Ed n Edd nEddy
JF-Expert Member
- May 3, 2011
- 5,345
- 6,078
Hawa jamaa huwa wanajiona wako sahihi kumbe their very stupid aseeee
Nilianzisha uzi kama huu mwaka jana kwenye kipindi hiki hiki, NI AIBU KUBWA
Ndiyo maana Jamii yetu imeharika si mdogo wa si mkubwa maana tumefika mahali tumekubali kila kitu nisawa.
Ebu pima na jifikirishe Bibi kumtongoza kijana mdogo ,hili linatupa elimu gani kwa vijana wadogo 2-12yrs . Naamini hiyo ni Elimu inatosha miaka mitatu mbele vijana tena wadogo watakuwa wakiwachangamkia Vibibi tena bila kusahau hawana cha kwenda Mwezi/wala Mimba hapo Upo?
Mie simo huu ushauri tu kuwa nivizuri kuepuka mambo haya!
of coz yes mabibi wanakatishwa viuno kama madensa wa twanga ani aibu kinoma
Ukitaka kutazama hiyo tv au kusikiliza hiyo redio ya unatakiwa uwe mvuta bangi mnywa viroba na uwe umelelewa na wahuni ndo utaiona nzuri.Hawa watu ni majanga tena hawafai hata kwa matumizi ya binadamu hawana adabu wana nidhamu!!Yatoka kwa Mdau
SERIKALI IANGALIE UDHALILISHAJI UNAOFANYWA NA CLOUDSTV KUPITIA KIPINDI CHA BIBI BOMBA
Posted on May 19th
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyohavina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha BIBI BOMBA kinachorushwa na TV hiyo. Nimehuzunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.
Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa Biology, akajibu ndiyo. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.
Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.
Kama kweli kinachofanyika katika kipindi kile ni kuwajali bibi wale kwa maana ya kuwapatia pesa wakishinda hebu wanaoendesha kipindi kile siku moja wawalete bibi zao na wawahoji maswali yale ya kishenzi tuone kama itakuwa sawa kwao, kwanini pesa iwe kigezo cha kudhalilisha watu wazima? Tena wanadhalilishwa na vijana wadogo wasio na chembe ya maadili? Hivi kweli kumwambia bibi mtu mzima amtongoze kijana mdogo halafu mbele ya skrini kila watu wa rika tofauti wanatazama wakiwemo watoto hapo tunafundisha maadili gani kwa jamii?
Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huutukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki
SERIKALI IANGALIE UDHALILISHAJI UNAOFANYWA NA CLOUDSTV KUPITIA KIPINDI CHA BIBI BOMBA|Mtizamo Huru