mimi mwenyewe nimewahi kuwapigia simu wakiondoe hicho kipindi kinadhalilisha mama zetu jamani, wakakata simu na kuizima kabisa
subiri ma-'GREAT THINKER' waje utaambiwa wewe ni b-12,mara adam mchomvu.....ukitaka uonekane una akili humu we ponda clouds tu
Sidhani kama Program inayoanzishwa na Adam Mchovu au sijui B 12 kweli itakuwa ya maana....Asante kwa jitihada zako, mkuu. Hawa jamaa sio bure--kuna watawala wanawalinda ndio maana wanaendelea na huu upuuzi wao wa kuwadhalilisha bibi zetu.
Una maana gani kupost huu uzi mara mbili? huoni kwamba unatujazia server bila sababau za msingi? Changia mada, kama huna hoja ya kuchangia, changanya miguu.
Uko wapi? Basi nenda kachangie huko ulikouona! Vinginevyo, changanya miguu....ama umetumwa na Ruge uje kutuvurugia mjadala?
sauti ya wengi ni sauti ya mungu.
na mimi naungana na wengi kuwaponda
Clouds TV kwangu mimi kipindi chenye maana ni Sports Bar peke yake na ni jumatatu tu....
Mkuu, kuna uhusiano gani kati ya hivi vipindi viwili--BIBI BOMBA & AFYA CHECK?
usirukie tu comment ya mtu bila kujua alielengwa alisema nini. niliemjibu alisema yeye anapenda sports bar tu kwenye vipindi vya clouds ndio nikamuuliza hapendi afya check ya dr issack?. hio bibi bomba yenu endeleeni tu na mjadala.
Sawa. Nilidhani umechanganya madesa, kumbe ulikuwa unagawa elimu. Hakuna tatizo.
Some Jerry Springer types of shows show the extent of freedom of expression, this freedom should reigns supreme, as long as laws are not broken.
Kama hupendi usiangalie, watu wa kutosha wakiacha kuangalia Clouds wenyewe itabidi wabadili vipindi.
Clouds wanaweza kuendelea na vipindi kama hivi ikiwa tu kuna watu wanavipenda.
Clouds is just a mirror which shows the true image of you, change and stop blaming the mirror.
Kama unafikiri nawalaumu Clouds hujanifahamu bado.
Rudia kusoma halafu fikiri kwa makini.
Kama kuna kipengere unahitaji msaada kukielewa uliza tu.
mmi nilikuwa nasisitiza ulichosema kwa maneno mengine lakini ujumbe ule ule.