Hili tatizo nimeliripoti kwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, TAMWA, TCRA, TAWLA, LHCRA na kila mahali lakini mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyechukua hatua. Hata hawa TAMWA juzi tuliona wakiandamana kuwatetea wasichana wa Nigeria waliotekwa na Boko Haram, lakini hatujawahi kuwasikia wakiwatetea hawa mabibi zetu wanaodhalilishwa hadharani kama nyumbu wa Serengeti.
Nadhani Clouds TV wana ubia na CCM na serikali yake ndio maana wanavunja haki za binadamu bila kuchukuliwa hatua yoyote ya kisheria. Bw Asa Mwambene (Mkurugenzi wa Habari, Maelezo) anajua kufungia vyombo vya habari kwa maelekezo ya wanasiasa tu. Sidhani kama ana meno ya kuweza kuwazuia Clouds TV waache udhalilishajiwao huu. Mwaka wa jana tumeshuhudia Radio Clouds wakipigwa faini ndogo ya Tsh 5M huki Radio Imaan FM wakipigwa faini na kufungiwa kwa miezi 6 kwa makosa yanayofanana. Sababu ya Clouds kupigwa faini peke yake bila kufungiwa huku Imaan wakipata adhabu zote mbili kwa kosa lilelile wanazijua serikali ya CCM na mafisadi wake.
Nashangaa kwanini viongozi wa nchi hii wameamua kuziba masikio na kuvaa miwani ya mbao kwa matatizo yanayowasibu wanyonge. Nadhani kama ingekuwa bibi zao ndio wanaodhalilishwa kama hivi wasingekubali. Haya yote yanatokea kwa sababu ya utawala dhaifu wa serikali ya kifisadi ya CCM; na inaonyesha ni jinsi gani serikali ya CCM isipojali matatizo ya wanyonge. Lakini ipo siku ukombozi utapatikana na udhalilishaji kama huu utafikia kikomo. Tuombe Mungu atusaidie kuufutilia mabali utawala huu kengeufu na usiojali kero za walalahoi.