CIA walimuua Bob Marley?

CIA walimuua Bob Marley?

Michael jackson

Ku synthesize kwenye Biological Lab zao virusi vinavyo changanya akili system nzima ya kinga ya mwili (AIDS) a Biological mass destruction weapon!!!

Wanadamu wangapi Duniani wamepoteza maisha kutokana na tatizo hili, wanakwenda kusingizia Sokwe wa Equatorial forest nchini Congo.
 
Ku synthesize kwenye Biological Lab zao virusi vinavyo changanya akili system nzima ya kinga ya mwili (AIDS) a Biological mass destruction weapon!!!

Wanadamu wangapi Duniani wamepoteza maisha kutokana na tatizo hili, wanakwenda kusingizia Sokwe wa Equatorial forest nchini Congo.
Nmekupata mkuu..but what things are u try to justify...???
 
* Raisi wa Chile Salvador Allende.
* Mohammad Mossadegh (IRAN).
* Robert F. Kennedy.
* Maurice Bishop (Grenada).
* Garry Web - US journalist.
* Che Guevara.
* Walter Rodney (Guyana)
Mkuu unaweza kuekezea kidogo kifo cha Walter Rodney kilikuaje na alifia wap mana huyu jamaa nlimsoma kweny world history book kinachohusu mambo ya capitalism
 
Wafuatao ni wahanga wa mauaji yaliyofanywa na CIA
Bob Marley
JF Kennedy
Ernesto che Guevara
Patrice Lumumba
Hugo Chavez

Ongezea unaowajua wengine...
Kanumba
Ngwair
Nyerere
John Walker
Mtoto wa dandu
 
CIA ndio walitekeleza hata naishi ya Martin Luther King kipindi hiko CIA wanajiita KU KLUX KLAN
Upo sahihi mkuu... Special interegensi unit hiyo Ku Klux Klan ilianzishwa na FBI huko USA kwa ajili ya kuwa assassinate front liners Wa black independence movement waliokua wanajalibu kuleta emancipation kwa blacks kuhus haki zao na kujikomboa na utumwa
 
Actually CIA waliua hadi yale mabasi ya JADIDE ya enzi zile, walipomaliza wakaua hadi simbaluwala then wakahamia arachuga na kuua master city

siku hizi CIA wapo pale machinjioni pugu wanaua sana ngombe usiku😱
 
Ukishakula vya wanaume halafu ukawageuka hayo ndo matokea yake. Mengine yote polojo tu.
 
Mkuu unaweza kuekezea kidogo kifo cha Walter Rodney kilikuaje na alifia wap mana huyu jamaa nlimsoma kweny world history book kinachohusu mambo ya capitalism

Alifia kwao Gayana, walitega bom kwenye gari yake likamlipukia na kumuua, Serikali ilidai kwamba yeye ndiye alibeba bom akiwa na lengo la kwenda kulipua gereza kuwachia wafungwa kwa bahati mbaya likamlipukia yeye, huo ulikuwa ni uongo, mtu msomi na mweledi kama Rodney hasingeweza kufanya kitendo cha kijinga kama hicho.

Ukweli wa mambo ni kwamba mpango wa kumumaliza Rodney ulisukwa na CIA. Marekani ilikuwa na wasi wasi na Rodney kutokana na misimamo yake, kumbuka miaka hiyo vita vya baridi kati ya Urusi na nchi za magharibi vilikuwa vimepamba moto, Marekani walifikiri kama jamaa anaweza kuwania kiti cha Urais na akishinda basi nchi yake inaweza kuwakaribisha Warusi/Wacuba wakaweka vituo vyao vya kudumu vya kijeshi, wakaingilia influence ya Wamarekani kwenye backyard yake! Marekani uzichukulia baadhi ya nchi ya Carribean, Amerika kusini kama ni backyard yake.

Kumbuka hata Maurice Bishop aliuwawa kutokana na sababu hizo hizo na nchi yake ya Grenada kuvamiwa na kikosi cha Navy ya Marekani kwa amri ya Reagan.
 
jimmy Hendrix,James Brown waliuwawa ns hao hao
James Brown (soul Brother No. 1) amefariki miaka ya hivi karibuni karne ya 21 muda mrefu tu baada ya kustaafu uimbaji kama ilivyo kwa Barry White. Hivyo kusema Brown aliuawa na "hao hao," inaweza isiwe sahihi. Bob Marley alikuwa mwanamapinduzi na nyimbo zake ziliashiria hilo. Marley alikuwa sauti ya wanyonge wa Carribean na weusi kwa jumla. Vuguvugu lao la "Rastafarian", halikusomeka vizuri katika siasa za miaka hiyo. Mtakumbuka Walter Rodney mwanamapinduzi toka Carribean (Mhadhiri UDSM miaka ya sitini kuingia sabini) mwana-Rastafari kutokana na kuvaa nywele zao, aliuwawa kwa shambulio la bomu huko Guyana baada ya kujihusisha na siasa za huko. Kitabu chake "Jinsi Ulaya Ilivyodumaza Maendeleo ya Afrika", hakikuwavutia wakubwa wa magharibi. Ukiunganisha mzunguko huo wa akina Rodney, Marley na hapo nyuma George Padmore na Marcus Garvey na vuguvugu lao la "Turejee Afrika" unaweza ukakubali ya kwamba Marley aliuawa na wakoloni mambo leo na taasisi kaidi za zama hizo kama CIA kutokana na uanamapinduzi wake na mvuto mkubwa aliokuwa nao kwa vijana wanyonge weusi wa Jamaica na Afrika na Amerika ya Kusini.
 
Wafuatao ni wahanga wa mauaji yaliyofanywa na CIA
Bob Marley
JF Kennedy
Ernesto che Guevara
Patrice Lumumba
Hugo Chavez

Ongezea unaowajua wengine...

Salvador Allende wa Chile alifariki September 11, 1973 akisema "Wananchi wa Chile, nina imani nanyi na mustakabali wa nchi yenu. Ubeberu sasa umeinuka na kufika juu sana. Ni kwa kunishindilia risasi tu ndipo watakapoweza kunizuia nisikamilishe programu niliyopewa na wananchi."
 
amini tu ndo ilivyo! CIA wasikie kwa jirani,kati ya nyimbo zinazoishi na zitaishi siku nyingi zaidi ni nyimbo za reggae(roots)! salute kwako mkuu,leo nakula reggae tu "live concert za bob marley"
Jah don't work for CIA (rats race)
 
Alifia kwao Gayana, walitega bom kwenye gari yake likamlipukia na kumuua, Serikali ilidai kwamba yeye ndiye alibeba bom akiwa na lengo la kwenda kulipua gereza kuwachia wafungwa kwa bahati mbaya likamlipukia yeye, huo ulikuwa ni uongo, mtu msomi na mweledi kama Rodney hasingeweza kufanya kitendo cha kijinga kama hicho.

Ukweli wa mambo ni kwamba mpango wa kumumaliza Rodney ulisukwa na CIA. Marekani ilikuwa na wasi wasi na Rodney kutokana na misimamo yake, kumbuka miaka hiyo vita vya baridi kati ya Urusi na nchi za magharibi vilikuwa vimepamba moto, Marekani walifikiri kama jamaa anaweza kuwania kiti cha Urais na akishinda basi nchi yake inaweza kuwakaribisha Warusi/Wacuba wakaweka vituo vyao vya kudumu vya kijeshi, wakaingilia influence ya Wamarekani kwenye backyard yake! Marekani uzichukulia baadhi ya nchi ya Carribean, Amerika kusini kama ni backyard yake.

Kumbuka hata Maurice Bishop aliuwawa kutokana na sababu hizo hizo na nchi yake ya Grenada kuvamiwa na kikosi cha Navy ya Marekani kwa amri ya Reagan.
umeniumbusha Manuel Noriega, US ilipoivamia Panama na kumkamata
 
Back
Top Bottom