Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ukizungumzia kimbinu Enzo Maresca amemzidi Liam Rosenior but alichowin kocha huyu mpya nikawajengea Chelsea mentality ya ushindi kwa kuwajaza upepo kitu ambacho Maresca amefeli aliweza tu tukikutana dhidi ya team kubwa pekee, pili kocha hajataka kupaka rangi nyingi nyingi amewataka wachezaji Wajikite kwenye basic za mpira, kuongeza intensity ya game, kucheza direct football hakutaka kubadilisha kwa kiasi kikubwa
Mapema bado kutoa tathmini, angalau tuangalie kwa mechi 8-10 atazocheza nazo Rosenior, isijekuwa ni nguvu za soda wachezaji wanapambania kupata no kwa kocha mpya baada ya hapo tunarudi kule kule utumwani Misri...
 
Kulikuwa na wakati ambapo uongozi wa Chelsea ulitaka kumsajili Adama Traoré wakati alipokuwa akiichezea Wolverhampton Wanderers.
Kwa uhalisia, yeye si mchezaji wa mpira wa miguu bali ni mchezaji wa rugby au mwanamieleka vile.

 
Si bado mechi moja anafikisha mechi nane
Rosenior bado anapata matokeo, lakini kiwango cha uchezaji hakiridhishi. Nilisema huko nyuma na narudia tena.

Huenda wachezaji bado hawajamuelewa kikamilifu.
Huenda pia safu ya ulinzi inamuangusha.
Huenda pia kushuka kwa ubora wa Caicedo, Palmer, James kunamuathiri sana — hawa wachezaji hawako kwenye viwango vyao. Hata Pedro Neto hayupo kwenye ubora wake tena. Hata Cucurella kabla ya mechi ya jana alikuwa hachezi vizuri ila jana alipotokea benchi ndipo aliingia na moto.

Hata wachezaji wachanga kama Garnacho, Gittens, Delap na Hato waliokuwa wanaonyesha kuimarika kipindi cha Enzo maresca, sasa wamepotea. Ni kama wamerudi mwanzo kabisa.

Nampenda Liam Rosenior kama kocha — ni mtu positive, anaongea sana na wachezaji — lakini nimeona udhaifu ambao ukiachwa ukae muda mrefu unaweza kumzuia kufika kiwango cha juu zaidi.

1) Anawaaonea huruma sana wachezaji.
Huwezi kuwaonea huruma wachezaji wasiojituma na kucheza vizuri mara kwa mara kama Disasi, Badiashile na wengineo. Mchezaji akishindwa kucheza vizuri, tupa nje atakuja kukufuzisha kibarua.

2) Hana ile nguvu ya ku-command kama alivyokuwa nayo Enzo Maresca.
Hiyo authority ndiyo iliyomsaidia Maresca kuwafanya hawa vijana wafuate maelekezo yake na kucheza vizuri na kutwaa makombe mawili ya haraka haraka. Rosenior anatakiwa kuweka msimamo: wachezaji wajue anataka nini, na wasipofuata maelekezo, wapigwe benchi hata kama ni wachezaji muhimu.

3) Anakuwa mkarimu kupita kiasi kwenye muda wa kucheza.
Anafanya rotation kubwa kupita kiasi na kuwapa dakika wachezaji ambao hawajastahili. Gittens, Garnacho, Delap na wengine hawapaswi kuanza mechi labda zile za umuhimu mdogo au kucheza dakika 45 hadi wakomae kiakili na kujua kufanya maamuzi sahihi ya kiume wanapokuwa uwanjani.
 
Mapema bado kutoa tathmini, angalau tuangalie kwa mechi 8-10 atazocheza nazo Rosenior, isijekuwa ni nguvu za soda wachezaji wanapambania kupata no kwa kocha mpya baada ya hapo tunarudi kule kule utumwani Misri...
Hata mechi 10 hazitoshi, yule mbeba mizigo Potter alicheza mechi tisa bila kupoteza lakini baada ya kubanguliwa na timu yake ya zamani Brighton 4-1 alipotea kuanzia hapo hadi akafukuzwa. Pamoja na mechi nyingi tunatakiwa kumpima kwenye mechi kubwa na hizi mechi za timu zinazoweka mabasi na makontena nyuma. Akipita vipimo hivyo ndipo tumuite kocha mzuri. Kwa muda Rosenior kaanza kazi ni January, huyu muda mzuri wa kumuasses ni May. Timu ibaki top 4 na iende mbali kwenye UCL (angalau robo fainali) angalau hizo ligi mbili. Sio FA na Carabao cup hizi ligi sio size ya Chelsea kutumia kumpima kocha.
Matokeo ya Graham Potter mechi 10 za kwanza (Alianza kazi Chelsea mwezi Septemba 2022, na mechi zake 9 za kwanza zilichezwa kati ya 14 Septemba 2022 na 25 Oktoba 2022.)
  1. Chelsea 1–1 Salzburg– UCL - 14 September 2022
  2. Crystal Palace 1–2 Chelsea – Premier League
  3. Chelsea 3–0 AC Milan – UCL
  4. Chelsea 3–0 Wolves – Premier League
  5. AC Milan 0–2 Chelsea – UCL
  6. Aston Villa 0–2 Chelsea – Premier League
  7. Brentford 0–0 Chelsea – Premier League
  8. Chelsea 1–1 Man United – Premier League
  9. Salzburg 1–2 Chelsea – UCL - 25 Oktoba 2022.
  10. Brighton 4–1 Chelsea – Premier League
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.
-Fabrizio Romano

1769945628487.png
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.

Chelsea hawakufurahishwa na maneno na nia ovu ya Borussia Dortmund kutaka kumsajili kabisa Aaron kwa kuwa Chelsea inamuona Aaron kama sdehemu ya kudumu ya mradi

-Fabrizio Romano

View attachment 3537500
Hii taarifa ni njema sana kwangu kwani inathhirisha kuwa zile taarifa za mwanzoni kwamba eti Aaron amekataa mpango wa kupelekwa mkopo Strasbourg. Pia hii taarifa ina maan sasa Mamadou Sarr atarudishwa Chelsea ili tuondokane na simanzi ya kumuona Badiashile kila mechi akicheza Ndombolo badala ya kandanda 🤣
1769946244497.png
 
Huu unayama ndio ninaotamani kuuona kwenye ligi sio tu mash8ndano mengine. Inaniuma sana tunakaa m8aka 10 hatujagusa PL. Bado sijaangalia Full Match ya huyu kocha
 
Hii taarifa ni njema sana kwangu kwani inathhirisha kuwa zile taarifa za mwanzoni kwamba eti Aaron amekataa mpango wa kupelekwa mkopo Strasbourg. Pia hii taarifa ina maan sasa Mamadou Sarr atarudishwa Chelsea ili tuondokane na simanzi ya kumuona Badiashile kila mechi akicheza Ndombolo badala ya kandanda 🤣
View attachment 3537503
🚨 Taarifa Maalum: Mamadou Sarr anatarajiwa kufika London Jumatatu hii. Chelsea itavunja mkataba wake wa mkopo na Strasbourg.
Aaron Anselmino ataelekea upande wa pili na atajiunga Strasbourg kwa mkopo.

@RMCsport
 
Tizi la nguvu
Hapo vipi?

 
🚨 Taarifa Maalum: Mamadou Sarr anatarajiwa kufika London Jumatatu hii. Chelsea itavunja mkataba wake wa mkopo na Strasbourg.
Aaron Anselmino ataelekea upande wa pili na atajiunga Strasbourg kwa mkopo.

@RMCsport
Sarr anafanana sana na Badiashile utafikiri ni mdogo wake.
 
🚨🔵 Aaron Anselmino kwenda RC Strasbourg, mambo yamekamilika! Makubaliano ya mkopo hadi mwisho wa msimu yamefikiwa.

Hakukuwa na mpango wa kurejea Borussia Dortmund kwa beki huyo wa Argentina, na Chelsea wamechagua RC Strasbourg kama chaguo bora zaidi kwa maendeleo yake.

Hatua za mwisho za kiufundi zinatarajiwa kufuatia.
-Fabrizio Romano

View attachment 3537500
Chelsea hawakufurahishwa na mwenendo na nia ovu ya Borussia Dortmund kutaka kumsainisha Aaron Pre Agreement ili ajiunge nao msimu ujao kwa kumsajili kabisa. Chelsea inamuona Aaron kama sdehemu ya kudumu ya mradi na Hayupo kwa mauzo - Not For Sale!
@JacobsBen
 
Chelsea iliamua siku mbili zilizopita kujiondoa kwenye mazungumzo ya kumsajili beki chipukizi wa Rennes, Jeremy Jackuet, baada ya kufanya uamuzi wa kumwamini kikamilifu beki wake kijana kutoka akademi: Josh Acheampong (19), na pia kuvunja mikataba ya mkopo ya Mamadou Sarr (20) na Aaron Anselmino (19).

Hivi karibuni, klabu hiyo ilipokea ofa kubwa kutoka kwa moja ya timu kubwa barani Ulaya kwa ajili ya Josh Acheampong, lakini Chelsea ikaikataa moja kwa moja, ikizingatia kuwa Josh anaonekana kama sehemu ya muda mrefu ya mradi wa sasa wa Chelsea. Vilevile, Chelsea ilikataa jaribio la Borussia Dortmund la kutaka kumnunua Aaron Anselmino majira ya kiangazi wakati akiwa kwenye mkopo, ikisisitiza kuwa Anselmino hauzwi, na ikaamua kuvunja mkopo wake mapema ili kumpeleka kwa mkopo kwenye klabu dada ya Rennes kwa kipindi kilichosalia cha msimu.

Na hii Jumatatu, Chelsea inajiandaa kumrejesha Mamadou Sarr kutoka Strasbourg, hatua inayosisitiza zaidi dhamira yao ya kuwaamini mabeki wao vijana.

Maamuzi haya yote yakamfanya Jeremy Jackuet na kambi yake kufikiria upya msimamo wao wa awali wa kuupendelea mradi wa Chelsea. Kwa Chelsea kufunga mlango, Jackuet sasa ameamua kukubali ofa ya Liverpool, ambao jana walikubaliana kulipa €70 milioni ili kupata saini ya beki huyo chipukizi mwenye kipaji.

1770015952314.png
 

📰🎙️ MKUTANO WA WANAHABARI | Liam Rosenior (Kabla ya Mechi na Arsenal)​

Mwandishi: Liam, tayari una kikosi chako cha kwanza?
Rosenior: Hapana. Sijawahi kuwa nacho. Kwa sababu ya mahitaji ya kimwili—Premier League, Ligue 1, Champion League—unahitaji kikosi kipana na kukitumia ipasavyo msimu mzima. Nimekuwa hapa wiki chache tu, bado najifunza kundi hili. Nachagua kikosi sahihi cha kuanza, na pia nachagua kikosi sahihi cha kumaliza mchezo.

Mwandishi: Wachezaji wa akiba wanaendelea kubadilisha mechi, ni ubora wa kiufundi?
Rosenior: Daima kuna kipengele cha kiufundi, lakini sehemu kubwa ni hali ya kisaikolojia. Wachezaji wanaoingia wamekuwa na athari kwenye kila mchezo kwa sababu wanaingia kusaidia timu, si kujilinda wao binafsi.

Mwandishi: Habari za Estevão?
Rosenior: Anapitia kipindi kigumu sana binafsi. Sitamwekea presha. Lazima mambo yawe sahihi kwake kwanza.

Mwandishi: Arsenal ndiyo wanaopewa nafasi. Unaweka vipi muktadha wa mchezo huu?
Rosenior: Huo ndiyo ukweli. Wako mbele kwa bao moja na wako nyumbani, kwa hiyo wanatarajia kusonga mbele. Sisi tunapaswa kuusukuma mchezo mbali kadiri tuwezavyo, tuufikishe mbali, halafu tufanye kipindi cha pili kuwa kikubwa na kujaribu kuugeuza.

Mwandishi: Jamie Gittens?
Rosenior: Alisikia maumivu kwenye msuli wa nyuma ya paja. Sijui ukubwa wa tatizo bado. Ni bahati mbaya sana kwa sababu nilitaka aanze na aonyeshe uwezo wake. Natumai si mbaya sana.

Mwandishi: Je, Jumanne ni “mchezo mkubwa” kwa kikosi hiki?
Rosenior: Ndiyo. Wanaweza kucheza kwenye mechi kubwa na wanaweza kufanya vizuri kwenye mechi kubwa. Jumanne bila shaka ni mchezo mkubwa.

Mwandishi: Maoni yoyote kuhusu wasiwasi ambao Arsenal wamekuwa nao kwenye mechi zao za karibuni?
Rosenior: Tutaona. Sisi tutaenda kucheza mchezo wetu.

Mwandishi: Kipaumbele chako ni nini kati ya sasa na muda wa kuanza mchezo?
Rosenior: Kupona. Kupumzika. Ni wiki nyingine yenye mechi tatu na itakuwa mechi ya nguvu sana kimwili. Kazi yangu ni kuandaa timu vizuri kadiri niwezavyo, mengine yote ni kelele pembeni.

Mwandishi: Filip Jorgensen yuko karibu kurudi?
Rosenior: Yuko karibu. Natumai ni dhidi ya Arsenal, au mchezo unaofuata.

Mwandishi: Enzo Fernández, hali yake ya kiafya inaonekana kuwa ya kiwango cha juu tena?
Rosenior: Yuko fiti. Unamuona akiingia kwenye boksi dakika ya 92, 93. Ana uwezo wa kipekee wa mwili, anapona haraka. Takwimu za umbali anaokimbia ni za juu kabisa. Ukiongeza ubora na uongozi wake, ninaufurahia sana kufanya kazi naye.

Mwandishi: Taarifa za kumhusisha Mamadou Sarr, lolote la kusema?
Rosenior: Sisemi kuhusu wachezaji wa klabu nyingine. Sijawahi kufanya hivyo na sitaanza leo.

Mwandishi: Matokeo mazuri ni uthibitisho kuwa wewe ndiye mtu sahihi kwa kazi hii?
Rosenior: Nitakuwa mkweli, sijali kuhusu hilo. Niko hapa kufanya kazi. Tukifika fainali, ni jambo kubwa kwa Chelsea Football Club, si kuhusu mimi. Muda utaonyesha, lakini hilo si jambo lililo mbele ya fikra zangu.

Mwandishi: Ujumbe wa mwisho kwa mashabiki?
Rosenior: Mtupime kwa uchezaji wetu. bidii ya kucheza, nidhamu, umoja, udhibiti. Kama hivyo ni vitu visivyojadilika, ushindi unakuwa matokeo, si matumaini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom