Nilichokiona kwenye mechi ya jana, pamoja na kauli ya Enzo Fernández kwenye ile interview, kinaonyesha wazi kuwa wachezaji wa Chelsea wamechukizwa sana na kufukuzwa kwa Enzo Maresca. Sio kwamba Maresca alikuwa kocha bora kupindukia, bali walikuwa tayari wameshazoea mfumo wake—ghafla akafukuzwa katikati ya msimu. Hilo limeporomoa kabisa morali ya wachezaji.
Rosenior si kocha mbaya, lakini mbinu zake ni tofauti kabisa na zile za Maresca. Kwa sasa ni kama wachezaji wamerudishwa
square one kujifunza upya. Mechi zilizobaki zitakuwa kama pre-season kwao; hakuna UCL, hakuna Europa, wala Conference League. Kwa kifupi, msimu wa Chelsea umeisha.
Kwa upande wangu, ninafurahia kwa sababu angalau wamiliki watakuwa wamepokea ujumbe kwamba mbinu zao na “project model” yao imefeli. Wanapaswa kufanya marekebisho makubwa.
Kukosa UCL kutaiingizia Chelsea hasara kubwa—zaidi ya milioni 400 kama ilivyotokea msimu uliopita. Pia kutashusha morali ya wachezaji wakubwa, na wengi wao watataka kuhama. Hata wale watakaobaki, kiwango chao kinaweza kushuka kwa sababu ya kukosa malengo makubwa.
Mambo Wamiliki Wanapaswa Kujifunza
1) Kuheshimu mwendelezo wa timu
Hata kama kuna tofauti binafsi na kocha, kama anatoa matokeo na timu inacheza vizuri, avumiliwe. Maamuzi ya mihemko ya kufukuza makocha katikati ya msimu yameharibu kila kitu.
2) Usajili uwe wa kimkakati, sio wa majaribio
Chelsea inahitaji:
- CB mmoja au wawili wazoefu wenye ubora wa juu
- Winga wenye uwezo wa kubadili mchezo
- Striker wa kiwango cha Igor Thiago au zaidi
- CM mkabaji wa kuweka balance kwenye midfield
- Na mwisho, kuwauza wachezaji wanaotaka kuondoka Chelsea
Mashabiki wenzangu, kilichobaki sasa ni kuangalia kama usajili wa dirisha lijalo unaweza kutufuta machozi.