Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Tatizo la safarti hii sio la mchezaji mmoja mmoja
Kocha kapoteza dressing room kabisa, kila mchjezaji anacheza hovyo kuanzia Kipa hadi striker sipokuwa Estevao tu alipoingia angalau alionyesha nia ya kufungia Chelsea magoli
Unaona kabisa wachezajo wote hawana morale, wanamgomea kocha au uongozi
Sawa ila bado Lavia n tapeli kitu ambacho nilikuwa mnakataa.
Of course estevao alivyoingia alionyesha kujaribu kufanya jambo tofauti na hao matapeli waliocheza dkk 90
 
Mimi huwa nikiwambia hapa tuna wachezaji wenye quality ndogo sana aka MATAKATAKA. Kuna baadhi ya matakataka hapa jukuani huwa wanakataa tena wanaenda mbali na kuanza kuwatetea. Hivi huwa mnabisha nini sasa, yaani mnabishana na ukweli.!?

Klabu kama Chelsea washindani wake ni hizo klabu zinazo fanya vizuri kwenye ligi mbalimbali, lakini cha ajabu klabu inasajili wachezaji wa hovyo hovyo tu. Tuna lundo kubwa la matakataka kuanzia kocha.
 
Aisee, sema fixtures ya Chelsea imekaa kibabe Sana... Kwa form hii mechi Saba zijazo ni za Moto Sana..
 
Tapeli wakuu kwenye hii project ni hao directors wengine wote ni sub set ya matatizo
Wawekezaji wamekuja na akili zao za kuendesha club ya mpira kama duka la mangi.
Wakaajiri wakurugenzi ambao wao ndio walitakiwa kuwaambia namna uwekezaji wa mpira unatakiwa kua kwa sababu wao ndio wanajua mpira na parameters zake
kama unaona mwajiri anamalengo yakinadharia pekee si walitakiwa kuwaambia ukweli wakishikilia msimamo wao wajiuzulu
Sasa kama wako ofisini inamaana hii standard ya timu wameridhika nayo na wanaiaminisha board kwamba project ipo kwenye right track

Ndio maana sasa hivi hata suala la kufukuza kocha kwa hawa directors wa level za Brighton wanaweza kumleta hata kocha wa Brentford kisa kafanya vyema kwenye long ball
 
Mimi huwa nikiwambia hapa tuna wachezaji wenye quality ndogo sana aka MATAKATAKA. Kuna baadhi ya matakataka hapa jukuani huwa wanakataa tena wanaenda mbali na kuanza kuwatetea. Hivi huwa mnabisha nini sasa, yaani mnabishana na ukweli.!?

Klabu kama Chelsea washindani wake ni hizo klabu zinazo fanya vizuri kwenye ligi mbalimbali, lakini cha ajabu klabu inasajili wachezaji wa hovyo hovyo tu. Tuna lundo kubwa la matakataka kuanzia kocha.
Tunakujua mzee wa matakataka na leo tunaheshimu maoni yako.
Ila shida yako ni moja tu, siku timu inacheza vizur hadi kubeba makombe unapotea!
 
Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.

Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.

Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.

Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.

Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza​

1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.

2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
  • CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
  • Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
  • Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
  • CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
  • Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.
 
Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.

Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.

Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.

Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.

Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza​

1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.

2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
  • CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
  • Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
  • Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
  • CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
  • Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.
Wamarekani ni matapeli hutaona wakimleta kocha mkubwa kaliba ya akina Mourinho au Conte maana hawataki kuheshimu professional na maamuzi ya makocha chini ya uongozi wao.

Kiufupi Chelsea tumepigwa sana kukubali wadhamini wawe Wamarekani.
 
Mashabiki wa Arsenal washenzi sana 😭
Leo wakishinda:
“Asante Chelsea kwa Kai Havertz 🙏💙”
“Asante Chelsea kwa Kepa 🙏😂”
“Asante Chelsea kwa Noni Madueke 🙏🤣”

Kesho wakifungwa:
“F*** you Chelsea 😡🤬”

Arsenal 0- 2 Man City Finali ya EFL, Carabao Cup
 
Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.

Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.

Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.

Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.

Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza​

1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.

2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
  • CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
  • Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
  • Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
  • CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
  • Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.
Wajifunze kuuza hisa zao. Wakae pembeni.
 
Liam Rosenior si kocha wa kiwango cha Chelsea, lakini kumfukuza pekee yake hakutatatua chanzo cha matatizo makubwa ndani ya klabu. Tatizo letu la msingi lipo kwenye mfumo wa mradi (project model) pamoja na sera na falsafa zinazouendesha, hasa namna tunavyosajili wachezaji na namna tunavyowaajiri makocha.

Kwa sasa tunasajili wachezaji wadogo sana badala ya kuchanganya na wachezaji wenye uzoefu, na tunawaajiri makocha wachanga badala ya makocha waliothibitishwa na wenye njaa ya mataji. Huu ni mzunguko wa hatari.

Hata kama uongozi ukiamua leo kumfukuza Rosenior kwa sababu mambo hayaendi vizuri, bado watamleta kocha mwingine mbichi, asiye na uzoefu wa kushughulika na kikosi ambacho chenyewe ni wabichi—kina Gittens, Garnacho, Estevão, Mamadou Sarr na wengine wa umri mdogo.
Matokeo yake tutakuwa tunaongeza vurugu juu ya mfumo tayari uliojaa vurugu.

Kwa kifupi:
Tatizo si Rosenior peke yake; tatizo ni mfumo mzima unaotengeneza mazingira ya kushindwa.

1774302619076.png
 
Makenge yakipigwa yanakuwa kimya, yanakimbilia mapangoni huko, hata kichwa nje hayatoi
 
Mnavyoelekea hata conference league next season hamtacheza.......

Waangalie spurs, wanashuka daraja kizembe sana !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom