Comparing: Lowassa vs Pinda

Comparing: Lowassa vs Pinda

Mh!! Bora familia iliyo na afya na elimu kwa pesa za baba mwizi kuliko familia iliyo na kwashakoo na ujinga wa kukosa elimu kwa sababu ya baba mvivu na mwogopa wezi wa utajiri wa nyumba yake.
 
OF COURSE... NIONESHE MWIZI AMBAYE NI LEGELEGE... WEZI WOTE WACHAPAKAZI.... WANAFIKIRIA NJE YA KIBOX NDO MAANA WANAPATA AKILI YA ZIADA YA KUIBA.. Kibaka anakuzidi ujanja ndo maana anakukwida simu.. jambazi ivoivo lina silaha we huna, mwizi wa mkeo anatoa moto ambao wewe huwez ndo maana anaendelea kuiba... angekua mdebwedo km we kwanin aendlee? Kama ni hela bas kakuzidi ndo maana. Na fisadi ivoivo! SASA hiyo ni fikra tukuka kweli ati tuhalalishe wizi kisa wanaupeo zaidi ya wasio wezi? WAKE UP! Simaanishi ugoigoi uendekezwe katikati ya wajanja hasi hawa!!!

NAKUBALIANA NA WW KABISA. Lowassa ni mchapakazi sana sema tatizo lake ni hilo la ufisadi tu. otherwise kazi anaiweza wajameni.
 
Mnasahau Pinda anabanwa na so called "Mtandao", yeye aliwekwa pale kuweka balance baada ya kuona wananchi wameanza kuhoji nguvu ya mtandao. To his suprise amejikuta hana nguvu au meno ya kiutawala, amebaki kutumika kama sauti ya kulainisha maovu ya CCM. Haja JK hampi ushirikiano wa kutosha na hamjengi kama namba mbili wake. Pinda kama Pinda ana dhamira nzuri ila hana nguvu ya kisiasa wala ya kiutawala ndio maana amebaki kuwa "vuvuzela la CCM" wkt mambo yapokuwa magumu. Na yeye anashindwa kutoka sababu ana future political ambitions.
 
hata kama ni MWIZI always LOWASSA amekuwa mchapa kazi na ni mtu mwenye maamuzi bila kuogopa

Nakubaliana na wewe hata jela wanafanya kazi, kwa hiyo sehemu yake ni huko ili akafanye kazi. Tangu lini mwizi awe kiongozi wakati mahakama na jela zipo?.

We do not need wezi in decision making positions kwa sababu hapa ndipo walipotufikisha. Lowassa amelitia hasara sana taifa hili kwa sababu ya ufisadi wake na mpaka leo anatuumiza kichwa na ufisadi wa Dowans and yet wanaodai GREAT THINKERS wanamtaka awaongoze.
 
UMBUZI WA SADAKA HUU HAPA SOMA HOTUBA YAKE KWA KIFUPI

Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa. Mheshimiwa Dk. Mwakyembe ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni "Natural Justice".

Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.
Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu hata kama wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.


Mbona alipokuwa na nafasi hakujitetea alibaki kulalamika?

Lakini nimjuavyo angekuwa "innocent" si mjinga kiasi hicho, kuacha aitwe Fisadi/Mwizi na jamii katika maisha yake yote.

Kama ni mambo ya Mbuzi wa Sadaka, vipi ndugu Msabaha?

Jiulize ni nani aliwai kukiri kuwa fisadi hapa Tz? au hatuna mafisadi humu nchini???

TAFAKARI NA CHUKUA HATUA!
 
mwisho wa siku utasifia bora kuwa na mtoto jambazi aliekunulia gari kuliko mwanao mwalimu wa primary anayekupandisha daladala.

kesh Tena utaneda mbali na kusema bra Rostam azizi anayetoa pesa yake mfukoni kujenga daraja kuliko Dr slaa amabaye kazi yake ni kuongea tu.
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?

Hii nchi inao viongozi wengi sana wenye uwezo mkumbwa na nia ya kuipeleka mbele kimaendeleo.

Sioni iweje uniambie bora nichague kati ya FISADI mchapakazi na Mpalilia Ufisadi asiyechapakazi?

Sichagui yeyote mwenye hizo sifa ulizotaja!


 
ANA MSIMAMO NI SHUJAA ASIYETETEREKA SOMA HOTUBA YAKE AKIACHIA NGAZI HAPA
Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe. Kama katika chombo hiki haki haitaonekana kutendeka nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia. Kwa nhiyo nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba naona si sahihi, nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana, nimeonewa sana katika hili.
Maana zimechukuliwa tuhuma zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijauliza. Kulikuwa na shida gani kuniuliza, kwa nini muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo yangu. Sisi wote hapa ni wanasiasa tukianza kuamini minong'ono ya mitaani niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi, Tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana

Kwako wewe mwizi ni shujaa, ulikuwa mmoja wa waliompokea kwa shangwe Monduli eh?
 
Kwa anaye mjua yule legwainani yule!!atakubaliana na mimi kwama EL nimchapa kazi uwezi kumlinganiha na pinda japo kila mmoja anamapungufu yake!!Kwanza anayekumbuka sakata la mnazi mmoja,sakata la city water hivyo niujasiri kwanza akiwa waziri wa mifugo na maji aliwawekea wananchiwake maji,Mabwawa yakutosha hakuna shida ya maji,akiwa waziri mkuu akawawekea mjiwao kwenye mazingira safi,rami,miradi,Na alikuwa na mipango yakupitisha barabara hadi serengeti kupitia monduli,Shule za kata ndo usiseme the guy is :A S thumbs_up:

Sina simile na mwizi, kwanza ingekuwa CHINA hata msingekuwa mnaongelea kama kiongozi bora, angekuwa keshauwawa kwa mkono wa sheria.
 
Kwa hii thred nimekushusha kiwango balaaaaa.Yani nafkiri humjui lowassa kiundani zaidi ya mimi niliyewahi kuishi kwake.Kwa taarifa yako huyu jamaa na Rostam mpaka sasa ivi ndo wanaongoza nchi na kampuni yao inaitwa CCM na JK na Pinda ni waajiriwa wao.Samueli sita walimnyima kazi ile ya mwanzo baada ya kuona kijana anafundisha wenzake kugomagoma.Sasa basi kwa taharifa yako Lowasa ni next level au kwa jina lingine ni mojawapo wa Tanzanians Tycoons.Lowasa ni mjanja sana katika michezo michafu kwa mwavuli wa kuongoza.Lowasa haibi million ila ni mkali kusimamia vimiradi vya wananchi vya mamilioni.Jamaa akikwapua anakwapua kuanzia figure za bilions na ni mjuzi balaa wa kujisafisha tena mbaya zaidi hadi makanisani.Sasa basi hapa ni the home of great thinkers na sio great talkertives.lowassa Hafai hata marehemu baba wa taifa alituonya dhidi ya huyu mtu bora mara elfu kumi hata makamba na ukilaza wake.

Endorsed! Well done ndugu
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?

Ni jambo la baya na la hatari sana kujaribu kuwa na fikra kama yako wachilia mbali kuthubutu kuweka chapisho la kusema "bora Lowassa kuliko Pinda". The two are both utterly and absolutely abomination to the service and propserity of the country, how do you repudiate or differentiate one to another?

Na kama nchi yenu imekuwa duni na ovyo namna hii, na kama giza limetanda kiasi cha mwanga pekee ni kuona Lowassa ana nafuu kuliko Pinda, basi Tz haina tumaini lolote lililobaki. Sijui nia yako mwandishi ni ipi? ni upotoshaji, ufinyu wa uchambuzi au ni nini...tafadhli nisaidie nia yako kwa chapisho kama hili ni nini?
 
munamuonaje PINDA-si mchapa kazi, anajiliza, analalamika maofisa kununua magari ya bei juu,hapingii rushwa kivitendo,ni ndumila kuwili (leo A kesho Z),anajifanya mtu wa kanisa,mtoto wa mkulima (bora angekuwa mtoto wa bilionea) anayechekelea nchii ikiangamia,

LOWASA-ni mchapa kazi anayeogopwa na maofisa wenzake serikalini (sifa muhimu),ana ujasiri na kujua maana ya cheo chake ni fisadi kivitendo (hana tofauti na PINDA asiyeupinga ufisadi).

hapa ni bora nchi kuwa na lowasa fisadi mchapakazi, kuliko PINDA mpalilia ufisadi asiyechapa kazi?

Mmeanza kumsafisha eeeh naona kampeni za 2015 zimeanza
 
Mh!! Bora familia iliyo na afya na elimu kwa pesa za baba mwizi kuliko familia iliyo na kwashakoo na ujinga wa kukosa elimu kwa sababu ya baba mvivu na mwogopa wezi wa utajiri wa nyumba yake.
big up! tungekuwa na electronic device ya kutrace nanma hela ya watanzania inavyoporwa kwa uvivu na undumilakuwili na kutotambua mamlaka yake nadhani kwa PINDA zingekuwa nyingi kuliko ile mil 152 @day ya LOWASSA
 
big up! tungekuwa na electronic device ya kutrace nanma hela ya watanzania inavyoporwa kwa uvivu na undumilakuwili na kutotambua mamlaka yake nadhani kwa PINDA zingekuwa nyingi kuliko ile mil 152 @day ya LOWASSA

Martina Martina,somtime unagonga mawe,umekunywa supu ya ulimi nini?
 
Hapa sio mahali pa kumsafisha Lowassa. Better find another forum.
Describe Lowassa in one word:
1.MWIZI
2.
3.
wee mwehu, ni kiongozi gani ccm sio mwizi?? kuanzia huyo mkulu wenu hadi kinyangarika wa mwisho, weezi wooote, pinda ni kama lijoka la kibisa, ni waziri mkuu afu amekalia kutoa majibu ya 'mi nadhani'..pumbaf...lowasa kwa sie watu wa chini tulimuona poa, acha aibe..nani asiyeiba..shule za kata mnazolalamika kuwa hazina walimu wala vitendea kazi ni lowasa..alizijenga then baada ya kuondoka pinda wenu na serikali yake wa,eshindwa kuweka walimu na vitendea kazi./ angekuwepo lowasa angesema nataka nikute kila shule ina walimu kumi na vitendea kazi vya kutosha then watendaji wa halmashauri wangejicheki wenyewe..na ungeona wangetafutana na kazi ingefanyika..kifupi mimi nataka lowasa awe presidaa na aendelee kuiba na awawajibishe halmashauri na sie wa chini tunufaike kidogo..mtoto wa mkulima my ass..
 
bora kufuga mwizi mmoja kuliko wezi wengi...lowasa ni mwizi mmoja lkn mwenye maendeleo....
 
PINDA NI ZAIDI YA LOWASA

Nimependa Maada iliyokuwa ikijaribu kumsafisha LOWASA na mazuri yake, ila ni kweli alifanya kazi kama nyuki usiku na mchana may be kwasababu ya usaiba sina uhakika zaidi.

Ila Jamani mi naona kasi aliyonayo mtoto wa mkulima ni kasi nzuri ambayo ni kasi zaid ya ile ya Lowasa, maana kila kundi likigoma kwasasa utasikia tunamtaka mtoto wa mkulima.

PINDA VS LOWASA NANI ZAIDI? MAONI JAMANI
 
Ubora wao unaupima kutumia vigezo gani? Mbona thread is too shallow? In my opinion both are failures. Pinda = very weak, cannot make decision, false pretender, hana uwezo wa kusimamia mambo.
Na huyo Lowassa = sio mwaminifu, mfuja mali za nchi, ana jazba, halitakii mema taifa na watru wake kwa kuiba mali za watanzania na kujilimbikizia binafsi.

Sijaona bora ila naoma wote mambomu!
 
Pinda naye kapata mgao wa Dowans, ndiyo wale wale, hakuna mtu safi anaweza patikana CCM wote wanaangalia masilahi yao tuuuuuuuuu.Dawa ni kuanzisha tifu kama huko arabuni hawa mbwiga wa CCM wana turostisha tu
 
Back
Top Bottom