📰🎙️ MKUTANO WA WANAHABARI | Liam Rosenior (Kabla ya Mechi na Arsenal)
Mwandishi: Liam, tayari una kikosi chako cha kwanza?
Rosenior: Hapana. Sijawahi kuwa nacho. Kwa sababu ya mahitaji ya kimwili—Premier League, Ligue 1, Champion League—unahitaji kikosi kipana na kukitumia ipasavyo msimu mzima. Nimekuwa hapa wiki chache tu, bado najifunza kundi hili. Nachagua kikosi sahihi cha kuanza, na pia nachagua kikosi sahihi cha kumaliza mchezo.
Mwandishi: Wachezaji wa akiba wanaendelea kubadilisha mechi, ni ubora wa kiufundi?
Rosenior: Daima kuna kipengele cha kiufundi, lakini sehemu kubwa ni hali ya kisaikolojia. Wachezaji wanaoingia wamekuwa na athari kwenye kila mchezo kwa sababu wanaingia kusaidia timu, si kujilinda wao binafsi.
Mwandishi: Habari za Estevão?
Rosenior: Anapitia kipindi kigumu sana binafsi. Sitamwekea presha. Lazima mambo yawe sahihi kwake kwanza.
Mwandishi: Arsenal ndiyo wanaopewa nafasi. Unaweka vipi muktadha wa mchezo huu?
Rosenior: Huo ndiyo ukweli. Wako mbele kwa bao moja na wako nyumbani, kwa hiyo wanatarajia kusonga mbele. Sisi tunapaswa kuusukuma mchezo mbali kadiri tuwezavyo, tuufikishe mbali, halafu tufanye kipindi cha pili kuwa kikubwa na kujaribu kuugeuza.
Mwandishi: Jamie Gittens?
Rosenior: Alisikia maumivu kwenye msuli wa nyuma ya paja. Sijui ukubwa wa tatizo bado. Ni bahati mbaya sana kwa sababu nilitaka aanze na aonyeshe uwezo wake. Natumai si mbaya sana.
Mwandishi: Je, Jumanne ni “mchezo mkubwa” kwa kikosi hiki?
Rosenior: Ndiyo. Wanaweza kucheza kwenye mechi kubwa na wanaweza kufanya vizuri kwenye mechi kubwa. Jumanne bila shaka ni mchezo mkubwa.
Mwandishi: Maoni yoyote kuhusu wasiwasi ambao Arsenal wamekuwa nao kwenye mechi zao za karibuni?
Rosenior: Tutaona. Sisi tutaenda kucheza mchezo wetu.
Mwandishi: Kipaumbele chako ni nini kati ya sasa na muda wa kuanza mchezo?
Rosenior: Kupona. Kupumzika. Ni wiki nyingine yenye mechi tatu na itakuwa mechi ya nguvu sana kimwili. Kazi yangu ni kuandaa timu vizuri kadiri niwezavyo, mengine yote ni kelele pembeni.
Mwandishi: Filip Jorgensen yuko karibu kurudi?
Rosenior: Yuko karibu. Natumai ni dhidi ya Arsenal, au mchezo unaofuata.
Mwandishi: Enzo Fernández, hali yake ya kiafya inaonekana kuwa ya kiwango cha juu tena?
Rosenior: Yuko fiti. Unamuona akiingia kwenye boksi dakika ya 92, 93. Ana uwezo wa kipekee wa mwili, anapona haraka. Takwimu za umbali anaokimbia ni za juu kabisa. Ukiongeza ubora na uongozi wake, ninaufurahia sana kufanya kazi naye.
Mwandishi: Taarifa za kumhusisha Mamadou Sarr, lolote la kusema?
Rosenior: Sisemi kuhusu wachezaji wa klabu nyingine. Sijawahi kufanya hivyo na sitaanza leo.
Mwandishi: Matokeo mazuri ni uthibitisho kuwa wewe ndiye mtu sahihi kwa kazi hii?
Rosenior: Nitakuwa mkweli, sijali kuhusu hilo. Niko hapa kufanya kazi. Tukifika fainali, ni jambo kubwa kwa Chelsea Football Club, si kuhusu mimi. Muda utaonyesha, lakini hilo si jambo lililo mbele ya fikra zangu.
Mwandishi: Ujumbe wa mwisho kwa mashabiki?
Rosenior: Mtupime kwa uchezaji wetu. bidii ya kucheza, nidhamu, umoja, udhibiti. Kama hivyo ni vitu visivyojadilika, ushindi unakuwa matokeo, si matumaini.