Yani ni udhalilishaji, sasa mantiki ya kipindi kama kile ni nini? si bora hata wangeandaa kipindi ambacho wanawakusanya hao mabibi na kusimulia watoto hadithi za zamani, angalau watapata cha kujifunza sio huu ----- wanaoufanya sasa hivi.
Mimi nilikuaga mfuatiliaji mzuri sana wa vipindi vya clouds , lakini kipindi kama kile cha saa kumi cha kina kibonde kilinifanya niachane kabisaa na hiii radio, watu w azima kazi kuongea upuuzi na kucheka ovyo kama mashoga, yani wanaudhi sana, upuuzi ni mwingi sana kwenye vipindi vyao.
Can this prevent the humiliation of our grans? Read, digest and understand the post well before commenting.
Mimi sio mtazamaji mzuri wa Clouds TV kwa kuwa vipindi vyake vingi ni vya ovyo--havina mvuto wala mafundisho ya maana. Jana, kwa bahati mbaya, nilitazama kipindi cha 'BIBI BOMBA' kinachorushwa na TV hiyo. Nimehudunishwa sana kuona jinsi bibi na mama zetu wanavyodhalilishwa hadharani. Bibi zetu huulizwa maswali ya kidhalilishaji.
Bibi mmoja aliulizwa kama aliwahi kula mboga inayoitwa 'Biology', akajibu 'ndiyo'. Hili ni swali linalohusu ufahamu na kwa wabibi wale ambao hawakwenda shule, hawajui biology ni nini. Si hivyo tu, hata wale walioishia la saba hawajui biology ni kitu gani. Kuwauliza mabibi swali kama hili ni kuwadhalilisha kitaaluma kwa kuwa tu hawakwenda shule.
Bibi mwingine aliombwa amtongoze kijana yule anayewauliza maswali hadi amkubali. Bibi akatekeleza agizo hilo laivu mbele ya skrini ya TV! Huu ni udhalilishaji wa hali ya juu.
Wizara ya jinsia inapaswa kukataza udhalilishaji huu wa kijinsia. Nasi wananchi tuache kushabikia upumbavu huu--tukatae kuwapigia kura bibi wanaoshiriki.
Bibi wa miaka 70 anapofundishwa apozi kama Black American thug na kuambiwa aseme "whatsup ma nigger" na kufanya ndio tangazo la mara kwa mara, huu ni udhalilishaji na ushenzi!!
Clouds TV (Ruge na team yake) mlipoanzisha shindano hili la BIBI BOMBA nilifikiri wanataka kuwatumia bibi hawa kwa ajili ya kutukuza uTanzania wetu, utamaduni wetu na mchango wao ili kufanya vijana wafahamu utamaduni wetu ambao unaanza kusahaulika katika jamii. Lakini tunachokishuhudia hivi sasa ni kinyume chake. Ni udhalilishaji usiovumilika wanaofanyiwa bibi na mama zetu. Haingii akilini kumuimbisha bibi wa miaka 65- 70 nyimbo za muziki wa kizazi kipya au kumvalisha suruali wakati tunazo nyimbo zetu za kabila mbalimbali na pia tunafahamu kabisa katika maisha ya kawaida bibi hao hawavai hivyo!
Ruge umekosea sana(wewe ndiye msimamizi wa TV yako kufanya marekebisho. Jipe muda fuaitili shindano hilo uone kama kuna lolote la maana jamiiinajifunza. Badili maramoja; itapendeza na kuleta maana zaidi kama bibi hawa watashidanishwa kwa mambo yenye maadili na kudumisha utamaduni wetu Watanzania
EJL
Niache kuangalia BIBI BOMBA kwa mtonyo Gani?
Siangaliagi tv japo ipo hm
Naenda kublock clouds tv kwenye kingamuzi kwa faida ya familia yangu. Thanx kwa aliyeleta hii habari katusaidia tusioangalia tv.
The mental power by which one controls ones thought,actions and decisions..Do you believe in freedom of the will?