Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mimi huwa nikiwambia hapa tuna wachezaji wenye quality ndogo sana aka MATAKATAKA. Kuna baadhi ya matakataka hapa jukuani huwa wanakataa tena wanaenda mbali na kuanza kuwatetea. Hivi huwa mnabisha nini sasa, yaani mnabishana na ukweli.!?

Klabu kama Chelsea washindani wake ni hizo klabu zinazo fanya vizuri kwenye ligi mbalimbali, lakini cha ajabu klabu inasajili wachezaji wa hovyo hovyo tu. Tuna lundo kubwa la matakataka kuanzia kocha.
Tunakujua mzee wa matakataka na leo tunaheshimu maoni yako.
Ila shida yako ni moja tu, siku timu inacheza vizur hadi kubeba makombe unapotea!
 
Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.

Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.

Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.

Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.

Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza​

1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.

2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
  • CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
  • Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
  • Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
  • CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
  • Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.
 
Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.

Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.

Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.

Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.

Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza​

1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.

2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
  • CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
  • Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
  • Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
  • CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
  • Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.
Wamarekani ni matapeli hutaona wakimleta kocha mkubwa kaliba ya akina Mourinho au Conte maana hawataki kuheshimu professional na maamuzi ya makocha chini ya uongozi wao.

Kiufupi Chelsea tumepigwa sana kukubali wadhamini wawe Wamarekani.
 
Mashabiki wa Arsenal washenzi sana 😭
Leo wakishinda:
“Asante Chelsea kwa Kai Havertz 🙏💙”
“Asante Chelsea kwa Kepa 🙏😂”
“Asante Chelsea kwa Noni Madueke 🙏🤣”

Kesho wakifungwa:
“F*** you Chelsea 😡🤬”

Arsenal 0- 2 Man City Finali ya EFL, Carabao Cup
 
Liam Rosenior si kocha wa kiwango cha Chelsea, lakini kumfukuza pekee yake hakutatatua chanzo cha matatizo makubwa ndani ya klabu. Tatizo letu la msingi lipo kwenye mfumo wa mradi (project model) pamoja na sera na falsafa zinazouendesha, hasa namna tunavyosajili wachezaji na namna tunavyowaajiri makocha.

Kwa sasa tunasajili wachezaji wadogo sana badala ya kuchanganya na wachezaji wenye uzoefu, na tunawaajiri makocha wachanga badala ya makocha waliothibitishwa na wenye njaa ya mataji. Huu ni mzunguko wa hatari.

Hata kama uongozi ukiamua leo kumfukuza Rosenior kwa sababu mambo hayaendi vizuri, bado watamleta kocha mwingine mbichi, asiye na uzoefu wa kushughulika na kikosi ambacho chenyewe ni wabichi—kina Gittens, Garnacho, Estevão, Mamadou Sarr na wengine wa umri mdogo.
Matokeo yake tutakuwa tunaongeza vurugu juu ya mfumo tayari uliojaa vurugu.

Kwa kifupi:
Tatizo si Rosenior peke yake; tatizo ni mfumo mzima unaotengeneza mazingira ya kushindwa.

1774302619076.png
 
Makenge yakipigwa yanakuwa kimya, yanakimbilia mapangoni huko, hata kichwa nje hayatoi
 
Mnavyoelekea hata conference league next season hamtacheza.......

Waangalie spurs, wanashuka daraja kizembe sana !
 
Enzo na kauli zake recently inaonekana anawatema, mchezaji ana potential, anaona project mbovu haieeleweki bora asepe zake

"We will see after world Cup" , hii kauli ni nzito sana !
 
