Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea wamevunja rekodi ya Napoli na Conte ya kutokufungwa nyumbani tangu 8 Desemba 2024, takribani miezi 13 na siku 21 bila kupoteza katika Uwanja wa Diego Armando Maradona.

Ushindi huu mkubwa pia umehitimisha safari ya Napoli kwenye UEFA Champions League msimu huu.
The Blues boys wanasonga mbele vifua wazi na majigambo.
 
Usipumbazwe na hayo matokeo anapata, pale hamna kocha.
Hivi raha mnapata wapi mkiwa mnapinga tu, mnatengeneza upinzani ndani ya ushabiki. Nakubali kama kuna mambo hayaendi vizuri ukipinga inamake sense. Lakini hata timu ikishinda kocha kabahatisha, akifungwa takataka hajui mpira..
Enzo Maresca alijitahidi hivyo hivyo mkamwita takataka, hata alipobeba makombe mawili bado mlimkebehi.
Mnapata wapi raha ya mpira kama kila wakati mnapinga tu na kuopose kila jambo ndani ya Chelsea.
Hamieni kule kwenye timu zinazofanya vizuri
Arsenal wanafanya vizuri, kashinda UEFA zote na kwenye ligi anaongoza. Nendeni huko mtuachie Chelsea yetu takataka tunajua jinsi ya kupambana nayo
 
Chelsea kwa kumaliza nafasi ya 6, wanaweza kukutana na Monaco, Qarabag, Newcastle au PSG katika hatua ya 16 bora. Mechi za hatua ya 16 bora zinaweza kuanza kati ya machi mwanzoni au katikati
 
Usipumbazwe na hayo matokeo anapata, pale hamna kocha.
Kocha mzuri ni pamoja nakuona mistake yako nakusahihisha haraka na kwa wakati sahihi hiki ndicho alichofanya kocha wetu Gittens kazingua nakumtoa angalia aina ya substitution alizofanya ni za akili sana na nachopendea sana kwa huyu kocha Chelsea Sasa hivi inacheza soka la haraka ukilinganisha na mpira wa Maresca na ndio maana unamuona Joao Pedro yupo kwenye form ni aina ya mpira unaomfit
 
Kocha mzuri ni pamoja nakuona mistake yako nakusahihisha haraka na kwa wakati sahihi hiki ndicho alichofanya kocha wetu Gittens kazingua nakumtoa angalia aina ya substitution alizofanya ni za akili sana na nachopendea sana kwa huyu kocha Chelsea Sasa hivi inacheza soka la haraka ukilinganisha na mpira wa Maresca na ndio maana unamuona Joao Pedro yupo kwenye form ni aina ya mpira unaomfit
Kuna maneno ya wahenga wa soka wanasema
Kocha anayejua kushinda wakati timu haichezi vizuri au wakati hana wachezaji wazuri huyo ni kocha hodari sana
Zipo mechi ambazo ingekuwa ni Chini ya Enzo Maresca angeshindwa tena sana, ikiwemo hii dhidi ya Napoli, mechi dhidi ya Brentford nk
Rosenior akitulia akapewa mabeki wazuri akawazoea wachezaji na wachezaji nao wakamzoea, atakuwa bonge la kocha mwenye kushinda mechi nyingi sana
 
Chelsea ni mabingwa wa dunia
Wamepitisha kichapo kwa kila bingwa aliyesimama mbele yao.
Wamewakaza mabingwa wa Ulaya na Ufaransa bila huruma.
Wamewapasuapasua mabingwa wa Italia katika uwanja wao mgumu na wenye hofu.
Wamewasambaratisha mabingwa wa Hispania.
Wamewavunja vipande vipande mabingwa wa England.
Chelsea ikishinda dunia yote inafurahi na anayekasirika ni mchawi tu na Arsenal
 
Mfumo wa uchezaji wa Rosenior utawanufaisha sana akina Joao Pedro na Palmer na hata Estevao Willian
Sababu
Rosenior atamtumia sana Joao Pedro kama namba 9
Atamchezesha sana Esetvao Willian na kumpa uhuru tofauti na Maresca
Atampa uhuru wa kucheza Palmer, Enzo Fernandez tofauti na Maresca alivyowabana wacheze kama anavyotaka
Estevao Willian, Enzo Frenandez na Cole Palmer wakicheza kwa uhuru watatumia uwezo wao wote kucheza vizuri
 
Joao Pedro juu ya tofauti kati ya Liam Rosenior na Enzo Maresca:

"Nadhani Liam anatumia ukatili zaidi. Anataka tucheze zaidi kwa nguvu na kwa umakini. Enzo anataka tuwe na mpira zaidi; ni mzuri sana pia, lakini hiyo ndiyo tofauti."
1769667722385.png
 
Mfumo gani ni bora kwetu kati ya 4231, 3421
Hizo ni mipangilio tu ya wachezaji wanapoanza kucheza. Mpira ukidunda, formation inabadilika kulingana na falsafa ya kocha. Unaweza kuta 343 ya Conte ni tofatuti kabisa na 343 ya Liam Rosenior. Rosenior anatumia mifumo hiyo yote. Chelsea tusimtumie Fofana kwenye CCB hata kama tutatumia mfumo gani, hafai kabisa hapo. Anayejaribu vizuri ni Chalobah. Chelsea kusema ukweli haina CCB mzuri hata Colwill na Mamadou Sarr sio wazuri kivile hapo. Alikuwa ni Silva tu ndiye mzuri kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kuusoma mchezo na kuhisi hatari kabla haijatokea
 
Mfumo wa uchezaji wa Rosenior utawanufaisha sana akina Joao Pedro na Palmer na hata Estevao Willian
Sababu
Rosenior atamtumia sana Joao Pedro kama namba 9
Atamchezesha sana Esetvao Willian na kumpa uhuru tofauti na Maresca
Atampa uhuru wa kucheza Palmer, Enzo Fernandez tofauti na Maresca alivyowabana wacheze kama anavyotaka
Estevao Willian, Enzo Frenandez na Cole Palmer wakicheza kwa uhuru watatumia uwezo wao wote kucheza vizuri
Kwa game ndogo zile za wapinzani wanapaki bus mfumo huo ndio rafiki wa kuwachezesha wote Palmer, Estevao na Enzo Fernandez
 
Mbili kati ya timu hizi aidha zitakutana na Chelsea au Barcelona kwente hatua ya 16 bora
1769711918320.png
 
Jamie Caragher kuhusu Chelsea kurudi UCL 2025/26
"Sidhani kama Chelsea inaweza kufuzu zaidi ya hatua ya makundi kwenye mashindano ya klabu bingwa ya bara la ulaya"
Jamie Caragher kuhusu Chelsea kushinda Kombe la Dunia kwa Vilabu,
"Huwezi ita kombe la Dunia wakati Mabingwa wa Uingereza, Uhispania, Ufaransa na Italia hawakushiriki"
 
Yaani chelsea tunacheza mpira mbovu sana, side ways pass na maback pass kwa kipa kama yote, nawaangalia Aston Villa hapa mipira inavyopitishwa kati sio poa.

Screenshot_20260129_232211_X.jpg

Inabidi kocha aache kiburi cha kutokumwanzisha huyu mwamba.
 
Yaani chelsea tunacheza mpira mbovu sana, side ways pass na maback pass kwa kipa kama yote, nawaangalia Aston Villa hapa mipira inavyopitishwa kati sio poa.

View attachment 3536335
Inabidi kocha aache kiburi cha kutokumwanzisha huyu mwamba.
Palmer anaumwa, mnataka aje kuwa kama Reece James?
Jana na ubovu wake katoa assists 2
Naamini wachezaji wakimzoea Rosenior, hicho kitu unachosema utakiona vizuri tu. Strasbourge ndivyo walivyokuwa wanacheza chini ya Rosenior
Kwa sasa mchezaji mbunifu na mwenye kuweza kumuona na kumhudumia striker akiwemo Joao Pedro ni COLE PALMER. Tumuombee apone na arudi kwenye fitness yake
 
Roadmap yote ya UEFA Champion League hii hapa
Uwezekano wa Chelsea na Barcelona kukutana hakuna hadi fainali
1769777861769.png
 
Mfumo wa kipumbavu sana, kila wakati ni kurudisha mpira nyuma. Ndio maana nawambia huyu Kocha bado sio sahihi kwa timu kama Chelsea
Mfumo wa uchezaji wa Rosenior utawanufaisha sana akina Joao Pedro na Palmer na hata Estevao Willian
Sababu
Rosenior atamtumia sana Joao Pedro kama namba 9
Atamchezesha sana Esetvao Willian na kumpa uhuru tofauti na Maresca
Atampa uhuru wa kucheza Palmer, Enzo Fernandez tofauti na Maresca alivyowabana wacheze kama anavyotaka
Estevao Willian, Enzo Frenandez na Cole Palmer wakicheza kwa uhuru watatumia uwezo wao wote kucheza vizuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom