CNN ni sehemu ya CIA: Mtazamo wao kuhusu Serikali yetu ni mtazamo wa Jumuiya ya Kimataifa. Tusiwapuuze!

Donald Trump ni mzungu mwenye tabia zote za madikteta weusi wa Africa. Bahati iliyowaokoa wamarekani ni Katiba yao imara iliyosimamisha taasisi Imara zenye nguvu na huru ambazo haziwezi kuendeshwa au kuyumbishwa kirahisi na maamuzi ya mtu mmoja.
Donald Trump alishasema CNN ni fake news kazi yao ni kufanya propogada kwa maslahi ya main stream media. Ukitaka kujua mengi zaidi kuhusu hii fake news watch Fox News hao ndio kiboko yao. Wamarekani wengi hawaangalii CNN
 
Mkuu CNN ni kituo cha tv ambacho kipo kimaslahi zaidi na kilitumika kwa kiasi kikubwa katika kampeni za urais wa Marekani dhidi ya Donald Trump

Mkuu CNN wapo biased sana katika kuripoti mambo ya human rights ukichukulia masuala ya Palestine kwa hiyo haiaminiki sana. Kuhusu mahusiano ya serikali ya awamu ya sita na nchi za magharibi Chadema wasitegemee kupata support yeyote kwani mahusiano yameimarika sana hata leo tumeona serikali Marekani ikiikabidhii chanjo za covid 19 kwa Waziri wa Afya wa Tanzania masuala ya human rights serikali ya awamu ya 6 kwa kipindi kifupi imeonyesha mabadiliko makubwa mpaka Chadema wameshtuka kuona umaarufu wao unaanza kushuka kwa kasi mpaka wakaja kuanzisha vurugu za kudai katiba mpya.
Mbowe alifanya ziara Tanzania nzima lakini mapokezi aliyopata yalikuwa madogo sana. Sasa Tundu Lissu, Mbowe na Maria Sarungi kukimbilia hizi main stream media kama CNN haiwezi kuwasaidia wanatakiwa wawe nasubira kama Rais Samia Suluhu Hassan alivyoahidi atashughulikia masuala ya katiba baada ya kujenga uchumi baada ya taifa kuathirika kwa kiasi kikubwa kiuchumi kwa ajili ya janga la Covid19
 
Very strange!

Huna sababu ya kutahayari kuhusu nchi yako inazungumzwaje na vyombo vya habari vya nchi za nje.

Nchi yetu ni nchi huru, a sovereign country wao wanasema. Kama nchi huru kuna mambo fulani tutayafanya kivyetu vyetu kinamna namna zetu.

Kama tutataka kila kitu tunachokifanya kionekane kiko sahihi kwa mtazamo wa vyombo vya habari vya kimataifa basi tukubali kwamba nchi yetu iwe kitengo kimojawapo miongoni mwa vitengo vya Aljazeera na CNN.

Ili kabla hatujanywa maji au hatujala chakula au hatujavaa nguo au hatujaenda choo tuwaulize mabosi wetu CNN kwamba hivi haya tunayotaka kuyafanya ni sahihi siyo sahihi? Tuna kibali chenu au hatuna kibali chenu? Mtatuzungumzia vizuri au hamtatuzungumzia vizuri?

Very strange indeed!

Mimi kilio changu ni kuona hii nchi imejaa watu walioelimika kweli kweli, wanaoweza kuzisoma nyakati na kupambanua mambo, na kugundua kwamba hapa duniani mchezo ni survival of the fittest, na kila mmoja anaangalia maslahi yake. Maslahi ya Marekani na vyombo vyake si lazima yawe maslahi ya Tanzania na vyombo vyake. Pale tutakapoona maslahi mapana ya nchi zetu yanashabiiana tutapatana, pale maslahi yasipokwenda sawa, mfano iwapo tafsiri za demokrasia haziendi sambamba na dira ya uchumi na amani ya nchi, tutaonana wabaya tu.

Mbona na wao wako hivyo tu? Mara ngapi wamepindua democratically elected regimes duniani kote kisa viongozi waliochaguliwa wameenda kinyume na maslahi ya nchi za magharibi?
 
Mwendambinguni alimfundisha kuumiza Sasa a ha atekeleze aliyoa hiwa mshaambiwa hatabasirika no Yule yulw
 
Very strange!

Huna sababu ya kutahayari kuhusu nchi yako inazungumzwaje na vyombo vya habari vya nchi za nje.

Nchi yetu ni nchi huru, a sovereign country wao wanasema. Kama nchi huru kuna mambo fulani tutayafanya kivyetu vyetu kinamna namna zetu.

Kama tutataka kila kitu tunachokifanya kionekane kiko sahihi kwa mtazamo wa vyombo vya habari vya kimataifa basi tukubali kwamba nchi yetu iwe kitengo kimojawapo miongoni mwa vitengo vya Aljazeera na CNN.

Ili kabla hatujanywa maji au hatujala chakula au hatujavaa nguo au hatujaenda choo tuwaulize mabosi wetu CNN kwamba hivi haya tunayotaka kuyafanya ni sahihi siyo sahihi? Tuna kibali chenu au hatuna kibali chenu? Mtatuzungumzia vizuri au hamtatuzungumzia vizuri?

Very strange indeed!

Mimi kilio changu ni kuona hii nchi imejaa watu walioelimika kweli kweli, wanaoweza kuzisoma nyakati na kupambanua mambo, na kugundua kwamba hapa duniani mchezo ni survival of the fittest, na kila mmoja anaangalia maslahi yake. Maslahi ya Marekani na vyombo vyake si lazima yawe maslahi ya Tanzania na vyombo vyake. Pale tutakapoona maslahi mapana ya nchi zetu yanashabiiana tutapatana, pale maslahi yasipokwenda sawa, mfano iwapo tafsiri za demokrasia haziendi sambamba na dira ya uchumi na amani ya nchi, tutaonana wabaya tu.

Mbona na wao wako hivyo tu? Mara ngapi wamepindua democratically elected regimes duniani kote kisa viongozi waliochaguliwa wameenda kinyume na maslahi ya nchi za magharibi?
Kwanza Tanzania inqzsidi kujupikq a cnn rfq bbf ndiyo habari ya Dunia
 
Nimejaribu kutafakari uchambuzi wa CNN kuhusu kushikiliwa kwa Freeman Mbowe, kuna kitu wanaongelea sana pale "timing of arrest". Nadhani exposure yao ni kubwa sana kwa siasa za mataifa mbalimbali ikiwemo siasa za bara la Africa. Tunafahamu katika tools za kupatia taarifa kwa mashirika ya kijasusi kama CIA ni kuptia vyombo hivi vilivyoenea duniani kote, mfano BBC inatumika na MI6, kuna Aljazeera huko Asia na kadhalika.

Kiuhalisia CNN inaichambua hali yetu ya kisiasa kama ya mwaka mmoja uliopita na ikimnasibisha Mama yetu na Hayati Magufuli. Inasema kuwa yeye alikuwa msaidizi wake so inawezekana ameamua kuendeleza mfumo ule. Kimataifa hii inaturudisha kule tulipotoka, kule kwenye matamko ya jumuiya ya kimataifa, kule kwenye kuanza kututenga na kumuandama Rais wetu.

Tanzania siyo kisiwa hivyo tunapaswa kujenga taswira nzuri kimataifa. Simaanishi Sheria zisifuatwe la hasha lakini hizi sheria zinazoleta makosa yanayomnyima mtu Dhamana hata Samia alishazuia kutumika hovyo. Tunakumbuka kesi ya kina Mbowe ambayo walishinda kwa rufaa na kurudishiwa fedha zao, ikumbuke Mbowe alishakaa ndani miezi mi4 kama Sugu na Lema na wengineo.

CNN wanahoji je kudai katiba mpya, kukusanyika, kufanya kusanyiko wa kisiasa ni "Constitutional Rights" (Wao wameziona wapi hizi haki?) means wamesoma katiba yetu.

Kwa jicho la tatu maana yake wao wanaona kama Serikali yetu inatunyima haki zetu za kikatiba. Hii ina maana mbaya sana kwa 6th Regime ya JMTkimataifa hasa kipindi hiki ambacho Mama anataka kuifungua nchi kuongeza wawekezaji na kuleta Maendeleo ya kiuchumi.

Serikali ipambane na wavunja Sheria,iendelee kupambana na ugaidi lakini isiwabambikie kesi hasa kwa makosa yanayonyima dhamana.

Kazi na iendelee!




Je wanamwonea mtu? Miwani zao unauwezo wa kuzivaa!?
 
Kujua kinachoendelea unahitaji kuangalia picha halisi kwa marefu na mapana.

Ishu sio mbowe kupewa kesi ya ugaidi ishu ni watanzania kupumbazwa kuhusu Mbowe ili chanjo za corona na uhuru ambao mtanzania anapoteza kila siku zinavyoenda .
Pesa ya corona imeingia wenye pesa zao wanataka tufuateasharti ambayo 75% ya waTz wanaona ni ya kipuuzi sasa tunafanyaje?kwakuwa mbowe nae kapokea fungu lake basi M/kiti kakubali kuwa centre of attention kuwapumbaza watu.

Hapa ishu ni Agenda ya corona inavyopenyezwa kupitia Mbowe.

Mbowe hajawahi kuwa na kashfa ya ugaidi ukiona kapewa tuhuma z ugaidi laZima ujue lengo ni nini na kujua lengo laZima uanagalie tanzania kwa ujumla.

Huu ni mpango ambao wenyewe uelewa na wasioshabikia siasa tu ndo wataelewa.
 
Back
Top Bottom