Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Quantity ✅️
Quality ❎️
Makocha wanaweza kweli kuwa average but tuna lundo la wachezaji below average. Refer timu ya kipindi cha kwanza na cha pili
Hivi bodi ya usajili inafanya vetting ya kutosha au ni maelekezo tu toka kwa wafanyabiashara "Todd Boehly na alliances*???
 
Mzee wa takataka, tatizo matokeo yakiwa kama leo hivi ni kama haupendezwi maana hauji kabisa kuchangia ila matokeo yakiwa kama yalivyokuwa halftime vile ni kama ndo furaha yako nashindwa kuelewa kama ni shabiki kweli wa chama letu pendwa ze blues au huwa unacomment nyakati ambazo una hasira tu ndo maana sijawahi kuona compliment hata kwa bahati mbaya
50% hatuna wachezaji bora kama enzi za akina Michael Ballack, Didie Drogber, pia mabeki ni ronyoronyo sana, 2 matches timu inaruhusu magoli mawili tena first half?

Ukikutana na timu yenye ukuta kama Arse8 ndiyo basi tena.
 
Walikuwa active kipindi cha kwanza wakati Westham A inacheza na Westham B
Sasa wanaume Chelsea FC imeingia kucheza na Westham A na comeback ya kiume wamepotea, hapo ndio mimi nawashngaa sana. Ndio maan nina wasiwasi kama wote humu tunaosema Chelsea Chelsea kama ni wafuasi wa Chelsea kweli
Kwa maana walioitwa ni wengi bali wateule ni wachache
- Mathayo 22:14
- Mathayo 7:21
Bado everage players ni zaidi ya 50%-60% wanaotufanya tuonekane wasaliti. Kuruhusu magoli mawili kwa Napoli na Westharm Utd ni upumbavu utaotugharimu sana baadaye.
 
Ukizungumzia kimbinu Enzo Maresca amemzidi Liam Rosenior but alichowin kocha huyu mpya nikawajengea Chelsea mentality ya ushindi kwa kuwajaza upepo kitu ambacho Maresca amefeli aliweza tu tukikutana dhidi ya team kubwa pekee, pili kocha hajataka kupaka rangi nyingi nyingi amewataka wachezaji Wajikite kwenye basic za mpira, kuongeza intensity ya game, kucheza direct football hakutaka kubadilisha kwa kiasi kikubwa
Mapema bado kutoa tathmini, angalau tuangalie kwa mechi 8-10 atazocheza nazo Rosenior, isijekuwa ni nguvu za soda wachezaji wanapambania kupata no kwa kocha mpya baada ya hapo tunarudi kule kule utumwani Misri...
 
Kulikuwa na wakati ambapo uongozi wa Chelsea ulitaka kumsajili Adama Traoré wakati alipokuwa akiichezea Wolverhampton Wanderers.
Kwa uhalisia, yeye si mchezaji wa mpira wa miguu bali ni mchezaji wa rugby au mwanamieleka vile.

 
Si bado mechi moja anafikisha mechi nane
Rosenior bado anapata matokeo, lakini kiwango cha uchezaji hakiridhishi. Nilisema huko nyuma na narudia tena.

Huenda wachezaji bado hawajamuelewa kikamilifu.
Huenda pia safu ya ulinzi inamuangusha.
Huenda pia kushuka kwa ubora wa Caicedo, Palmer, James kunamuathiri sana — hawa wachezaji hawako kwenye viwango vyao. Hata Pedro Neto hayupo kwenye ubora wake tena. Hata Cucurella kabla ya mechi ya jana alikuwa hachezi vizuri ila jana alipotokea benchi ndipo aliingia na moto.

Hata wachezaji wachanga kama Garnacho, Gittens, Delap na Hato waliokuwa wanaonyesha kuimarika kipindi cha Enzo maresca, sasa wamepotea. Ni kama wamerudi mwanzo kabisa.

Nampenda Liam Rosenior kama kocha — ni mtu positive, anaongea sana na wachezaji — lakini nimeona udhaifu ambao ukiachwa ukae muda mrefu unaweza kumzuia kufika kiwango cha juu zaidi.

1) Anawaaonea huruma sana wachezaji.
Huwezi kuwaonea huruma wachezaji wasiojituma na kucheza vizuri mara kwa mara kama Disasi, Badiashile na wengineo. Mchezaji akishindwa kucheza vizuri, tupa nje atakuja kukufuzisha kibarua.

2) Hana ile nguvu ya ku-command kama alivyokuwa nayo Enzo Maresca.
Hiyo authority ndiyo iliyomsaidia Maresca kuwafanya hawa vijana wafuate maelekezo yake na kucheza vizuri na kutwaa makombe mawili ya haraka haraka. Rosenior anatakiwa kuweka msimamo: wachezaji wajue anataka nini, na wasipofuata maelekezo, wapigwe benchi hata kama ni wachezaji muhimu.

3) Anakuwa mkarimu kupita kiasi kwenye muda wa kucheza.
Anafanya rotation kubwa kupita kiasi na kuwapa dakika wachezaji ambao hawajastahili. Gittens, Garnacho, Delap na wengine hawapaswi kuanza mechi labda zile za umuhimu mdogo au kucheza dakika 45 hadi wakomae kiakili na kujua kufanya maamuzi sahihi ya kiume wanapokuwa uwanjani.
 
Mapema bado kutoa tathmini, angalau tuangalie kwa mechi 8-10 atazocheza nazo Rosenior, isijekuwa ni nguvu za soda wachezaji wanapambania kupata no kwa kocha mpya baada ya hapo tunarudi kule kule utumwani Misri...
Hata mechi 10 hazitoshi, yule mbeba mizigo Potter alicheza mechi tisa bila kupoteza lakini baada ya kubanguliwa na timu yake ya zamani Brighton 4-1 alipotea kuanzia hapo hadi akafukuzwa. Pamoja na mechi nyingi tunatakiwa kumpima kwenye mechi kubwa na hizi mechi za timu zinazoweka mabasi na makontena nyuma. Akipita vipimo hivyo ndipo tumuite kocha mzuri. Kwa muda Rosenior kaanza kazi ni January, huyu muda mzuri wa kumuasses ni May. Timu ibaki top 4 na iende mbali kwenye UCL (angalau robo fainali) angalau hizo ligi mbili. Sio FA na Carabao cup hizi ligi sio size ya Chelsea kutumia kumpima kocha.
Matokeo ya Graham Potter mechi 10 za kwanza (Alianza kazi Chelsea mwezi Septemba 2022, na mechi zake 9 za kwanza zilichezwa kati ya 14 Septemba 2022 na 25 Oktoba 2022.)
  1. Chelsea 1–1 Salzburg– UCL - 14 September 2022
  2. Crystal Palace 1–2 Chelsea – Premier League
  3. Chelsea 3–0 AC Milan – UCL
  4. Chelsea 3–0 Wolves – Premier League
  5. AC Milan 0–2 Chelsea – UCL
  6. Aston Villa 0–2 Chelsea – Premier League
  7. Brentford 0–0 Chelsea – Premier League
  8. Chelsea 1–1 Man United – Premier League
  9. Salzburg 1–2 Chelsea – UCL - 25 Oktoba 2022.
  10. Brighton 4–1 Chelsea – Premier League
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.
-Fabrizio Romano

1769945628487.png
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.

Chelsea hawakufurahishwa na maneno na nia ovu ya Borussia Dortmund kutaka kumsajili kabisa Aaron kwa kuwa Chelsea inamuona Aaron kama sdehemu ya kudumu ya mradi

-Fabrizio Romano

View attachment 3537500
Hii taarifa ni njema sana kwangu kwani inathhirisha kuwa zile taarifa za mwanzoni kwamba eti Aaron amekataa mpango wa kupelekwa mkopo Strasbourg. Pia hii taarifa ina maan sasa Mamadou Sarr atarudishwa Chelsea ili tuondokane na simanzi ya kumuona Badiashile kila mechi akicheza Ndombolo badala ya kandanda 🤣
1769946244497.png
 
Huu unayama ndio ninaotamani kuuona kwenye ligi sio tu mash8ndano mengine. Inaniuma sana tunakaa m8aka 10 hatujagusa PL. Bado sijaangalia Full Match ya huyu kocha
 
Hii taarifa ni njema sana kwangu kwani inathhirisha kuwa zile taarifa za mwanzoni kwamba eti Aaron amekataa mpango wa kupelekwa mkopo Strasbourg. Pia hii taarifa ina maan sasa Mamadou Sarr atarudishwa Chelsea ili tuondokane na simanzi ya kumuona Badiashile kila mechi akicheza Ndombolo badala ya kandanda 🤣
View attachment 3537503
🚨 Taarifa Maalum: Mamadou Sarr anatarajiwa kufika London Jumatatu hii. Chelsea itavunja mkataba wake wa mkopo na Strasbourg.
Aaron Anselmino ataelekea upande wa pili na atajiunga Strasbourg kwa mkopo.

@RMCsport
 
Tizi la nguvu
Hapo vipi?

 
🚨 Taarifa Maalum: Mamadou Sarr anatarajiwa kufika London Jumatatu hii. Chelsea itavunja mkataba wake wa mkopo na Strasbourg.
Aaron Anselmino ataelekea upande wa pili na atajiunga Strasbourg kwa mkopo.

@RMCsport
Sarr anafanana sana na Badiashile utafikiri ni mdogo wake.
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.
-Fabrizio Romano

View attachment 3537500
Chelsea hawakufurahishwa na mwenendo na nia ovu ya Borussia Dortmund kutaka kumsainisha Aaron Pre Agreement ili ajiunge nao msimu ujao kwa kumsajili kabisa. Chelsea inamuona Aaron kama sdehemu ya kudumu ya mradi na Hayupo kwa mauzo - Not For Sale!
@JacobsBen
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom