Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

1768753979657.png
 
Kuna tetesi PSG wanamtaka Enzo Fernandez mwisho wa msimu.

Kama mtakumbuka juzikati nilisema kitu kuhusiana na biashara wamiliki wa club. Hapa PSG anaenda kupigwa mpunga mrefu sana na kama itashindikana kuuzwa, Enzo ataenda kuwa mfia timu kwa sababu ana mkataba mpaka 2032.

Tunaleta mapenzi kwenye biashara za watu
Ni kweli PSG na Real Madrid wanamtaka Enzo Fernández. Nasikia PSG wako tayari kutoa hadi €150 milioni. Sijasikia bado kama wamiliki wa Chelsea wameweka bei au wanataka kiasi gani.

Enzo amekasirika kwa sababu kocha wake kipenzi, Enzo Maresca, ameondoka Chelsea — siyo kwa sababu ya biashara au maamuzi ya wamiliki kama wengine wanavyodai.

Kati ya wachezaji wote walionunuliwa kwa ajili ya mradi wa muda mrefu, nguzo kuu zilikuwa Enzo Fernández na Moisés Caicedo. Hao wawili hawakununuliwa kwa sababu ya biashara ya kuuzwa.

Ni kweli wamiliki wana mapungufu, na malengo yao ya muda mrefu hayakubaliki kwa mashabiki wengi — nami nikiwemo — lakini kuna upotoshaji mkubwa kuhusu mfumo mzima wa mradi wa Chelsea. Wamiliki wanataka kujenga timu yenye ushindani wa kubeba makombe makubwa kwa miaka mingi, huku wakihakikisha mfumo wa uendeshaji unakuwa endelevu. Wale waliowahi kusoma au kufanya kazi kwenye miradi ya maendeleo wanaelewa vizuri dhana ya uendelevu.

Klabu nyingi kubwa Ulaya zinaporomoka kifedha kwa sababu hazijiendeshi kwa faida. Chelsea ikiwa na nguvu ya pesa inaweza kusajili vipaji vyovyote duniani, lakini hilo linawezekana tu kama klabu haiendeshwi kwa hasara. Kwa hiyo kama Enzo Fernández ataondoka kwa sababu ya kutoridhika, hakuna wa kumlaumu. Ataondoka yeye, atakuja mwingine.

Shida inakuja hata mimi naweka walakini ni kusisitiza malengo ya muda mrefu huku malengo ya muda mfupi na wa kati wameacha kuweka ambako mashabiki wengi ndiko wanakotaka. Kusubiri Chelsea ianze kubeba makombe baada ya miaka miatno hadi 10 hakuna mtu ambaye yuko tayari kusubiri huko ni mbali sana.
 
Wamiliki wanataka kujenga timu yenye ushindani wa kubeba makombe makubwa kwa miaka mingi, huku wakihakikisha mfumo wa uendeshaji unakuwa endelevu. Wale waliowahi kusoma au kufanya kazi kwenye miradi ya maendeleo wanaelewa vizuri dhana ya uendelevu.
Dhana ya uendelevu au maono ya wamiliki naitilia mashaka kutokana na kinachoendelea. Ukitaka kujenga timu ya ushindani mbeleni ni lazima kuna vitu usacrifise kufikia hayo malengo.

Wamiliki wameshindwa kuacha kocha awe huru na timu yake kiasi wanataka wawe wanaingia mambo mengi ya wachezaji. Maana yake wakiona kocha anafanya jambo ambalo litaenda kinyume na biashara yao iwe rahisi ku interfere kulinda msingi wao.

Kwa hapo tu hiyo project waliyonayo siioni ikitekelezeka. Kwasababu tutakua tunaenda mbele na kurudi nyuma.
 
Mbn

Mbn pesa nyingi sana!!!?,kwa mnaomjua huyu dogo uwezo wake vipi
Hiyo ni bei ya clabu ya Rennes, Ofa ya sasa ya Chelsea kwa Jérémy Jacquet iko chini ya €65 milioni ambayo Rennes wanaitaka, lakini kiasi halisi bado hakijathibitishwa hadharani. Mazungumzo yanaendelea, na Chelsea tayari wamewatuma wawakilishi kwenda Ufaransa kusukuma dili hilo liendelee.
 
Dhana ya uendelevu au maono ya wamiliki naitilia mashaka kutokana na kinachoendelea. Ukitaka kujenga timu ya ushindani mbeleni ni lazima kuna vitu usacrifise kufikia hayo malengo.

Wamiliki wameshindwa kuacha kocha awe huru na timu yake kiasi wanataka wawe wanaingia mambo mengi ya wachezaji. Maana yake wakiona kocha anafanya jambo ambalo litaenda kinyume na biashara yao iwe rahisi ku interfere kulinda msingi wao.

Kwa hapo tu hiyo project waliyonayo siioni ikitekelezeka. Kwasababu tutakua tunaenda mbele na kurudi nyuma.
Ndg hii model klabu nyingi zilziofanikiwa ndizo zinafuata
Unakumbuka majeruhi ilivyokuwa inaandama sana Chelsea?
Unakumbuka tulivyokuwa tunaionea wivu klabu kama ya Barcelona kwenye kuthibiti majeruhi?
Sasa ni kwa sababu ya huu mfumo ambao Chelsea kwa sasa inatumia
Medical team ndio yenye mamlaka kuhusu muda wa kurudi majeruhi, load management kupitia rotations na usajili wa wachezaji unasimamia na Sporting Directors
Timu zlizofanikiwa kwa kutumia mfumo huu ni pamoja na:
  1. Bayern Munich
  2. Barcelona
  3. PSG
  4. Juventus
Hawa wamiliki walianza kwa kumpa kocha mamlaka tukasajili majina makubwa yakaja kuflop chini ya Tuchel, alipoondoka, hayo matakataka hayakuwafaa makocha waliofuata.
Matakataka mengine yameng'ang'ania na kugoma kupunguza mshahara kama Sterling anakula m,shahara wa bure tu. Je mnataka turudi huko. La hata mimi siungi mkono

Mchezaji mkongwe mwenye kutaka mshahara mkubwa wengi wao wanakuja kuifanya Chelsea a retirement center.

Naunga mkono kusajili wachezaji wazoefu lakini wenye sifa hizi
chini ya miaka 25
Anakubali mshahara mdogo ili asibetweke akija
Au tusajili mchezaji wa umri mkubwa asiye na madhara kama Tosin, alisajiliwa bure na mshahara mdogo hata akitaka kuuzwa inakuwa rahisi
 
Hiyo ni bei ya clabu ya Rennes, Ofa ya sasa ya Chelsea kwa Jérémy Jacquet iko chini ya €65 milioni ambayo Rennes wanaitaka, lakini kiasi halisi bado hakijathibitishwa hadharani. Mazungumzo yanaendelea, na Chelsea tayari wamewatuma wawakilishi kwenda Ufaransa kusukuma dili hilo liendelee.
Sawa
 
Everton wana mpangoi wa kumpa Arsenal Ubingwa
Too bad
Hongereni Arsenal, enedleeni kumng'ang'ania huyo mganga wenu
Man City drop points 2-0
Aston Villa drops points by losing 1-0
Liverpool drops points by drawing 1-1
 
League position:
Man Utd - 5th
Chelsea - 6th

Man Utd - Draw a game
Chelsea - Draw a game

Chelsea - Sack their coach
Man Utd - Sack their coach.

Chelsea's new Coach wins first match
Man Utd's new coach wins first match

Man Utd wins 2-0
Chelsea wins 2-0

The Evil twins 😂😂😂
 

Attachments

  • FB_IMG_1768765399625.jpg
    FB_IMG_1768765399625.jpg
    52.4 KB · Views: 7
Matukio ya Fainali ya AFCON kati ya Senegal na Morocco

Marefa wameharibu AFCON ya mwaka huu kwa kuipendelea Morocco. Sijui Morocco imewapa nini. Hadi kufikia dakika za mwisho, Senegal walifikiria kugomea penalti na fainali ya AFCON 2026 kutokana na maamuzi ya ajabu ya waamuzi ya kuwanyima goli la wazi na pia kuwaminya sana Senegal kwenye mechi kwa kuwapendelea Moroko waziwazi.

Inaonekana Sadio Mané ametumia ushawishi wake mkubwa kuwashawishi wachezaji warudi uwanjani, kinyume na msimamo wa kocha na maafisa wa Senegal ambao walitaka timu iondoke uwanjani.

Morocco walikosa penalti yao, ambapo Brahim Díaz alijaribu Panenka lakini akampa Edouard Mendy mpira kilaini mno. Mchezo ukaendelea, timu zikaingia muda wa nyongeza zikiwa 0–0.

Dakika ya 4 ya muda wa nyongeza, Pape Gueye akafunga bao kali na kuipa Senegal uongozi wa 1–0 dhidi ya Morocco.

Hekima na utulivu wa Mané vimeisaidia Senegal kutwaa ubingwa wa AFCON 2026 — ubingwa wao wa pili baada ya ule wa mwaka 2021.

FT: Senegal 1 – 0 Morocco

Hongereni Senegal kwa ushindi.
Hongera Edouard Mendy kwa kuokoa penalti muhimu na kuipeleka Senegal kwenye ubingwa.

Panenka ni kisusio cha Mendy — laiti Brahim Díaz angejua, angechagua staili nyingine kabisa ya kupiga penalti.

 
Mabeki wa kati ambao tunaowahitaji na tusiowahitaji
✅Levi Colwill — Beki wa kisasa, anacheza mpira vizuri, mwepesi, anafaa kabisa mustakabali wa Chelsea.
✅Mamadou Sarr — Kipaji kikubwa, mguu wa kushoto, beki mkali na mwenye uwiano mzuri.
✅Jérémy Jackuet — Kiwango cha juu cha uwezo, mwepesi, mwenye nguvu na anasogeza timu mbele.
🔵 Aaron Aneslimno — Bado hajakomaa kwa majukumu ya kikosi cha kwanza kwenye ligi kama ya EPL.
Tunawahitaji lakini sio wa kuwategemea sana
🟨 Wesley Fofana - Ni mzuri akiwa fiti, lakini upatikanaji na uimara wa muda mrefu inatia wasiwasi.
🟨 Trevoh Chalobah — Ni beki mzuri, lakini mtindo wake hauendani na mradi wa sasa.
Wanaweza kuondoka
🔴 Tosin Adarabioyo — Makosa mengi, hawezi kumudu mchezo chini ya presha. Hawezi kumudu 1v1 na ni mzito kurudi kulinda goli akishotoka nje ya eneo la hatari
🔴 Benoît Badiashile — Mzito kugeuka na kufanya tackling, na kwenye high line anateseka sana. anapoteza mipira sana na kuiweka Chelsea kwenye hatari ya kufungwa magoli ya hovyo
Anahitaji Mkopo Zaidi
 
Huyu jamaa akiwa fit, Chelsea una uhakika wa kupata clean sheet.
View attachment 3515191

Mabeki wa kati ambao tunaowahitaji na tusiowahitaji

Tunawahitaji lakini sio wa kuwategemea sana
🟨 Wesley Fofana - Ni mzuri akiwa fiti, lakini upatikanaji na uimara wa muda mrefu inatia wasiwasi.
🟨 Trevoh Chalobah — Ni beki mzuri, lakini mtindo wake hauendani na mradi wa sasa.
Wanaweza kuondoka
Ndiyo
 
Wakati umefika wa kusajili malapulapu na mazagazaga kujaza kikosi
Wakisajili wazuri mbona hamsemi?
Enzo Fernandez mmemuita takataka sasa anatakiwa na timu kubwa na atanunuliwa kwa bei kubwa
PSG Wameshaweka Euro 150M
Kuna sehemu jana Chelsea wamewabip Real Madrid kuwa Enzo yuko sokoni
Aondoke ndio mjue umuhimu wake.
Bei Chelsea wanataka ni
£180m/€207m/$241.2m
1768813729240.png
 
Dhana ya uendelevu au maono ya wamiliki naitilia mashaka kutokana na kinachoendelea. Ukitaka kujenga timu ya ushindani mbeleni ni lazima kuna vitu usacrifise kufikia hayo malengo.

Wamiliki wameshindwa kuacha kocha awe huru na timu yake kiasi wanataka wawe wanaingia mambo mengi ya wachezaji. Maana yake wakiona kocha anafanya jambo ambalo litaenda kinyume na biashara yao iwe rahisi ku interfere kulinda msingi wao.

Kwa hapo tu hiyo project waliyonayo siioni ikitekelezeka. Kwasababu tutakua tunaenda mbele na kurudi nyuma.
Embu naomba unisaidie kitu, ni kidhibitisho gani ambacho kinaonyesha wamiliki wanamuingilia kocha?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom