mkono Marytina.

Hata hizi shule za kata wanazojivunia CCM, na ambazo mamia ya maelfu ya wanetu wanasoma huko pamoja na mapungufu yake, ni 101% kazi ya Lowassa.

Katika kuchagua mashetani wawili kwa kweli nitamchagua Lowassa...
 
hata kama ni MWIZI always LOWASSA amekuwa mchapa kazi na ni mtu mwenye maamuzi bila kuogopa
 
hata kama ni MWIZI always LOWASSA amekuwa mchapa kazi na ni mtu mwenye maamuzi bila kuogopa

NAKUBALIANA NA WW KABISA. Lowassa ni mchapakazi sana sema tatizo lake ni hilo la ufisadi tu. otherwise kazi anaiweza wajameni.
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?

Bora kuwa na nchi isiyo kuwa na akina Lowasa kuliko kuwa na Pinda pia!! Bora kufunga wezi wote kuliko kuwatetea.
 
Uko right kabisa Lowasa ni mchapakazi na mimi ninamkubali lakini hafai kuwa raisi, anatakiwa awekwe sehemu ya kuchapa kazi.
Swali: Je wizi ameacha lini na atawezaje kufanya kazi independently huku rostam, patel, ..... wako nyuma yake?
 
Umenena MARYTINA, unajua huwa najiuliza huku kujiliza kwa waziri mkuu ni kwamba hajui wajibu na mamlaka yake? au ndo yupo kama picha bora yeye mkono uende kinywani? ni kweli EL ni mashine katika kuchapa kazi apewe nchi na watanzania wataona tutakavyopiga hatua,kama ufisadi si atabanwa na watendaji akileta za kuleta tunampiga chini na kunyang'anya mali zake.
 
Utalinganishaji watu wabovu, Mvivu, mwizi, hohehahe asiyejua mamlaka aliyopewa.

Pinda mlinganisheni na akina SUmaye, Warioba, Malecela na siyo kumlinganisha na fisadi Luwasa. Pinda na Luwasa hawatufai, wote, yes.
 
Hapa sio mahali pa kumsafisha Lowassa. Better find another forum.
Describe Lowassa in one word:
1.MWIZI
2.
3.

simsafishi Lowassa,nimemtaja kama ni fisadi in this sred,lowassa ni mchapa kazi ni jasiri ni fisadi.
Nitajie ingalao sifa positive moja ya PINDA, nawaambia bora mawaziri wakuu wote waliopita kuliko huyu PINDA, ebu fikiri kama PINDA angelikuwa rais ya TUNISIA yangeepukika ndani ya mwaka mmoja?
 
Sure... naunga mkono.... Mtoto wa mkulima hajiamini sana.... nahisi kama ana nidhamu ya woga. Siipendi hii tabia... ukipewa mamlaka fanya kazi kosoa bila kujali utamuudhi nani uli mradi uwe na unatimiza wajibu.... Namwona Mh Pinda kama mtu mwoga flani hivi... Ndo maana utendaji serikalini umekuwa mbovu mara dufu...

1. Pinda - Mwadilifu mwenye nidhamu ya woga!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
2. Lowasa - Fisadi - Anajiamini... somehow mchapa kazi!!!!!!!!!!

Mhh!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!:kev:
 
Utalinganishaji watu wabovu, Mvivu, mwizi, hohehahe asiyejua mamlaka aliyopewa.

Pinda mlinganisheni na akina SUmaye, Warioba, Malecela na siyo kumlinganisha na fisadi Luwasa. Pinda na Luwasa hawatufai, wote, yes.

ndio wote wametutelekeza ila shetani yupi kati ya hawa ni afadhali, miaka 150 ijayo watoto wa wajukuu wetu watamuonaje huyu pinda mnafiki, bora uwe na mtu aliyejipambanua kuliko mtu anajifanya wa madhabahuni kumbe mbwea.
 
Umenena MARYTINA, unajua huwa najiuliza huku kujiliza kwa waziri mkuu ni kwamba hajui wajibu na mamlaka yake? au ndo yupo kama picha bora yeye mkono uende kinywani? ni kweli EL ni mashine katika kuchapa kazi apewe nchi na watanzania wataona tutakavyopiga hatua,kama ufisadi si atabanwa na watendaji akileta za kuleta tunampiga chini na kunyang'anya mali zake.

Kupewa nchi hapana. Hapa tunamfananisha na Pinda. Sasa unless wachapakazi wengine wote wafe, abaki yeye na Pinda, ndo anaweza kupewa nchi.

Ukimpambanisha Lowassa na Magufuli, Lowassa anaachwa mbali sana. Ukimleta kumpambanisha na vichwa vya CHADEMA, Lowassa anaweza kuwa kama wa 7 hivi au hata chini ya hapo...
 
si kweli,wengi wanaojua mambo na kuyaangalia katika upeo na ukweli wake watakubaliana nami kuwa Lowasa ni kiongozi na mtawala mchapa kazi wa kweli kuliko kiongozi yeyote nani ya CCM,wengi ni wanafki ila Lowasa sio mnafki na alitolewa mbuzi wa sadaka ndio hapo matatizo yalipoanza,CCM wakimsimamisha Lowasa kugombea Uraisi 2015 japo hawatashinda lakini wataisumbua CHADEMA kuliko kumsimamisha JUHA mwingine yeyote
Kumbe ilihitajika sadaka kuiokoa sisiem katika sakata la richmond !!!! na kwa misingi hiyo mbuzi wa sadaka hubebeshwa madhambi yasiyo yake, tunaomba utujuze vizuri mkuu son of soil jinsi gani EL hahusiki na sakata lile na badala yake yeye a qualify kuitwa mbuzi wa sadaka ili tusiendelee kuisakama hiyo sadaka ya sisiem
 
uko right kabisa lowasa ni mchapakazi na mimi ninamkubali lakini hafai kuwa raisi, anatakiwa awekwe sehemu ya kuchapa kazi.
Swali: Je wizi ameacha lini na atawezaje kufanya kazi independently huku rostam, patel, ..... Wako nyuma yake?

mkuu,ww unaona sehemu gani inamfaa?
 
simsafishi Lowassa,nimemtaja kama ni fisadi in this sred,lowassa ni mchapa kazi ni jasiri ni fisadi.
Nitajie ingalao sifa positive moja ya PINDA, nawaambia bora mawaziri wakuu wote waliopita kuliko huyu PINDA, ebu fikiri kama PINDA angelikuwa rais ya TUNISIA yangeepukika ndani ya mwaka mmoja?

Tuko boti moja!Naona hoja hapa ni yupi bora kati ya MWIZI MCHAPAKAZI LOWASSA na MPOLE MDHAIFU PINDA..Mie kwa upande wangu ni bora Mpole Mdhaifu Pinda!
 
Hapa sio mahali pa kumsafisha Lowassa. Better find another forum.
Describe Lowassa in one word:
1.MWIZI
2.
3.

Wewe mwenyewe mwizi, unataka kutuhakikishia una survive na salary yako.
 
Back
Top Bottom