Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hivi Shaka kweli anafaa kuja Chelsea au sijamfatilia hivi karibuni?
Anafaa kwa sababu yule hata akizima mtam,bo anaweza kubaki kama kocha msaidizi wa Alonso kwa sababu katika wachezaji Alonso amewafundisha, Xhaka ndiye aliyemshika vizuri. Kule Leverkjusen hakuwa tu mchezaji, alikuwa kocha msaidizi na wale wawili wanaendana kishenzi
 
Sasa huyo alioandika hapo si mtu tu anaamua kuandika, wapi Alonso amesema hivyo?! Alonso anamtaka Xhaka hataki hiyo takataka. Tunaambiwa ana mikimbio mizuri kama twiga.
Atamtakaje mchezaji anayetumikia ban?
 
BREAKING: Maelezo ya Enzo Maresca kuhusu kuachia ngazi Chelsea:

“Uamuzi ulikuwa wangu mwenyewe. Kujiuzulu kwangu Chelsea kuliufungua mlango wa kujiunga na Manchester City, club ambayo tayari niliifahamu vizuri. Nimefurahi sana kujiunga na Manchester City.

Ninatambua kwamba kuondoka kwangu Chelsea katikati ya msimu kulileta changamoto kwenye uendeshaji wa club na naomba radhi kwa hilo. Haikuwa nia yangu wala matakwa yangu.

Nilitendewa mazuri na kila mtu ndani ya Chelsea, na pamoja tulipata mafanikio na kumbukumbu ambazo nitaziheshimu daima.

Ninashukuru club, owners na mashabiki kwa kunipa nafasi hiyo.”
-Enzo Maresca
1782738620142.png
 
Haya mambo bhana 😂

Maressa alivoondoka Kuna kocha Kwenye ligi ya Brazil huko, Chelsea walienda kumu-approach Jamaa akakubali Ila badae akaja kujua kwamba kazi n ya kufundisha Strasbourg Na Sio Chelsea 😂

So jamaa akakataa kazi, na timu yake ilipojua hilo, wakamfukuza kazi

Hii ishu imewatokea Chelsea, afu Wanaanza kulialia 😂
 
BREAKING: Maelezo ya Enzo Maresca kuhusu kuachia ngazi Chelsea:

“Uamuzi ulikuwa wangu mwenyewe. Kujiuzulu kwangu Chelsea kuliufungua mlango wa kujiunga na Manchester City, club ambayo tayari niliifahamu vizuri. Nimefurahi sana kujiunga na Manchester City.

Ninatambua kwamba kuondoka kwangu Chelsea katikati ya msimu kulileta changamoto kwenye uendeshaji wa club na naomba radhi kwa hilo. Haikuwa nia yangu wala matakwa yangu.

Nilitendewa mazuri na kila mtu ndani ya Chelsea, na pamoja tulipata mafanikio na kumbukumbu ambazo nitaziheshimu daima.

Ninashukuru club, owners na mashabiki kwa kunipa nafasi hiyo.”
-Enzo Maresca
View attachment 3618394
Naona nao Man City wametoa tamko la kuomba radhi. Nadhani hii ni mpango mojawapo ya Chelsea pamoja na faini kuwataka watamke public makosa yao ili Mashabiki waache kuilaumu management kwamba ilimfukuza Enzo marseca

TAMKO
"Enzo Maresca amekuwa akichukuliwa na klabu kwa muda mrefu kama mlengwa katika mpango wetu wa kupokezana ukocha. Kama kocha wa zamani aliyefanikiwa ndani ya mfumo wetu, Enzo ana uhusiano mzuri na uongozi wa Klabu na anaelewa jinsi tunavyofanya kazi na kuendelea kukua.
"Tunaweza kuthibitisha kwamba mazungumzo ya siri yalifanyika kati ya wawakilishi waliochaguliwa wa City na Enzo Maresca katika msimu wa vuli na baridi wa mwaka 2025, wakati akiwa Kocha Mkuu wa Chelsea FC, kuhusu uwezekano wa yeye kurejea City katika nafasi ya kocha wa mpito wa uongozi iwapo Pep Guardiola angeamua kuondoka.
"Tunatambua taarifa ya Chelsea kuhusu muktadha wa kuondoka kwa Enzo kutoka Chelsea. Pia tunatambua muktadha ambao ruhusa ya mazungumzo ilitolewa, na tunatambua kuwa kuondoka kwake katikati ya msimu kulileta usumbufu katika msimu wa Chelsea."
-Man City
 
Haya mambo bhana 😂

Maressa alivoondoka Kuna kocha Kwenye ligi ya Brazil huko, Chelsea walienda kumu-approach Jamaa akakubali Ila badae akaja kujua kwamba kazi n ya kufundisha Strasbourg Na Sio Chelsea 😂

So jamaa akakataa kazi, na timu yake ilipojua hilo, wakamfukuza kazi

Hii ishu imewatokea Chelsea, afu Wanaanza kulialia 😂
Ila kumbuka kwa wakati ule management ilishambuliwa na kila mtu na morali ya team ilishuka na tangu hapo anguko la team ikawa kubwa in short Maresca ameleta madhara makubwa we imagine unaingia mkataba wa Siri na team nyingine huku unafundisha team nyingine tena ni kubwa shindani hiyo inatoa tafsiri gani?
 
Ila kumbuka kwa wakati ule management ilishambuliwa na kila mtu na morali wa team ilishuka na tangu hapo anguko la team ikawa kubwa in short Maresca ameleta madhara makubwa we imagine unaingia mkataba wa Siri na team nyingine huku unafundisha team nyingine tena ni kubwa hiyo inatoa tafsiri gani?
Yah Maressa alizngua parefu
 
TANGAZO RASMI LA KLABU YA CHELSEA KUHUSU ENZO MARESCA

“Klabu ya Chelsea inatambua kwamba msimu wa 2025/26 ulikuwa wa huzuni kubwa mno kwa Klabu na wapenzi wake wote. Sababu kuu ilikuwa machafuko makubwa yaliyotokana na mabadiliko ambayo Klabu ililazimika kufanya katika nafasi ya Head Coach wakati wa Krismasi.”

“Kutokana na mambo mapya yaliyojitokeza, tunaona ni muhimu kuwafafanulia wapenzi wetu yaliyotokea na kwa nini former Head Coach wetu aliondoka Klabuni tarehe 1 Januari 2026.”

“Mwaka jana katika vuli, Klabu iliarifiwa na former Head Coach wetu kwamba kunaweza kuwa na opportunity kwake kurithi nafasi ya Pep Guardiola mwishoni mwa season.”

“Ilikuwa wazi kwetu kwamba moyo wake ulikuwa umeegemea sana kutaka succeed Guardiola, na alikuwa amejitolea kabisa kufuata hiyo opportunity, ijapokuwa alikuwa chini ya mkataba wa muda mrefu ambao hakuwa na haki ya kuivunja.”

“Mwishoni mwa mwezi wa Desemba 2025, kocha mkuu wetu alijiuzulu ghafla na bila kutarajiwa. Tulihisi kuachwa, kwani ilikuwa dhahiri kuwa moyo na akili yake vilikuwa vimeelekea klabu nyingine na fursa nyingine, licha ya kuwa alikuwa amefika Chelsea mwaka mmoja tu uliopita.”

“Hakuna klabu inayotaka kubadilisha Head Coach wake katikati ya msimu. Hata hivyo, kwa kuzingatia uamuzi wake wa kutotimiza majukumu yake hadi mwisho wa msimu, Klabu haikuwa na njia nyingine ila kulinda wachezaji wetu, wapenzi wetu, na Beji yetu, na kukubali resignation yake.”

“Katika hali hii na kwa heshima ya pande zote kati ya maklabu, confidential settlement imefikiwa na Manchester City, ambayo inajumuisha payment ya compensation. Confidential settlement pia imefikiwa na kocha wa zamani, ambapo yeye atalipa compensation.”

1782760708035.png
 
Ila kumbuka kwa wakati ule management ilishambuliwa na kila mtu na morali wa team ilishuka na tangu hapo anguko la team ikawa kubwa in short Maresca ameleta madhara makubwa we imagine unaingia mkataba wa Siri na team nyingine huku unafundisha team nyingine tena ni kubwa hiyo inatoa tafsiri gani?
Yaani hata mim i sasa namuona Maresca kama ni Coward mkubwa kwenye midani ya kocha kuwahi kutokea duniani. Hata hiyo mil 20 haiwezi kufidia madhara aliyotuachia. Kaivuruga dressing room na kutugawa masdhabiki wengine tumekazana kulaumu wamiliki na SDs kumbe mchawi mkubwa ni Maresca. Amefanya hata mafanikio aliyoyapata msimu wake wa kwanza uonekane sifuri. Atazomewa sana kila akija Darajani. PUMBAFU SANA HUYO.
Namuombea hata asifanikiwe City afukuzwe mwaka wake wa kwanza haujaisha
 
Yaani hata mim i sasa namuona Maresca kama ni Coward mkubwa kwenye midani ya kocha kuwahi kutokea duniani. Hata hiyo mil 20 haiwezi kufidia madhara aliyotuachia. Kaivuruga dressing room na kutugawa masdhabiki wengine tumekazana kulaumu wamiliki na SDs kumbe mchawi mkubwa ni Maresca. Amefanya hata mafanikio aliyoyapata msimu wake wa kwanza uonekane sifuri. Atazomewa sana kila akija Darajani. PUMBAFU SANA HUYO.
Namuombea hata asifanikiwe City afukuzwe mwaka wake wa kwanza haujaisha
Tafsiri yake ni kwamba Enzo Maresca ni muhujumu team sijawahi kuona ujinga wa namna unafanywa na mzungu kwa kweli yaani alikuwa anafundisha lakini akili yake haipo Chelsea Tena ni team shindani na Man City si Bora ingekuwa huu ujinga kafanya kwa team zinazocheza ligi tofauti ingepunguza machungu
 
Tafsiri yake ni kwamba Enzo Maresca ni muhujumu team sijawahi kuona ujinga wa namna unafanywa na mzungu kwa kweli yaani alikuwa anafundisha lakini akili yake haipo Chelsea Tena ni team shindani na Man City si Bora ingekuwa huu ujinga kafanya kwa team zinazocheza ligi tofauti ingepunguza machungu
Unakumbuka Lopegui akiwa Kocha wa Spain huku anaingia mkataba wa Siri na Real Madrid wakati huohuo team ipo kwenye Mashindano ya kumbe la Dunia Russia.
Aliishia kufukuzwa Spain National Team na Madrid hakunaliza miezi mitano.

Enzo amejipatia mkosi kama Mbabe.
 
Real Madrid wakanusha kutaka kumsajili Enzo Fernández

TAARIFA RASMI – 03/07/2026

Kufuatia taarifa na madai yaliyotokea katika siku za hivi karibuni kuhusu tetesi za kwamba Real Madrid C.F. ina nia ya kumsajili mchezaji Enzo Fernández, klabu inapenda kufafanua kwamba haijafanya mawasiliano yoyote, iwe ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja, yanayolenga usajili wa mchezaji huyo, na pia haina mpango wowote wa kuanzisha operesheni hiyo.

Real Madrid inapenda kuonyesha heshima yake ya juu kwa Enzo Fernández, mchezaji bora ambaye ubora na historia yake vinajulikana wazi, pamoja na Chelsea FC, klabu ambayo Real Madrid ina uhusiano mzuri wa kitaasisi.

Kwa sababu ya heshima inayostahili taasisi kama Chelsea FC, na kwa misingi ya uaminifu wa kitaasisi ambao daima umeongoza utendaji wa Real Madrid, klabu inaona ni muhimu kukanusha kikamilifu uvumi usio na msingi na usioendana na ukweli.

Real Madrid inasikitika kwamba, licha ya ukweli kuwa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na klabu, bado zinaendelea kusambazwa taarifa zisizo sahihi ambazo zinachanganya mashabiki na kuleta madhara yasiyo ya lazima kwa taasisi na watu wanaohusika.

1783101571568.png
 
Viongozi wetu huwa Wanashida sana wanashindwa kutoa pound 20m alafu wanakuja kusajili kinda zaidi ya hiyo hela
Mwaka huu kinda wamesajiliwa kwa ajili ya academy. Huko nyuma walisajili hovyo na wamejifunza kwa maoni yangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom