Yaani sisi tumegeuka kula makapi ya Chelsea ili tuwanie top 4 kama Arsenal ya Unai
Yaani sisi tumewapa Havertz na Madueke wabebe ubingwa; sisi tumchukue kapi Granit Xhaka ili tujitutumue kuingia top 4 kweli. Dunia mviringo.
Namuheshimu sana Xhaka, ameiwezesha Levakusen kushinda kombe la Ujerumani mbele ya timu kubwa kama Bayern Munich na pia kuikokota Sunderland hadi michuano ya Ulaya katika uzee ule.
Ila wanachelsea tusifurahie sana, septemba jamaa anaingia 34 na mabosi wanataka kumpa mkataba wa miaka mitatu, yaani tutakuwa nae akiwa na miaka 34, 35 hadi 36.
Wakifanya hivyo wasimpe mshahara mkubwa ili tukitaka kumuuza Ligi ua Marekani au Saudi tusihangaike.
Nitiba ya muda mfupi, yeye akicheza na Caicedo atampa uhuru wa kuroam kwenye box kwa sababu Xhaka ni DM aliyetulia