Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

Mi nasema hivi,wale watangazaji ni wapenda chini.Kama unataka kuwa na babu wa kufikia basi endelea kuruhusu bibi zenu kwenda.

Hahahaaaa, kwa hiyo watawakula mabibi wa watu jamani?
 
Mwanzo nilidhan lengo la kipindi ni kuchukua yale mazur na changamoto ambazo bibi zetu wangeweza kuzirithisha kwa kizazi hiki ili kuweza kutunza maadili yetu ya kitanzania, lakini imekua kinyume wanachukua maujinga yao kuwafundisha. sijui wanalengo gani na malezi ya watoto wa leo na wa baadae, binafsi sioni maana ya kipindi kile, wanatumia fulsa ya umasikini wa bibi zetu
 
wao wanajua wanatuburudisha kumbe wanatukera, mbona wao hawawapeleki mabibi zao? watafute njia nyingine ya burudani, wawaache wazee wa watu wapumzike.
 
kuulizwa maswali ya kishule wakati hawakwenda shule, hapo bibi wanadhalilishwa KITAALUMA. the presenter's aim was to humiliate the grans academically--try to make them fools and making that 'folly' known to their viewers. this's pure academic discrimation. kwa wale wenye utovu wa maadili mtaona ni sawa lakini huu ni udhalilishaji wa dhahiri.

kama ndio hivii hamtawaelelwa kabsaaa
 
utter disgusting! niliwai kiona one time kwa kweli sikumaliza hata dk 10
 
Kuwa na heshma kwa wakubwa mkuu hata kama nawe ni mkubwa bac nivyema uwaheshim wengine
unashangaza.. sasa huyo bibi alieulizwa swali ambalo wala halijui.. kilichomfanya akubali kuwa alikula biology ni niniii?? maana huwezi kuitikia kitu usichokijua na kuwa ati umekifanya na kumbe hujawahi hata kukiona.. huu ni uzoba wa hao kina mama na wala tv haijawadhalilisha. alichotakiwa kufanya huyo mama alitakiwa ajibu kuwa sijawahi kula biology. na wala asingeonekana mjinga.
 
hahaha bibi anaruka hip hop hure oo ee' wangebadil mfumo mzima wa kipindi hakina tija.
wangekifanya kiwe na mafunzo hao bibi wangetufunza kusuka vikapu na vingne ving wanaweza c kuwaambia wavae milegezo,nmesense kbs

wanasaka mahela!!
 
Kuwa na heshma kwa wakubwa mkuu hata kama nawe ni mkubwa bac nivyema uwaheshim wengine

mkuu unataka niwe na heshima gani kwa hawa mabibi?? kwanza me naona wanajizalilisha tu na cha zaidi ni njaa ndio inasumbua.. maana wanakubali kujibu maswali hata wasiyojua kujifanya wanajua haya ndio matokeo yake.

nikuulize wewee JE UMESHAWAHI KULA BIOLOGY??? hebu nijibu afu ndo ntajua IQ yako imesimamia wapi
 
nimecheka comment za humu ndani lol..............

basi home ndio wanakipend hiko kipindi kweli mie nikatizama

hiyo siku walikua wanarembwa jamani jamani ilikua balaa halafu walivyorembwa

wakaambia watembee kkama mamiss
 
Maswali ya hovyo yanawafanya bibi zetu waonekane mazuzu katka jamii.wangetaka hivyo si watafute kijana bomba wamuulize hayo maswali yao ya facebook
 
kuulizwa maswali ya kishule wakati hawakwenda shule, hapo bibi wanadhalilishwa KITAALUMA. the presenter's aim was to humiliate the grans academically--try to make them fools and making that 'folly' known to their viewers. this's pure academic discrimation. kwa wale wenye utovu wa maadili mtaona ni sawa lakini huu ni udhalilishaji wa dhahiri.

hebu nambie umeshawahi kula BIOLOGY???? hapa nataka nione uwezo wako wa kujibu ili nikutofautishe na hao mabibi njaa
 
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudhunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.

Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.

Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.

Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.

Hapo nimechoka kabisa! Najua Bongo Serikali iko Likizo na hasa vitu kama hivyo maana vyombo hivyo kwa CCM ni sawa na Mto na Maji.

Ukiacha uadhalilishaji pia ni Utovu wa maadili.
Baraza la Habari Tanzania mpo!
Maana yake mbele ya safari vibibi huku mitaana vikianza kuchangamkiwa na hawa vijana wa Dot.com kwa ajiliya kufanyia mazoezi na mwisho wa siku mnaanza kulalamika wakati elimu husika ya mbinu hizo zinatolewa Bure TV hapa Bongo.

Wenzetu huko ulaya walianza hivi hivi mdogomdogo!
 
Kama hali ndio hii ya kila mtu kuona hawa jamaa ni shidah katika jamii, basi kuna umhimu wa TCRA kutazama upya kazi zao na vipindi pia.

Na jiuliza kitu kwanini station nyingi sijawaiona zikilalaimikiwa hapa kwa kazi kuna kitu hapa

cc; Ruge

Kwani wewe hujui kama hao TCRA ndo hao hao???? kwani tcra kazi yao ni ipi!!!!! yaani mimi binafsi sijaona kipindi cha maana ambacho kina mvuto wa kukitazama kupitia clouds tv...........................Hawa jamaa ni pumba....vuuuuuuu kabisa
 
nimecheka comment za humu ndani lol..............

basi home ndio wanakipend hiko kipindi kweli mie nikatizama

hiyo siku walikua wanarembwa jamani jamani ilikua balaa halafu walivyorembwa

wakaambia watembee kkama mamiss



Ndiyo maana Jamii yetu imeharika si mdogo wa si mkubwa maana tumefika mahali tumekubali kila kitu nisawa.

Ebu pima na jifikirishe Bibi kumtongoza kijana mdogo ,hili linatupa elimu gani kwa vijana wadogo 2-12yrs . Naamini hiyo ni Elimu inatosha miaka mitatu mbele vijana tena wadogo watakuwa wakiwachangamkia Vibibi tena bila kusahau hawana cha kwenda Mwezi/wala Mimba hapo Upo?

Mie simo huu ushauri tu kuwa nivizuri kuepuka mambo haya!
 
frema120 sikutaka kabisa kuchangia hii issue lakini umeniita nitauliza tu maswali machache:

Chukua majibu sasa.
1.wewe unaweza kumruhusu bibi/mama yako ashiriki?

Siwezi

2.unafikiri hao mabibi hawana watoto/wajukuu?

Wanao watoto, ila hawajiele kama wewe.

3.hao mabibi walilazimishwa kushiriki?

Njaa tuu, na mfumo mbaya wa serikar hii juu ya wazee wetu.

4.hiki kipindi mpaka kinaonyeshwa siku zote hizo kama kingekuwa kinakiuka maadili si kingefungiwa??

Walifungiwa, radio imani lakini cloudfm walipigwa faini kisani.



Ipo jengo tu sam njomaa road.
 
Last edited by a moderator:
Wakulaumiwa ni hao mabibi na watoto au wajukuu zao waliowaruhusu kujiingiza katika huo ujinga.

What if we deal with 'single point' that is Clouds TV?? tukicontrol TV tutakuwa tumewacontrol hao mabibi na watoto au wajukuu zao wanaowaruhusu kujiingiza katika huo ujinga!
 
Chukua majibu sasa.


Siwezi



Wanao watoto, ila hawajiele kama wewe.



Njaa tuu, na mfumo mbaya wa serikar hii juu ya wazee wetu.



Walifungiwa, radio imani lakini cloudfm walipigwa faini kisani.




Ipo jengo tu sam njomaa road.

dont hate the player hate the game.
 
Back
Top Bottom