Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

tatizo wengi wenu hamkuelewa logic ya kuwasajili hao wazee
Soma quote ya Gary Nevile hapo chini utaelewa
Siwezi fatilia huyu mpuuzi hata siku moja.
images(1).jpg
 
Wazee wanini!!, mwisho wakazime uwanjani kama Eriksen. Wenzenu wananunua vijana, nyie mnajaza vitoto na wazee. Nasema hivii tutapigwa kama ngoma.
Kwani Thiago Silva tulimsajili kwa umri wa miaka mingapi?
 
Wazee wanini!!, mwisho wakazime uwanjani kama Eriksen. Wenzenu wananunua vijana, nyie mnajaza vitoto na wazee. Nasema hivii tutapigwa kama ngoma.
Kwani tumewasajili wakafie uwanjani. Wale hawakusajiliwa kwa lengo kuu la kucheza. Washauri, waalimu, watia moyo na hamasa na uwepo wao tu unawafanya wadogo wale wakaze msiuli kama wanaume
 
Jude Bellingham kuhusu Henderson majira haya ya kiangazi:

“Wale (waliomcheka kuwa kwenye kikosi) hawajui wanachozungumza.”

“Anawafanya kila mtu acheke, anawaunganisha wote. Ikiwa kuna jambo ambalo wewe kama kijana wa miaka 22 au 23 unaona labda ni kubwa sana kwako kwenda kulishughulikia, yeye atakushughulikia.”

“Kama kuna tatizo kati ya wachezaji wawili, yeye huenda kulitatua na kuwaunganisha. Hana hata chembe ya ubinafsi linapokuja suala la kuisaidia timu. Jana alikuwa anafanya lay‑offs ili sisi tufanye mazoezi ya kumalizia (finishing). Yaani hilo ni jambo gani? Hahitaji kufanya hivyo, ni nahodha aliyeshinda UCL na Premier League.”

Morgan Rogers:“Ndio, ni mtu bora zaidi niliyewahi kukutana naye kwenye soka.”

(England YouTube Channel)

1785431700612.png
 
Kwani tumewasajili wakafie uwanjani. Wale hawakusajiliwa kwa lengo kuu la kucheza. Washauri, waalimu, watia moyo na hamasa na uwepo wao tu unawafanya wadogo wale wakaze msiuli kama wanaume
Naongezea hapo ndio maana wamesajiliwa kama free agent
 
Misha is back
Ahsante Mungu Mudryk wetu sasa anaruhusiwa kucheza, kifungo kimeondolewa
Atasafiri Jumapili kujiunga na wenzake Hong Kong.
-Fabrizio Romano
1785511579397.png
 
Jamie Gittens na Mudryk
Sasa hatuna haja ya kwenda sokoni kusak winga wa kushoto
1785512499822.png
 
🚨 Kesi imefungwa!
Mashitaka yote dhidi ya Chelsea yamefungwa na Premier League pamoja na FA.
💰 Faini jumla: TSh £20.75m.
✅ Marufuku ya usajili wa academy kwa miezi 9.
❌ Hakuna marufuku rasmi ya dirisha la usajili — isipokuwa kama klabu itavunja sheria katika madirisha mawili yajayo.
❌ Hakuna kupunguziwa pointi.

Mudryk karudi
Mashitaka 74 yamefungwa
Chelsea tunabeba FA na EPL msimu ujao
 
Kwani Thiago Silva tulimsajili kwa umri wa miaka mingapi?
Sasa brother unamfananisha Silva na hiyo takataka, ungesema "kwani Tosin tulimsajili akiwa na umri gani" ningekuelewa

Halafu Henderson ni mbovu tokea kijana, sasa sahivi mzee sijui atakua hali gani?

Tutapigwa mpk tuchakae.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom