Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

Clouds TV acheni kuwadhalilisha bibi, mama zetu!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
27,153
Reaction score
27,722
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudhunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.

Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.

Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.

Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.
 
...dah mkuu,yaani kama ulikuwepo eneo ambalo tulikuwa nasi tunasikiliza hicho kipindi(nilikuwa kwa kinyozi),kiukweli nasi tulijisikia fedheha kubwa sana kuona bibi na mama zetu,kuulizwa maswali ya kijinga namna ile,

Labda nami niwaombe Viongozi wa Clouds TV kwanza wakiangalie vizuri hiki kipindi kwani kina makosa mengi ya kiitaaluma na ikiwezekana watafute mtangazaji mwingine wa kuendesha hiki kipindi,huyo Babuu wa Kitaa hafai,kwanza umarekani mwingi,maneno ya mtaani mengi na maswali ya kijinga.
 
Inabid ipigwe ban .

Sio mantiki ya kipindi hicho

Wanawafundisha uhuni wa kusema maneno kama nigga.
 
Naona mnataka RUGE apige ban kupiga kale ka wimbo ka Hello hello Tz @ 50 !CCM Oyeee...
 
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.

Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.

Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.

Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.
Nashindwa kuamini kama vipindi vya clods tv vina haririwa (editing)!Ni upuuzi naushamba wahali ya juu kutumia wazee kama wale kujitafutia umaarufu kwa hadhira.Laiti kama ningekua TCRA clouds tv rungu lingewashukia.
Huwezikumuuliza mama au bibi yako eti mara ya mwisho kuhonga ni lini?kwa kivuli kwamba ni tv ya burudani,Hii ni burudani gani!!!
 
Jamani nashukuru nimeekutana na huu uzi yan kile kipindi huwa nakichukia kuliko vyote huwa nakuta watoto wanaanngalia nashindwa kuzima tv tu, kiukweli ni fedheha kubwa wanayoifanya hv serikali hawalioni hili mara wawaongeleshe maneno ya mitaani, hv vitu vinamsadia kingongwe yyt tz hii, yan clouds aaaarrgghh!!!!! Matapishi
 
Mimi nilikuaga mfuatiliaji mzuri sana wa vipindi vya clouds , lakini kipindi kama kile cha saa kumi cha kina kibonde kilinifanya niachane kabisaa na hiii radio, watu w azima kazi kuongea upuuzi na kucheka ovyo kama mashoga, yani wanaudhi sana, upuuzi ni mwingi sana kwenye vipindi vyao.
 
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.

Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.

Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.

Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.

Change the channel!
 
Bibi wa miaka 70 anapofundishwa apozi kama Black American thug na kuambiwa aseme "whatsup ma nigger" na kufanya ndio tangazo la mara kwa mara, huu ni udhalilishaji na ushenzi!!


Yani ni udhalilishaji, sasa mantiki ya kipindi kama kile ni nini? si bora hata wangeandaa kipindi ambacho wanawakusanya hao mabibi na kusimulia watoto hadithi za zamani, angalau watapata cha kujifunza sio huu ----- wanaoufanya sasa hivi.
 
Clouds TV (Ruge na team yake) mlipoanzisha shindano hili la BIBI BOMBA nilifikiri wanataka kuwatumia bibi hawa kwa ajili ya kutukuza uTanzania wetu, utamaduni wetu na mchango wao ili kufanya vijana wafahamu utamaduni wetu ambao unaanza kusahaulika katika jamii. Lakini tunachokishuhudia hivi sasa ni kinyume chake. Ni udhalilishaji usiovumilika wanaofanyiwa bibi na mama zetu. Haingii akilini kumuimbisha bibi wa miaka 65- 70 nyimbo za muziki wa kizazi kipya au kumvalisha suruali wakati tunazo nyimbo zetu za kabila mbalimbali na pia tunafahamu kabisa katika maisha ya kawaida bibi hao hawavai hivyo!

Ruge umekosea sana(wewe ndiye msimamizi wa TV yako kufanya marekebisho. Jipe muda fuaitili shindano hilo uone kama kuna lolote la maana jamiiinajifunza. Badili maramoja; itapendeza na kuleta maana zaidi kama bibi hawa watashidanishwa kwa mambo yenye maadili na kudumisha utamaduni wetu Watanzania


EJL
 
Niache kuangalia BIBI BOMBA kwa mtonyo Gani?

haaaaaa haaaaaa haaaaaaaaaas
haaaaaaaaaaaaaaaaaa haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaasss leo walikua wanaonesha Tanga na Asha Boko haya hana.

Nimesimitika bibi mmoja alivyokua anakatika hadi nooooma.
 
Back
Top Bottom