Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea imefungwa goli 25 hadi sasa. Walifungwa chache zaidi yetu ni Arsenal 17 na Man city 21
Ukiwa na viungo wazuri backline itakuwa nzuri automatically. Ukiwa na viungo wanaotoboka, hata uwe na mabeki wazuri wataachia tu. Viungo na mabeki wakiwa wazuri ni bora zaidi.
Asante kwa ushauri wako
Kuhusu viungo Koach ana mpango wa kuwatumia viungo wote ambao ni wazima
  • Enzo Fernandez kama namba 10
  • Andrfey Santos na Moises Caicedo kama pivot
Waliobaki ni wagonjwa
  • Romeo Lavia (Yuko injury na akija ni mechi moja au mbili anarudi kuuguza majeraha)
  • Dario Esugo (hatakuwepo kwa zaidi ya mwezi)
Sasa naona umeoan kwa nini wanataka kumuongeza kiungo
Lakini priority yenu ni beki kwa sasa mkuu kuliko mid.... hilo kila mtu anaona, hata asiejua mpira ! Enzo as 10, Palmer vp ? Wing ? 7 na 11 Palmer hafanyi vizuri kama namba 10[his natural position]
 
Lakini priority yenu ni beki kwa sasa mkuu kuliko mid.... hilo kila mtu anaona, hata asiejua mpira ! Enzo as 10, Palmer vp ? Wing ? 7 na 11 Palmer hafanyi vizuri kama namba 10[his natural position]
Malezi ya Cole Palmer ni complicated kwa msimu huu, tutamkosa mechi nyingi sana kwa sababu ya Groin injury yake ambayo walizembea akacheza mechi nyingi za mwanzoni huku akiwa majeruhi. Kwa kusema hayo Rosenior ataendl;ea kumtumia mara nyingi sana Enzo Fernandez kwenye namba 10
Hivi karibuni Ronior alisema na waandishi wa habari kuwa anataka kujenga timu chini ya Enzo Fernandez. Nadhani utaelewa anamaana gani. Hata Palmer akiwa mzima anaweza asicheze namba 10 angalau kwa msimu huu
 
John Terry kuhusu Chelsea ya 2004/05
“Ilikuwa kama kuwa na ngazi tatu za ulinzi,” aliyekuwa nahodha wa Chelsea John Terry aliieleza The Athletic kwa tabasamu la kuridhika. “Kama ungekuwa unajenga nyumba, ingekuwa kama kuwa na Claude Makelele kwenye lango la mbele, Ricardo Carvalho na mimi bustanini, na Petr Cech mlangoni. Hutapenya humo, sivyo?”

Terry alikuwa akifurahia sana kukumbuka msimu wa 2004-05, wakati Chelsea waliweka rekodi ya Premier League ambayo huenda ni ngumu zaidi kuvunjwa kuliko nyingine yoyote — kuruhusu mabao 15 tu katika mechi 38 za ligi walipotwaa ubingwa kwa kishindo.

Mwanzoni mwa msimu huu, baada ya wapinzani wa Arsenal kufunga mabao matatu tu katika mechi zao 10 za mwanzo, ilionekana kana kwamba kikosi cha Mikel Arteta kingeweza kutoa changamoto ya kweli kwa rekodi hiyo.

Hata hivyo, Jumapili dhidi ya Manchester United, walifungwa mabao matatu, na kufikisha jumla ya mabao 17 waliyofungwa — jambo lililowaweka mbali na rekodi ya kipekee ya Chelsea ya mabao 15 pekee.

1769530916412.png
 
Chelsea wanafikiria kunyakua hii chuma dirisha lijalo la kiangazi. Unasemaje.
Chelsea are CONSIDERING a move to sign Brazilian forward Endrick in summer.

1769536130550.png
 
Utabiri wangu kwa usiku wa leo mechi zinaanza saa tano usiku kwenye UEFA Champions League: msiwe na roho juu, Chelsea inashinda leo
  • Arsenal wakiwakaribisha Kairat Almaty – ushindi wa 4–0
  • Bayern Munich ugenini dhidi ya PSV Eindhoven – ushindi wa 2–1
  • Real Madrid ugenini kwa SL Benfica – ushindi wa 4–1
  • Liverpool nyumbani dhidi ya Qarabağ FK – ushindi wa 1–0
  • Tottenham Hotspur ugenini kwa Eintracht Frankfurt – ushindi wa 3–2
  • Chelsea ugenini kwa Napoli – ushindi wa 4–3
  • Barcelona nyumbani dhidi ya FC Copenhagen – ushindi wa 3–1
  • Athletic Club nyumbani dhidi ya Sporting CP – ushindi wa 1–0
  • Manchester City nyumbani dhidi ya Galatasaray – ushindi wa 3–1
  • Atlético Madrid nyumbani dhidi ya Bodø/Glimt – ushindi wa 2–0
  • Atalanta ugenini kwa Union Saint-Gilloise – ushindi wa 2–1
  • Inter Milan ugenini kwa Borussia Dortmund – ushindi wa 3–2
  • Juventus ugenini kwa AS Monaco – ushindi wa 3–2
  • Paris Saint-Germain (PSG) wakitoka sare ya 2–2 dhidi ya Newcastle United uwanjani Parc des Princes
🎯 Ikiwa haya yatatimia, basi ni usiku wa kichaa kabisa kwenye #UCL. Moto wa soka wa kweli! 🔥⚽️✨

1769620692838.png
 
Kwaheri Raheem Sterling.

Ukurasa umefungwa rasmi!


Chelsea na Sterling wameachana kwa makubaliano ya pande zote, ambapo Chelsea imemlipa takribani £10m kama sehemu ya mshahara wake uliobaki—kati ya karibu £22m katika mkataba uliotarajiwa kumalizika tarehe 30 Juni 2027.

Safari yake imekuwa na dalili za ubora wa kipaji, lakini ikajawa na kukosa umakini golini, maamuzi mabaya na kutotulia kulikokwenda kinyume na viwango vya Chelsea, hali iliyomtoa kabisa kwenye kikosi cha kwanza.

 
Napoli vs Chelsea

4-2-3-1

------João Pedro------

Neto --- Enzo -- Estevao--Gusto

--Santos---Caicedo --

Cucurella--Fofana--Jame(C)

--------Sánchez--------

Subs:
1) Jorgensen
2) Merrick
3) Acheampong
4) Badiashile
5) Chalobah
6) Hato
7) Palmer
8) Garnacho
9) Gittens
10) George
11) Delap
12) Guiu

1769626697731.png
 
Duniani kuna vituko, eti Fofana ni beki!
Fofana ni beki mzuri, kocha ndie kaboa kumfanya CCB, hili suala Enzo Marseca alishasema kwamba nyakati zote alizomjaribu Fofana kwenye CCB hakucheza vizuri. Fofana anafaa beki wa pembeni ndipo anacheza vizuri
Kocha asipobadilisha mfumo kwa kuweka Backline ya 4 tutafungwa mengi
Anatakiwa kuingizwa Chalobah ili Fofana aende kwenye nafasi yake
 
Hongereni Chelsea kwa kupanda hadi nafasi ya 6, hatua kwa hatua tunapanda pamoja, tukijenga nguvu ya pamoja.
FT:
Napoli 2–3 Chelsea
💙🔥

Ushindi mkubwa, mentality thyabiti, na moyo wa kupambana hadi mwisho.
Safari inaendelea na tunaelekea hatua ya makundi 16 bora kwa ushujaa kabisa.

1769637478054.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom