Dhana ya uendelevu au maono ya wamiliki naitilia mashaka kutokana na kinachoendelea. Ukitaka kujenga timu ya ushindani mbeleni ni lazima kuna vitu usacrifise kufikia hayo malengo.
Wamiliki wameshindwa kuacha kocha awe huru na timu yake kiasi wanataka wawe wanaingia mambo mengi ya wachezaji. Maana yake wakiona kocha anafanya jambo ambalo litaenda kinyume na biashara yao iwe rahisi ku interfere kulinda msingi wao.
Kwa hapo tu hiyo project waliyonayo siioni ikitekelezeka. Kwasababu tutakua tunaenda mbele na kurudi nyuma.
Ndg hii model klabu nyingi zilziofanikiwa ndizo zinafuata
Unakumbuka majeruhi ilivyokuwa inaandama sana Chelsea?
Unakumbuka tulivyokuwa tunaionea wivu klabu kama ya Barcelona kwenye kuthibiti majeruhi?
Sasa ni kwa sababu ya huu mfumo ambao Chelsea kwa sasa inatumia
Medical team ndio yenye mamlaka kuhusu muda wa kurudi majeruhi, load management kupitia rotations na usajili wa wachezaji unasimamia na Sporting Directors
Timu zlizofanikiwa kwa kutumia mfumo huu ni pamoja na:
- Bayern Munich
- Barcelona
- PSG
- Juventus
Hawa wamiliki walianza kwa kumpa kocha mamlaka tukasajili majina makubwa yakaja kuflop chini ya Tuchel, alipoondoka, hayo matakataka hayakuwafaa makocha waliofuata.
Matakataka mengine yameng'ang'ania na kugoma kupunguza mshahara kama Sterling anakula m,shahara wa bure tu. Je mnataka turudi huko. La hata mimi siungi mkono
Mchezaji mkongwe mwenye kutaka mshahara mkubwa wengi wao wanakuja kuifanya Chelsea a retirement center.
Naunga mkono kusajili wachezaji wazoefu lakini wenye sifa hizi
chini ya miaka 25
Anakubali mshahara mdogo ili asibetweke akija
Au tusajili mchezaji wa umri mkubwa asiye na madhara kama Tosin, alisajiliwa bure na mshahara mdogo hata akitaka kuuzwa inakuwa rahisi