Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

FIFA bado inamtambua cucurella kama mchezaji wa Chelsea, mana aliingia WC kama mchezaji wa Chelsea.

So Chelsea tuna mchezaji aliyeshinda wc 🔥
 
Hamna kitu hapo. Nimekaa pale
Alipokuwa target a Arsenal mlimremba sana, uzuri wa ushabiki unaanzia hapo, kama siasa tu. Candidate akiwa upande wenu hata kama ni mchafu mtamsafisha sana, akiwakana tu atapakwa matope hata ambayo hana
 
Sio mchezaji wetu huyo minywele mavuu
Ila pesa tumepokea 🤣 .
Marc Cucurella 💇‍♂️pekee ameipatia Chelsea takriban £250,000 kupitia FIFA Club Benefits Programme baada ya kufika fainali na kutwaa Kombe la Dunia 🏆.

Chelsea ilikuwa na wachezaji 11+ kwenye Kombe la Dunia 2026, na klabu ikaingia kwenye Top 6 za vilabu vilivyopokea malipo makubwa kutoka FIFA. Wachezaji waliowakilisha ni:
  1. Marc Cucurella — Spain ilitwaa kombe
  2. Enzo Fernández — alifika fainali
  3. Reece James — alicheza vizuri
  4. Moisés Caicedo — nahodha; alipita makundi
  5. Malo Gusto
  6. Trevoh Chalobah
  7. Kendry Páez
  8. Pedro Neto
  9. Nicolas Jackson
  10. Mamadou Sarr
  11. Mike Penders
  12. Jorrel Hato — walitolewa mapema
Kikosi cha mataifa mbalimbali = pesa ndefu kwa Chelsea.💰

Vilabu vingine vilivyofaidi posho ya FIFA World Cup ni:
  1. Manchester City — £2.62 milioni
  2. PSG — £2.12 milioni
  3. Arsenal — £2.05 milioni
  4. Bayern Munich — £1.96 milioni
  5. Barcelona — £1.87 milioni
  6. Chelsea — £1.80 milioni
1784608470270.png
 
Kuna mpendwa mmoja tulibishana hapa kuwa Behdad Eghbali siye anayehusika na sajili nyingi za Chelsea, na akawa ananibishana. Sana.

Sajili hizi Behdad Eghbali mwenyewe kazisimamia
  1. Enzo Fernández — 2023, Benfica, ~£107m
  2. Mykhailo Mudryk — 2023, Shakhtar Donetsk, ~£88m (pamoja na add‑ons)
  3. Moisés Caicedo — 2023, Brighton, ~£115m
  4. Cole Palmer — 2023, Manchester City, ~£40m + add‑ons
  5. Estevão Willian — 2024/25, Palmeiras, ~£50–60m (muundo wa malipo)
  6. Morgan Rogers — 2026, Aston Villa, rekodi ya klabu £117m
  7. Maxence Lacroix — beki wa Crystal Palace, wanadai ~£60m

1784641632161.png
 
Aston Villa wametuma maombi rasmi ya kumsajili kwa mkopo yenye kipengele cha kumnunua Alejandro Garnacho kwa lazima (Obligatory buy clause)
Mazungumzo bado yanaendelea vizuri

1784643092199.png
 
Kwa maoni yangu binafsi

Baada ya ujio wa Morgan Rogers ningependa Enzo Fernandez auzwe kwasababu nafasi kuu ya Morgan Rogers ni no 10 ingawa Kuna wakati anatumika kama Winga lakini nafasi anayocheza kwa ufanisi ni no 10 kwamaana hiyo kocha atapendelea kupanga no 10 wawili Rogers na Cole Palmer kumbuka kwenye hili eneo amekuwa akitumika Enzo Fernandez zaidi alafu chini huwa anacheza Caicedo na James au muda mwingine Caicedo na Santos au Caicedo na Lavia. Kwa kweli sijawahi kumkubali Enzo akicheza chini kwasababu Hana ile quality ya ukabaji kwahiyo Chelsea inabidi wamuuze alafu nafasi yake anunuliwe mtu mwingine.
 
Kwa maoni yangu binafsi

Baada ya ujio wa Morgan Rogers ningependa Enzo Fernandez auzwe kwasababu nafasi kuu ya Morgan Rogers ni no 10 ingawa Kuna wakati anatumika kama Winga lakini nafasi anayocheza kwa ufanisi ni no 10 kwamaana hiyo kocha atapendelea kupanga no 10 wawili Rogers na Cole Palmer kumbuka kwenye hili eneo amekuwa akitumika Enzo Fernandez zaidi alafu chini huwa anacheza Caicedo na James au muda mwingine Caicedo na Santos au Caicedo na Lavia. Kwa kweli sijawahi kumkubali Enzo akicheza chini kwasababu Hana ile quality ya ukabaji kwahiyo Chelsea inabidi wamuuze alafu nafasi yake anunuliwe mtu mwingine.
Morgan Rogers kasajiliwa kwa ajili ya LW zaidi ila kwa sababu anacheza nafasi zote za mbele anaweza pia kutumika kwenye double no. 10 ambayo Alosno ndio anapendelea zaidi yaani 3-4-2-1
Enzo Fernandez akiuzwa ni vyema zaidi ila hatusukumi bei, watoe pauni 120m
Ila asipouzwa anafit sana kwenye mfum o wa Alonso na ndio maan Alonso kasema angependa kufanya naye kazi
 
Michezaji ya kingereza sijawahigi kuielewa.
Si nuseme tu takataka kama mwenzake, unazugazuga nini. Sisi Chelsea asilia tunasonga mbele maana ninyi kuna siku hata Messi, Ronaldo, Mbape, Haaland nao mtasema ni matakataka
 
Si nuseme tu takataka kama mwenzake, unazugazuga nini. Sisi Chelsea asilia tunasonga mbele maana ninyi kuna siku hata Messi, Ronaldo, Mbape, Haaland nad ane mtasema ni matakataka
Siwezi kusema ni takataka mana simjui kihiivyo, ila kwa michezaji ya kiingereza labda aniprove wrong kama Palmer.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom