Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

palmer acheze winger ya kulia.. garnacho atoke aingie joao pedro na neto aende kushoto.
 
Garnacho vs Wan‑Bissaka

Hato vs Bowen

Gittens vs Souček

Summerville vs Gusto

HT
Chelsea 0–2 West Ham

Tumestahili kuwa nyuma.
Mabadiliko yalikuwa mengi kupita kiasi bila sababu.

Katika mechi zote Garnacho alizocheza Chelsea hii ya leo kacheza hovyo sana hadi inauzi
Jorrel Hato sijui alikuwa anafanya nini?
 
YES na ndio maana mashabiki wengi walitofautiana sana kuhusu usajili wa Garnacho kwa sababu huyo hawezi kabisa kupiga chenga ili kupeleka mipira golini kutokea pembeni. Gittens anaweza ila maamuzi yake bado ya kitoto sana. Sancho pekee ndie aliweza lakini tulimshindwa kwa sababu ya mshahara.
Mtu mwingine aliyekuwa anaweza nu Mudryk kabla hajafungiwa.
Akija Giovani Quenda akaungana na Estevao Willian ngoma itanoga huko kwenye wingers
Badiashile anampasia Hato anapeleka kwa Chaloba anapeleka kwa Sanchez, Sanchez anarudisha kwa Chaloba anampa Hato anapeleka kwa Badiashile anarudisha kwa Sanchez wanaendelea na mzunguko huo huo tena, hata kama tunae Dorku huo mpira unamfikia saa ngapi?!
 
Garnacho vs Wan‑Bissaka

Hato vs Bowen

Gittens vs Souček

Summerville vs Gusto

HT
Chelsea 0–2 West Ham

Tumestahili kuwa nyuma.
Mabadiliko yalikuwa mengi kupita kiasi bila sababu.
Kocha kawaweka benchi james na cucurella kwa pamoja.😂
 
Joao Pedro for Garnacho
Wesley Fofana for Badiashile
Cucurella for Jorrel Hato

Angalau tupumue
 
Kenge kbsa nyie
Pigweni tu hakuna namna afu kipigo kingine kinawasubiri jumanne
 
Garnacho vs Wan‑Bissaka

Hato vs Bowen

Gittens vs Souček

Summerville vs Gusto

HT
Chelsea 0–2 West Ham

Tumestahili kuwa nyuma.
Mabadiliko yalikuwa mengi kupita kiasi bila sababu.

Katika mechi zote Garnacho alizocheza Chelsea hii ya leo kacheza hovyo sana hadi inauzi
Jorrel Hato sijui alikuwa anafanya nini?
Kipindi cha kwanza ilikuwa ni Westham A vs Westham B
Kipindi cha Pili ndio Chelsea vs Westham
FT 3-2
Tunasonga mbele
1769888330145.png
 
Quantity ✅️
Quality ❎️
Makocha wanaweza kweli kuwa average but tuna lundo la wachezaji below average. Refer timu ya kipindi cha kwanza na cha pili
 
Hivi huyu Liam Delap ana tofauti gani na yule mhindi anayeitwa Armando Broja

Nilichokiona kwake leo ni kusukuma na kuwapiga vibega wachezaji wa West Ham. Hakukuwa na chochote zaidi. Striker asiye na faida.

1769889291806.png
 
Quantity ✅️
Quality ❎️
Makocha wanaweza kweli kuwa average but tuna lundo la wachezaji below average. Refer timu ya kipindi cha kwanza na cha pili
Hawa wachezaji sio, na hawatakuwa, wachezaji wa kuanza kwenye timu ya Chelsea angalau ndani ya misimu miwili. Liam Rosenior anatakiwa kuelewa hilo. Wote hawa wanapaswa kuingia kutokea benchi pale ambapo tumeshaua mchezo tayari.
  1. - Alejandro Garnacho
  2. - Jamie Bynoe‑Gittens
  3. - Jorrel Hato
  4. - Liam Delap
  5. - Benoît Badiashile
  6. - Malo Gusto - msimu huu amekuwa wa hovyo sana
  7. - Marc Guiu
  8. - Josh Acheampong
  9. - Tyrique George
 
Hivi huyu Liam Delap ana tofauti gani na yule mhindi anayeitwa Armando Broja

Nilichokiona kwake leo ni kusukuma na kuwapiga vibega wachezaji wa West Ham. Hakukuwa na chochote zaidi. Striker asiye na faida.

View attachment 3537131
Jackson angekuwa muingeleza au hispania angeimbwa sana, huyu delap hafiki hata nusu ya ubovu wa Jackson
 
Jackson angekuwa muingeleza au hispania angeimbwa sana, huyu delap hafiki hata nusu ya ubovu wa Jackson
Delap hamsogelei hata kidole kimoja cha Nicolous Jackson. Jackson akishindwa kukupa magoli anacheza anasumbua defence anatengeneza nafasi kwa wengine. Ila huyu, kinachomuweka Chelsea ni Uingereza wake tu na sasa tuna kocha Muingereza ndio basi tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom