Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

GOAL! João Pedro goal confirmed by VARChelsea 1-0 Brentford

1768669072860.gif
 
Tunaongoza HT kwa 1-0 ila tumeshushiwa mishale kama nyuki. UZembe wa Brentford na umahiri wa Caicedo ndio umetuokoa

Leo James na Palmer hawako mchezoni, Tosin ni spana mkononi, muda wowote atatutosa
ningemshauri Rosenior afanye mabadiliko aingie Santos badala ya Palmer, Enzo aende mbele.
Ebu mcheki hap Tosin kwenye build up ya Brentford, mzigo mzito sana. Robert Sánchez analazimika kuiokoa Chelsea kutokana na beki wake mwenyewe; Tosin amekuwa mzigo mkubwa kwa kikosi na anawaweka kwenye hatari mara kwa mara.

 
Mlichopata jana ni ile new manager bounce. It explains ni kivipi mliafford kupata magoli mawili na mkaamini yule dogo ni mzuri mkampa namba game dhidi ya Brentford.

But we all know y'all are shit. Lampard bado begi la nguo kaliweka standby.
 
Mlichopata jana ni ile new manager bounce. It explains ni kivipi mliafford kupata magoli mawili na mkaamini yule dogo ni mzuri mkampa namba game dhidi ya Brentford.

But we all know y'all are shit. Lampard bado begi la nguo kaliweka standby.
Arsenal mlichoambulia jana ni dakika 96 mkizurura kwenye mapori ya West Bridgford kama watalii wasio na Google Maps, na hamkuweza kupata njia ya kutoka. Bado mkiwa mmechanganyikiwa, mkitafuta “bounce‑back” ambayo haikuwahi kufika. Mwishoni, mlisherehekea tu clean sheet nyingine. Hongereni sana. Leo Aston Villa wanashinda na kufanya gape kuwa 4 points. Nightmare ya Man City inafifia anakuja monster wa Villa Park
 
Arsenal mlichoambulia jana ni dakika 96 mkizurura kwenye mapori ya West Bridgford kama watalii wasio na Google Maps, na hamkuweza kupata njia ya kutoka. Bado mkiwa mmechanganyikiwa, mkitafuta “bounce‑back” ambayo haikuwahi kufika. Mwishoni, mlisherehekea tu clean sheet nyingine. Hongereni sana. Leo Aston Villa wanashinda na kufanya gape kuwa 4 points. Nightmare ya Man City inafifia anakuja monster wa Villa Park
Inabidi uwe haujui mpira kiasi kikubwa mno ili ulichoandika ukiamini kwa nguvu zote.

Mpira siyo hisia. Kuna takwimu. Kuna observation. Kuna historia.

Tumia hivyo vikuongoze.
 
Inabidi uwe haujui mpira kiasi kikubwa mno ili ulichoandika ukiamini kwa nguvu zote.

Mpira siyo hisia. Kuna takwimu. Kuna observation. Kuna historia.

Tumia hivyo vikuongoze.
Wewe huo utumbo unaoandikaga ndii much know sana eh! Arse Anal
 
Hehehe iangalie timu yako ikipambana kupata nafasi ya CL.
We jamaa kamdomo ni kareeefu kila mahali upo, yaani umeshajiaminisha Arsenal wanabeba kombe!! Punguza pupa Arsenal haiwez kuambulia chochote. Tunza hii.
 
Hehehe iangalie timu yako ikipambana kupata nafasi ya CL.
Wakati ule Arsenal mkihemea nafasi ya 8 na europa nyingi mmeshiriki mmeshindwa kuweka impact, hii misimu miwili ya CL ndio mnajiona mabingwa wa mara zote wa PL na UCL, timu yenyewe ya kugangia njaa tu, ikipita msimu huu mbebe kombe msibebe mtateseka sana huko mbeleni.

Arsenal vs Chelsea — Ulinganisho wa Misimu

Arsenal Chelsea
2005–2014 ukame wa makombeChelsea walishinda makombe mengi: EPL (2005, 2010), UCL (2012), UEL (2013), FA Cups
2007/08 kuporomoka mwishoniChelsea walimaliza 2, wakafika fainali ya UCL
2011 – kipigo cha 8–2Chelsea walimaliza 2, msimu thabiti bila kombe
2013 – kufungwa fainali ya Carling CupChelsea walishinda Europa League
2015–2017 kuporomoka kwa enzi ya Wenger2015/16 Chelsea walimaliza 10 (shida), 2016/17 wakashinda EPL
2016/17 – nafasi ya 5Chelsea walishinda Premier League
2017/18 – nafasi ya 6Chelsea walimaliza 5 , wakashinda FA Cup
2018/19 – kupoteza fainali ya EuropaChelsea waliwafunga Arsenal na kushinda Europa League
2018/19 – nafasi ya 5Chelsea walimaliza 3 + wakashinda Europa League
2019 – Emery kufukuzwaChelsea walimaliza 4 chini ya Lampard
2019/20 – nafasi ya 8Chelsea walimaliza 4 + wakafika fainali ya FA
2020/21 – nafasi ya 8Chelsea walishinda Champions League
2021 – kukosa Ligi za UlayaChelsea walimaliza 3 + wakafika fainali mbili
2022/23 kuporomoka kwenye mbio za ubingwaChelsea walimaliza 12 - Timu kuuzwa na mabadiliko makubwa ya kimfumo, kiuongozi na wachezaji
2023/24 kupoteza ubingwa siku ya mwishoChelsea walimaliza 6
2024/25 kutolewa UCL na BayernChelsea walishinda Conference league na FIFA Club World Cup
 
We jamaa kamdomo ni kareeefu kila mahali upo, yaani umeshajiaminisha Arsenal wanabeba kombe!! Punguza pupa Arsenal haiwez kuambulia chochote. Tunza hii.
Angalau naongea ukweli. At the mean time iangalie timu yako ikipambana kupata nafasi ya CL
 
Chelsea jana haikucheza vizuri sana
Ubora wa Sanchez na kukosa umakini kwa wachezaji wa Brentford ndio iliyotupa point 3, goli mbili na clean sheet jana

Hata hivyo kocha mzuri ni yule anayeshinda mechi hata kwa hali ngumu
Nakuapia angekuwa Enzo Maresca hii mechi angeshindwa asubuhi na ampema kwa sababu ya ufahidhina wake kwenye kupanga timu na kufanya sub. Na pia ni mfahidhina kwenye player roles uwanjani.
Simsifii kwa sababu ni mapem,a mno ila namuona Rosenior akifanikiwa zaidi ya Maresca Chelsea. Tusubiri tuone
1768730666360.jpeg
 
Kuna tetesi PSG wanamtaka Enzo Fernandez mwisho wa msimu.

Kama mtakumbuka juzikati nilisema kitu kuhusiana na biashara wamiliki wa club. Hapa PSG anaenda kupigwa mpunga mrefu sana na kama itashindikana kuuzwa, Enzo ataenda kuwa mfia timu kwa sababu ana mkataba mpaka 2032.

Tunaleta mapenzi kwenye biashara za watu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom