Kwa upande wangu huu mpira wake na ule wa Maresca hata siuelewi. Ni kwa kua labda naangalia mechi za timu nyingi tofauti tofauti.Uharaka wa kurudisha mpira nyuma? Hakuna kocha pale ile ni takataka. Uliona mfumo wa mtaalamu Conte? Timu shindani na inayo jua nini inafanya inapaswa kupeleka moto muda wote kama walivyo fanya Napoli.
Sisi Chelsea bado tuna lundo la wachezaji matakataka wakiongozwa na kocha. Kiufupi sisi bado sana kuingia kwenye ushindani haswa, tutaishia kushinda makombe ya bonanza tu ila yale makombe ya kibabe tutayasikia kwa majirani.
Huo ndio ukweli mchungu acheni kuwa mnajipa matumaini hewa.
Jana nilikua naangalia Espayol Vs Alaves, watoto mipira inapita kati kati mpk raha hakuna mpira wa kizee maback pass, nikajiuliza hii chelsea yangu itaweza siku moja kucheza hivyo kweli??!