Enzo na kauli zake recently inaonekana anawatema, mchezaji ana potential, anaona project mbovu haieeleweki bora asepe zake

"We will see after world Cup" , hii kauli ni nzito sana !
Coutinho alipoondoka Liverpool → timu ikawa moto 🔥⚽
Hazard alipoondoka Chelsea → tukabeba UCL 🏆💙
Arsenal na Man United wakiondoka mchezaji mzuri → timu inadidimia 📉😭
 
Coutinho alipoondoka Liverpool → timu ikawa moto 🔥⚽
Hazard alipoondoka Chelsea → tukabeba UCL 🏆💙
Arsenal na Man United wakiondoka mchezaji mzuri → timu inadidimia 📉😭
Wacha tuone, sio kwa Chelsea hii inayo_dema dema !!!!! Enzo ni uti wa mgongo wa project yenu
 
Huko nyuma niliwahi kusema, huu mradi usipoleta matund amazuri ndani ya muda mfupi, wachezaji muhimu watataka kutoka na italeta impact mabaya sana kwenye performance kwa sababu utakuwa na wachezaji muhimu ambao wako demotivated.
Enzo Fernandez na Cole Palmer wanataka kutoka kwenye mradi. Low form ya Palmer nilikuwa na wasiwasi nayo ni kama hataki tena kuichezea Chelsea.
Sas aukichanganay na Chelsea kukosa UCl msimu ujao, dirisha la kiangazi itakuwa na patashika kubwa, tusubiri tuone
 
Enzo Fernández alipoulizwa ni mji gani anaoupenda zaidi, alijibu:

“Napenda mji wa Madrid; unafanana na Buenos Aires.”
Kutaka kuondoka ni jambo linaloonyesha wazi ukweli kwamba wazo la huu mradi lilikuwa uongo tangu mwanzo. Eti wachezaji wachanga watabaki pamoja kwa muda mrefu na kuunda timu itakayotawala Ligi ya Uingereza na Klabu Bingwa Ulaya kwa miaka ming, hilo lilikuwa ndoto tu.

Sasa Enzo Fernández, jiwe kuu la huu mradi, akiwa na miaka 25—umri ambao alitarajiwa kuchangia zaidi katika kuisaidia timu kushinda makombe—ndiye kwanza anayetaka kuondoka.

1774842693276.png
 
Enzo Fernández alipoulizwa ni mji gani anaoupenda zaidi, alijibu:

“Napenda mji wa Madrid; unafanana na Buenos Aires.”
Kutaka kuondoka ni jambo linaloonyesha wazi ukweli kwamba wazo la huu mradi lilikuwa uongo tangu mwanzo. Eti wachezaji wachanga watabaki pamoja kwa muda mrefu na kuunda timu itakayotawala Ligi ya Uingereza na Klabu Bingwa Ulaya kwa miaka ming, hilo lilikuwa ndoto tu.

Sasa Enzo Fernández, jiwe kuu la huu mradi, akiwa na miaka 25—umri ambao alitarajiwa kuchangia zaidi katika kuisaidia timu kushinda makombe—ndiye kwanza anayetaka kuondoka.

View attachment 3564370
Kwa kweli ninathamini kile ambacho Enzo Fernández anafanya kwa kufichua uozo na panya waliokuwa wakijificha nyuma ya huu mradi wa Chelsea. Wamiliki bado wanaamini mambo yanaenda vizuri, ilhali kila kitu kinaporomoka huku wao wakijifanya hawalioni. Kwa dhati kabisa, naamini siku moja Cole Palmer naye atapata njia ya kujitoa kwenye huu mradi wa ajabuajabu, ili hatimaye wamiliki watambue ni kwa kiasi gani waliharibu mambo kwa kulazimisha mkakati wa kuajiri watoto na makocha wasio na uzoefu.
 
Cucurela nae anasema anatamani one day arudi la liga, hakuna asiyejua huyu ni mwana-catalan,......

Enzo anakuambia ataman sana akaishi jiji la Madrid!

Waja wa laana nyie, wachezaji wote muhimu watasepa , hizi interview haziji kwa bahati mbaya, ni planned!!!!

Sio mbaya mtabakia na kina hato, gittens, garnacho , delap kupambania badge!!!!!

Project la mchongo.... mmeingia cha kike kwa wamarekani, kocha Rose bado yupo yupo sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom